Ulikuwa mwanafunzi wa aina gani katika maisha yako ya shule?

Ulikuwa mwanafunzi wa aina gani katika maisha yako ya shule?

Toto lisiloeleweka.. darasani kipanga, halafu kwenye matukio ya hivyo natokea, kwenye matokeo mazuri nimo,kwenye watoro sikosekani. Wenye busara nimo, magumashi huku uchochoroni na wahuni wenzangu tunachoma kushi.. sio mpiga misuli lakini pepa fresh.

Primary nilipata msala mzito nikala saana mikwaju na wanangu. Mwalimu wangu wa hisabati alikuwa akinilinda saana kwenye misala misala

O level nikapiga mwalimu nikatimuliwa.
Nikahamia school ya seminary na ni muislam siku sijui wanakula mkate wa bwana nikaunga nikala, wanangu hawana mbavu,
Nikahama 4m 3 nikarudi islamic misala deile, almanusura nitimuliwe hostel, ila walimu wangu wakanitetea nikarudi. Usoni sura ya wema, matokeo mazuri, ila mimi miyeyusho yeyusho tu, kila sekta nimo [emoji1787]

A level sasa [emoji1787], msala wa kumtia mtu mimba, nikawa sitimbi school, ticha wangu wa physics alikuwa ananikubali kinooma jinsi nilivyokuwa naitendea haki FIZIKIA, sasa akawa hanielewi class hanioni, kimasomo nishashuka kumbe msala wa mimba ushanivuruga, shule ishakuwa ngumu.
Si ndio akanirukia hewani, sauti yake nikaifananisha na demu mmoja nishamsalandia saana kabla ya msala, nikampotezea, siwezi mapenzi ya kuchi kuchi hotae mimi, dah, madam kapiga simu sauti inakuja kuja akaniuliza ushajua unaongea na nani, nikavunga, akauliza tena, nikataja jina la yule mrembo, akawa kama ndio yeye,kilichofata nikashusha punch line za kibabe mnoo, mtoto naona kalainika tu, mwishoooni kabisa madam akataja jina la ubini wangu ........... mie mwalimu wako wewe..
Dah! Nikakosa pozi, akapiga, nikapokea akaniambia kumbe haya ndio yanakufanya una drop school huonekani, lakini ile ilikuwa too late kuniokoa form 6 yote ni kama sikusoma, kwa msala wa mimba.

Namkumbuka saana madam yule kidato cha 5 na 6 mwanzoni alinikubali mnooo, fizilia ilikuwa ni kama nimezaliwa na isac mewton, hiyo mechanics ilikuwa inanitii tu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nilikuwa sitaki kuonewa.

Nilipiga walimu wawili, mmoja primary, mmoja secondary.

Nilimpiga kibao mtoto wa rais primary kwa sababu alileta mashauzi baba yake rais darasani.

Nilikuwa mtu wa kuwarusha watu kila mtu alinijua.

Siku hizi rafiki zangu wakiniona nimekuwa "model citizen" wanashangaa sana.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
nilikuwa maarufu ghafla mzazi akapigiwa simu acha kabisaa hata home walikuwa hawajui kama nina simu kwahiyo ni kasheshe juu ya kasheshe ule mwezi ulikuwa mchungu sana kwangu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] messages hazikuwa mbaya??

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
Mwanafunzi wa kwanza kula hela ya 4k Tanzania mpaka leo record yangu haijavunjwa[emoji1]
Nilipew zawad ya kupanda ndege kwa7b ya kufaul vzr.. that day Nilikuw n furah balaa[emoji28]
 
Duh sipatii picha hiyo fedheha haaaaaaah uliweza kusove vipi sasa?

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
Nilikuwa nanyooshewa vidole achaa tuu nilikuwa nachekwaa,baba alivokuja shule nilichapwaa sanaa,mzee alinkamata akachomeka kichwa changu kwenye mguu yake hili nisikukuluke nilipigwaaa hakujali hata kama mimi ni wa kike,hadi maskio yaliziba wiki nzima
 
Nilikuwa nanyooshewa vidole achaa tuu nilikuwa nachekwaa,baba alivokuja shule nilichapwaa sanaa,mzee alinkamata akachomeka kichwa changu kwenye mguu yake hili nisikukuluke nilipigwaaa hakujali hata kama mimi ni wa kike,hadi maskio yaliziba wiki nzima
Duh duh balaa so baada ya hapo mshikaji ukamuacha?

Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
Binafsi mimi nilikua mvivu sana kusoma (ila nilikua nabukua), sipendi kufanya test (nasingizia ugonjwa).

Ukinisaidia kwenye pepa lazima nikupite, nilikua najua sana kumodify majibu ya msaada.

Sikupenda kuwa kiongozi ila niliishi kama kiongozi.

Tiririka.
Nilikuwa mtukutu sana, na wa mwisho kila mtihani
 
Primary
Daftari na zile biki niemchukua hadi namaliza STD 7

Muandika notes ubaoni
Kwenye macho ya wengi nilionekana mpole
Bahati ya kupendwa sana na walimu karibia wote
Popular sana kutokana na ajali iliyoweka uhai wangu kwenye tundu la sindano.
Ibada
Uwezo wa kawaida ila ndo Mungu kama aliamua kuniinua baada ya ile ajali nilianza kukimbiza sana hadi naondoka..Elimu yangu ilikuwa mteremko sana.
Olevel hiyo.


Advance
Mpole mwenye kushirikiana na majasusi ya shule [emoji38]
Nilikuwa nawachajia simu zao maana nilikuwa na access na funguo za sehemu yenye switch.
Tulikubaliana ntawasaidia kuchaji ila mkikamatwa msinitaje kabisa.
Ibada zaidi,yaani chuo na primary ni sehemu niliyomtumikia Mungu zaidi kuliko kipindi chochote.
Elimu yangu ilikuwa na misukosuko.
Popular kwenye baadhi ya masomo na handwriting yangu ilinipa kujulikana.

Chuo
Mpole hivyohivyo
Ibada
Nilipigwa sana matukio na rummate,,ananipiga exile naona na macho yangu.
Nikajifunza ukali.
Handwriting yangu kama kawa ikanipa umaarufu.
Milima ,mabonde,mteremko, Yaani kiuelimu nimepitia vipindi vyote kulingana na semester.
 
Mvivu kusoma ila nafaulu kwa msuli pepa, walimu walikua wananiaminia kua nna akili sana ila binafsi nilijiona bado hizi sio akili zangu.
Darasani sijibu maswali na sababu kuu ni kua hicho kipindi mi sisomi mambo ya nyuma nshasahau mpaka likaribie pepa.

Mpole sana, na sura ya kipadre.
Nilitaminiwa na mamanzi ila kwa ukauzu wangu sikubandua wengi.
Wewe ni mimi kabisa,nilikuwa na ufaulu wa wastani,ila somo la maths kidogo nilkuwa nalipiga piga sana kutokana ni somo ambalo baba alikuwa anapenda kunifundisha toka primary madarasa ya chini,somo ambalo nilkuwa siliwez mpaka leo ni english,masomo mengine nilkuwa nikiyaotea napiga mpaka B

Mwepesi kusahau mwalimu akiniuliza alichofundisha jana hata sikumbuka,nilkuwa napenda kukaa nyuma sana,sinyooshi mikono kujibu maswali
 
Smart Sana kichwani ila Mbabe
Kiufupi Mwanafunzi mzuri.
Nimekua mzuri kila hatua
Shida tu ni ubabe kutopenda kuonewa wala kuonea.
Malezi yangu pia yalichangia... Mitaa ilinilea.
 
....Uungwana ukitaka kujua ukoje au ulikuwaje uliza watu walio kuzunguka kuhusu wewe.......chukua hii.......
.....Shortly after restoring the sight of the blind man at Bethsaida Jesus asks his disciples “Who do men say that I am?” and after getting several answers – John the Baptist, Elijah, one of the prophets – he asks Peter, “Who do you say that I am?” Peter replies: “You are the Messiah.”
 
mm ndio nlikua sielewek kabsa kwa watoro nipo kwa wenye akil nipo daftar n moja limejkunja ilo kama kitabu cha tiket yote kwa yote nkapata chet 😂
 
Back
Top Bottom