Ulikuwa mwanafunzi wa aina gani katika maisha yako ya shule?

Ulikuwa mwanafunzi wa aina gani katika maisha yako ya shule?

Binafsi mimi nilikua mvivu sana kusoma (ila nilikua nabukua), sipendi kufanya test (nasingizia ugonjwa).

Ukinisaidia kwenye pepa lazima nikupite, nilikua najua sana kumodify majibu ya msaada.

Sikupenda kuwa kiongozi ila niliishi kama kiongozi.

Tiririka.
Nlikuwa mvivu wa kusoma pia ila nlikuwa nafaulu tu. Hilo likanifanya nijione mimi nafaa kuishi abroad niwe mgunduzi... Baadaye nimkawaza kuwa rubani au daktari.
Alaaniwe aliyeniinteroduce kwa fruity loops ambayo sasa inaitwa FL studio aisee hii program ilinitoa kwenye reli kabisa hiyo miaka 2007. Badala ya kuzingatia masomo mimi nikawa busy na fruity loops nikisikiliza muziki nasikia synth, piano roll, kicks, bass nawaza nikifka home tu naanza nayo. Hapo nilikuwa o'level. Kilichofuata sasa badala ya kuwa rubani leo nafuga kuku lakini poa tu bado na deal na ndege maana hata kuku ni ndege
 
Nilikuwa mwanafunzi ninae onekana innocent mda wote muoga wa fimbo kiasi kwamba mpaka adhabu nilikuwa nasamehewa wana weza piga class lote ila mimi nikaachwa

Mwanafunzi nisiye ongea ila nikiwa na dom uko napayuka sana na mkorofi sana ila nikija machoni kwa walimu cool person
 
Anonymous Nobody. Najulikana kama mmoja wa wapokea zawadi kwenye tatu bora baada ya hapo napotea kusikojulikana. GHOST.
 
Mimi shule na unga unga mwana mpaka leo nipo skuli naunga hapa kesho napaper nipo kuchat
Kindergarten uko nilikua napusua kisenge
Primary nikaloose haaaaah Sjui nililogwa
0-level ndo kabisa shetani ms*ng* nikafail
Chuo sasa uko nikapiga fresh Kwa umafia
Chuo kingine sasa ndo naungua unga naama na kunyanyuka


Sent from my Nokia C2 using JamiiForums mobile app
 
_ Niliishi dunia yangu mwenyewe, O-level nilikua mkimya sana to the point nikapewa barua ya kumleta mzazi shule.

Darasani nilikua najibu maswali magumu pekee ( yaani nikiona hakuna aliyenyoosha mkono kujibu swali only then ndio nilikua nanyoosha mkono na kujibu swali)

For some reasons nilikua maarufu shule nzima.

_ A-level mambo yalibadilika kidogo.

_ Chuo kikuu paka leo sikumbuki nilikua mwanafunzi wa aina gani hahaha
 
*Nilikuwa mpole kiasi, sio muongeaji sana, ila nilikuwa na aibu zaidi ya mtoto wa kike.

*Nikichelewa kuingia darasani siingii mpaka nipate kampani ya washikaji.

*Nilikuwa smart sana kwa mavazi ikitokea siku umeme umekatika na sijapiga pasi basi siendi shule.

*Darasani nilikuwa vizuri ila nilikuwa mtoro sana, kama 4m 4 ilipita miezi mi4 sijaenda shule na home wanajua ila sifatiliwi kutokana nilikuwa nasimamia shughuli za mzee.

*Nilikuwa nawaazima pesa wanafunzi hadi walimu na nilikuwa sina tabia ya kuwadai.

*Nilikuwa MALAYA hakuna mfano, yani ni mwanaume MALAYA kweli kweli. Nilipiga sana wanafunzi wenzangu na walimu wa field.

*Darasani kwetu kulikuwa na wasichana 40 ila katika hao mademu zangu walikuwa 29 ndani ya darasa moja.

*Nilikuwa maarufu sana shule, kufika kidato cha pili nikawa nafahamika shule nzima kwa sifa za umalaya na nilikuwa nafatiliwa sana na wanawake..

Mtanisamehe kwa hizi screenshots zisizo na maana ila hii thread imenikumbusha mbali sanaa.


Screenshot_20230416-211011_Gallery.jpg
Screenshot_20230416-210848_Gallery.jpg
Screenshot_20230416-214828_Messenger.jpg
Screenshot_20230416-215306_Messages.jpg
 
Mimi nilikua mtoro na hom wanajua nipo shule, mimi nilikua nakaa hata miezi sifiki shule!!

Kuna ticha mnoko ndo alisababisha yote haya,, yule pimbi alikua ananisaka kwa kosa ambalo sihusiki na alikua ameapa sana class akinidaka nitajuta.

Nilisoma kuanzia form two mpk four bila kunishika tunapishana tu.
 
Nilikuwa mtu wa kupambishwa..ni doko ila ukinijaza upepo nafanya vitu vya hatari sana..nilishawahi kupiga soksi iliyowekwa jiwe ndani na nikafunga goli.ila hadi leo vidole vya miguu vibovu..
Kupanda juu ya mizambarau na kupiga samasoti ilikuwa ni kawaida.shule michezo mingi sikuwa siriaz nilikuwa FAILURE sana.ila nilijigundua nna akili nikiwa COLLEGE.
Ww kama mshkaji wngu fulan primary ukimjaza anaweza kitu cha hatari sana
 
Secondary sikuwahi kuwahi darasani tangu nipo form one japo ilikua ni boarding..mpaka na maliza shule zote sikuwahi kufanya morning speech.
Nilichokuwa nakimudu vizuri ni kuwafanyia vurugu viongozi wanaa na maspy Ile kijasusi piga na kupotea..Kuna tukio Moja Kuna kiongozi tulipanga tukamloweshe kwenye deka lake , Ile shule ni heri uchapwe kuliko kumwagiwa maji baridi lilikua ni Kali Sana, kumbe siku hiyo hakulala yeye kulikua na mgonjwa amewekwa pale na mashuka mengi. Sisi hatukujua Hilo piga nua za kutosha halafu nduki, niliumia Sana baadae
 
Mpaka nakaribia kumaliza shule, form five walijua mi six na six walijua mi ni five.

Sikua mtoro ila ni watu watano tu kwa shule nzima ndo walifahamu jina langu halisi.

Sikua kipanga wala sikua kilaza, sikua muongeaji wala mpole sana.

Ilihali nilikua PCM lakini nilishasoma kwenye michepuo yote iliyokuepo pale shule. Kuna watoto wa tukuyu na kyela walikua na kelele sana, so nilikua naingia mara HKL, HGK, EGM CBG n.k, yani nikiona pana utulivu tu mimi humo humo. Na mwalimu akiingia sitoki.
Dah tunafanana mkuu mi nilikua ghost student yani darasa lolote nachil tu.. chuo nacho ndo hivo hivo yani hata majina ya malecture nilikuwa siyafahamu hata classmates wengi siwajui nilikua napata tabu sana kwenye group discussion mana kila siku naonekana mpya wana hawajui nilikotokea sababu discussion ikiisha tu kuniona ni mbinde sana
 
Wewe ni mimi kabisa,nilikuwa na ufaulu wa wastani,ila somo la maths kidogo nilkuwa nalipiga piga sana kutokana ni somo ambalo baba alikuwa anapenda kunifundisha toka primary madarasa ya chini,somo ambalo nilkuwa siliwez mpaka leo ni english,masomo mengine nilkuwa nikiyaotea napiga mpaka B

Mwepesi kusahau mwalimu akiniuliza alichofundisha jana hata sikumbuka,nilkuwa napenda kukaa nyuma sana,sinyooshi mikono kujibu maswali
Hiyo ya kusahau nilichofundishwa nimekuja kuacha kidogo chuo, maana lecturers wanoko huwa wanatoa kile alichokiongea class, alikokichimba anajua yeye.
Hapo kidogo nilikua makini
 
Mimi na rafiki yangu tulikuwa tunaitwa miss Corridor. Ilikuwa ikifika saa 2 usiku mwalimu wa zamu akiondoka tuu na sisi prepo imeisha hapo tutaingia kila darasa, hkl,hge,hgk,pgm,egm,hgl. Darasa la hkl tuliita jumba la starehe full kelele.

Humo kazi yetu ilikuwa kuhamasisha kelele tupige stori pia kuchukua vimemo kutoka kwa mchumba kupeleka kwa mchumba. Hapo kwenye vimemo ilikuwa lazima tuweke kituo tufungue tusome kilichoandikwa ndio tufikishe. Inshort nilikuwa mpiga kelele na mbea maarufu. Nikaja kutulia form six baada ya kupenda kwa mara ya kwanza[emoji1][emoji1][emoji1] nikaacha na tabia zote.
@Chizi Maarifa alikubamba huko?
 
@Chizi Maarifa alikubamba huko?
Wala hata hanijui, naona juzi kaishiwa kiki tena kila akijizungusha kwenye nyuzi za watu hatrend akaniandikia uzi tena. Kwangu anatafuta kiki alishajua akiniongelea anapata attention humu
 
Kaa chini myamalize sio vizuri kutesa mubaba
Wala hata hanijui, naona juzi kaishiwa kiki tena kila akijizungusha kwenye nyuzi za watu hatrend akaniandikia uzi tena. Kwangu anatafuta kiki alishajua akiniongelea anapata attention humu
 
Kaa chini myamalize sio vizuri kutesa mubaba
Mkuu tutayamaliza vipi wakati sio baba wa mtoto wangu na hatujuani?? Mimi namwangalia tuu anavyonitukana na mtoto wangu kwenye nyuzi zake koz namchukulia hana akili. Baba wa mtoto yupo humu na sio yeye
 
Mkuu tutayamaliza vipi wakati sio baba wa mtoto wangu na hatujuani?? Mimi namwangalia tuu anavyonitukana na mtoto wangu kwenye nyuzi zake koz namchukulia hana akili. Baba wa mtoto yupo humu na sio yeye
@Chizi Maarifa alikifanyia nini kibaya mbona umemchukia ivyo

Mpe nafasi nyingine mlee mtoto atabadilika
 
Mimi na rafiki yangu tulikuwa tunaitwa miss Corridor. Ilikuwa ikifika saa 2 usiku mwalimu wa zamu akiondoka tuu na sisi prepo imeisha hapo tutaingia kila darasa, hkl,hge,hgk,pgm,egm,hgl. Darasa la hkl tuliita jumba la starehe full kelele.

Humo kazi yetu ilikuwa kuhamasisha kelele tupige stori pia kuchukua vimemo kutoka kwa mchumba kupeleka kwa mchumba. Hapo kwenye vimemo ilikuwa lazima tuweke kituo tufungue tusome kilichoandikwa ndio tufikishe. Inshort nilikuwa mpiga kelele na mbea maarufu. Nikaja kutulia form six baada ya kupenda kwa mara ya kwanza[emoji1][emoji1][emoji1] nikaacha na tabia zote.
Aisee
 
Back
Top Bottom