Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nilikuwa Dallas, TexasWakuu Salaam:
Leo October 14 inatimia miaka 21 tangu muasisi wa Taifa hili atutoke duniani.
Wakati kifo chake kimetangazwa, binafsi mimi sikua na uwelewa kuhusu hilo hivyo sijukujua chochote kinachoendelea. Mwaka wa 2000+ ndiyo naelewa sasa.
Kuuliza uliza, kipindi kile tulikua Moshi wakati hiyo taarifa imetoka na ilitangazwa usiku.
Ulikuwa wapi ulipopata habari hizi?
Inawezekana hii trh 14 oktoba , sio trh halisi ya kifo cha Baba wa taifa letuKwa yanayoendelea nchini chini ya CCM wala sina haja ya kukumbuka chochote ndani ya watu wa CCM.
Uwe muasisi, uwe kada, uwe shabiki n.k
Twende na Lissu.
Alikuwa na kingereza kibovu kama cha Meko ?Nashukuru nilikuwa napenda kusikia taarifa ya habari itv iliyokuwa ikitangazwa kwa lugha ya kiengereza kuhusu afya ya babu kule alikokuwa uingereza.
Ni Langfered masako na sijui yuko wapi kwa sasa.
Utasikia.
The condition of mwalimu julius kambarage nyerere who has been hospitalised at st Thomas is said to be bad since today evening.
He has been head operated in order to restore his health condition with negative success.
All the people are ordered to pray for Mwalimu as ordered by President Mkapa.
Tommorow evening our president will fly to London to see his condition.
Oooh hazikuisha siku babu huyooo katembea.
Rip Our babu Nyerere.
Sent using Jamii Forums mobile app
Meko kashindikana yule kwa kiingereza kibovu.
Halafu Ras simba hataki kurudisha ada yetuMeko kashindikana yule kwa kiingereza kibovu.
Anyway, ni suala la mjadala zaidi, maana wao walimu walikuwa wanakuja shule kama kawa, sasa kwanini walikuwa hawafundishi? Angali hata hawakuwa kwenye msiba wa Nyerere?Yule si alikua na hadhi ya kipekee hapa kwetu, walivyosimamisha masomo ilikua sawa...
Ila maisha yako kasi, Mkapa kaondoka kumekua tofauti, maisha yamebadilika.
DubaiWakuu Salaam:
Leo October 14 inatimia miaka 21 tangu muasisi wa Taifa hili atutoke duniani.
Wakati kifo chake kimetangazwa, binafsi mimi sikua na uwelewa kuhusu hilo hivyo sijukujua chochote kinachoendelea. Mwaka wa 2000+ ndiyo naelewa sasa.
Kuuliza uliza, kipindi kile tulikua Moshi wakati hiyo taarifa imetoka na ilitangazwa usiku.
Ulikuwa wapi ulipopata habari hizi?
Oh!Nilikuwa wakati huo nina umri wa miaka 44 tumekaa na mzee mmoja wakati huo alikuwa na umri wa miaka 55 bar tunakunywa baada ya kusikia tu yule mzee alilia kama mtoto mdogo unavojua Konyagi ukilewa kisawasawa mtu akikuambia tu wewe mpumbavu unaweza lia machozi sasa mimi japo nilikuwa nakunywa beer niliingiwa na simanzi pia nikalia.
MUNGU AMUWEKE PEMA RAISI WETU BABA WA TAIFA
pia mungu amuweke pema yule mzee niliyekuwa naye maana naye alifariki mwaka huu January akiwa na 76
Dah!Nilikuwa nimemaliza la saba na nikawa najishughulisha na biashara ya ndizi.....kuna brother mmoja mpangaji wetu alikuwa anazitoa kijijini huko na kuzileta hapo mjini; akawa ananipatia kidogo niuze ili nami nisikae hivihivi. siku ya habari ya msiba kulikuwa kuna mahafali yetu ya kumaliza la saba.............yakaghairishwa na hatukufanya tena!
Naskia hii tarehe ni official annoucement tu ila yeye alikua ameshafiriki siku kadhaa nyumaInawezekana hii trh 14 oktoba , sio trh halisi ya kifo cha Baba wa taifa letu
Sent using Jamii Forums mobile app
Story yako inasisimua!!Duuh,hii huwa inanikumbusha mbali sana. Tukio hili la kifo cha Baba wa Taifa huendana na kumbukumbu ya Mimi kuachwa na demu wangu kipenzi.
Nakumbuka nilikua Mwaka wa kwanza SUA demu alikua Mwaka wa kwanza UDSM. Dalili za kuachwa zilikuwepo, Weekend ya tarehe 8 nilikua nimeenda ili kujua hatma ya penzi letu. Nilifikia kwa mshkaji wangu Hall 9 na demu alikua akiishi hall 3.
Usiku huo niliofika hakuwepo chumbani, kesho yake tarehe 9 jmosi nilienda nikakutana na room mate wake akaniambia "shem, huyu mwenzako Alisha hama chumba anaishi oyster Bay huwa anakuja asubuhi na gari baadae ya vipindi anaondoka. Kwa hiyo kumpata hadi darasani wakati wa vipindi "
Nilipiga moyo konde nikaondoka kurudi kwa mshkaji wangu, siku yangu iliharibika kabisa.
Sikurudi Morogoro niliamua kubaki ili nijaribu kuonana nae jtatu. Nilianza kuhudhuria vipindi vyake vyote kuanzia jtatu hadi Nyerere alivyofariki ndo nikarudi.
Kwa hiyo RIP Nyerere Rip mapenzi
Tuliipata taarifa mchana tukiwa shule ya Msingi Saba saba iliyoko Tarime,wakati huo nipo Darasa la Tatu A,Nakumbuka bendera zilishushwa nusu mlingoti n kuna ki-dada kilikuwa kinaitwa NEEMA MATIKO/MWITA,sina kumbukumbu vizuri la jina la Mzazi wake ila lake ni Neema,kiukweli alilia sana mpaka akatufanya darasa zima tukaangua vilio!
Bado sijajua Nyerere alikuwa mtu wa aina gani lakini alipendwa na kila mtu,si watoto wala watu wazima,UZALENDO HUU WA ZAMANI UMEPOTELEA WAPI SIKU HIZI?
Wewe si yule alopoteza 300,000/ za Msiba....!!?Huu uzi tayari upo humu zamani sana