Ulikuwa wapi wakati kifo cha Mwalimu Nyerere kimetangazwa?

Ulikuwa wapi wakati kifo cha Mwalimu Nyerere kimetangazwa?

Shikamoo bro. Mi nilikua la 3. Njia nzima nilikua naangalia angani nikijua kwakua Baba wa Taifa amefariki wakoroni wanakuja any time. Yaani mawazo yangu Nyerere ni kama Anold Shwaziniga yaani yeye ndio kamanda mwenyewe.
Oyaa! Salimia na hapa! [emoji41][emoji41]
 
Nilikuwa mbeya, nimeajiriwa serikalini.

Nilimlilia sana Mwalimu Nyerere.

Nilikumbuka elimu ya bure niliyopata, nililia sana.

Nilkmlilia Mwalimu Nyerere mpaka akanijia kwenye ndoto, ananionesha alivyozidiwa na madaktari walivhojitahidi kuushtua moyo lakini ikashindikana.

Aliniaga na akasema nimeondoka sitarudi tena acha kulia.

Mbali ya Mwalimu watu wengine wawili niliwahi agana nao mmojawao ni Marehemu Papa Yohana yule aliyewahi tembelea Tanzania,

Namshukuru Mungu kwa yale maono hayo makubwa hivyo.

Endelea kuPumzika vizuri huko Mbinguni Mwalimu Nyerere.
Mamndenyi Nakupenda!
 
sisi wengine baba yetu wa taifa ni mkapa maana tulizaliwa zama zake[emoji849][emoji849]
 
Mimi nilikuwa mwanza nyumbani,baadae nilitoka kwenda kupata moja moto moja baridi huku nikiangalia taarifa ya habari,baadae taarifa maalumu iliingia,lkn alikuwepo jamaa mmoja mlevi alikuja akazima tv na kusema nyerere ni nini?!, mzoga huo wa nini sisi,siku hiyo nilishudia kile ambacho sipendi nikikumbuke lkn pia siwez kukisahau,yule mtu alipigwa mpk aliuwawa hivihivi kizembe kizembe,
Dah Aisee!
Ni machungu watu walikua nayo juu ya kifo cha Mwalimu hlf mtu analeta utani
 
Siku kama ya leo marehemu Ben alitangaza, saa nne asubuhi kuwa Mwalimu ametangulia. Tulikuwa darasani, radio ya mchoma chipsi pembeni ya darasa letu ndo ilitupasha habari, kipindi kile ukisikia wimbo wa Taifa unapigwa redioni, mnakuwa shupavu kutaka kujua nini kimetokea, hivyo tulivyosikia tu huo wimbo, wote kimyaaa kusikiliza.

Ila wengi tulioishi maeneo ya karibu na kwa mwalimu tulishajua mambo yameharibika kule kabla ya tarehe tajwa, barabara ya kwenda kwa mwalimu ilikarabatiwa, walianza kukarabati nyumbani kwake, magazeti nayo yakiripoti; "Kawawa arudi na siri nzito" akitoka kumuona mwalimu St Thomas, mara Mwalimu apumulia mashine kwa 100%, magazeti ya Alasiri na Dar Leo yakiripoti hivyo, mara mortuary ya Muhimbili inakarabatiwa. Yote hayo yalikuwa kati ya tarehe 1 na 10 mwezi wa 10.

Nilikuwa darasani
Kwahiyo hii 14 tunapigwa kamba ?
 
Wakuu Salaam:

Leo Oktoba 14 inatimia miaka 21 tangu muasisi wa Taifa hili atutoke duniani.

Wakati kifo chake kimetangazwa, binafsi mimi sikua na uwelewa kuhusu hilo hivyo sijukujua chochote kinachoendelea. Mwaka wa 2000+ ndiyo naelewa sasa.

Kuuliza uliza, kipindi kile tulikua Moshi wakati hiyo taarifa imetoka na ilitangazwa usiku.

Ulikuwa wapi ulipopata habari hizi?
Nikisema watu wataanza kusema niwape salamu
 
Ilikua siku ngumu, nilipigwa fine mbuzi (kubambuliwa) na mwenyekiti wa kijiji kwa kosa la kwenda shambani kulima wakati tunamsiba wa Taifa.
 
NIlikuwa shule tena tuko darasan ndio tunapewa hizo habari mida ya saa 4 iv

Nilikuwa darasa la 4 wakati huwo

Msamvu Primary school
 
NIlikuwa shule tena tuko darasan ndio tunapewa hizo habari mida ya saa 4 iv

Nilikuwa darasa la 4 wakati huwo

Msamvu Primary school
1999 = Darasa la 4 = 10 to 12 yrs of age

Kama hukuMadelu, basi leo upo na miaka kama 34 mpaka 36. Ushaachama na ujana ahahahahahah
 
Nakumbuka to tulikuwa tunachoma tanuru la tofari. RTD walipo tangaza basi waliokuwa wakubwa sana walipigwa na butwaa
 
Back
Top Bottom