Ulikuwa wapi wakati kifo cha Mwalimu Nyerere kimetangazwa?

Nilikuwa mbeya, nimeajiriwa serikalini.

Nilimlilia sana Mwalimu Nyerere.

Nilikumbuka elimu ya bure niliyopata, nililia sana.

Nilkmlilia Mwalimu Nyerere mpaka akanijia kwenye ndoto, ananionesha alivyozidiwa na madaktari walivhojitahidi kuushtua moyo lakini ikashindikana.

Aliniaga na akasema nimeondoka sitarudi tena acha kulia.

Mbali ya Mwalimu watu wengine wawili niliwahi agana nao mmojawao ni Marehemu Papa Yohana yule aliyewahi tembelea Tanzania,

Namshukuru Mungu kwa yale maono hayo makubwa hivyo.

Endelea kuPumzika vizuri huko Mbinguni Mwalimu Nyerere.
 
Huu uzi tayari upo humu zamani sana
Walikuwa watoto, sahizi ndo wanauelewa huu uzi.

Jf vimejaa vitoto hadi kero. Siku zote nilijua kuna watu wazima humu kumbe ninabishana na watoto tu. Kila siku ni CDM kumbe wamezaliwa wakati inazaliwa.

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Mm kipind hicho nilikua na miaka mitatu sikua naelewa chochote Ila mwaka 2001 kama sikosei ililetwa kalenda yenye picha ya mwl nyerere pale nyumban nikakuta Dada yangu kaikumbatia picha huku analia badae wakaibandika ukutani kila siku nikawa naiangalia ndio baadae bibi akawa ananielekeza nikwa naelewa kua kumbe ndo mana Siku ile dada alikua analia ndo nikaanza kumjua mwl nyerere kuanzia hapo
 
Nilikuwa tayari graduate naongoza mradi Fulani. Nilienda stationary moja nikakuta wahudumu wote wanalia, nikawauliza Kuna Nini wakasema Nyerere kafariki. Ilikuwa huzuni Sana ila Mimi sikushtuka Sana maana vyombo vya habari vilitujenga kisaikolojia kwa muda Kama wiki nzima hasa magazeti yalikuwa kila siku yanaandika kwamba Nyerere haponi tujiandae kwa msiba mzito.
 
Nilikuwa darasa la Tano Buzuluga shule ya Msingi hapo Mwanza Ng'wanzalima! Tukiwa chini ya uongozi wa mwalimu mkuu mama Emmanuela Kamani. Kuna wadada walikuwa wanaimba sana zile nyimbo akina Joyce Magoma, Bhoke Ndera, Namana Elias na wengine.
 
Mimi nilikuwa mwanza nyumbani,baadae nilitoka kwenda kupata moja moto moja baridi huku nikiangalia taarifa ya habari,baadae taarifa maalumu iliingia,lkn alikuwepo jamaa mmoja mlevi alikuja akazima tv na kusema nyerere ni nini?!, mzoga huo wa nini sisi,siku hiyo nilishudia kile ambacho sipendi nikikumbuke lkn pia siwez kukisahau,yule mtu alipigwa mpk aliuwawa hivihivi kizembe kizembe,
 
Kwa yanayoendelea nchini chini ya CCM wala sina haja ya kukumbuka chochote ndani ya watu wa CCM.

Uwe muasisi, uwe kada, uwe shabiki n.k

Twende na Lissu.
Unadhibitisha utaahilaa wako mbele ya kandamnasi,ni kweli mpumbavu hajifichi,
 
Nilikuwa darasa la kwanza, kijiji chetu hakipo mbali na Butiama ninachokumbuka niwatu wazima hasa vijana wakijijini kuhamia Butiama kwa mwalimu, waliporudi wakawa wanatusimulia jinsi walivyokuwa wakila na kunywa bure, siku ya mazishi tulisikia mizinga ya kijeshi wazee wa kijijini wakiongozwa na babu yangu walikuwa wamekusanyika kwababu wakisikiliza Redio Tanzania, huku tukizuiwa kucheza wala kupiga makelele, hakika kilikua kipindi cha majonzi kijiji chetu kilikuwa kimepoa sana, hapo ndipo nilipoanza kusikia story nyingi kuhusu Mwl Nyerere
 
nazaliwa
 
[emoji1787][emoji1787]
 
Nilikuwa nasoma std 1 Mambo pr. School Lushoto Tanga...
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Dah watu walikuwa hawana utani yani wakapiga hadi wakaua.
 
Shikamoo bro. Mi nilikua la 3. Njia nzima nilikua naangalia angani nikijua kwakua Baba wa Taifa amefariki wakoroni wanakuja any time. Yaani mawazo yangu Nyerere ni kama Anold Shwaziniga yaani yeye ndio kamanda mwenyewe.
[emoji23][emoji23][emoji23]huyo tukimwita sozniga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…