Vocal Fremitus
JF-Expert Member
- Oct 20, 2016
- 1,287
- 6,648
Mm pia nacheza na hii kanuni. Kuna wakati pisi inajua kabisa ww ni handsome, pesa ndogo ndogo hazikupigi chenga na una kausafiri kako lkn unamtongoza anakupiga chini.Ndio maana uwa sitongozi ovyo ovyo. Nalinda hii brand.
Guess what? Hakupigi chini kwa vile hakupendi. Ila anataka kuvimba mtaani au kwa watu kua yeye hababaiki na status! Yani anakupiga chini ili kupandisha brand yake. Ndio wale utaskia, "Yule dada ni noma katongozwa mpaka na wenye magari lkn kawapiga chini!"
Halafu unakuta msela anaekubaliwa ni choka mbaya tu halafu hana time nae kabisa 😀. Anapigwa mimba na jamaa anasepa. Baadae utashangaa pisi inakufata kukuomba matunzo ya mtoto ambae sio wako!