Ulishawahi kulazwa kituo cha polisi na mkeo?

Ulishawahi kulazwa kituo cha polisi na mkeo?

huwezi kufa kwa kupigwa makofi mashavuni
Hivi,mashavu yapo sehemu gani ya mwili wa binadamu?Siyo sehemu hatarishi?
NB;Umewahi kuchabangwa kofi hadi ukaona "dubleduble",mate laini kuruka kutoka mdomoni na kuvimba mashavu?Unajua kama ukimpiga mtu makofi kwa nguvu unaweza kumtegua hadi mishipa ya shingo ambayo ni hali ya hatari sana na anaweza akafa?
 
Mkuu ni kweli nilikuwa na kosa ambapo kisheria nilipaswa kufikishwa mahakamani.

Afande alinifuata korokoroni alfajiri akanipa njia ya kujinasua kwenda mahakamani nayo ni kumpa 50k, nilimuelewa na ndivyo tulivyomalizana kishikaji kwa kumpa afande hiyo hela, sijui afande alivyomwambia mke wangu, Ila my wife aliniambia tu kuwa kafuta kesi hivyo twende nyumbani.

Hasira ilibaki kwangu niliyelala kituoni usiku mzima, sikuongozana naye kurudi nyumbani.
ukute afande alivyokuweka nguvuni akaenda kulala kwako halafu asubuh ukampongeza na lififte
 
Akikuvunjia heshima itabidi mzungumze nini hapo?
Mchape viwili vitatu ili ajue nani ni mwamba kwenye familia. Akileta ukaidi mtimue arudi kwa mamaye.
Kama uliweza kumtongoza kwa lugha nzuri yenye ushawishi hadi akaja kuishi na wewe,unashindwaje kumpa na kumzoesha lugha za mvuto na ushawishi ili aendelee kukusikiliza bila majibizano na vurugu?Kipigo ni ushahidi kwamba huna uwezo wa kujieleza ukaeleweka.Rejea kwa mleta uzi alivyotupwa selo kwa kushindwa kujieleza kwa askari kwa umakini,kutulia na kushawishi askari.
 
Hivi,mashavu yapo sehemu gani ya mwili wa binadamu?Siyo sehemu hatarishi?
NB;Umewahi kuchabangwa kofi hadi ukaona "dubleduble",mate laini kuruka kutoka mdomoni na kuvimba mashavu?Unajua kama ukimpiga mtu makofi kwa nguvu unaweza kumtegua hadi mishipa ya shingo ambayo ni hali ya hatari sana na anaweza akafa?
ukipgwa kofi la sikioni lazima ukate network ila ukiwa na precision ya kulenga shavu uwez kuua
 
ukipgwa kofi la sikioni lazima ukate network ila ukiwa na precision ya kulenga shavu uwez kuua
Basi,kwa nini utegemee kulenga shavu tu wakati unajua unayemtwanga kofi siyo kisiki kwamba hatakwepa na ukampiga sehemu nyingine kwa bahati mbaya?Na kwa nini uivute suluhu ya haraka kwa kipigo tu?Hakuna njia nyingine itakayokupeleka kwenye suluhu sahihi?
 
Kwenye heading nilielewa kwamba wewe na mkeo mlilala kituo cha polisi ila kumbe mkeo ndiye alikulaza kituoni.


Pole sana!

Ila huyo Mnyiramba achana naye jumla.

Kawaida mwanamke akishakupeleka polisi hapo hakuna mapenzi.

Kwanza anaweza akakuua!
Mimi kuna mmoja aliwahi nipeleke, nikaitwa dawati la jinsia, nikaenda.
Wakaanza ngonjera na vitisho kuwa nimempiga. Nikawaambia aeleze vizuri kosa ni lipi, aksema hakuwapikia watoto alikuwa anajisikia vibaya. Akaulizwa kama alitoa taarifa kwangu, akakataa.

Kimwanamke kimoja kikaanza, hata kama hakupikia watoto, huna haki ya kumpiga. Nikamuuliza unao ushahidi kama nimempiga, akasema mimi nimepokea malalamiko, nina uwezo wa kukuweka lockup. Nikamwambia, majadilianao yameishia hapa, nipelekeni mahakamani.

Basi wakachachamaa kuwa nina kiburi, watamsaidia mke wangu na watanipa fundisho, nikasema nasubiri. Kimbembe ikawa mke wangu hataki niwekwe lockup. Maana anajua jinsi nilivyokuwa na react sikuwa natania, ndoa ingeisha. Wakamwambia aandike maelezo, mimi nawekwa lockup then mahakamani. Wife akawajibu sina ushahidi mahakamani, na sitaki awekwe lockup maana hana kosa. 😂

Kilichoendelea ni yeye kukoswa kofi na kidada kimoja, eti unatusumbua. Kidogo akaja OCD akasikiliza marumbano, akawambia msizunje ndoa za watu, huyu dada anampenda mmewe, waacheni huru.

Kurudi home hana hata nauli, anatembea kwa miguu. Nikampa nauli ya daladala, nikapanda boda boda nikaondoka. Home nikawachukua watoto nikaondoka nao kwenda matembezi bila kumpa taarifa. Jioni hatukurudi, 😂😂 ngoja niishie hapa story ndefu na inachekesha mwishoni.
 
huwezi kufa kwa kupigwa makofi mashavuni
Kofi la shavu, kajaribu kulikwepa, kapepesuka, kajigonga ukutani, mara macho yameageuka nje ndani. Hapo majirani walisikia ukipayuka NTAKUUA WEWE, NTAKUUA, umekimbiza hospitali, mwenyekiti wa mtaa kashauri nenda polisi kajisalimishe, upo umeshikiliwa na polisi baada ya muda unapata taarifa kazinduka yupo kwenye oxygen. Ukiachiwa hapo mambo ya kupiga unastaafu, mtu akikukera unajiondokea.
 
Ndo maana wanawake wa Kenya 🇰🇪 wanawadharau Sana nyinyi jamaa wa Kenya.
Mwanamke akizingua Sana kichapo hakikwepeki.
Kuna mambo yakikukuta kwenye maisha na ukatoka salama yanakukumbusha kuwa mstaarabu sana, unaweza itwa dhaifu ila wewe unajua unakwepa nini. Mojawapo ni hili la kupiga watu.
 
Basi,kwa nini utegemee kulenga shavu tu wakati unajua unayemtwanga kofi siyo kisiki kwamba hatakwepa na ukampiga sehemu nyingine kwa bahati mbaya.Na kwa nini uivute suluhu ya haraka kwa kipigo tu?Hakuna njia nyingine itakayokupeleka kwenye suluhu sahihi?
as anger management consultant hua nashauri sana wateja wangu kuwalamba vibao wanao wakwaza ukimdunda mkwazaji una release dopamine unakua stress free hii inakuepusha na kumuua huyo bwege huko mbeleni au wewe mwenyewe kujiua au kua mlevi kupindukia kupambana na stress mtu akikwaza usisite kumlamba mambata usiangalie umri jinsia wala cheo as longer as amekuuzi na yuko within proximity mkutanisshe na shambulio la kudhuru mwili
 
Ndo maana wanawake wa Kenya 🇰🇪 wanawadharau Sana nyinyi jamaa wa Kenya.
Mwanamke akizingua Sana kichapo hakikwepeki.
Na utegemee mengi na hutakiwi kujiliza wala kutia huruma na kusema ni bahati mbaya;-
-kuumiza,kujeruhi/kuvunja mlengwa.
-kutia kilema cha muda au kudumu.
-kujenga chuki kwa muathirika,ndugu na jamii.
-kuwa mgeni rasmi kwenye majengo ya serikali(mwenyekiti,mtendaji,polisi,mahakamani na magereza).
-kutumia rasilimali fedha,muda,akili nk kwa mambo yaliyohitaji usuluhishi wa maneno tu.
-kubadilisha uhalisi wa majina ya mtu kwa kumpandisha cheo na kuwa marehemu.
Upo tayari kwa hayo?
 
Ni miezi tisa imepita sijarudi home hadi leo na sina mpango wa kurudi, nilimwachia kila kitu likiwemo jukumu la kulipa kodi ya nyumba
Mlikuwa na watoto? Je umefanya utaratibu wa talaka? kama bado huyo bado ni mkeo na wewe umetelekeza familia, anaweza nazisha mengine na ukalazwa tena ndani kwa muda mrefu.
 
as anger management consultant hua nashauri sana wateja wangu kuwalamba vibao wanao wakwaza ukimdunda mkwazaji una release dopamine unakua stress free hii inakuepusha na kumuua huyo bwege huko mbeleni au wewe mwenyewe kujiua au kua mlevi kupindukia kupambana na stress mtu akikwaza usisite kumlamba mambata usiangslie umri jinsia wala cheo as longer as amekuuzi na yuko within proximity mkutanisshe na shambulii la kudhuru mwili
Mshauri wa aina yako ni wa kufungwa kamba ngumu ya katani mikononi na miguuni,kupandishwa kwenye carriers au boots za mabasi ya kuelekea Dodoma.Na ukifikishwa huko ni moja kwa moja upelekwe kwenye ile hotel ya nyota tano inayoitwa "Milembe Resorts and Hotels" uishi kwa raha hata miaka mitano.
 
Back
Top Bottom