Ulishawahi kulazwa kituo cha polisi na mkeo?

Ulishawahi kulazwa kituo cha polisi na mkeo?

Wala usipige. Ondoka zako nenda bar au kwenye starehe nyingine. Kushachafuka watu wanatembea na magonjwa ni sababu tu ya kumalizia ndo inahitajika. Unakuwa muuaji wakati ulipiga tu kofi.
Hiyo mbinu ilinisaidia mara nyingi sana, wife akianzisha fujo tu nafungua mlango natembea hatua 20 niko grocery, nikirudi ni kulala tu.
 
Huko kumalizana kishikaji,,ndio kumalizana gani??embu fafanua inaweza kuwa ni mbinu Bora ya kutumia endapo na Mimi huyu wangu naye akibahatika siku kunipeleka Kwa wafanyakazi wenzangu
Eti kwa wafanyakazi wenzako alafu hujui "kumalizana kishkaji"🤣🙌
 
Sasa hasira za nini dada yangu mweupe mweupe 🤩
Subiri kwanza, we ni nani? Yupi? JF bwana! 😂😂😂

Ila mkuu umenikera sana jinsi ulivyomtreat huyo mwanamke wako kwenye hilo suala, yawezekana una mazuri yako kwake, lakini hilo specifically umekosea sana, ndio maana Masai dada hapo juu amekuuliza kama bado mpo pamoja. Ilitosha sana huyo dada kutokukuangalia usoni tena.
 
Mhusika ameisema kwa kejeli nami nikamuuliza kwa kejeli kwanini mkeo hakuwa na nauli? Ameisema as if it is funny wakati si kitu kizuri.
His wife did unwise act to his husband,he called Kanjo on him wich caused his husband to sleep in cell.fortunately to him and unfortunately to his wife the marriage ended there.
So, we can't expect him to narrate the story in remorseful way.

Wanawake mtafute hakima walizokuwa nazo mama zetu.
Kesi kama hizi zilikuwa zinaishia uani tu.
 
Malizia stori mkuu

Duuh

Pole na hongera 😂😂 aiseee

Malizia mkuu🙌

Endelea 🙄
Sikurudi nyumbani kwa siku tatu.
Tulipokuwa tunakaa sio mbali na kwao, ni mji mmoja. Nikaamua kuwapeleka watoto kwa bibi yao (mama yake) lakini nikamsimulia kilichotokea na kumuomba asimwambie nataka kumfundisha tu asiwe anapenda kukimbilia polisi kwa tatizo dogo kama hilo. Mama akakubali (alikuwa ananipenda sana kama mkwe anaemjali) akawa anampigia simu mwanae kuhakikisha yuko salama (huruma ya mzazi) lakini hasemi chochote kuhusu watoto.

Baada ya siku 3 nikarudi home peke yangu, akauliza watoto nikamwambia siku ile ulivyoamua kuwaacha na njaa ulitegemea wanaangaliwa na nani? Nimeona huwajali nimewapeleka kituo cha watoto yatima😅. In short aliteseka sana mpaka kujua watoto walipo, maana polisi aliogopa kurudi tena, nyumbani kwao hakutaka kuwaeleza ukweli wa tukio maana ni aibu kwake na kwao nakubarika sana wangembadikikia wote.

NB: ukitaka kumaliza kiherehere cha mwanamke, waweke karibu ndugu zake, hasa mama. Automatically anakosa mtetezi kwao.
 
Subiri kwanza, we ni nani? Yupi? JF bwana! 😂😂😂

Ila mkuu umenikera sana jinsi ulivyomtreat huyo mwanamke wako kwenye hilo suala, yawezekana una mazuri yako kwake, lakini hilo specifically umekosea sana, ndio maana Masai dada hapo juu amekuuliza kama bado mpo pamoja. Ilitosha sana huyo dada kutokukuangalia usoni tena.
Kwenye emoj nitakujibu, subiri. 🤭

-Dada yangu naomba unionyeshe baya nililomfanyia huyo mpezi wangu.?
-Naomba ushauri wako, ningefanyaje kwa tukio hilo?
Napenda kujifunza
 
Niliwekwa ndani na mke wangu baada ya mimi kugoma kutoa mchango wa kumdhamini kaka yake aliyekamatwa na pembe za ndovu.

Zilitakiwa milioni 5 kumdhamini kaka wa mke wangu, ndugu zake walijikusanya wakachanga milioni 3. Zile mbili zilizopungua mke wangu alikuja kuniomba nitoe hizo hela ili kukamilisha malipo ya dhamana.

Sikuwa na hiyo hela, nilimwambia wazi kuwa sina hela. Kilichotokea sasa baada ya kumwambia hivyo alinifokea kwa ukali akinituhumu kuwa nina roho mbaya na sipendi kusaidia ndugu zake Ila naweza kuhonga malaya tu huko mitaani.

Sikufurahishwa na hayo aliyoniambia so nilimfata na kumcharaza kwa vibao vitatu vya shavu ili kumshikisha adabu. Alipiga yowe la uchungu na kutoka baru akatokomea sijui wapi huko.

Baada ya kama lisaa limoja hivi nilipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni polisi akinitaka nifike kituoni, nilishangaa Ila niliitikia wito.

Nilipofika kituoni mshangao wangu ukawa mkubwa zaidi baada ya kumkuta mke wangu yupo hapo na alifika hapo kuripoti kuwa nimemshambulia kwa kukusudia. Nilishindwa kujitetea maana ni kweli nilimpa Kichapo.

Afande aliyeshughurikia hayo malalamiko ya mke wangu alisema hawezi kulimaliza hilo suala muda huo maana ilikuwa ni saa mbili usiku, atalishughurikia kesho yake asubuhi. Afande alimtaka mke wangu arudi nyumbani Ila mimi sikuruhusiwa kurudi nyumbani bali nilitakiwa kulala hapo kituoni.

Muda mfupi baada ya mke wangu kuondoka niliamriwa na afande wa zamu kuvua viatu na mkanda wa suruali kisha nikasukumwa kwenye kachumba kasiko na dirisha wala taa nikawa nimelala polisi kwa mara ya kwanza.

Nililala kwa usiku mmoja tu, asubuhi tuliyamaliza mambo ya kipolisi kishikaji nikaachiwa huru asubuhi hiyo.

Nikiwa na hasira kali sikurudi home niliamua tu kuachana na huyo mwanamke wa kinyiramba.

Tuliowahi kulazwa polisi na wake zetu tujuane hapa.
Huu uelewa wangu kdg niingie Chaka. Nilijua unamaanisha ulilala na mkeo polisi kwa maana wote mlishikiliwa kumbe mke ndo alikusababishia kulala polisi. Pole sana!
 
Daaah aisee nakumbuka hapo majuzi kati aunt(mshangazi) alisema nimechukua laptop yake...

Alinitishia kunipeleka polisi.
ilibidi niende polisi aiseeee

Alikuja kuiona mana wanasema alisahau kwa gari la rafiki ake sijui.
Mpaka leo nimemkaushia tuu maana naona ana wenge sana aiseeee
🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌
 
Sikurudi nyumbani kwa siku tatu.
Tulipokuwa tunakaa sio mbali na kwao, ni mji mmoja. Nikaamua kuwapeleka watoto kwa bibi yao (mama yake) lakini nikamsimulia kilichotokea na kumuomba asimwambie nataka kumfundisha tu asiwe anapenda kukimbilia polisi kwa tatizo dogo kama hilo. Mama akakubali (alikuwa ananipenda sana kama mkwe anaemjali) akawa anampigia simu mwanae kuhakikisha yuko salama (huruma ya mzazi) lakini hasemi chochote kuhusu watoto.

Baada ya siku 3 nikarudi home peke yangu, akauliza watoto nikamwambia siku ile ulivyoamua kuwaacha na njaa ulitegemea wanaangaliwa na nani? Nimeona huwajali nimewapeleka kituo cha watoto yatima😅. In short aliteseka sana mpaka kujua watoto walipo, maana polisi aliogopa kurudi tena, nyumbani kwao hakutaka kuwaeleza ukweli wa tukio maana ni aibu kwake na kwao nakubarika sana wangembadikikia wote.

NB: ukitaka kumaliza kiherehere cha mwanamke, waweke karibu ndugu zake, hasa mama. Automatically anakosa mtetezi kwao.
Asieee🙌
 
Mimi mke wangu alichukua 3M ya biashara akamkopesha shoga yake anaedaiwa kwenye mikopo nyonya damu wakati shoga yake hana kazi yoyote itakayo msaidia kulipa hilo deni.
Ikabidi niende polisi mwenyewe nikawaambia polisi waniweke ndani maana nikibaki nje ntamuua wife.
Lucha kama lucha
 
Back
Top Bottom