Ulitumia dawa au matibabu gani kupona ugonjwa uliokusumbua kwa muda mrefu?

Ulitumia dawa au matibabu gani kupona ugonjwa uliokusumbua kwa muda mrefu?

Abie

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
289
Reaction score
535
Wakuu salaam,

Watu wengi tumekuwa tukihangaika kupata matibabu ya magonjwa mbalimbali yanayotusumbua kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote. Tunatembelea hospitali mbalimbali, kupata vipimo na kupewa dawa (medications) tofautitofauti lakini mwisho wa siku hatupati nafuu.

Lakini kwa upande mwingine inawezekana kuna ambao wamehangaika lakini mwisho wa siku wakapata dawa na wamepona. Hivyo basi uzi huu ni special kwa kutoa ushuhuda wa namna ulivyopona tatizo lililokusumbua kwa muda mrefu.

Inawezekana ulisumbuliwa na ama kifua, fangasi, maumivu ya kichwa, kiuno, vidonda vya tumbo kwa miezi au miaka kadhaa halafu ukapata dawa na imekusaidia. Kwahiyo karibu utoe ushuhuda wako wa namna ulivyopona ili watu wengine iwasaidie.

Karibu sana.
 
Kuna wakati mtu unaumwa mpaka unakata tamaa. Liwalo na liwe. Sio kama unasikia maumivu constantly, No. Ila tatizo ulilonalo haliishi miaka na miaka na hospitali nyingi ulisha pita.
Kabisa asee yaani unaweza kuta ugonjwa ni mdogo tu lkn unakuondolea comfortability.
 
Nilishawahi kusumbuliwa na vidonda kwenye lips nikateseka kwa muda usiopungua miezi 8, nilitumia aina nyingi sana za dawa bila kupata nafuu. Mtu unatumia vidonge vya dozi ya mwezi lakin hakuna mafanikio.

Mtaani jamaa wakawa wananiwaza labda uyu mtu anazama kunako utamu kwa kila mraka. ( uvinz ).

Mpaka pale nilipokuja kupata ugunduzi kwamba ni allergy ndipo mwanga wa kupona ulipoonekana.
Kujua kwamba una allergy ni mtihani ila mtihani mkubwa ni kujua chanzo au sababu ya iyo allergy.


Nashukuru niko poa sasa.
 
Mi mwenyewe nasumbuliwa na kifua kikavu, yaani muda wote kuna kitu kinakua kooni ukikitoa ( is like makohozi) kina rudi kingine, ni mwaka wa pili now zunguka hospitali mbalimbali,piga X ray hawaoni ugonjwa. Naishia kupewa antibiotics na hazinisaidii. Sijui ni nini hiki na hata nitaponaje
 
Mi mwenyewe nasumbuliwa na kifua kikavu, yaani muda wote kuna kitu kinakua kooni ukikitoa ( is like makohozi) kina rudi kingine, ni mwaka wa pili now zunguka hospitali mbalimbali,piga X ray hawaoni ugonjwa. Naishia kupewa antibiotics na hazinisaidii. Sijui ni nini hiki na hata nitaponaje
Pole sana
 
Mi mwenyewe nasumbuliwa na kifua kikavu, yaani muda wote kuna kitu kinakua kooni ukikitoa ( is like makohozi) kina rudi kingine, ni mwaka wa pili now zunguka hospitali mbalimbali,piga X ray hawaoni ugonjwa. Naishia kupewa antibiotics na hazinisaidii. Sijui ni nini hiki na hata nitaponaje
Pole sana mkuu
 
Meno yalikua yananisumbua na kila likianza kuuma natumia kila aina ya dawa na ushauri kutoka kwa wadau wa kila aina ila maumivu yalikua yanaongezeka tu hadi hatimaye naishia kuling'oa, ikaja kutokea jino lingine likaanza maumivu makali nikawa najaribu kila aina ya dawa ila wapi, siku moja nasafiri kwenye bus huko Tanzania, jino likiwa kama linaniua vile, akaibuka jamaa mmoja alikua anauza madawa kwenye bus.

Akatangaza kwenye baadhi ya dawa yake, anayo pia ya maumivu ya jino, nikanunua dawa fulani hivi ya unga unga mweupe, nikatia kwenye jino baada ya muda mfupi likaacha kuuma, na la kushangaza likapata nafu halijawahi kunisumbua tena, tatizo sikuchukua namba za jamaa maana kwa uvumbuzi wake anaweza akapiga hela sana.
 
Back
Top Bottom