Ulitumia dawa au matibabu gani kupona ugonjwa uliokusumbua kwa muda mrefu?

Ulitumia dawa au matibabu gani kupona ugonjwa uliokusumbua kwa muda mrefu?

Nilishawahi kusumbuliwa na vidonda kwenye lips nikateseka kwa muda usiopungua miezi 8, nilitumia aina nyingi sana za dawa bila kupata nafuu. Mtu unatumia vidonge vya dozi ya mwezi lakin hakuna mafanikio.

Mtaani jamaa wakawa wananiwaza labda uyu mtu anazama kunako utamu kwa kila mraka. ( uvinz ).

Mpaka pale nilipokuja kupata ugunduzi kwamba ni allergy ndipo mwanga wa kupona ulipoonekana.
Kujua kwamba una allergy ni mtihani ila mtihani mkubwa ni kujua chanzo au sababu ya iyo allergy.


Nashukuru niko poa sasa.
Ulitumia dawa gani, ili tatizo linanisumbua mwaka wa 8 saivi
 
mi nasumbuliwa na vidonda mdomon"" mara kwene ulimi,, kwene ngoz unaweza ukahis pengne umejiuma lakin hakuna jaman,, vinapona mata vinalud tena nifanyeje sasa ngoma nimepima hakuna!!
 
Ulitumia dawa gani, ili tatizo linanisumbua mwaka wa 8 saivi
Mkuu sikutumia dawa yoyote, vidonda vyangu vilikuwa vinasababishwa na jua, yaani nikiwa juani mda mrefu basi usiku habari ntaipata lips kuuma na hatimae vidondo.

Mpaka leo hii nikikaa juani tu mda kiasi lazima vitokee. Pia kupanda toyo kwa safari ndefu ule upepo pia ulikua unaniletea ivyo vidonda.

Kazi yako inakufanya ukutane na changamoto za namna iyo??
 
mi nasumbuliwa na vidonda mdomon"" mara kwene ulimi,, kwene ngoz unaweza ukahis pengne umejiuma lakin hakuna jaman,, vinapona mata vinalud tena nifanyeje sasa ngoma nimepima hakuna!!
Mkuu angalia mswaki unaotumia iyo shida alishawah kuwa nayo mtu wangu wa karibu.

Je, mswaki wako umechanua kama sketi ya mwanafunzi wa shule??
 
Mkuu sikutumia dawa yoyote, vidonda vyangu vilikuwa vinasababishwa na jua, yaani nikiwa juani mda mrefu basi usiku habari ntaipata lips kuuma na hatimae vidondo.

Mpaka leo hii nikikaa juani tu mda kiasi lazima vitokee. Pia kupanda toyo kwa safari ndefu ule upepo pia ulikua unaniletea ivyo vidonda.

Kazi yako inakufanya ukutane na changamoto za namna iyo??
Mkuu angalia mswaki unaotumia iyo shida alishawah kuwa nayo mtu wangu wa karibu.

Je, mswaki wako umechanua kama sketi ya mwanafunzi wa shule??
Mimi tatizo langu ni mdomo kukauka kuchanika na hatimae kubanduka ngozi ya juu pia lips zimevimba na ni nyekundu
nb sina tatizo jingine lolote la kiafya
 
Mkuu angalia mswaki unaotumia iyo shida alishawah kuwa nayo mtu wangu wa karibu.

Je, mswaki wako umechanua kama sketi ya mwanafunzi wa shule??
Tatizo langu ni mdomo/lips kukauka kuchanika na hatimae ngozi ya juu kwenye lips kutoka ,lips zimevimba na ni nyekundu
 
Bangi ni dawa ya sikio, je ni sikio liwe na tatizo gani ndiyo litibiwe na bangi?
 
mi nasumbuliwa na vidonda mdomon"" mara kwene ulimi,, kwene ngoz unaweza ukahis pengne umejiuma lakin hakuna jaman,, vinapona mata vinalud tena nifanyeje sasa ngoma nimepima hakuna!!
Jaribu kutumia vitamin B (vidonge). Za 500 tu.
 
Naomba msaa tafazali uume wangu ausimami nikiwa na mwanamke ,ila uko nasimama nikiwa peke yangu

Naomba anaejuwa dawa anisaidiye [emoji24][emoji24][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Wakuu salaam,

Watu wengi tumekuwa tukihangaika kupata matibabu ya magonjwa mbalimbali yanayotusumbua kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote. Tunatembelea hospitali mbalimbali, kupata vipimo na kupewa dawa (medications) tofautitofauti lakini mwisho wa siku hatupati nafuu.

Lakini kwa upande mwingine inawezekana kuna ambao wamehangaika lakini mwisho wa siku wakapata dawa na wamepona. Hivyo basi uzi huu ni special kwa kutoa ushuhuda wa namna ulivyopona tatizo lililokusumbua kwa muda mrefu.

Inawezekana ulisumbuliwa na ama kifua, fangasi, maumivu ya kichwa, kiuno, vidonda vya tumbo kwa miezi au miaka kadhaa halafu ukapata dawa na imekusaidia. Kwahiyo karibu utoe ushuhuda wako wa namna ulivyopona ili watu wengine iwasaidie.

Karibu sana.
Duh
 
Meno yalikua yananisumbua na kila likianza kuuma natumia kila aina ya dawa na ushauri kutoka kwa wadau wa kila aina ila maumivu yalikua yanaongezeka tu hadi hatimaye naishia kuling'oa, ikaja kutokea jino lingine likaanza maumivu makali nikawa najaribu kila aina ya dawa ila wapi, siku moja nasafiri kwenye bus huko Tanzania, jino likiwa kama linaniua vile, akaibuka jamaa mmoja alikua anauza madawa kwenye bus.

Akatangaza kwenye baadhi ya dawa yake, anayo pia ya maumivu ya jino, nikanunua dawa fulani hivi ya unga unga mweupe, nikatia kwenye jino baada ya muda mfupi likaacha kuuma, na la kushangaza likapata nafu halijawahi kunisumbua tena, tatizo sikuchukua namba za jamaa maana kwa uvumbuzi wake anaweza akapiga hela sana.
Ilikuwa mji gani hapa Tanzania? Maeneo gani? Bus za kuelekea wapi?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom