Ulitumia kiasi gani cha fedha ama umepanga kutumia kiasi gani cha fedha kugharamia harusi yako?

Ulitumia kiasi gani cha fedha ama umepanga kutumia kiasi gani cha fedha kugharamia harusi yako?

Suala la Kuoa ama kuolewa bado litaendelea kuwa ni hitaji muhimu miongoni mwa Jamii ya watu wengi Ulimwenguni.

Kwa Tanzania, tunazo Ndoa za aina mbalimbali ambazo zinatambulika kisheria ambazo ni Ndoa za Kidini, Kimila na Kiserikali.

Mara baada ya kufunga Ndoa, maharusi wengi Kwa kushirikiana na jamii zao, hupenda kufanya sherehe. Sherehe hizo huambatana na michango Kwa walio wengi kupitisha Kadi kwaajili ya kuomba kuchangiwa kufanikisha sherehe za harusi zao.

Japo baadhi hufanya sherehe za harusi zao pasipo kuomba michango Kwa ndugu/jamaa na marafiki. Wao hugharamia Kila kitu wao wenyewe na hao ndugu/jamaa na marafiki hupewa Kadi za mwaliko kuweza kuhudhuria sherehe tu.

Kwa utafiti usio rasmi, sherehe za harusi hupendwa zaidi na Wanawake kuliko Wanaume. Wanaume wako tayari kufunga Ndoa za kimya kimya lakini sio Wanawake.

Je, ulitumia fedha kiasi gani kufanikisha harusi yako ama umepanga kutumia fedha kiasi gani kwaajili ya harusi yako na mwenzi wako?

Binafsi, nilitumia kiasi cha shilingi milioni 10 kuweza kufanikisha harusi yangu na Bibi yenu miaka kadhaa iliyopita 🤗🙏

Sikuhitaji kuchangiwa fedha kufanikisha sherehe ile, bali niliweza kujipanga mwenyewe Kwa muda wa miaka 5.

Nilifungua akaunti maalumu Benki (Fixed deposit account) ambayo nilikuwa nina ruhusiwa kuweka fedha pasipo kutoa Kwa muda wa miaka 5 hivi, japo nilikuwa napata interest kidogo za Benki.

Baada ya miaka 4 hivi, nilikwenda kuchungulia fedha nikakuta nina milioni 9.35 so nikaanza maandalizi kujiandaa na harusi Mwaka unaofatia.

Mind you, tayari nilikuwa nina Cheti cha Ndoa ya Serikali na mwenzangu lakini yeye Kiu yake ni lazima tukafunge ile ya Kanisani 🙌

Kuna wakati nilikuwa nafanya biashara ya kununua na kuuza mazao ya nafaka. Nilikuwa naenda Mashambani, nawakopesha fedha Wakulima then wakati wa mavuno nilikuwa naenda kukusanya mazao hasa zao la Mpunga.

Kwahiyo kwenye ile harusi, sikuwa na hofu ya Chakula maana tayari nilikuwa nina stock ya magunia ya kutosha ya Mpunga.

Wanasema harusi ni kula na Kunywa. Kwahiyo nilijiandaa kwenye eneo hili.

Kwenye upande wa Chakula niliandaa wali mweupe,Pilau, chips, mtori, nyama za kukaanga, kachumbali

Vinywaji niliandaa Soda na Maji tu.

Niliandaa Kadi za Mwaliko za watu 300 lakini walifika watu 358 japo hili nilijua lazima lingetokea maana harusi yenyewe niliifanyia Kijijini kwahiyo wengi ni wale watu mnajuana. Kwahiyo niliweka chakula na Vinywaji Kwa zaidi (excess budgeting)

Pamoja na Wageni waalikwa, usiku ule nilikuwa na Mchungaji pamoja na Mwinjilisti ambao walishiriki kuanzia mwanzo wa harusi hadi tunamaliza tukio majira ya saa 9 usiku.

Gharama za mavazi za Wapambe niligharamia mwenyewe kuanzia mavazi ya Kanisani hadi Ukumbini 🙌

Niliamua kukodisha Ma-MC wawili ili kunogesha sherehe 🤗

Pete nilinunua zenye ppt ya dhahabu, kuogopa zisije kupauka.

Mchanganuo wa Bajeti yangu kufanikisha sherehe ile, nimeambatisha kwaajili ya wengine kujifunza.

Kumbukeni, hata kama umeoa bado unaweza kuja kuozesha watoto wako miaka ijayo. Baadhi yetu mnaweza kuwa Wanakamati kwenye harusi za wengine pia

Kwahiyo Harusi zitaendelea kufanyika hata baada ya kufa kwetu maana tutakuwa tumeacha Kizazi chetu kinaendelea Kuoa na kuolewa.
Mi nilikuwa na watu 6 kamati,kikao dk 20 basi,na budget yetu ilienda vizuri kabisa 25m , Harusi ilifungwa DSM,ukumbi Golden Memory -Sinza
 
Mie pia nilikua na kamati ndogo nzito...harusi ilikua ukumbi wa moja ya fukwe za hotel...ma mc walikua wa tatu..wawili watangazaji wa redio maarufu za mjini...ilikua na section ya ma djs wa town kadhaa..vigoo kadhaa wa vyama na serikali....
Hapo lazima kulikuwa na mashoga waliohudhuria.
 
jamii ya mabanianai wafanyabiashara na wanaojua nini mana ya maisha walishaachana na huu ushamba wa kufanya sherehe kubwa za ndoa kwa kuchanga pesa na kuzipeleka kwenye ukumbi na ushamba kama huo

wao huchanga pesa na kuzitumia kukuza mji wa anae oa na sherehe hufanyika hapohapo kwenye huo mji mf kamati ikichanga ml30 jua hizo zitatumika kujenga au kukuza mji na sherehe itafanyika apo na ni kwa muda mchache watu wanatawanyika kuendelea na shuhuli zao

wabongo masifa sasa sherehe kwanzia kwa mke hadi ndoa jumla 90m bada ya shuhuli zote wanakwenda kupanga huku mchango wa pesa zote wamewatajirisha watu wa ukumbi na ndoa ni yao
 
Mi nilikuwa na watu 6 kamati,kikao dk 20 basi,na budget yetu ilienda vizuri kabisa 25m , Harusi ilifungwa DSM,ukumbi Golden Memory -Sinza
Hongera sana Mkuu, budget ya 25M sio mchezo

Natamani kujua japo kidogo, kwenye kiasi hicho cha Fedha, component ipi ilikuwa na gharama kubwa
 
jamii ya mabanianai wafanyabiashara na wanaojua nini mana ya maisha walishaachana na huu ushamba wa kufanya sherehe kubwa za ndoa kwa kuchanga pesa na kuzipeleka kwenye ukumbi na ushamba kama huo

wao huchanga pesa na kuzitumia kukuza mji wa anae oa na sherehe hufanyika hapohapo kwenye huo mji mf kamati ikichanga ml30 jua hizo zitatumika kujenga au kukuza mji na sherehe itafanyika apo na ni kwa muda mchache watu wanatawanyika kuendelea na shuhuli zao

wabongo masifa sasa sherehe kwanzia kwa mke hadi ndoa jumla 90m bada ya shuhuli zote wanakwenda kupanga huku mchango wa pesa zote wamewatajirisha watu wa ukumbi na ndoa ni yao
Kubadirika hapo sio rahisi, nadhani Kuna haja tuendelee kupewa somo pengine tutaelewa mbele ya safari

Japo hoja yako ina mashiko sana. Vipi hicho kiasi kingekuwa kinachangwa kumpa Mtaji Bwana harusi 🤗
 
Nikikumbuka harusi yangu😂
1. Muziki 50000/=
2. Ukumbi wa kanisa 25000/=
3. Usafiri wafanyakazi wenzangu niliwapa ten ten magari matatu
Mengine nikikumbuka nacheka sana😂 Bora niishie hapahapa
 
Sitofanya sherehe ya harusi...
Gauni langu nataka liwe zuri sanaaa... nipige picha za ukumbusho nikitoka kanisani

Baada ya kanisani kila mtu akale kwao!
This will never happen, wewe tutakuozesha Kwa harusi kubwa.
Jiandae kisaikolojia
 
Hicho kiasi kilitosha kugharamia nini na nini Mkuu?

Nahisi haikuweza kutosha kununua hata koti na necktie
Ndoa ya kiislamu, kanzu na kilemba nlikuwa navyo tayari, shela la Bi harusi tulikodi Kwa 20k tu, 10k nilimpa aliyenifunga kilemba kichwani. 20k nilimpa mdogo wa mke wangu ambae aligoma kupisha mlangoni wakati naondoka na dada yake Hadi nitoe chochote kitu.
Msafara wa magari matatu langu moja na mengine walijitolea washkaji wa kazini kwangu, mpiga picha pia alikuwa mshkaj wa kazini ambapo alitumia camera ya ofisini pia. Hayo yote ni nje ya mahari.
Nkarudi nyumbani na mke kiroho safi
 
Back
Top Bottom