Ulitumia njia gani kuishi kwa mtu bila kukuchoka?

Ulitumia njia gani kuishi kwa mtu bila kukuchoka?

LA7

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2019
Posts
655
Reaction score
2,369
Ndugu zangu humu hamjambo wote?

Humu ndani kuna wakati tunakuwa au tumewahi kuishi kwa watu au ndugu, lakini huwa baada ya kuishi kwa kipindi fulani mkiwa pamoja linakuja suala la kuchokana au kuchokwa. Hii inatokana na wewe kuhitaji msaada wao zaidi hasa wa hifadhi na chakula.

Sasa mimi nakumbuka nilipoacha kazi kwa Wahindi nikaenda kuishi kwenye familia moja huko Gongo la mboto, kutokana na maisha ya hiyo familia kuwa ni ya hali ya chini hivyo ilibidi nitumie akili sana ili wasinichoke.

Kwanza kabisa ilikuwa nikienda baharini kuvua samaki, nikirudi nabeba samaki kama wa 20,000 hivi maana nilikuwa nikienda Msasani au Feri nilikuwa namaliza hata mwezi ndio nashuka Gongo la mboto.

Baada ya kucha kazi ya uvuvi nikawa tu pale nyumbani, sasa ilikuwa maji ni ya shida kidogo ila uyapate ni umbali kama wa Km 1 hivi, kwahiyo nilihijitahidi sana maji yasiishe ndani, na kunawakati nikipiga saidia fundi narudi nyumbani na mazaga ya kula pale nyumbani. Kuna wakati nilimsaidia mama kufua, kufanya usafi wa ndani, kupika hasa ugali.

Nilifanya mambo mengi tu, ila zaidi ni baada pia ya kuonyeshwa upendo na ile familia.

Mpaka leo hii huwa wanatamani nirudi japo nilishajitegemea. Ila nikienda kuwasalimia mwendo ni ule ule, japo zingine mama ananiambia niache maana nimeshakuwa na familia na mimi.

Pia Mungu aibariki ile familia, nilijuana nao toka 2014 mpaka leo hii tumekuwa kama ndugu.
 
Ningependa kujua undugu/ukaribu wako na hiyo familia ulikuaje?

Ila ulitumia njia nzuri sana. Ila kuishi kwa watu mtihani aisee.
chanzo cha kukutana nao ilikuwa Huyo baba mwenye nyumba alikuja kufanya kazi sehemu nilipokuwa mm nafanya alipoiacha ndo akanikaribisha kwake maana mm muda huo nilikuwa naishi kwenye bot nililokuwa nafanyia kazi
 
Ndugu zangu humu hamjambo wote?

Humu ndani kuna wakati tunakuwa au tumewahi kuishi kwa watu au ndugu, lakini huwa baada ya kuishi kwa kipindi fulani mkiwa pamoja linakuja suala la kuchokana au kuchokwa. Hii inatokana na wewe kuhitaji msaada wao zaidi hasa wa hifadhi na chakula.

Sasa mimi nakumbuka nilipoacha kazi kwa Wahindi nikaenda kuishi kwenye familia moja huko Gongo la mboto, kutokana na maisha ya hiyo familia kuwa ni ya hali ya chini hivyo ilibidi nitumie akili sana ili wasinichoke.

Kwanza kabisa ilikuwa nikienda baharini kuvua samaki, nikirudi nabeba samaki kama wa 20,000 hivi maana nilikuwa nikienda Msasani au Feri nilikuwa namaliza hata mwezi ndio nashuka Gongo la mboto.

Baada ya kucha kazi ya uvuvi nikawa tu pale nyumbani, sasa ilikuwa maji ni ya shida kidogo ila uyapate ni umbali kama wa Km 1 hivi, kwahiyo nilihijitahidi sana maji yasiishe ndani, na kunawakati nikipiga saidia fundi narudi nyumbani na mazaga ya kula pale nyumbani. Kuna wakati nilimsaidia mama kufua, kufanya usafi wa ndani, kupika hasa ugali.

Nilifanya mambo mengi tu, ila zaidi ni baada pia ya kuonyeshwa upendo na ile familia.

Mpaka leo hii huwa wanatamani nirudi japo nilishajitegemea. Ila nikienda kuwasalimia mwendo ni ule ule, japo zingine mama ananiambia niache maana nimeshakuwa na familia na mimi.

Pia Mungu aibariki ile familia, nilijuana nao toka 2014 mpaka leo hii tumekuwa kama ndugu.
Bila kujali undugu au ukaribu na familia hiyo siri moja tu itakayowafanya wasikuchoke, piga kazi hasa zile wasizoziweza au zilizo ngumu zaidi. Ukimaliza kuwa mcheshi na kila mtu, leta kicheko kwenye familia. Usiingilie mambo ya familia mwenyeji, kaa kwa adabu ya hali ya juu. Siku ukiondoka watalia.
 
Watoto wa Ile nyumba walikua hawapendi kazi ngumu kama vile kupakua magunia ya mkaa .. kwani walikua wanauza mkaa jumla na reja reja
Pia walikua wanauza Mchele hvo magunia mazito Yale ya kilo 100+ niliyabeba mimi.
Kazi Yao kunitisha
Pia nilikua nikienda kanda ya ziwa nakuja na mazaga zaga yote ya Kanda ya ziwa.
Mpaka Leo huwa tunasaidiana sana .
 
Nyie vijana hivyo ndivyo inapaswa kuishi kwa ndug jamaa au rafiki... Ukijifanya unataka kuishi kama mtoto wa mwenye nyumba maisha yatakushinda ndani ya wiki moja... Maisha ya kuamka na kulala muda unaotaka au kutegea kazi za nyumban, hizi tabia fanya kwenu...
Ukisikia mtu anakuambia alivyokua anaishi kwa ndug au jamaa zake alikuwa ananyanyaswa na kuteswa, tambua alikuwa ni mpumbavu na mvivu asiye msaada...
 
hata mimi nilikuwa naishi kwa blaza wangu from another mother baada ya kumaliza.chuo .asubuhi nadamka
1. Nasafisha gari lake ndani njee.
2.namwagilia maua na usafi mdogomdogo pale home.
3.natumwa fulani.kununua mazagazaga
4. sebureni naenda kukaa nikiitwa tu.
5. nawapiga Twitt watoto wa brather .
6.watoto wakiumwa namsaidia shemeji kuwapeleka hospitali na shuleni.
7.chaa ajaabi lila.mwisho.wa.mwezi.bother alikuwa.ananikunjia.kitu.kama laki.tatu hivi kibindoni.ila.sharti.shemeji.asijue.chochote .kuhusu kunipa.hela nikaishi siku napata kazi niliondoka kwa.majomzi sanaa.licha.ya blaza KUNIPA.nyumba ya kwani.nilimgomea nikaenda.kuanza.maisha.ya.single.room uswahilini
 
Back
Top Bottom