Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 31,913
- 65,514
Na wewe ni muharibifu, mi nanyoa 200 tu. Yaani kiwembe 200 nampa jamaa aninyoeRoho imeniuma sana nimezoea kunyoa 2,500/-
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na wewe ni muharibifu, mi nanyoa 200 tu. Yaani kiwembe 200 nampa jamaa aninyoeRoho imeniuma sana nimezoea kunyoa 2,500/-
OKWI we ni noma nimecheka sanaWakati fulani mwaka juzi nikawa na safari ya kikazi Musoma. Sikuwahi kufika Musoma kabla kwa hiyo sikuwa mwenyeji wa maeneo nilitegemea boda.
Nikashuka stend nikamwambia boda nipeleke lodge nzuri nzuri. Baadae nikaona nisichemke ngoja nimshirikishe mwenyeji wangu. Mwenyeji wangu sikuwa nafahamiana naye wala kuonana. Kwa vile alijua ile kazi ni ya kibosi sana akaamini natakiwa kulala hotel yenye hadhi. Akamwelekeza boda pa kunipeleka.
Kufika daaah, nakuta hotel kali ghorofa kadhaa. Nje napokelewa na mabendera ya nchi mbalimbali.
Nikamwambia bodaboda mmenileta cha kike. Muhudumu mrembo kabisa akaja kunipokea nikiwa mchafu vumbi na kabegi mgongoni kama nimetoka kuchimba mitaro.
Nikamwambia boda usiondoke lolote linaweza kutokea. Tayari muhudumu akawa amenihukumu kwamba sina uwezo wa kulala pale. Akaniambia lakini kaka hapa chumba ni kuanzia elfu 50!
Nikamwambia mimi sijauliza bei nimeuliza chumba. Kufika reception kila mtu anaonyesha wasiwasi huyu mteja kapotea. Basi nikamwambia nataka chumba cha juu.
Akanijibu tuangalie tu vya chini kule juu ni kuanzia elfu 70. Nikaona aaaahhhh japo nilitaka chumba cha 20 ila hapa inabidi niweke heshima tu bila kujali chochote.
Nikachukue chumba cha 70. Nikarudi mapokezi kwenye watu wengi walionitilia mashaka. Nikaanza kulipa bills kwa sauti.
Nikawaambia sikilizeni, ninakaa siku 2 nitalipa 140,000 yote, halafu dada chukua buku 10, mlipe boda buku ya nauli na buku 4 ya kunisubiri. Halafu elfu 5 baki nayo umenipokea vizuri nimepenta, lakini mwambie boda naomba namba yake.
Ndugu msomaji yote hayo niliyafanya kulinda heshima dhidi ya wajinga wachache ambao walinihukumu kwa mwonekano.
Lakini pia kujitabiria mambo makubwa mbeleni kwamba ipo siku nitakaa meza moja na wakuu, nitakula na wakuu na nitalala lodge moja na wakuu.
Je, ulishawahi kufanya jeuri ya pesa hata kama huna kingi, ili kulinda heshima yako au kujitabiria ukuu?!!
Laki nne per night?Asallee miaka hyo ndo kwanzaa nmepata kazi ofisi ya wazungu inayosimamiwa na ngozi nyeusi kavu zaidi ya goti.
Kamshahara ka kienyeji lakini sishindwi kununua kadeti. Bwan bwana, nmeingia mkoa mapumziko mafupi ya kusalimia wazee, si nkapata pisi ya chuo. Manka flani rangi ya mtume kingledha kingi, punde si punde ni birthday yake. MSela wangu akaniambia haitakua poa usipotimba, bora twende tukatie baraka. Mwamba bila hiyana, gari la kuazima, nkatia na wese haooo na mwanangu kwenda kuchukua watoto twende tukaenjoy maskukuuu.
Picha linaanza nmefka hostel kwao najua wanatoka wawili (yaan pisi yangu na ya msela), ghafla zkatoka toto 6 jumla na zimetupia mapaja njenje kama matikiti kipindi cha msimu. Maini yakacheza tumboni, nkasema ya nini kuaibika wakat ndo kwaanza nasororea hata sijamkaza? Nkawaambia panda twende, pesa iko.
Kaa ukijua manka anaamini mimi n mfanyakazi Nairobi huko kwaio nko mboga hatari. In short shangwe lilikua jingi sana, hela natoa tu maana nshaubeba msalaba kama hamonenga. Mpka saa tisa kamili nshachoma kama laki 4 na nmeambulia mabusu mengi. Kuna mda nlishusha bucket za bia ile nataka kufungua naskia kijastibikozi mmoja anasema "subiri tupige snapu". Nkamwambia snapu ya nyoko? Bia nilipie na nizingoje? Mi nkaanza kugida. Nliona bora nifidie tu hela yangu.
Kumi na moja asubuh nkiwa nmechoka sana, nkamwambia, oi, chukua fego hapo maana nna umeme, yule manzi hakuona soo kuniambia, "si imebaki hyo kaki hapo mfukoni, leta tuichukulie fegi". Siku ikaisha nkarudi na stressi. Huo mwezi kazininwatu waliteseka sana maana ilikua kichaa kapewa rungu. All in all baadae nlikuja kukula sana ile pisi. Hela yangu nilifidia yoooote kwakweli.
Mwandiko si jeuri yangu! Wahed!
Maarufu kama "le grand"Inaitwa Gland Victoria mkuu. Ila kuna mkendo pia bei nafuu room kali tu
View attachment 2505336
Le grandMkendo lodge room ni elfu 30 alienda ile yenye swimming pool mtaa WA chini jina limenitoka kidogo!
Hiki ndio kinanifanya nikienda mgahawa wa watu lazima niulize bei kabla ya kuagiza.Niwe na pesa au nisiwe nazo, uhuru wangu na kujitambua mwenyewe nataka nini ni muhimu kuliko kujali nitaonekanaje na walimwengu wanataka nini.
Kama heshima yako inalindwa na pesa, huna heshima, hiyo ni gharama tu.
Nina tabia ya kutoa pesa kumaliza shida, si kutafuta heshima.
Pia, hata kama unajali walimwengu wanakuonaje, unaweza kufikiri unaweka heshima kwa kutumia pesa kubwa, halafu watu wakakudharau kwa kukuona mjinga huna pesa halafu unajitutumua kujionesha unazo.
Unanunua dharau kwa bei kubwa.
Gily umetisha sanaYule demu aliponipa mzigo tako tatu wadhungu hao. Nikasingizia sijala ngoja nile nimpe show za WWE John cena you can't see mee. Nikala chips ndizi mishikaki. Nikampq romance kupima oil naona huyu kashaiva nikachomeka kupiga take tatu wajapan hao. Nikaona sasa hapa mbona kazi sana. Nikaona ngoja nizuge zuge kuangalia vipindi vya wanyama kwenye TV. .
Alipoamka nikaona nitumie nafasi hii kumuonyesha show ya kibabe. Kupiga tako nyingine tani aisee wazee hawajakosea siku ya kufa nyani kweli miti yote huteleza. Kupiga tako nikajikaza yani kufika tako ya tano tu tena nimejikaza nikawa na uma na meno wahindi haoo. Aisee what an embarrassing day.
Kurudi kwenye mada, ili kurudisha heshima nikamuliza demu hivi unaishi wapi? Akajibu magomeni nimepanga chumba elfu 70. Nikaanza kujiongelesha hapa inabidi upange sinza chumba laki na hamsini. Nataka nikukipie kodi ya miezi kumi. Kwanza kabla sijasahau shika hii laki. Ukifika nyumbani nakutumia hela nyingine ununue vitu vya nyumbani hiyo laki ni nauli tu. Hata samsung unayotumia sio simu ya maana nakununulia iphone.
Alipoondoka na laki yangu nikatupa line nikasajili line nyingine kwa mpita njia. Huyu dada tulikutana kwenye mwendokasi. Hata mwendokasi sipandi tena nawasiwasi naweza kukutana nae huko 😬😬😬
😅😅😅😅Mimi na mshikaji wangu tulikuwa na tabia ya kuopoa totoz za chuo kila weekend tunaenda kula bata.
Siku moja tupo kiwanja, wakajipendekeza marafiki wa mademu zetu na wao walikuwa kiwanja hicho, na walikuwa pisi kali kwelikweli, tukaona ngoja tuweke heshima ili na wao tuwaburuze kimasihara...
Tulitumia sana.. tukachukua usafiri kuwarudisha, muda wa kulipa nauli ndio mshikaji wangu alipoharibu hali ya hewa..
Alijisachi akapata mshituko akasema kwa nguvu MUNGU wangu nimekula hela ya kodi sijui nitamueleza nini yule mzee, wale mademu wakabaki wanashangaa.
Heshima ikawa fedheha
Ila mademu nao bwana. Acha tu waendelee kuwa single mothers.yaani anafanya birthday party ana kodi na Ukumbi huku akijua hana uwezo?subiri kidogo
Nakumbuka kuna mchizi wangu aliambia kuna demu kamtongoza halafu siku hiyo amempa mwaliko wa Birthday party viwanja flani town so mchizi wangu aliomba scot yangu.
kilichotokea niliondoka na huyo demu wake baada birthday kuisha na urafiki ukaisha hadi leo
ilikuwa hivi baada ya kufika pale mimi nilikuwa pembeni pembeni tu kwasababu sina ninaemjua ukiacha nilivyotambulishwa kwa shem mwenye party yake tu basi so, mchizi wangu akawa yupo bize na demu wake tu
Ghafla kukawa kuna vikao vya dharula huku sura za waalikwa Azi-relate na tukio husika kumbe bwana yule demu mwenye ile party kuna rafiki yake alimpa pesa kwa ajili ya lile eneo la shughuli kakimbia na hela na party imeanza mwenye ukumbi anasema siwajuhi ondokeni kabla sijaita polisi😅😅😅😅 wapuuzi wakumbwa
ghafla tukajikuta tupo watatu mimi na jamaa wangu na shem sasa ikapelekea niulize swali maana yule jamaa wangu ni ROFAA tu watu wa vijiweni vijiweni wale ... NI KIASI GANI CHA PESA YA UKUMBI KINAHITAJIKA HAPA ? shemu akajibu ni laki na 80 tu na hapa mimi nina elfu 50 tu.
Mwanaume nikaona mbona ni hela chumvi tu nikamwabia JAMES [ mwanangu ] mimi nalipia unasemaje ? daah mwanangu we lipia tutajua cha kufanya. nikatoa wallet nikatoa mia hamsini cash nikampa james huku demu Anaona Si-unajua sisi watoto wa mjini atutembei kama MAITI.... kimoyomoyo hapo nasema..🥴🥶🥶
itaendelea
kiukweli yule demu alikuwa ni mtamu sana sijapata kuona alikuwa analia vilio vyote halafu ni mdogo mdogo nilijilia vyangu usiku ule siwezi kusahau
Mwangu ulipata mke Daktari moja kwa moja? Ningekushangaa kama usingemuoa.Mimi ilikuwa sio kuleta heshima ila ilikuwa sifa.iko hivi nilienda dodoma kwenye harusi ya sista nilikaa meza moja na pisi kali 2 ukafika muda wa kuchangia bibi harusi kulikuwa na phase mbili,phase ya kwanza ilikuwa kikapu kinapita kwenye kila meza yoyote anaweka alichonacho'muda ule nilikuwa nipo tungi balaa kutaka kuonyesha sifa mfukoni nilikuwa na laki 8 nikawa naweka narusha rusha elfu 10 kwenye kapu mpaka laki 8 yote ikaisha.
Baadae wale wadada wakaniambia weee kaka pesa zote umetoa wapi mbona umechangia hela nyingi hivyo!! Nikawaambia kawaida kisha nikawapotezea.
Ikaja phase 2 kwenda kumtunza bibi harusi pale mbele ili kuonesha sifa nikaenda ATM nikatoa mil 1.5 pisi kali moja ikanishauri sana nisiende kuchangia tena pesa nilizotoa awali zinatosha.
Baada ya harusi kuisha asubuhi nikajikuta nipo room yenye muonekano kama hostel kumbe yule sista nilivyozima alinikokota mpaka chuoni kwao alikuwa ni mwanafunzi wa udaktari md5 akanikabidhi pesa yangu 1.5mil alizitunza coz nilikuwa tungi sana..kifupi huyo dada ndio mke wangu hivi sasa..sifa zilinisaidia kupata mke bora aliyekuwa yupo sealed
🤣🤣🤣🤣🤣Kama huna , huna tu .Mkuu nilikuwa nalipwa laki 2 kwa siku. Hapo nina posho ya wiki 2. Sema nilitia ubahili kufanya saving
Fanya kazi upate maendeleo acha kupoteza muda kwa wanawake.yaani kuna pisi kila nkikutana nayo nahisi nna bahati mbaya, huwa tunakutana nikiwa naendesha pikipiki (hii ni kitokana na nature ya kazi yangu)
sasa ubaya anaringa ananiona kama sio hadhi yake na kuniona kama bodaboda
huu uzi ntakuja kuureply kwa hasira pale ntakapomaliza hasira zangu zote siku atakayojichanganya kunijua.
ChaiYaani watu wanajua ku underate watu. Kuna siku nilienda kwenye duka moja kubwa wnauza kila aina ya bithaa. Nilienda bila gari, daladala zinashusha hapo mbele ya hiyo supermaket. Wale wa dada waliniona wakati na shuka. Wakanipigia hesabu labda nimekuja kutembea mule. Kufika wakaja vijana ambao niliongea nao kabla, wakanipandisha kwenye furniture na vifaa vya umeme. Nilinunua bidhaa za 15m, kutoka pale wale wadada wanashangaa. Sasa hivi nikienda wananichangamkia balaa. Wa bongo shida sana.
Ukifatilia huu uzi mwanzo mwisho unaweza kusema vijana wa Tanzania wana kipato kizuri sana ila shida ni mbususu zinawalia pesa sana.Umenikumbusha leo wife amenipa stori ya kijijini kwao kuna ndugu anaumwa kalazwa hospitali. Anko wake akatumwa akauze ng'ombe hela ya matibabu ipatikane. Kauza laki 5 halafu akazima simu siku 3. Wakamsaka wanakuja kumkuta na laki 1 tu nne zote kapiga pombe na kuhonga
ChaiTumeumbwa tofauti..
Mie napenda Kujishusha, low key..
Dharau nazipenda sana.. Yaan mtu kunionesha dharau (Akifikiri sina uwezo flani ila kiuhalisia ninao huo uwezo 10x times) najiskia raha sana. Sijui nikoje
Chai kwa nini? Yaani unaona kutoa mil 15 ni chai? Kwani haiwezekani? Ndio nyienyie tunawasema kudharau watuChai
Ukute ana gorofa sasaKuna jamaa anakujaga na baiskeli ofisini kila mtu huwa anamshangaa. Kuna siku bosi akamdis kama utani..Ifike wakati vijana wangu muwe na magari ya kuanzia 15m na mwenye baiskeli ajiangalie....
Sasa hapo mjanja nani, mjinga nani?Hii bwana ni Kwa hisani ya wife.
Wife hakupenda dharau toka Kwa mdada mwenzake,ilikuwa 2017 nilikuwa nimepanga kwenda shopping na wife akasema ananisindikiza na kuhakikisha napata viwalo freshi,na kama nilijua nilimpa hela akae nazo yeye Mimi kazi yangu ni kujaribu na kuchukua,ilikuwa bajeti kama 300,000.
Sasa wakati tunatoka Duka moja na kuingia lingine,yeye akawahi kutangulia Duka lingine kabla yangu,sasa kwakuwa alikuwa amevaa hijabu basi Yule sista duu WA shop akamchukulia poa kumbe hajui wife alikuwa duu hasa enzi zake Ila nilimbadilisha na kuwa mwanamke anayejistiri.
Wife akaniambia kuna mdada anamchukulia poa ngoja amuonyeshe Ila binafsi sikubariki wazo la wife lkn nikasema ngoja niwazoom nione itakuwaje,pale pamba ilikuwa bei kuanzia 15,000 mpaka 20,000.
Nikachagua kama pamba 4 ambazo nilizipenda wife akasema ongeza moja tulipe 100,000 chap basi kwakuwa nilijua wife anataka point tatu muhimu nikaona nisimwangushe,kweli ikapatikana ya tano wife akatoa 100,000 chap,mpaka hapo wife aliondoa dharau za Yule sista duu
Ni hayo Tu!