Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Yeah hili liko wazi. Mtoto atanyanyasika tu akikaa mahali ambako mwanamke sio ndugu yake. Hawezi kuwa huru lazma atasumbuliwa kihisia tu. Wanawake wengi wana roho za kishetani sana wakikaa na ndugu za waume zao. Tena hasa huyo ndugu awe na uchumi mzuri balaa huwa zito. Kwa niliyopitia staki kuja kuona mtoto wangu anakaa mahali ambapo sio kwao.

Bora tushindie mikate na chai ila sio kumpeleka kwa baba wadogo au baba wakubwa wake. Yani hata nikifa bora akae na shangazi yake tu. [emoji1787]
Mme wa shangazi naye vipi akisema mnaniletea mizigo! Labda sio wajita ninao wajua mimi walivyo wabinafsi atamfukuza mchana kweupe
 
Kwenye shida ndugu zako Mara nyingi hukupenda na kukuomba msaada Tena watakuona Kama mfalme au malkia wao. [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Siku ukiishiwa au kupata shida unabaki na mkeo uliyekuwa unampuuza na kuwaona ndugu ndiyo namba moja mke namba 3.
 
Sijawahi ishi kwa mtu toka nimezaliwa. Ila tumeishi na ndugu wa Baba, Mama na Jamaa.

Nilochojifunza

Kila mtu aishi kwao
Kuna makabila wanapenda kusukumia watu watoto wao sijui wapoje, bora mtu aliyekuwa anakuja kutafuta maisha si kupeleka mtota akasomee hapo afadhali ukae na wanao usaidiwe kama ni ada basi.
 
Kuna makabila wanapenda kusukumia watu watoto wao sijui wapoje, bora mtu aliyekuwa anakuja kutafuta maisha si kupeleka mtota akasomee hapo afadhali ukae na wanao usaidiwe kama ni ada basi.
Kila mtu na aishi kwao.
Watu hawana shukurani, ataishi nawe akiondoka ataenda sema alikuwa anateswa
 
Habari za muda huu, ni siku tulivu sana hapa. Jiji la Dar es Salaam kumekucha salama, ingawa kulikuwa na upepo wa baridi sana, poleni na natumaini kila mmoja wetu ni mzima kabisa. Nawatakia kila la kheri katika pilika za kuijenga Tanzania kuwa kubwa tena, yenye amani na upendo. Twende kwenye mada.

Kuna kipindi kwenye Life cycle ya kimaisha ilinifanya nihamie kwa uncle wangu kuishi nae ili kuangalia uwezekano wa kufanya maisha. Enzi zile ndio nimemaliza masomo nipo home tu nikapata mchong huo, nilikuwa very excited sana na hili, maana nilikuwa ninavuta picha fulani hivi kabla ya kufika kwa uncle Dar.

Siku mbili baada ya kupewa taarifa ya safari nilijiandaa lakini ilikuwa ghafla sana kutokana na uchu wa safari ya kuja huku hata watu niliokuwa nawadai pesa zangu wengi niliwapotezea, kitu ninachojutia sana.

Siku ya safari ikawadia, panda nikapanda basi safari mpaka Dar, nifika mida ya saa moja hivi enzi za ubungo terminal pale, akaja mshakaji aliyekuwa anakaa kwa huyo uncle, wakanichukua freshi mpaka home.

Hapo nipo so excited na wishes nying sana how it's going to be in the up coming day's, nikachil, nikafika home. Yale mapokezi tuu yakanidropisha point. Yule mke wake alikuwa anagubu sana, nilivyofika nikaona hapa chakike.

Picha linaanza kulipokucha tunaamshwa saa kumi na moja tufanye usafi, duuhh nilichoka. Kumbe wanafuga mbwa, sehemu padogo mbwa wanajisaidia, morning ni kuzoa na kusafisha kumwaga maji, nilichoka. Ila nikajikaza kumbe bado kuna kuosha magari usiku unaamshwa uoshe, kibaya zaidi ni kila siku iwe mvua au jua.

Kibaya zaidi ni huyo mke wake alikuwa na visa na maneno ya shombo, mara hataki watu watoke nje ya geti anafunga, mara hataki watu wakae sebuleni, hata kunywa maji ya kwenye friji jau, akinunua matunda mpaka akupe yeye na atakupa wakati linaanza kuharibika ukila atakuja kuongea mpaka ujute.

Kwa kipindi kile ilikuwa ni mateso sana, sabuni ya kuogea unajinunilia, mafuta ya kujipaka pia, tulikuwa tunajitegemea kama tumepanga hata kipindi tunaenda K/Koo ilikuwa ni taabu sana.

Ilinipasa kuishi kama mtoto wa miaka kumi kushuka chini, maana ni kama sikuwa najielewa. Maana watu walikuwa wanakuja pale wanashangaa tunawezaje kuishi na hawa, hata wadogo zake na yule mama walishindwa kukaa nae, wengine walikimbia na kutoroka. Ila ndo changamoto tunazokutana nazo katika maisha ya wengi wetu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sitoleta mikasa hapa maana ni mingi mnooo
Ila nashauri kitu kimoja NDUGU TUWASAIDIE PALE TUNAPOWEZA NA MISAADA IWAFIKIE KULEKULE WALIKO!
Sio uwalete kwako, hapanaaaa
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] hawa ndio wale wenzangu na mimi mafridge wameyakuta ukubwani kwa hiyo mle ndani ya fridge anapaona kama peponi hivi
Tulikuwa tuna fungiwa fridge na funguo! Tv mnatizamia dirishani enzi za mchezo wa Tausi loh Mama alikuwa mchoyo yule j2 Ndiyo mtakula milo 3 akiwepo Mshua na ni Dr nawaza hao wagonjwa huko mhhh ila aliachika[emoji3]
 
Nilifika kwa ndugu yangu na katika kukaa pale ikatokea Hela shilingi Elfu 20 imepotea.

Mama mwenye nyumba akaanza maneno, Tabia hii ya Wizi haikuwepo kabisa hapa nyumbani sijui nani ameiletea [emoji848][emoji849]

Na ndio nilikuwa na siku moja tu, tangu kufika hapo.
 
Bora nyie mlinyanyaswa na mashemeji zenu...
Miaka fulani ya nyuma nilimtembelea ndugu yangu maana alikuwa analalamika sifiki kwake.

Nikapewa chumba nyumba ndogo ya nje ambayo alikuwa anakaa bro na mke wake ila chumb changu kinajitegemea tofauti kabisa na jamaa, hata choo nilikuwa namtumia cha nje ila jamaa kwake ilikuwa ni master bedroom.

Sasa huo usiku mkojo umenibana, ile natok nje tu nakutana na 2 grown Dobermanns with cropped ears na mwingine hadi mkia amekatwa[emoji15][emoji15]. I was like hee kumbe humu ndani kuna mbwa tena wakubwa hivi na hawaniambii hawa si wauwaji kabisa kwa kweli sikupenda[emoji1787][emoji1787]. Ikabidi nirud geto, nikampigia simu bro akaja akawashika mbwa nikaenda msalani.

Ilikuwa kero maana karibia kila siku nampigia jamaa anisindikize chooni kama mtoto mpaka jau, jamaa akanipanga hawana shida hao wakishakuzoea. Kesho yake nikawa nipo nao karibu tunacheza nao mixa wanapewa maelekezo wanizoee, yule mmoja alinirukia yani over nilitupiwa kakiroba cha kilo 50!! Nilipata ka upenyo nilijikuta nasepa ka upepo, yule mbwa anakuja nyuma ananikimbiza, anadhani tunacheza kumbe mwenzie ndio nasevu hivo[emoji1787][emoji1787]. Ilifika wakati ikifika kuanzia saa 9 au kumi sinywi maji mpaka kesho yake!

Sasa huo usiku nataka kwenda chooni kama kawaida, ile nafungua mlango tu yakanyanyuka masikio yamewasimama kama antenna yani kama washajiandaa kwa kitu fulani so alerted, nikasema hapana nikarud ndani pigia sana bro simu haipatikani. Mkojo unazidi kubana na ndani hakuna hata chupa. Nikachungulia tena nikawaona wako mbali kidogo nikachomoka kama mkuki mpaka chooni, yalikuja kwa kasi yakaanza kuparua mlango. Wakat nataka nirudi nkayaona yamesimama kwa mbali kidogo yapo serious sio mchezo, nikayachekiii nikaanza kuambaa ambaa na fence kuutafuta mlango wa geto, nayo yakaanza ku move kunifata. Nikajisemea hapana hii sio ishara nzuri nikarudi mbio mpaka chooni, majamaa yakaja speed mpaka pale mlangoni yanaunguruma mixa kuparua mlango.Nilienda na simu chooni, piga sana simu ya jamaa haipatikani nikajisemea leo nimeisha[emoji16]. Nikavuta ndoo ya chooni nikakaa kuanzia saa 9 hivi kuelekea 10mpaka 12 hadi nikapitiwa na usingizi na ile baridi sio poa. Nashukuru Mungu choo kilikuwa kisafi.

.......hapo sijaelezea tukio lengine la kukimbizwa na hao mbwa kidogo ning'atwe hawakuwa wamefungwa vizuri plus kukojoa mlangoni.....

Asubuhi baada ya kuyafungia namimi ndio nikajifanya natoka chooni, yule mzee akaniuliza umeingia chooni saa ngap sijakuona?! I was pissed off sikutaka hata kumwambia yaliyonikuta maana mjadala ungekuwa mrefu na sikuwa n huo mda wa kuanza kuoneana huruma, kwanza nausingiz/kichwa kinauma na hapo nafikiria kama naweza pata bus la saa mbili au la[emoji1787]. Jioni yake nikaaga kesho narud kwetu, mzee akamaind sana akapiga simu nyumbani sikubadili maamuzi. Kesho yake asubuhi nikasepa!

Zile siku chache nilizokaa pale ndani zilikuwa ni mateso, wale mbwa walinikosesha raha kabisa hasa usiku. Maana mda wote ilibidi niangalie huku na huku nijue wako wapi kabla sijafanya movement kama vile navuka barabara maana wana eneo kubwa. Na hadi leo sijawahi kwenda tena!
Japo niliwapendea ile tough and aggressive looking yao lakini haiondoi ukweli kwamba mimi na mbwa bado haziivi kivileee.

View attachment 2693982
Hahahhahah mbwa hawanaga mazoea,wangekupalura
 
Habari za muda huu, ni siku tulivu sana hapa. Jiji la Dar es Salaam kumekucha salama, ingawa kulikuwa na upepo wa baridi sana, poleni na natumaini kila mmoja wetu ni mzima kabisa. Nawatakia kila la kheri katika pilika za kuijenga Tanzania kuwa kubwa tena, yenye amani na upendo. Twende kwenye mada.

Kuna kipindi kwenye Life cycle ya kimaisha ilinifanya nihamie kwa uncle wangu kuishi nae ili kuangalia uwezekano wa kufanya maisha. Enzi zile ndio nimemaliza masomo nipo home tu nikapata mchong huo, nilikuwa very excited sana na hili, maana nilikuwa ninavuta picha fulani hivi kabla ya kufika kwa uncle Dar.

Siku mbili baada ya kupewa taarifa ya safari nilijiandaa lakini ilikuwa ghafla sana kutokana na uchu wa safari ya kuja huku hata watu niliokuwa nawadai pesa zangu wengi niliwapotezea, kitu ninachojutia sana.

Siku ya safari ikawadia, panda nikapanda basi safari mpaka Dar, nifika mida ya saa moja hivi enzi za ubungo terminal pale, akaja mshakaji aliyekuwa anakaa kwa huyo uncle, wakanichukua freshi mpaka home.

Hapo nipo so excited na wishes nying sana how it's going to be in the up coming day's, nikachil, nikafika home. Yale mapokezi tuu yakanidropisha point. Yule mke wake alikuwa anagubu sana, nilivyofika nikaona hapa chakike.

Picha linaanza kulipokucha tunaamshwa saa kumi na moja tufanye usafi, duuhh nilichoka. Kumbe wanafuga mbwa, sehemu padogo mbwa wanajisaidia, morning ni kuzoa na kusafisha kumwaga maji, nilichoka. Ila nikajikaza kumbe bado kuna kuosha magari usiku unaamshwa uoshe, kibaya zaidi ni kila siku iwe mvua au jua.

Kibaya zaidi ni huyo mke wake alikuwa na visa na maneno ya shombo, mara hataki watu watoke nje ya geti anafunga, mara hataki watu wakae sebuleni, hata kunywa maji ya kwenye friji jau, akinunua matunda mpaka akupe yeye na atakupa wakati linaanza kuharibika ukila atakuja kuongea mpaka ujute.

Kwa kipindi kile ilikuwa ni mateso sana, sabuni ya kuogea unajinunilia, mafuta ya kujipaka pia, tulikuwa tunajitegemea kama tumepanga hata kipindi tunaenda K/Koo ilikuwa ni taabu sana.

Ilinipasa kuishi kama mtoto wa miaka kumi kushuka chini, maana ni kama sikuwa najielewa. Maana watu walikuwa wanakuja pale wanashangaa tunawezaje kuishi na hawa, hata wadogo zake na yule mama walishindwa kukaa nae, wengine walikimbia na kutoroka. Ila ndo changamoto tunazokutana nazo katika maisha ya wengi wetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Siyo tu kuishi kwa ndugu, hata kusafiri na kufikia kwa ndugu, jamaa ama rafiki ni shughuli pevu.

Kama huna sababu kuishi/kufikia kwa ndugu ama jamaa EPUKA KABISA!
 
Back
Top Bottom