Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Uliwahi kupata mikasa gani kwa kuishi kwa ndugu?

Siku nshaondoka naanza life nikatoka kizungu kwa binamu.
Oven taka zote nnazo.
Dah siku wamekuja kusalimia kuna binti kalala mle ndani ana mimba.
Ikawa anhaa weh hivi tumekupa umeleta jeuri umekuja ukaoa.
Wakabeba tena vyoote[emoji1787][emoji1787][emoji1787].
Wakatimua navyo.
Demu nae anasema kumbe vitu sio vyako?
Katimua,
Nikaona afadhali sasa niko huru[emoji119]
Na mimba kampelekea nani zawadi?

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Kwakuwa ni kwa ndugu yako ulitaka uwe unajifungulia tu friji unakula unachotaka sio?

Hutaki kuzoa mavi ya mbwa unataka azoe Nani?
Vijana wanataka waishi kifalme waamke saa 4 Asubuhi wakute chai mezani wanywe kisha house girl atoe vyombo, wakishamaliza kunywa chai warudi chumbani kuchati wakisubiri chakula cha mchana waje waitwe na dada wa kazi.
 
Mwaka 2008 kuna jamaa kama watano walikuja dar kumtembelea jamaa yao. Wawili kati yao walikuja na wake zao na mmoja alikuwa na mtoto mchanga. Jamaa aliwaribisha vizuri ila wakati wa msosi akaenda nao kwenye mgahawa wale yeye akaagiza wali magarage wageni wakaagiza wali kuku ugali mbuzi nk ilipokuja bili akalipa sh mia nane tu ya wali alio kula wageni libidi walipie walichokula baada ya hapo wakarudi tena kwa jamaa na jamaa akawa anawapigisha tu story za kuwauliza mambo ya kijijini etc ilipo fika usiku akawapeleka gesti ya bei nafuu na kuwaambia watalipia hela asubuhi.. kesho jamaa waliondoka bila kuaga. Jamaa alikuwa kauzu zaidi ya dagaa
Watu 5 kwa pamoja? Ulikuwa ugeni mzito huo, ila jamaa yako naye kauzu kweli kweli ha ha ha ha.

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Mwaka 2008 kuna jamaa kama watano walikuja dar kumtembelea jamaa yao. Wawili kati yao walikuja na wake zao na mmoja alikuwa na mtoto mchanga. Jamaa aliwaribisha vizuri ila wakati wa msosi akaenda nao kwenye mgahawa wale yeye akaagiza wali magarage wageni wakaagiza wali kuku ugali mbuzi nk ilipokuja bili akalipa sh mia nane tu ya wali alio kula wageni libidi walipie walichokula baada ya hapo wakarudi tena kwa jamaa na jamaa akawa anawapigisha tu story za kuwauliza mambo ya kijijini etc ilipo fika usiku akawapeleka gesti ya bei nafuu na kuwaambia watalipia hela asubuhi.. kesho jamaa waliondoka bila kuaga. Jamaa alikuwa kauzu zaidi ya dagaa

Kuna yule jamaa alisimuliaga kuwa baba yake aliwapeleka wageni kulala wodi ya hospital [emoji23][emoji23][emoji23][emoji13]
 
Duh ila ndugu wa mume jamani kuishi nao yataka moyo.nimekuja kugundua kwanini watu wengi wanaishi na ndugu zao kuliko ndugu wa mume.nikiishi na mdogo wangu namtuma nitakavyo hata nguo zangu nampa anifulie hutomsikia kunung'unika, ndugu wa mume mtume hata mara moja ukoo wao mzima watajua . Nako hapa naishi na wifi yangu kaachika kwa mume wake yaani ni kero jamani nyumba imekuwa kama na wanawake wawili mimi napanga kipikwe hiki yeye anapika kile mavyakula anapika mengi anaishia kumwaga yaani ilimradi fujo.hapa napanga na mimi niondoke niende kuishi kwa kakaangu
I bet kuna mambo hamuendi sawa!

Wewe ni mke sawa hata yeye ni ndugu wa mumeo na ana haki kwa ndugu yake vilevile ila tu mipaka isivuke!

Swala la chakula ifike muda liwe kawaida tu kwenu wanawake... hiyo ni rizq tu, mwisho wake ni kwenda chooni na kupata nguvu maisha yaendelee. Msichukiane au kuchukia watoto wa wenzenu kisa chakula.

Wanawake hamkaagi pamoja mkapendana na kuelewana. Binafsi najua umeanza kufikiria kama kaja hapo kukutawala au kukunyima raha HAPANA!
 
My story, mazingira ni kijijini.

Nilihamia kwa uncle nikiwa 9yrs old baada ya home kutokuwa hapasomeki kutokana na uhohehahe wa home. Ilikuwa rahisi kwenda kwa uncle sababu nilikuwa naishi huko kwa bibi(kabla hajafariki, baada ya kufariki nilipelekwa nyumbani) ambapo mji ulikuwa mmoja kama tunavyojua vijijini kaya huwa zipo pamoja kwa asilimia kubwa.

Lengo la kwenda uncle ilikuwa ni kupata unafuu wa maisha, bila hiyana nilipokelewa vizuri ila nilipoulizwa jinsi nilivyoondoka home nilidanganya kuwa nimeondoka kwa ruhusa ila home nilitoroka, kule kwa uncle nilisema nimekuja nitakuwa nawasaidia kuchunga ng'ombe. Bila hiyana wakakubali maana walikuwa wananifahamu tangu nikiwa naishi kipindi bibi yupo hai. Wao pia walikuwa wanajua hali halisi ya nyumbani kwetu

Nature ya uncle na mkewe ni uonevu, kunyanyasa mtu yeyote asiyekuwa mtoto wao wa rika lolote anayeishi hapo, tabia hiyo inajulikana na watu wote mtaani.

Maisha yakaanza bana, kwa kuwa nilisingizia nimekuja kuwasaidia kuchunga nikaianza hiyo kazi. Nikawa napigishwa kazi nyingi sana hapo nyumbani mbali na kuchunga, nikawa kila kazi ikitokea nalazima niitwe nikaifanye hata kama ni kazi ndogo ambayo watoto wao wanaweza kuifanya, kama sipo(nimeenda kucheza kwa majirani lazima nitafutwe niinde nikaifanye, ilifikia kipindi nikawa natoka bila wao kujua ili nikacheze kwa majirani kukwepa kazi ndogo ndogo ila na wao wakawa wananiambia nisitoke maana nilikuwa natoka baada ya lunch, kumbuka hapo nikiwa sijaenda kuchunga).

Nikawa natumwa kwenda kusaga unga mashineni ila mzigo ninaoupewa ni mkubwa hadi nasota, nikiwa najikongoja nao kichwani nakutana na watu hadi wanashangaa na kusema mama fulani hafanyi vizuri anampa mtoto mzigo mkubwa, endapo ikitokea anaandaa mzigo halafu majirani wakawa pale kwenye kupiga story na akaambiwa mbona unamfungia mzigo mkubwa sana anasema sio mkubwa na huyu ni mtoto mkubwa. Watu wanabaki kumuangalia tu.

Mwaka mmoja baadae nikiwa pale nikafundishwa kuendesha baiskeli, hapa palikuwa nafuu nikawa napiga kazi nyingi kwa baiskeli. Kusaga ikawa jambo nafuu, kuchota maji ikawa kazi yangu(watoto wao wanafanya kwa hiari, jla mimi ni shurti na siwezi kukataa)

Baada ya wao kuona napiga kazi vizuri wakaamua kunipeleka/kuniandikisha shule nikiwa umri ushaenda (10yrs) ingawa kwa kijijini ilikuwa kawaida. Mimi pia nilikuwa nataka shule nikafurahi bila hiyana, kwa umri huo tulikuwa wanafunzi wengi tukaenda kuanzishwa darasa la pili. Hapa kwenye kunipeleka shule walicheza kama The late Pele maana kwa miaka kadhaa hadi nimalize la saba lazima wanifaidi katika kazi, na kweli walinifaidi maana nilikuwa mtiifu sana.

Kuhusu sare za shule na daftari nilikuwa najinunulia mwenyewe kupitia kufanga vibarua vya kulima hasa msimu wa kulima, mara nyingine wao wananipa kibarua kwenye shamba lao napiga kazi wananipa hela naenda kununulia daftari, nikiwa shule endapo daftari ikiisha labda ya somo la hisabati nikiomba hela nitaambiwa kachanganye kuandika, yaani nikaandikie kwenye daftari ama la kiswahili au sayansi. Kwa hali hii nikawa nikipata hela naitunza ili ije inisaidie kununua daftari. Wakati mimi napambana na hali hii ila watoto wao hela zao wakipata kwenye vibarua wanaenda kununulia soda, biskuti, pipi hadi zinaisha maana madaftari yakiisha tu wananunuliwa mengine.

Kwenye msosi ikawa ni mwendo wa kupunjwa kama ni maziwa mimi nitaambulia nusu kikombe wengine wanapata kikombe full halafu mimi ndio kinara wa kwenda kuchunga, watoto wao wanaona hiyo hali ila hawasemi, mara nyingine uncle anajishtukia ananiongezea kutoka kwenye maziwa yake na endapo mkewe akiwa karibu na akiona anachukia kiaina. kitendo cha kupunjwa kila mtu aliyewahi kuishi pale asiye mtoto wao alikipitia. Pia unaweza kupewa mboga zilizoisha muda wa matumizi yaani mboga ya juzi unaweza kuipewa leo uitumie na usiweze kusema kitu, unaishia kugusa na kula tonge kavu kavu.

Ikiwa sijaenda kuchunga halafu ni weekend huwa tunafua nguo za shule, mimi nitaambiwa fua nguo zote hadi za wanawe hata kama wapo na hawana kazi maana suala la kufua wanamuachia mama yao na yeye ananipa huo msala. mara nyingine nilikuwa napewa nguo za mume wake naambiwa zifue, kama hamna maji hapo nyumbani naambiwa nenda kafulie mtoni.

Wakati wa kulima mimi nitaaamshwa alfajiri saa kumi na moja ila watoto wao wanaamka muda wowote wakipenda na mara nyingine wakisema hawaendi kulima waachwa, mimi siwezi kufanya hivyo maana mziki wake si wa kitoto nitakaoupata kuanzia kuchezea stick hadi kunyimwa msosi(binafsi sikufikia level ya kunyimwa msosi ila wapo waliowahi kunyimwa), stick ndio nimezichezea sana pamoja na kutukanwa kwa kosa dogo tu.

Life langu la primary likawa hivyo hadi nikamaliza la saba na sasa nishasahau hizo tabu zote na kupitia wao ndio inekuwa chachu ya kubadili maisha ya kwetu niliyoyakimbia enzi hizo ingali ni mdogo na endapo nisingekimbia sijui kama ningekuwa hapa nilipo sasa, hata kama ningekuwa hapa sasa labda sijui ningepitia njia gani maana mlango wa kutokea ulikuwa mgumu sana.

Jambo zuri walilokuwa nao hawa walezi walikuwa na exposure ya elimu japo kunipigisha kwata za kazi ila walikuwa wanafurahia maendeleo yangu mazuri kwenye masomo na walikuwa wanajidai mtaani kuhusu hasa wakiwa wanaambiwa sifa zangu na juhudi shuleni.

Nawapa MAUA yao hawa walezi walinitoa jalalani kama yule Prof wa awamu iliyopita.
 
Wanawake waone hivi ni watu wabaya sana that's why hata wao hawapendani,ukimkuta ametokea maisha ya shida akaja kukutana mwanaume mwenye nazo ,ubinafsi ,roho mbaya,chuki hata visa utaona, matatzo mengi source ni women

Sent from my Infinix X624 using JamiiForums mobile app
Wifi yangu mmoja aliolewa tokea maisha ya shida, alivyofika ndani yaani mbona tulijuta. Chakula kinapikwa kinawekwa chumbani. Enzi hizo nasoma, ikafika time mi nikazira msosi wa home. Siku ya siku ndio braza anashtuka eti we huwa unakula wapi maana ht nilikuwa nikiwakuta wanakula mi sijali wala nn. Nilimwambia braza muulize mkeo. Mungu si Juma wala Abdalah ubaya wa wifi ulifika mpk lwa mama mkwe na mashemeji, kiliwaka sana mpk akaachika na sasa karudi kule kule kwenye maisha yake ya taabu.
 
I bet kuna mambo hamuendi sawa!

Wewe ni mke sawa hata yeye ni ndugu wa mumeo na ana haki kwa ndugu yake vilevile ila tu mipaka isivuke!

Swala la chakula ifike muda liwe kawaida tu kwenu wanawake... hiyo ni rizq tu, mwisho wake ni kwenda chooni na kupata nguvu maisha yaendelee. Msichukiane au kuchukia watoto wa wenzenu kisa chakula.

Wanawake hamkaagi pamoja mkapendana na kuelewana. Binafsi najua umeanza kufikiria kama kaja hapo kukutawala au kukunyima raha HAPANA!
Sijui kama umenielewa, huyu wifi yangu katoka kwa mume wake kaja hapa kwa kaka yake kuishi.ishu inayokuja kwa mfano hapa kwangu nina ratiba ya chakula asubuhi mchana na jioni,asa utakuta ratiba yangu jioni ni kupika hiki yeye atapika kile,hafu maagizo yote hela huwa namuachia binti wa kazi lakini ukirudi ulicho tegemea kukuta sicho kuuliza ooh aunt kasema tupike hiki. Kwahiyo ni kama anataka niishi apendavyo yeye.na sio kama hivyo vingine yeye hatumii hapana anatumia ila fujo tu.

Hapo bado atapika sufuria kubwa la chakula kesho unakikuta kwenye dustbin.haya asubuhi ataamka atapika chai ya rangi hapa kwangu kuna bili ya maziwa bado atapika na uji🙄 sio kama anamtoto wala hanyonyeshi siku mbili kilo ya sukari kwisha. hapo sijazungumzia mafuta,huwa nanunua viazi kwaajili ya chai lakini yeye kila siku asubuhi atapika chips anywe na chai,asa nakuta mafuta hayakai vile nlivyokusudia kumuuliza dada mnatumiaje mafuta aunt anapika chips kila mara asubuhi.na sio mjamzito .sawa kwake alikuwa yeye pekeyake na mume wake huenda alikuwa anaishi hivyo lakini mimi ninafamilia na sio kama tumetusua maisha jamani mimi na mume wangu wote ni wahanga wa ajira tuko mtaani tunaunga unga tu na tumepanga bado kwanini haelewi? Kila pesa tunayoipata tunaipangilia sana
 
Wanawake waone hivi ni watu wabaya sana that's why hata wao hawapendani,ukimkuta ametokea maisha ya shida akaja kukutana mwanaume mwenye nazo ,ubinafsi ,roho mbaya,chuki hata visa utaona, matatzo mengi source ni women

Sent from my Infinix X624 using JamiiForums mobile app
Hivi sijui kwa nini...wanawake waliotoka kwenye dhiki wakaolewa mahali penye unafuu huwa wanakuwa washenzi sana
 
Duh ila ndugu wa mume jamani kuishi nao yataka moyo.nimekuja kugundua kwanini watu wengi wanaishi na ndugu zao kuliko ndugu wa mume.nikiishi na mdogo wangu namtuma nitakavyo hata nguo zangu nampa anifulie hutomsikia kunung'unika, ndugu wa mume mtume hata mara moja ukoo wao mzima watajua . Nako hapa naishi na wifi yangu kaachika kwa mume wake yaani ni kero jamani nyumba imekuwa kama na wanawake wawili mimi napanga kipikwe hiki yeye anapika kile mavyakula anapika mengi anaishia kumwaga yaani ilimradi fujo.hapa napanga na mimi niondoke niende kuishi kwa kakaangu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] uache nyumba yako uende kwa kaka au unatania
 
Sijui kama umenielewa, huyu wifi yangu katoka kwa mume wake kaja hapa kwa kaka yake kuishi.ishu inayokuja kwa mfano hapa kwangu nina ratiba ya chakula asubuhi mchana na jioni,asa utakuta ratiba yangu jioni ni kupika hiki yeye atapika kile,hafu maagizo yote hela huwa namuachia binti wa kazi lakini ukirudi ulicho tegemea kukuta sicho kuuliza ooh aunt kasema tupike hiki. Kwahiyo ni kama anataka niishi apendavyo yeye.na sio kama hivyo vingine yeye hatumii hapana anatumia ila fujo tu.hapo bado atapika sufuria kubwa la chakula kesho unakikuta kwenye dustbin.haya asubuhi ataamka atapika chai ya rangi hapa kwangu kuna bili ya maziwa bado atapika na uji[emoji849] sio kama anamtoto wala hanyonyeshi siku mbili kilo ya sukari kwisha. hapo sijazungumzia mafuta,huwa nanunua viazi kwaajili ya chai lakini yeye kila siku asubuhi atapika chips anywe na chai,asa nakuta mafuta hayakai vile nlivyokusudia kumuuliza dada mnatumiaje mafuta aunt anapika chips kila mara asubuhi.na sio mjamzito .sawa kwake alikuwa yeye pekeyake na mume wake huenda alikuwa anaishi hivyo lakini mimi ninafamilia na sio kama tumetusua maisha jamani mimi na mume wangu wote ni wahanga wa ajira tuko mtaani tunaunga unga tu na tumepanga bado kwanini haelewi? Kila pesa tunayoipata tunaipangilia sana
Kulea mawifi wa namna hiyo ni kazi. Pole sana.
 
Ni kazi Sana hata madogo wanakuzarau inabid uvumilie.kuna ile system madogo wamekunywa either soda au juice wameshindwa kumaliza eti unaitiwa unakumepaka shombo ya michipsi soda au juice ety mmpe uncle nilikuwa sipend kinouma hizo piga

Hata wakibaisha msosi unaitiwa nilikuwa sipokei

Sent using Jamii Forums mobile app
Unakula makombo

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Chanzo Cha yote hayo ni njaa hukosefu wa chakula .

Mimi Nina kilo miatano za mchele na gunia mbili za maharage na Nina pesa za Mboga Sasa ukija kwangu kunitembelea huwezi kugombana na mtu .


Wanawake wana njaa Sana Mnabidi kulifahamu hilo Kama hauna chakula Cha kutosha usimlete ndugu ikiwa unakaa na Mwanamke ataishia kumnyanyasa Mimi nimejionea haya Mambo Nina ndugu yangu yeye anakaaga na vyakula magunia Mengi ya kutosha Sasa pale kwake ndugu wa mke na wa Mume wanakula na kusaza huwezi kuona ugomvi ukitokea Sasa njoo huku kwa Hawa sijui Mwalimu sijui nurse sijui nani huko pamoto Sana.
Nimerudia kusoma,sijaona ulichobakisha umemaliza yote kabisa njaa mbaya
NB;katika yote tuhakikishe akili hailiwazi tumbo kwanza
Then environment ya house pia ina favor sana unakuta kijumba kidogo hakina hata nyumba ya nje au vyumba vya wageni hapo lazma interaction ya mgeni na mwenyeji inakua Kubwa haimpi Uhuru mwenyeji wala mwenye mji kujitawala
Tujitahidi tujenge hata vyumba viwili na ka choo kwa nje for visitors inasaidia kupunguza kero
 
Sijui kama umenielewa, huyu wifi yangu katoka kwa mume wake kaja hapa kwa kaka yake kuishi.ishu inayokuja kwa mfano hapa kwangu nina ratiba ya chakula asubuhi mchana na jioni,asa utakuta ratiba yangu jioni ni kupika hiki yeye atapika kile,hafu maagizo yote hela huwa namuachia binti wa kazi lakini ukirudi ulicho tegemea kukuta sicho kuuliza ooh aunt kasema tupike hiki. Kwahiyo ni kama anataka niishi apendavyo yeye.na sio kama hivyo vingine yeye hatumii hapana anatumia ila fujo tu.hapo bado atapika sufuria kubwa la chakula kesho unakikuta kwenye dustbin.haya asubuhi ataamka atapika chai ya rangi hapa kwangu kuna bili ya maziwa bado atapika na uji[emoji849] sio kama anamtoto wala hanyonyeshi siku mbili kilo ya sukari kwisha. hapo sijazungumzia mafuta,huwa nanunua viazi kwaajili ya chai lakini yeye kila siku asubuhi atapika chips anywe na chai,asa nakuta mafuta hayakai vile nlivyokusudia kumuuliza dada mnatumiaje mafuta aunt anapika chips kila mara asubuhi.na sio mjamzito .sawa kwake alikuwa yeye pekeyake na mume wake huenda alikuwa anaishi hivyo lakini mimi ninafamilia na sio kama tumetusua maisha jamani mimi na mume wangu wote ni wahanga wa ajira tuko mtaani tunaunga unga tu na tumepanga bado kwanini haelewi? Kila pesa tunayoipata tunaipangilia sana
Mwenyewe hapo anaona anatumbua mali za kaka yake na sio wewe
 
Back
Top Bottom