Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Unakuta kampuni kwa mfano inaitwa bakheresa co.ltd, lakini kwenye bidhaa zake anatumia azam au Metl kwenye bidhaa anatumia mo...! Hii huwa inanichanganya sana mkuu, hebu nisaidie imekaaje hiyo

Hapa inakua hivi, unakuta kampuni inasajiliwa kama ulivyosema hapo juu.. Lakini hiyo kampuni ina biashara zaidi ya moja na inataka kila biashara itumie jina lake tofauti lakini kampuni inakua ile ile moja.

Hapo kinachofanyika ni kufungua majina ya biashara (business name) au tuseme branding name ambazo umiliki wake ni wa kampunj. Maana majina ya biashara yapo ya aina 3 ambazo ni Sole Proprietor, Partnership na Corporate (hii ya mwisho ndo tunayozungumzia)

Mfano mwengine hata tiGo sio kampuni bali ni jina la biashara linalomilikiwa na Kampuni ya MIC Tanzania Limited.
 
mnhhhhhhh
Mkuu mi nilienzisha uzi huu nina kampuni inayohusika na mambo haya ya Business Consultation ila tu sikuamua kuweka tangazo kama tangazo bali niliamua kutoa elimu ya bure tu, kwa ataehitaji atanitafuta.. ila lengo halikua kutangaza huduma nazofanya, lengo lilikua ni kuelimishana.. unapokuja na kuweka tangazo lako kwenye uzi wangu unakosea kwa vitu vifuatavyo

1. Huwezi kuweka tangazo lako kwa mtu ambae anafanya huduma hiyo hiyo, ni kama ukaweke mabango ya Kilimanjaro kwenye mkutano wa Uhai

2. UNAHARIBU MAANA YA HUU UZI! Anaweza kuja mtu mgeni hapa akajua ni tangazo la biashara wakati unapaswa kuwa ni wa kuelimishana..

Acha mara moja
 
Share capital huwa haina impact kweny kodi.
kodi ya kampuni inakatwa kwenye faida utayopata kwa mwaka… 30% ya faida ndio kodi yako utayolipa TRA.

Kwa mfano mawakala wa huduma za kifedha mfano Mpesa hua wanakatwa 10% ya commission zako kama Withholding Tax kama ilivyoanishwa na TRA wenyewe. Sasa nawezaje kuclaim haya malipo mwisho wa mwaka ili kuweza kufidia hiyo 30% ya corporate Tax ya kila mwaka?
 
Mkuu mi nilienzisha uzi huu nina kampuni inayohusika na mambo haya ya Business Consultation ila tu sikuamua kuweka tangazo kama tangazo bali niliamua kutoa elimu ya bure tu, kwa ataehitaji atanitafuta.. ila lengo halikua kutangaza huduma nazofanya, lengo lilikua ni kuelimishana.. unapokuja na kuweka tangazo lako kwenye uzi wangu unakosea kwa vitu vifuatavyo

1. Huwezi kuweka tangazo lako kwa mtu ambae anafanya huduma hiyo hiyo, ni kama ukaweke mabango ya Kilimanjaro kwenye mkutano wa Uhai

2. UNAHARIBU MAANA YA HUU UZI! Anaweza kuja mtu mgeni hapa akajua ni tangazo la biashara wakati unapaswa kuwa ni wa kuelimishana..

Acha mara moja
Mkuu huyo achana naye tu maana nimeangalia hata anachojibu ni tofauti na kile nilichouliza Hawa ni wale wanaotanguliza malipo kabla ya elimu yenyewe.
IMG_20220222_074328.jpg
 
Mtaji wa chini kabisa wa kuanzishia Limited Company kisheria ni kuanzia 20,000-1,000,000
1.Ina maana mkuu nikiwa na 20,000-1,000,000 kwa mara ya kwanza naweza sajili kampuni yangu na ikawa limited au unamaanishaje..????

2.Na ni changamoto gani zinazoweza kujitokeza baadaye Kama ni hivyo...??
 
Kwa mfano mawakala wa huduma za kifedha mfano Mpesa hua wanakatwa 10% ya commission zako kama Withholding Tax kama ilivyoanishwa na TRA wenyewe. Sasa nawezaje kuclaim haya malipo mwisho wa mwaka ili kuweza kufidia hiyo 30% ya corporate Tax ya kila mwaka?


Malipo ya withholding tax huwa yanaingia kama Credit ambayo inaenda kupunguza Corporate tax yako..

Mfano labda baada ya kuandaa hesabu zako ikaonekana kwamba Corporate Tax yako inapaswa kuwa Milion 1 lakini ukakumbuka kuwa kwa mwaka mzima ulilipia Withholding tax ya 800k.. basi hapa Corporate tax yako itapungua kutoka 1Milioni mpaka 200k..

Na hata kama ukiwa unadaiwa Corporate Tax lakini ukawa mlipaji mzuri wa Withholding Tax basi hiyo pia itakusaidia kupunguza deni lako la Corporate Tax
 
1.Ina maana mkuu nikiwa na 20,000-1,000,000 kwa mara ya kwanza naweza sajili kampuni yangu na ikawa limited au unamaanishaje..????

2.Na ni changamoto gani zinazoweza kujitokeza baadaye Kama ni hivyo...??

1. YES, Inakuwa Limited Company.. Nachomaanisha kiundani ni kwamba sheria za makampuni wameweka hisa za mtaji (share capital) ambayo hii ni kama thamani ya kampuni kwa lugha rahisi, Ianzie kati ya 20k-1M

Ukifungua kampuni ya share capital yoyote kati ya hiyo Brela watataka ulipie sh 167,200 tu kama Registration Fee yako.

Ingawa kadri utavyokua unapandisha mtaji wa kampuni basi na gharama za usajili nazo zitazidi kuongezeka.. mfano mtu mwenye kampuni kati ya milion 5-20 yeye Registration fee yake huwa ni 332,200

2. Kufungua kampuni ambayo utaonesha una mtaji mdogo changamoto kubwa inaeza kukupata kwenye uombaji wa tender, maana sehemu nyengine wanaweza wakaangalia thamani ya kampuni yako wakaona ni ndogo sana hivyo hutoweza kumudu tender yao kwa jinsi wanavyotaka.

Na vile vile kuna baadhi ya leseni za biashara kama ukiweka mtaji mdogo mamlaka haiwezi kukupa leseni (japo ni biashara chache maana nyingi unaweza kupewa leseni pasipo kuzingatia mtaji wako wa kampuni)
 
Malipo ya withholding tax huwa yanaingia kama Credit ambayo inaenda kupunguza Corporate tax yako..

Mfano labda baada ya kuandaa hesabu zako ikaonekana kwamba Corporate Tax yako inapaswa kuwa Milion 1 lakini ukakumbuka kuwa kwa mwaka mzima ulilipia Withholding tax ya 800k.. basi hapa Corporate tax yako itapungua kutoka 1Milioni mpaka 200k..

Na hata kama ukiwa unadaiwa Corporate Tax lakini ukawa mlipaji mzuri wa Withholding Tax basi hiyo pia itakusaidia kupunguza deni lako la Corporate Tax

Naomba nipate mawasiliano yako Boss!
 
Naomba nimsaidie maana naona kaleta mada chokozi lakini hana majibu, VRN navyofahamu mimi ni vat registration number kwa lugha mama ni namba ya usajili wa vat.Faida yake ni kama umesajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani yaani vat risiti zote za mauzo yako au manunuzi inatakiwa namba ya muuzaji na mnunuzi kama wote ni vat register ionekane kwenye risiti sababu ukiuza sana kuliko kununua unapeleka tra hiyo vat na kinyume chake ukinunua sana na ukawa haujauza sana basi ile tofauti ya manunuzi na uuzaji unarejeshewa na tra.Ili uweze rejeshewa risiti lazima iwe na hiyo vrn ya aliyekuuzia na ya kwako kwenye risiti ya manunuzi.
Naonaga mzee wangu mmoja anafanya hii, ana acountant wake consultant company anawapelekea then anarudishiwa hio pesa.
Kitu sijaelewa hapo kwenye maelezo yako ni huo utafuti kati ya manunuzi na uuzaji, kwanini wanakurudishia huo utofauti?
Huo utofauti unamaanisha nini?
 
1. YES, Inakuwa Limited Company.. Nachomaanisha kiundani ni kwamba sheria za makampuni wameweka hisa za mtaji (share capital) ambayo hii ni kama thamani ya kampuni kwa lugha rahisi, Ianzie kati ya 20k-1M

Ukifungua kampuni ya share capital yoyote kati ya hiyo Brela watataka ulipie sh 167,200 tu kama Registration Fee yako.

Ingawa kadri utavyokua unapandisha mtaji wa kampuni basi na gharama za usajili nazo zitazidi kuongezeka.. mfano mtu mwenye kampuni kati ya milion 5-20 yeye Registration fee yake huwa ni 332,200

2. Kufungua kampuni ambayo utaonesha una mtaji mdogo changamoto kubwa inaeza kukupata kwenye uombaji wa tender, maana sehemu nyengine wanaweza wakaangalia thamani ya kampuni yako wakaona ni ndogo sana hivyo hutoweza kumudu tender yao kwa jinsi wanavyotaka.

Na vile vile kuna baadhi ya leseni za biashara kama ukiweka mtaji mdogo mamlaka haiwezi kukupa leseni (japo ni biashara chache maana nyingi unaweza kupewa leseni pasipo kuzingatia mtaji wako wa kampuni)
Okay nimekuelewa mkuu kwa hiyo ili usisumbuliwe kupata leseni na vibali vingine Hadi kampuni ikakamilika inatakiwa ufungue kampuni yenye mtaji kiasi gani ..???
Na itagharimu kiasi gani Hadi kampuni ikakamilika....????
 
Okay nimekuelewa mkuu kwa hiyo ili usisumbuliwe kupata leseni na vibali vingine Hadi kampuni ikakamilika inatakiwa ufungue kampuni yenye mtaji kiasi gani ..???
Na itagharimu kiasi gani Hadi kampuni ikakamilika....????

Labda kwanza tujue ni kampuni itayojihusisha na nini zaidi!? Maana upande wa leseni za biashara kila leseni ina ada yake kutegemea na aina ya biashara unayofanya
 
Nilifunga biashara toka 2016 na kodi makadirio ni 1.5mil kwa mwaka ila sijawahi lipa na sijawahi andika barua, hapo inakuwaje maana nilienda funga nikakuta deni limefika 7.5mil mwaka 2019

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilifunga biashara toka 2016 na kodi makadirio ni 1.5mil kwa mwaka ila sijawahi lipa na sijawahi andika barua, hapo inakuwaje maana nilienda funga nikakuta deni limefika 7.5mil mwaka 2019

Sent using Jamii Forums mobile app

Biashara yako ni ya kampuni au binafsi!? Deni ambalo limeongezeka limetoka kwenye Principle tax au limetokana na Penalty/Interest!?
 
Ilikuwa sole proprietorship
Penalt, Interest, Principal Tax

Sent using Jamii Forums mobile app

Principle amount ikishaingia kwenye system na imeingizwa kihalali pasipo kutokea makosa yoyote basi hiyo inapaswa kulipwa.

Penalty na Interest unaweza kuomba msamaha Kwa Regional Manager kwa kujaza fomu ya APPLICATION FOR REMISSION OF INTEREST/PENALTY (lakini hii ni ngumu kidogo kukubaliwa though unaweza kujaribu)

Maana changamoto deni likishaingia kwenye system ndio lishaingia na njia rahisi ya kuliondoa ni kulipa.

Ukiona kama njia hiyo hapo juu imeshindikana basi kaa nao chini mkubaliane payment plan na uanze kulipia kidogo kidogo (hii unakubaliwa bila shida) huku mambo yako mengine kma vile kupewa Tax Clearance yakiendelea.
 
Wakati wa JPM tuliagizwa tupeleke tin namba zetu , nini madhumuni ya zoezi lile.
Lingesaidia vipi kudhibiti wafanyakazi hewa kwenye kampuni binafsi?
Kodi ya paye ambayo inalalamikiiwa na waajiri kuwa wanalipa kodi wakati mwajiri ni wakala tu ingeisaidia vipi?
Kwa nini kusiwe na juhudi kubwa za kuhakikisha kila kampuni mhasibu wake anajua kodi kama hajui basi mtaalambwa kodi aajiriwe.?
 
Back
Top Bottom