Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Kwenye kulitumia hilo jina katika kampuni inakuwaje? Unalisajili tena au

Ukishamaliza kuli’cease’ hilo jina kama nilivyoelezea hapo juu basi unafanya usajili wa kampuni kwa taratibu za kawaida.. maana bila kulifunga hilo jina ukitaka kulisajili kama kampuni Brela watakataa watasema majina yanafanana
 
Ukishamaliza kuli’cease’ hilo jina kama nilivyoelezea hapo juu basi unafanya usajili wa kampuni kwa taratibu za kawaida.. maana bila kulifunga hilo jina ukitaka kulisajili kama kampuni Brela watakataa watasema majina yanafanana
Sasa kwa case yangu nikisajili kampuni kwa jina tofauti na ile sole proprietor lakini details ni zile zile si haina shaka mkuu???
 
Mambo vip!,

Upo kwenye mchakato wa kufungua Kampuni ya kutoa mikopo wa wajasiria mali pamoja na wakulima wadogo wadogo mtaji wa biashara ya namna hii ni millioni 20 na kuendelea.

Hapa mhusika mkuu anakuwa hana kash ya kuanzia ila lengo ni kufungua kampuni kwanza ili baadae kuanza kuwashawishi watu waweke pesa zao iki kufikia kiwango cha chini cha kuanzia ili biashara ianze yaani kuweza kuchukua leseni BOT, Swali nitafanyaje ili kufikia hatua hiyo
 
Mambo vip!,
Upo kwenye mchakato wa kufungua Kampuni ya kutoa mikopo wa wajasiria mali pamoja na wakulima wadogo wadogo mtaji wa biashara ya namna hii ni millioni 20 na kuendelea.
Hapa mhusika mkuu anakuwa hana kash ya kuanzia ila lengo ni kufungua kampuni kwanza ili baadae kuanza kuwashawishi watu waweke pesa zao iki kufikia kiwango cha chini cha kuanzia ili biashara ianze yaani kuweza kuchukua leseni BOT, Swali nitafanyaje ili kufikia hatua hiyo

Hapo inabidi uanze na hatua ya awali kabisa ya usajili wa kampuni upande wa Brela (ukipitia post za juu hapo nimeelezea kwa kina)

Ila tu ili mbeleni usije kukwama hakikisha kabisa angalau mtu mmoja katika kampuni awe amesomea mambo ya fedha,uhasibu au uchumi.

Ukishamalizana na Brela basi utaenda TRA kwa ajili ya kuchukua TIN ya kampuni pamoja na Tax Clearance.

Mpaka kufikia hapo itakua umefikia hatua ya kwenda kuchukua leseni BOT, kama utaamua kukusanya hela mpaka kufikia huo mtaji wa kima cha chini unaotakiwa (Milioni 20) ni sawa.

Ila hizo hapo juu ndio hatua za kuanza nazo mpaka ufikie hatua unayotaka kama ulivyouliza
 
Ngoja nikujibu jibu la maelezo marefu kidogo kwa faida yako na wote kwa siku zijazo.

Mnapokadiriwa kodi na TRA labda mwanzoni mwa mwaka, na unaona miezi inaenda ile biashara imekua ndivyo sivyo au imekufa kabisa jitahidi kabla mwaka haujaisha katoe taarifa TRA ili wabadilishe makadirio yako ya kodi, utawaambia umeenda kufanya ammendment ya makadirio ya kodi (TRA hawapendi hiki kitu ila ni inawezekana)

Kama una ushahidi wa kusupport unayoyaongea inakua vizuri zaidi, kama kodi labda ilikua 250k unaweza ukajikuta umepunguziwa hadi 100k

Ukikaa ukisubiri mpaka mwaka uishe kabisa hiyo kodi ni lazima utailipa, hata utoe sababu gani

Kama wewe ni mfanyabiashara ambae hutunzi kumbukumbu za hesabu wala huandai mahesabu ya mwaka (Tax under Presumpitve) HAKUNA PENALTY.. ingekua ni mfanyabiashara ambae unatunza kumbukumbu na kupeleka hesabu penalty ni sh 75,000 kwa kila mwezi unaochelewa na kwa kampuni penalty ni sh 225,000 kwa mwezi

Kama biashara umefunga tangu kipindi hiko andika barua kabla ya mwezi March tarehe 31 mwaka huu, usisubiri mwisho wa mwaka

Ahsante
 
Ukishamaliza kuli’cease’ hilo jina kama nilivyoelezea hapo juu basi unafanya usajili wa kampuni kwa taratibu za kawaida.. maana bila kulifunga hilo jina ukitaka kulisajili kama kampuni Brela watakataa watasema majina yanafanana

Shukran sana
 
Habari mkuu,,
Umesema wakurugenzi wa kampuni wanatakiwa wawe kuanzia wawili
Na wote inatakiwa wawe wamefikisha miaka 18 Sasa mfano mimi nataka kufungua kampuni yangu na mkurugenzi wa pili nahitaji kumuweka mtoto wangu Sasa shida hajafikisha miaka 18 maana kwa Sasa ana miaka 5 nafanyaje na sitaki kumuweka mtu mwingine...????
 
Naomba unielekeze jinsi ya kujaza makadirio ya kodi online maana nimeingia tovuti ya TRA sioni mahala naweza kujaza hiyo form.please assist
 
Unaandika barua kwenda TRA kuwajulisha kuwa umefunga biashara, na utaandika barua kwenda halmashauri uliyochukua leseni ya biashara ili kuwajulisha waifunge leseni yako

Nini. Madhara ya kutokufanya hivyo???


Nataka kufungua kampuni ya ku import bidhaa china kuweka brand yangu na kuuza tanzania.Ni agricultural chemicals sasa nahitaji kujua utaratibu wa kuwa na kampuni ya ku distribute product na je unaweza kujua aina ya vibali navyohitaji kufungua kampuni ya kuuza supply chemical??
 
Habari mkuu,,
Umesema wakurugenzi wa kampuni wanatakiwa wawe kuanzia wawili
Na wote inatakiwa wawe wamefikisha miaka 18 Sasa mfano mimi nataka kufungua kampuni yangu na mkurugenzi wa pili nahitaji kumuweka mtoto wangu Sasa shida hajafikisha miaka 18 maana kwa Sasa ana miaka 5 nafanyaje na sitaki kumuweka mtu mwingine...????

Ukisoma vizuri niliandika ili mtu awe mkurugenzi wa kampuni kwanza kabisa inabidi awe amefikisha Miaka 21.. sio 18 mkuu.

Tukija kwenye swali la msingi huyo mtoto wako wa miaka mitano hawezi kuwa mkurugenzi wa kampuni kwa sasa, kama hutaki kumueka mtu mwengine zaidi ya yeye basi suala lako la kusajili kampuni kwa sasa litakua limeshindikana.
 
Naomba unielekeze jinsi ya kujaza makadirio ya kodi online maana nimeingia tovuti ya TRA sioni mahala naweza kujaza hiyo form.please assist

Anza kwa kuingia tovuti hii eFiling System | Login ukishaingia kwa kuwa huna account itabidi uanze na Registration. Kwenye Registration utatumia TIN yako kuingiza then utapata sms kwenye namba yako ambayo itakua na Passcode za kuingilia, baada ya hapo system itakuwezesha kucreate password

Ukimaliza hizi process utalogin kwa kutumia Username yako (ambayo ni TIN) pamoja na password uliyoweka, then utaenda sehemu ya Unfilled Return utachagua sehemu husika.

Kwa msaada zaidi ni vizuri ukanicheki kwa WhatsApp ili niweze kukuassist au nkutumie kabisa User Guidlines yake
 
Nini. Madhara ya kutokufanya hivyo???


Nataka kufungua kampuni ya ku import bidhaa china kuweka brand yangu na kuuza tanzania.Ni agricultural chemicals sasa nahitaji kujua utaratibu wa kuwa na kampuni ya ku distribute product na je unaweza kujua aina ya vibali navyohitaji kufungua kampuni ya kuuza supply chemical??

1. Usipoandika barua ya kufunga biashara na kufunga leseni ya biashara basi manispaa na TRA wote watakuhesabiakama bado unafanya biashara ila unakwepa kulipa kodi. Hivyo basi utakutana na makadirio yako ya kodi kwa TRA kwa mika ambayo hujaonekana na upande wa manispaa siku utayoenda kwa ajili ya kurenew leseni utakutana na Penalty.

2. Kama nilivyosema awali Utaratibu wa kufungua kampuni ya aina yoyote ile huwa unafanana ila utofauti unakuja kwenye leseni na vibali.

Kama umepitia huu uzi vizuri nimeelezea utaratibu mzima nafikiri sina haja ya kurudia mkuu.

Upande wa Leseni, hiyo leseni yako ni Kundi A ambayo inapatikana Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia wakala wake BRELA.

Lakini kabla hujaomba Leseni hiyo unapaswa kupata kibali kutoka kwa Mkemia mkuu wa serikali (Government Chemist and Laboratory Agency)
 
Naomba niulize, kuna biashara nilifungua 2020 na wakanikadiria kodi 200k kwa mwaka. Ila sikuweza kuifungua. Nilipowafata kutaka kuifunga wakasema mpaka mwaka uishe na mpaka nilipe kodi ya mwaka. Mwaka 2021 mwishoni nilikuwa mbali so nikashindwa kuwaandikia barua na kulipa deni la kodi. Je,
Penalt ni Tshs ngapi/asilimia ngapi? Nikiwaandikia barua ya kufunga biashara mwisho wa mwaka huu?
Mkuu jitahidi umalizane nao kabla ya 31 March.
Sheria ya kodi ni ngumu na hazijawekwa kutufavour sisi wafanyabiashara.
Penalty yake ni cummulative aisee.
 
Mkuu Habari ya uzima!
Inawezekana kubadilisha business name (sole proprietor) to limited company?
 
Mkuu Habari ya uzima!
Inawezekana kubadilisha business name (sole proprietor) to limited company?

Inawezekana... Unachotakiwa kufanya kabla hujaanza usajili wa kampuni inabidi ufunge kwanza jina la biashara hilo ambalo umelisajili, Huduma hii inaitwa "Ceasation of business name" na inalipiwa sh 10,000 tu. Kuna fomu utapaswa kujaza na kuziwasilisha kwa njia ya mtandao (ORS)

Wakati wa kufunga hilo jina la biashara itabidi utoe sababu kuwa unalifunga ili uweze kutumia jina hilo katika kampuni.

Baada ya kukamilisha kufunga jina la biashara sasa hatua inayofuata ni kuanza usajili wa kampuni, Hapa itabidi uanze kuandaa kwanza Memorandum

Katika sehemu ya kuweka objectives(shughuli ambazo unazifanya au unatarajia kuzifanya) hakikisha objective no 1 itakua ni kutake over hilo jina la biashara na shughuli zake zote ziwe katika kampuni.

Baada ya hapo taratibu za kawaida za usajili wa kampuni zitaanza.
 
Inawezekana... Unachotakiwa kufanya kabla hujaanza usajili wa kampuni inabidi ufunge kwanza jina la biashara hilo ambalo umelisajili, Huduma hii inaitwa "Ceasation of business name" na inalipiwa sh 10,000 tu. Kuna fomu utapaswa kujaza na kuziwasilisha kwa njia ya mtandao (ORS)

Wakati wa kufunga hilo jina la biashara itabidi utoe sababu kuwa unalifunga ili uweze kutumia jina hilo katika kampuni.

Baada ya kukamilisha kufunga jina la biashara sasa hatua inayofuata ni kuanza usajili wa kampuni, Hapa itabidi uanze kuandaa kwanza Memorandum

Katika sehemu ya kuweka objectives(shughuli ambazo unazifanya au unatarajia kuzifanya) hakikisha objective no 1 itakua ni kutake over hilo jina la biashara na shughuli zake zote ziwe katika kampuni.

Baada ya hapo taratibu za kawaida za usajili wa kampuni zitaanza.
Okay na ukiwa unafungua kampuni ukadanganya mtaji wa kufungulia kampuni mfano mtaji uliopo ambao nataka kuanza nao ni 30 milion alafu Mimi nikawaambia mtaji wangu ni kuanzia 1M Hadi 5 M afu wakanikubalia kufungua hapo badaye kutakuwa na shida gani ....????
 
Back
Top Bottom