Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Uliza swali lolote linalohusiana na kampuni katika upande wa kodi na usajili

Utaratibu wa kusajili kampuni ya aina yote ile huwa unafanana, utofauti huwa unakuja kwenye kupata vibali na leseni za biashara.

Ili kusajili kampuni mpya kwanza kabisa inabidi waanzilishi wa kampuni muwe wawili na kuendelea, na pia kama wote ni watanzania ni lazima muwe na namba ya kitambulisho cha Taifa (NIDA) pamoja na namba za TIN zenu binafsi, ila kama kuna raia wa kigeni inabidi awe na passport ya kusafiria.

Baada ya hapo taratibu nyengine zitafuatia kama vile kuandaa Memorandum and Articles of associtaion ya kampuni, kujaza documents nyingine za usajili (Form 14b na Ethics and Intergrity form) pamoja na kufanya usajili wenyewe kwa njia ya mtandao wa ORS (Online Registration System)
Muanzilishi wa kampuni lazima wawe wawili na kuendelea!? Akiwa mmoja anakosa bigezo vya kusajili kampuni
 
Okay na ukiwa unafungua kampuni ukadanganya mtaji wa kufungulia kampuni mfano mtaji uliopo ambao nataka kuanza nao ni 30 milion alafu Mimi nikawaambia mtaji wangu ni kuanzia 1M Hadi 5 M afu wakanikubalia kufungua hapo badaye kutakuwa na shida gani ....????

Share capital huwa haina impact kweny kodi.
kodi ya kampuni inakatwa kwenye faida utayopata kwa mwaka… 30% ya faida ndio kodi yako utayolipa TRA.
 
Muanzilishi wa kampuni lazima wawe wawili na kuendelea!? Akiwa mmoja anakosa bigezo vya kusajili kampuni

Yes waanzilishi wa kampuni binafsi wasipungue 2 na wasizi 50. Chini ya hapo haitowezekana kusajili kampuni.
 
Mkuu nina maswali hap..naamini utanisaidia
1.nina kampuni 2 nilisajili brela mda sasa nataka zipate tin na vrn nipe garama na process
2.nina machine imefungwa na tra hivi haina namna nikapambana nikaifungua bila kulipa deni..maana halilipiki
 
Hapo inabidi uanze na hatua ya awali kabisa ya usajili wa kampuni upande wa Brela (ukipitia post za juu hapo nimeelezea kwa kina)

Ila tu ili mbeleni usije kukwama hakikisha kabisa angalau mtu mmoja katika kampuni awe amesomea mambo ya fedha,uhasibu au uchumi.

Ukishamalizana na Brela basi utaenda TRA kwa ajili ya kuchukua TIN ya kampuni pamoja na Tax Clearance.

Mpaka kufikia hapo itakua umefikia hatua ya kwenda kuchukua leseni BOT, kama utaamua kukusanya hela mpaka kufikia huo mtaji wa kima cha chini unaotakiwa (Milioni 20) ni sawa.

Ila hizo hapo juu ndio hatua za kuanza nazo mpaka ufikie hatua unayotaka kama ulivyouliza
Ahsante, nimesha lipa clearance tax kwa bahati mbaya Kampuni haija takeoff kwa miaka minne mbele, je kuna gharama zozote japo sijaanza kufanya biashara.
 
Share capital huwa haina impact kweny kodi.
kodi ya kampuni inakatwa kwenye faida utayopata kwa mwaka… 30% ya faida ndio kodi yako utayolipa TRA.
Ni nini maana halisi ya kuweka makundi ya mitaji kama haina athari kwenye kulipa kodi.. Maana halisi ya makundi ya mitaji ni nini?
 
Ahsante, nimesha lipa clearance tax kwa bahati mbaya Kampuni haija takeoff kwa miaka minne mbele, je kuna gharama zozote japo sijaanza kufanya biashara.
Harafu hapa pia mtaalamu wa fedha hata ngazi ya certificate bado anafiti mkuu.
 
Mkuu nina maswali hap..naamini utanisaidia
1.nina kampuni 2 nilisajili brela mda sasa nataka zipate tin na vrn nipe garama na process
2.nina machine imefungwa na tra hivi haina namna nikapambana nikaifungua bila kulipa deni..maana halilipiki

1. Utaratibu wa kupata TIN ni unapaswa kwenda TRA ya mkoa wako wa kodi ukiwa na vifuatavyo

A. Certificate of Incorporation
B. Memorandum
C. Mkataba wa Pango
D. Vitambulisho vya Madirector
E. Utajaza na fomu za TIN ya kampuni zinazopatikana TRA

Kuhusu VRN hii kuna fomu maalum ya kujaza na kisha unaapply, wakiona una vigezo utapewa na wakiona hauna basi utanyimw(kigezo kikuu ni kufikisha turnover ya milioni 100 kwa mwaka au uwe na business plan ambayo itaonesha una uwezo wa kufikia turnover hiyo kwa mwaka)

Japo kuna kampuni ambazo zimewekwa katika makundi maalum huwa wanapata bila turnover mfano ujenzi, mawakili, consultation n.k

2. Dawa ya deni ni kulipa mkuu[emoji23] ila ukitaka hizo namna tutafutane private ntakupa mbinu tu za kisheria zinazokubalika ukaweza kusonga mbele
 
Wakuu naomba kuuliza namna ya kufungua NGO na requirements zake ni zipi....natanguliza shukrani

Nna utaratibu mzima wa kuanzisha NGO na kusajili (japo mi sideal na masuala hayo, ikikupendeza nitafute kwa whatsapp nikutumie pdf yake upitie, kwa hapa nashindwa kuattach
 
Mkuu naomba kuuliza swali lingine Tena hivi ili usajiri kampuni iwe limited inatakiwa iwe na mtaji kiasi gani...???

Mtaji wa chini kabisa wa kuanzishia Limited Company kisheria ni kuanzia 20,000-1,000,000
 
Ahsante, nimesha lipa clearance tax kwa bahati mbaya Kampuni haija takeoff kwa miaka minne mbele, je kuna gharama zozote japo sijaanza kufanya biashara.

Yaani unapochukua TIN tu ya kampuni unakua umejiweka katika list ya kampuni zinazopaswa kucomply na sheria za kodi, kama haufanyi biashara hakikisha ritani zote za kodi zinazokuhusu uziwasilishe kwa wakati. Endapo utazembea utakuja kukutana na Penalty nyingi sana huko mbeleni ambazo hutoweza kuzilipa. So muhimu hata kama kampuni iko dormant jitahidi tu kutuma ritani kwa wakati, na kwa kuwa hufanyi biashara utakua unawasikisha kama NIL Return
 
Unakuta kampuni kwa mfano inaitwa bakheresa co.ltd, lakini kwenye bidhaa zake anatumia azam au Metl kwenye bidhaa anatumia mo...! Hii huwa inanichanganya sana mkuu, hebu nisaidie imekaaje hiyo
 
Kusajili kampuni kea ORS Kuna vikwazo gani, kampuni yangu tangu 2016 nahangaikia ORS sipati usajili japo ilikuwa na usajili was awali kabla ya ORS shida Nini,nifanyeje? Maana Kama Ni gharama nimetuma za kutosha Niko hoi
0748345628

SBJ CONSULTANCY SERVICES LIMITED
TUTAKUHUDUNIA
GHARAMA 200K
NDANI YA WIKI MOJA UTAPATA KILA KITU
 
Habari, napenda kuuliza kuhusu usajili wa Kampuni.
Kampuni imesajiliwa lakini mtaji ama gharama za kupata leseni ukakosa.
Je gharama za kila mwaka lazima mmiliki alipie hata kama hafanyi biashara.
HAPANA KA KAMA HAUFANYI BIASHARA UNAPASWA KUANDIKIWA RETURN YA NIL

HEBU KARIBU
SBJ CONSULTANCY SERVICES LIMITED
0748345628
TUTAKUHUDUNIA
KWA USAJILI WA KAMPUNI NK
 
Mkuu naomba kuuliza swali lingine Tena hivi ili usajiri kampuni iwe limited inatakiwa iwe na mtaji kiasi gani...???
NGO zinasajiliwa chini ya ofisi yaWizara ya Maendeleo ya jamii kwemye mfumo wa Nits..
0748345628


SBK CONSULTANCY SERVICES LIMITED NDANI
TUTAKUHUDUNIA
GHA
 
HAPANA KA KAMA HAUFANYI BIASHARA UNAPASWA KUANDIKIWA RETURN YA NIL

HEBU KARIBU
SBJ CONSULTANCY SERVICES LIMITED
0748345628
TUTAKUHUDUNIA
KWA USAJILI WA KAMPUNI NK

Mkuu mi nilienzisha uzi huu nina kampuni inayohusika na mambo haya ya Business Consultation ila tu sikuamua kuweka tangazo kama tangazo bali niliamua kutoa elimu ya bure tu, kwa ataehitaji atanitafuta.. ila lengo halikua kutangaza huduma nazofanya, lengo lilikua ni kuelimishana.. unapokuja na kuweka tangazo lako kwenye uzi wangu unakosea kwa vitu vifuatavyo

1. Huwezi kuweka tangazo lako kwa mtu ambae anafanya huduma hiyo hiyo, ni kama ukaweke mabango ya Kilimanjaro kwenye mkutano wa Uhai

2. UNAHARIBU MAANA YA HUU UZI! Anaweza kuja mtu mgeni hapa akajua ni tangazo la biashara wakati unapaswa kuwa ni wa kuelimishana..

Acha mara moja
 
Back
Top Bottom