Umasikini wa Watanzania chanzo chake ni kupenda kujenga nyumba ya kuishi kwanza badala ya kuanzisha biashara

Baba hapo kwenye asset na liability umewapiga watu kamba [emoji16][emoji16][emoji16].
Jengo lisilo generate income ni liability sababu linakusubiri upate income sehemu zingine Litafune income yako pia gari ya kutembelea nyumba ya kulala na kuamka zote ni liability zinatafuna tu income toka other sources unapata ni wadai wako kwenye personal finance nyumba ya kulala na kuamka na gari ya kutembelea sio Asset!!! Don't just think of company financial reports prepare your own personal financial reports kukariri !!! Prepare your own personal financial reports !!! Sio unakomaa tu za kampuni jiongeze
 
Point.
 
Point.
 
Kijana mtoa mada inaonyesha bado ni mwanafunzi au pengine ni graduate wa mwaka jana. Hana biashara wala hajui gharama za ku rent nyumba kwaajili ya familia.
 
kumbuka mahitaji muhimu matatu katika maisha "nyumba "ni mojawapo. Mtoa uzi sikuelewi.
 
Mkuu hizi definition za asset na liability umenukuu kutoka conceptual framework gani ya uhasibu?
 
Una akili ndefu sana mkuu, kuna ndugu zangu huwa nakosana nao sababu ya hii tabia ya kukusanya hela na kuzitupa ardhini kwa kigezo cha nyumba kwanza ilihal wahindi vizazi na vizazi wamepanga kariakoo na wana hela kuliko sisi wakimbilia majumba
 
Kwani mkuu kama una biashara, hip biashara so itaendelea kulea familia.Kama unanyumba ukfa familia itaanza kuyumba hela za matumizi.Jambo la kwanza duniani ni kula,kuvaa mwisho kulala.kwa nini tusijenge misingi ya uhakila wa kula kabla ya kulala.Kama hujala utahesabu kenchi mpaka asubuhi.
 
Mkuu hizi definition za asset na liability umenukuu kutoka conceptual framework gani ya uhasibu?
Mkuu hata mm naamini anavyoamini huyu chief ila hakuna uhasibu unaofundisha hivyo.....hakuna mtaala unaotaja asset km mali inayogenerate income ila tu hyo ni applicable zaidi kwa wajasiriamali na nafikiri muasisi wa hii kitu ni Robert Kiyosaki ktk kitabu chake cha RICH DAD POOR DAD
 
Inaanza kwanza shughuli itakayokuingizia kipato maana nyumba inajengwa kwa hela ambazo umeshachuma na zinaendelea kuingia. Hakikisha kabla hujafika 40 au watoto hawajaanza sekondari uwe na kwako otherwise itasumbua sana kufanikiwa
Exactly...mada ileweke hvyo wadau msitumie nguvu kubwa kama ww una 8ml jenga patapo kustir na inayobaki anza Biashara
 

Mkuu an asset kitafsiri kwa maana ya present economic resources zenye potential ya economic benefits. Economic benefits haziko limited to income tu, kuna savings hapo n.k

Na hiyo tafsiri ya asset haina exceptions zozote.

Whether ni personal asset au corporate asset, bado asset inabakia na tafsiri ile ile.

Whether ni personal financial report au corporate financial report, zote zinajumuisha asset zenye tafsiri ile ile.

Whether ni personal asset au corporate asset zote lazima zihudumiwe ili ziendelee kusapoti uzalishaji.

Establishing kwamba personal asset zinakula income huenda katika muktadha wa pale zinapohudumiwa in terms of improvement, repair, maintenance and any other capital and operating cost, this does not justify kuwa sio an asset hivyo basi ni liability.

Asset ni liability to the extent that, which source of finance was used to acquire such an asset.

Liability of an asset haiwi determined na whether hiyo asset inakutia hasara ama laah!

Muamuzi ni chanzo cha mapato(internal or external) ulichotumia kupata asset husika.

Pia lazima tuelewe hakuna asset isiyo na potential economic benefit. Ila kuna uwezekano wa economic benefits kuzidiwa na gharama ya kununua na kuendesha asset.

Mtu anaweza kuwa na mali binafsi lakini inasapoti uzalishaji wake au ana save significantly kuliko ambavyo angekuwa anatumia usafiri wa umma au amepanga.

Cha kuzingatia kabla ya kununua asset fanya cost benefit analysis ya asset husika then uamue kununua.
 
nyumba ndio biashara yenyewe hio, tujenge nyumba tupangishe
 
Mkuu hizi definition za asset na liability umenukuu kutoka conceptual framework gani ya uhasibu?
SIO CONCEPT YA KIUHASIBU NI YA KIUCHUMI

Mhasibu hata gari bovu liliolokuwa grounded kwenye vitabu vyake anaripoti kama ASSET!!!!!!!!!!
 
Tusipangiane ujue.
Lakini mkuu ujue tunafanya vitu vinavyo tupa amani na heshima. Na ndio maana ng'ombe kwa mfugaji ni kitu cha thamani wakati kwa mkulima ni nonsonse
 
SIO CONCEPT YA KIUHASIBU NI YA KIUCHUMI

Mhasibu hata gari bovu liliolokuwa grounded kwenye vitabu vyake anaripoti kama ASSET!!!!!!!!!!
According to accounting standard, ukiacha asset ya land na building, asset zingine kama magari, mashine n.k huwa zinashuka thamani, na standard inataka huku kushuka kwa thamani impact yake ionyeshwe kwenye balance ya asset.

Na asset ikifika point ya kuwa useless ina kuwa derecognized kwa maana ya kufutwa kwenye list ya asset zinazomilikiwa institution husika.

Kama kuna muhasibu ana recognize asset isiyo na thamani ni matatizo yake binafsi, lakn sio kweli accounting standard inaruhusu.
 
Hakuna mtu asiyependa kuwa na kwake,hao wahindi wangekuwa wazawa wangejenga tu fatilia wahindi wote wenye asili ya Tz wana nyumba zao,hivi kwa wenye nyumba wa Nchi ifike January anataka kodi yake wewe unataka ukamlipie mtoto ada atakuelewa..? Watu wanajenga kwanza awe huru na kukimbizana na kelele za wenye nyumba zisizokuwa na maana yoyote.. Sasa mimi nipo kwenye hatua ya rinta then nitafungua bness...
 
Kingine nenda benki kaombe mkopo waambie hauna nyumba ila una bness ya milioni100 kama huo mkopo watakupa kwa sababu gani..? Wanajua bness inaweza ikaporomoka na wakaingia deni ila ukiwa na nyumba yenye thamani hiyo watakupa mkopo koz wanajua ukifilisika nyumba ipo kufidia deni...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…