Umebaini tofauti gani Uwanja wa Mkapa na Uwanja wa Samia unaotarajiwa kujengwa Arusha?

Umebaini tofauti gani Uwanja wa Mkapa na Uwanja wa Samia unaotarajiwa kujengwa Arusha?

Mkuu uchanganuzi wako uko hauko sawa, mimi naapinga kwa kuangalia bei ya mfuko wa cementi kwa mwaka 2007 bila kuangalia factors zingine,mfukowa cementi ulikuwa sh 8000 mikoani,kwa Dar labda ni sh 5000,kwa sasa bei ya cementi kwa mikoani ni sh 23,000 kwa Dar sijui.
duuu ni juzi tu hapa nmetoka kununua mfuko wa cement kwa 17000 hiyo 23K ni kasi ya 5G.
nko mkoani
 
Hii nchi wajinga ni wengi sana. Yani kabisa mtu unalinganisha gharama za miaka 17 iliyopita na leo hii?
Mfano mdogo, mfuko mmoja wa cement mwaka 2007 ulikuwa bei gani na leo hii ni bei gani? Kibarua atakayepewa kazi pale atalipwa sawa na 2007? Hapo hatujaongelea skilled labor.

Wakati mwingine ni vyema kutumia akili kabla ya kupinga kila kitu.
Ndio liwe ongezeko la bilioni mia mbili kwa nusu kazi ndugu yangu, bora tuendelee kuitwa wajinga lakini sio kuingizwa sipo aisee
 
Kwa kweli watuonee huruma hawa viongozi wetu raisi atufafanulie hizi tofauti maana haingii akilini
Hata anajua basi maskini ya Mungu. Yeye akipelekewa anatia sahihi tu huku akiambiwa ajiandae kwenda shopping ya abayah dubai kwa kisingizio cha kongamano uchwara.
 
Hii nchi wajinga ni wengi sana. Yani kabisa mtu unalinganisha gharama za miaka 17 iliyopita na leo hii?
Mfano mdogo, mfuko mmoja wa cement mwaka 2007 ulikuwa bei gani na leo hii ni bei gani? Kibarua atakayepewa kazi pale atalipwa sawa na 2007? Hapo hatujaongelea skilled labor.

Wakati mwingine ni vyema kutumia akili kabla ya kupinga kila kitu.
Tuelimishane taratibu mbona ulipoachika hatukukunyanyapaa tuliishi na wewe Kwa upendo.
 
Wengi wa wachangiaji wa mada hatujawahi kujenga hata banda la kufugia kuku kwahiyo hatujui uhalisia wa gharama za ujenzi badala yake tumetanguliza ujuaji mwingi ambao hauna maana.
 
Tofauti kubwa mno, nusu ya idadi ya watu watakao kaa ongezeko la bilioni mia mbili, hata kama ilikua 200 sio hivyo isee!
Nondo, cement, mafuta, wages, urembo/nakshi, sehemu za huduma za ndani, thamani/faniture bei ya wakati huo na Sasa vinalingana?
Sikatai kuna weza kuwa na upigaji.
 
Pamoja na kwamba kuna vitu napinga kuhusu huu ujenzi ukianzia chaguo la mkoa, lakini tukumbuke pia hata uwanja wa Mkapa kulikuwa na upigaji mkubwa na kilichopangwa kujengwa hakikukamilika mpaka leo.
 
Mwaka 2007
Us dollar ilikuwa 1400
Leo ni zaidi ya 2500
Nadhani upigaji umo ila sio mkubwa kivile

Wacha tuibiwe japo kidogo
 
Uwanja wa Mkapa ulijengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya #Tanzania na #China, mpango uliopo mezani ni mchakato wa ujenzi wa uwanja mwingine wa kisasa ambao Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo imesema itawasilisha mapendekezo uitwe Uwanja wa Samia Suluhu Hassan.

Pia, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo nayo ilieleza mipango iliyopo ni kuwa Uwanja wa Samia ukamilike kabla ya Mwaka 2027 ili utumike kwenye Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).


Uwanja wa Mkapa
Mkoa: Dar es Salaam
Idadi ya siti: 60,000
Ulizinduliwa: Mwaka 2007
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 56 (Tsh. Bilioni 64 wakati huo)
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: Beijing Construction Engineering Group (BCEG)


Uwanja wa Samia
Mkoa: Arusha
Idadi ya Siti: 30,000
Kuzinduliwa: Kati ya Mwaka 2025 hadi 2027
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 112 (Tsh Bilioni 286) kabla ya kodi
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: China Railway Construction Engineering Group (CRCEG)

View attachment 2940937
View attachment 2940938
Muonekano wa Uwanja wa Samia unavyotarajiwa

View attachment 2940941
Uwanja wa Mkapa​
Angalia gharama zilizotumika kufanya marekebisho ya uwanja wa mkapa (bil 31 )
Kisha angalia gharama zilizotumika kurebisha uwanja wa Amaan Zanzibar kisha jiulize gharama za kujenga uwanja mpya zitakuwaje

Kwa kawaida kwenye mradi wowote Mkubwa wa serikali pesa lazima zipigwe. Hivyo hapo tunaweza kuwa tunaoigwa takribani 15-25% so tuwe wavumilivu
 
ni kweli gharama zimepanda, ila kiuhalisi thamani halisi ya uwanja wenye capacity ya 30k kwa standard zetu ni $60m, haizidi hapo!

kikawaida kiti kimoja kinagharimu $1000 (ndio simple calculation ya viwanja ilivyo), so at maximum uwanja wa 30k unaojengwa tanzania (nchi ambayo maeneo wazi ni mengi wala hulipi fidia) haikutakiwa kyzidi $60m
 
Uwanja wa Mkapa ulijengwa kwa ushirikiano wa Serikali ya #Tanzania na #China, mpango uliopo mezani ni mchakato wa ujenzi wa uwanja mwingine wa kisasa ambao Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu Utamaduni na Michezo imesema itawasilisha mapendekezo uitwe Uwanja wa Samia Suluhu Hassan.

Pia, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo nayo ilieleza mipango iliyopo ni kuwa Uwanja wa Samia ukamilike kabla ya Mwaka 2027 ili utumike kwenye Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).


Uwanja wa Mkapa
Mkoa: Dar es Salaam
Idadi ya siti: 60,000
Ulizinduliwa: Mwaka 2007
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 56 (Tsh. Bilioni 64 wakati huo)
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: Beijing Construction Engineering Group (BCEG)


Uwanja wa Samia
Mkoa: Arusha
Idadi ya Siti: 30,000
Kuzinduliwa: Kati ya Mwaka 2025 hadi 2027
Gharama za Ujenzi: Dola Milioni 112 (Tsh Bilioni 286) kabla ya kodi
Umiliki: Serikali ya Tanzania
Mkandarasi: China Railway Construction Engineering Group (CRCEG)

View attachment 2940937
View attachment 2940938
Muonekano wa Uwanja wa Samia unavyotarajiwa

View attachment 2940941
Uwanja wa Mkapa​
Hivi ni Ujenzi wa uwanja tu, ama pia itahusisha kujenga hayo majengo pembeni ya Uwanja!?
 
Back
Top Bottom