Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?
Sasa ngoja apande hizo korosha zake baada ya kukomaa miaka 5 kisha wenyeji wamuombe hati miliki ya hiyo ardhi, ndio atajua kuwa hajui.
 
Wapi usipokuwa huna pesa ni tamu?? Maisha ya Dar yanareflect maisha ya miji mingi Tanzania tofauti ni ndogo hususani kwenye wingi wa watu ambapo ni added advantage kwa Dar maana Kampuni nyingi zinafunguliwa na fursa za biashara.
 
Kijana wa daslam mafanikio kwake ni kumiliki samsung au iPhone, hata iwe ya laki 2 tu inatosha ilimrad isiwe tecno anaona katoboa, hapo anatafuta suruali fupi anavaa na viatu bila soksi, akipata earphone ya buku 3 na mewani nyeusi, akawa na account twitter basi ye hapo anaanza ukuda
 
Watu wa dar wana magumu sana basi tu
 
Hili la kupewa ardhi umenikumbusha mbali, mwaka 2011 nilienda Songea nikakutana na rafiki yangu mtumishi wa Uma ananiambia anamiliki acre zaidi 1,000 nikimwangalia hali yake ya kifedha hailingani kabisa na hizo heka maana nilikuwa nafananisha na bei za ardhi mikoa ya kaskazini.

Kuja kugundua kumbe yule mshenzi alinunua kwa 25,000 tu kwa heka na zingine kama kumi alipewa bonus ya kukalibishwa kijijini.
 
Aliyekwambia Tanzania haina wenyewe ni nani ?

Muulize yule Rwegasira aliyelima Vanilla kule Bukoba sasa hivi anashangaa.., Au Yule Namungo Chemtwara unadhani alivyokuwa analalamikia bei ya Korosho ipo chini gharama zake za dawa n.k. hazijarudi unadhani anapenda malalamishi ?!!!!

Tatizo watu mmekuwa brainwashed Makosa ya watunga Sera kutunga Sera mbovu yanahamishiwa kwa wabangaizaji wanaojitahidi kila kukicha mkono uende kinywani (tena bila kulalamika) sasa hizi kejeli nadhani ndio zitawafanya waseme enough is enough....
 
Watu wa dar wana magumu sana basi tu
Huo ndo ukwel Maisha ya dar ya kwenye media na uhalisia ni vitu tofauti wanaoishi maisha mazuri ni wachache asilimia kubwa maisha ni magumu kwenda kuoga inabidi uende na shuka lako ndo utundike iwe mlango wa bafu, hao ndo wanatakiwa waondoke watafute fursa mikoani ili kupambana na umasikini.
 
Samsung na iphone zinamilikiwa na vijana wa dar tu? Mbona Tecno, infinix na Itel zinatumiwa na vijana wengi Dar es salaam..

Sasa kama wachumi wameligrade jiji la Dar kama jiji la kibiashara ambalo linaimpact kubwa kwenye uchumi wa Tanzania unaanza kudiss kwa kutumia maisha ya vijana wachache waliamua kuishi lifestyle zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…