Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Umerogwa sio bure: Unang'ang'ania Dar es miaka mingi, kula kwa shida, kulala kwa shida, unasafiri kwa shida huku kuna ardhi Tanzania haina mwenyewe

Wazoefu wa kushika bomba kwenye daladala hawatakuelewa, wao kuamka saa 10 alfajiri kulala saa 6 usiku kama majinga.
#kataadaladala

Daladala ni kero

Daladala ni mateso

Daladala ni unyanyasaji

Daladala ni umaskini

Daladala ni usafiri wa makapuku na watu wa hovyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.
HII NI 99% ya wanaoanza kupambana tanzania haipigwi hatuna tofauti na vifaa vilivyopo stoo.
 
#kataadaladala

Daladala ni kero

Daladala ni mateso

Daladala ni unyanyasaji

Daladala ni umaskini

Daladala ni usafiri wa makapuku na watu wa hovyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama mazombi
Screenshot_20230817-182414.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bila salamu nawapa ujumbe wenu enyi watu.

Mnaweza kusema kuwa najiinua au nawakashifu ila Mimi siko huko. Ni upendo tu.

Waarabu wanasema fikisha ujumbe hata kama ni mchungu.

Miaka 5 inatosha kabisa mtu kupima bahati ya maisha Dar es salaam au mahali popote.

Unaishi Dar miaka zaidi ya 5 huna nyumba, huna kiwanja, kula kwako ndo kule unatafuta leo ili ule leo, kila siku kwenye daladala wewe ukichomoa pesa kubwa basi buku 2.

Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.

Tanzania hii kuna mahali kama Liwale huko Lindi ukifika kijiji chochote ukiomba ardhi ya kujenga au kulima unapewa bure kabisa. Yet wewe uko dar hata hatua 4 za ardhi Chanika huna . Umerogwa shituka

Kijijini wenzako wenye bidii wanamiliki pikipiki, gari, guta, nyumba, duka nk.

Kijijini ni bidii zako tu. Mjini kuna pesa kuliko kijijini ila kama kila ukihangahika huzipati za kukukwamua ni vyema utafute chimbo kijijini.

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?

Nakuuliza wewe unayelipwa laki 2 na Mwindi.
Upewe maua yako.
 
Bila salamu nawapa ujumbe wenu enyi watu.

Mnaweza kusema kuwa najiinua au nawakashifu ila Mimi siko huko. Ni upendo tu.

Waarabu wanasema fikisha ujumbe hata kama ni mchungu.

Miaka 5 inatosha kabisa mtu kupima bahati ya maisha Dar es salaam au mahali popote.

Unaishi Dar miaka zaidi ya 5 huna nyumba, huna kiwanja, kula kwako ndo kule unatafuta leo ili ule leo, kila siku kwenye daladala wewe ukichomoa pesa kubwa basi buku 2.

Unalala store (jiko, meza, sofa, feni, kitanda, pasi, bag la nguo na vitu vingine vyote ukifungua macho tu hivi hapa.

Tanzania hii kuna mahali kama Liwale huko Lindi ukifika kijiji chochote ukiomba ardhi ya kujenga au kulima unapewa bure kabisa. Yet wewe uko dar hata hatua 4 za ardhi Chanika huna . Umerogwa shituka

Kijijini wenzako wenye bidii wanamiliki pikipiki, gari, guta, nyumba, duka nk.

Kijijini ni bidii zako tu. Mjini kuna pesa kuliko kijijini ila kama kila ukihangahika huzipati za kukukwamua ni vyema utafute chimbo kijijini.

Braza alifika kijiji fulani kuuliza ardhi ya kulima huko chobingo akapewa upana wa hekari 5 urefu ajipimie mwenyewe.

Kama akilima hekari 40 na kupanda mikorosho baada ya miaka 5 atakuwa wapi?

Nakuuliza wewe unayelipwa laki 2 na Mwindi.
Huu ni ukweli mchungu sana, ardhi kwa ajili ya kilimo bado inapatikana kwa bei rahisi sana maeneo mengi ya nchi hii, naona maeneo mengine wakenya wanakuja kuchukua kwa njia ya uwekezaji sisi vijana tumejazana Dar,Arusha, na Mwanza tunashangilia na kubishana kuhusu Simba na Yanga.

Siku tukija kushtuka ardhi yote imeenda kwa wageni au inamilikiwa na wachache kisha vizazi vyetu vinaenda vibarua vya kupalilia dengu.
 
Kijana,

Kwa upande mwngne umenena vyema,

Kimsingi dar hapana utulivu kabisa,na uspokua mwangalifu unaweza kujikuta kipato chote kinishia kwenye matumiz na muda unazd kwenda .

Tuwe waangalifu mujini,yapo maisha mengne nje ya dar…yasiyo na mahangaiko mengi
 
Huu ni ukweli mchungu sana, ardhi kwa ajili ya kilimo bado inapatikana kwa bei rahisi sana maeneo mengi ya nchi hii, naona maeneo mengine wakenya wanakuja kuchukua kwa njia ya uwekezaji sisi vijana tumejazana Dar,Arusha, na Mwanza tunashangilia na kubishana kuhusu Simba na Yanga.​
INASIKITISHA SANA

Vijana wanahangaika na kuomba kazi zisizo na uhakika ajira portal hata buku mfukoni ni changamoto wanasubiria ajira ya 750k per month utakuta wengine huu mwaka wa tatu na zaidi yuko home anasubiri kuitwa kwenye interview nafasi 2 wanaofanyiwa interview 200

Wakati kuna kijana mwenzao sasa hivi anauza gunia moja la vitunguu 350,000 pale soko la Ilala hapo alilima heka 1 akatoa magunia 80

Tanzania ina vijana wa hovyo sana. Sekta ya kilimo na biashara ya mazao kuna fursa sana.

Tatizo vijana hawatembei, hawataki kujifunza kuhusu kilimo, wanachojua ni kwenda Kidimbwi na Kitambaa Cheupe

Kukodi shamba la ekari 1 maeneo yenye ardhi nzuri ya kilimo na baadhi unaweza kufanya hata irrigation hapa Tanzania ni 30,000 mpaka 70,000

Huwa nashangaa kijana anatoka mkoa wenye ardhi nzuri ya kilimo anakuja kuwa boda au machinga Dar
 
Back
Top Bottom