Umeshawahi kupiga One katika levo yoyote ya elimu? Tukutane hapa

Umeshawahi kupiga One katika levo yoyote ya elimu? Tukutane hapa

Msijipe moyo. Waliopiga one wengi wao wana maisha mazuri. Sema wengi wanaishia middle class. Wenye one wengi wao kufika daraja la juu kabisa ni changamoto. Huishia lile daraja la kuwa na nyumba moja, gari moja kama crown, spacio na jamii hiyo pamoja na familia inayoishi kizungu. Wale wa div three kushuka chini wengi wao huwa daraja la chini kabisa kimaisha na wachache huwa daraja la juu kabisa... hawakaagi katikati.
Bonge la Point Mkuu..
 
Maisha yangu ya Elimu yalikuwa Kawaida.. sijatoka Familia ya Kisomi.. ila I was certainly fast learner.

Shule ya Msingi nilitandika A wastani.. sikuwahi tumia nguvu kabisa ati nasoma. Basi tu nilikuwa najua.

Olevel Nilivoingia ngeli ilinipa shida kiasi kwamba nikabase saana.. na Physics (Engineering Science) na Maths.. Kufika Form Four sikuwa nashikika.. nikatia Kijiti.. sikuwa wa kwanza kutokana na nature ya shule ila nilikuwa top 10.

I was proud ukizingatia akili za kitoto, Advance nikaenda PCM.. sikugusa Pindi hata kidogo yaani.. niliingia shule kichwa kichwa.. ila kwa kuwa I was curious nilikuwa na viconcept kadhaa.. niliipenda saana Physics na Namba.. ila mitihani nikawa sitoboi.. nikipata saaaana ni 50,

Chemistry nikipataa saana ni 42.. Namba ndo nilikuwa napiga hizi 80, 90 ilikuwa kawaida.. (si mnajua namba haihitaji akili nyingi.. mazoezi tu)

Kufika ile first semester ya form six nilikuwa sifai.. Darasani naogopwa hata na wale walioshiba Mapindi ya Mjini.. ujue hapo mie ni msuli yatimaa yaani.. concept unaanza nayo from zero Mpaka unaelewa.. kitu inaitwa Calculus nilikuwa sifai.. Mpaka namaliza shule nilishindwa integral moja tu katika maisha yangu ya Alevel nayo ni integral ya Root ya SinX ila baadaye nikaja gundua haina integral lazima uaply numerical.

Physics ndo kabisa.. nilikuwa sifai.. ila sikuwahi iamini Physics

Ujinga wa Physics bhana inakubadilikia saa yoyote, ila nikawa Mjanja, Topics zote zenye nature ya umeme kama Tonics,Tism na statics swali halichomoi.

Achana na Dimension, sjui simple harmonic mara circular, hizi zilikuwa easy..

Utata ni Projectile asee.. Hakuna Topic Ngumu ya Physics kama Projectile..

Finally nilitia Adabu Necta.. Kijiti nilitia ila Mpaka leo najuta kwanini Physics nipate B.. wakati nilikuwa naiona A.

Baada ya Hapo nikaenda Mlimani kupiga Civil..

Those were the days..

My take: Matokeo bhana yanakuwa exciting pale unapokuwa mwanafunzi.. shule ikiisha matokeo hayana umuhimu tena.. kwenye kazi hizi za CV ni rare saana.. unaweka matokeo, asilimia kubwa wanahitaji tu CV relevant na kazi husika.
 
Nilipiga I ya Point 18 Ordinary Level Yombo Tech
Nilipiga I ya Point 09 Advanced Level HGL huko Kantalamba
Nilipiga GPA ya 3.2 Lower Second UDSM
.
.
Nimepoteza miaka 9 shuleni nilivyorudi kitaa waliofeli O' Level wamefanikisha yafuatayo;
1. Wana Biashara zilizoshamiri;
2. Wamejijenga kiuchumi na kimaisha;
3. Wamejijenga Kijamii;
4. Wamejijenga Kisiasa;

Kwa UFUPI;
Nimeajiriwa na Classmate wa STD VII ambaye hajui mlango wa darasa la Sekondari wala Chuo.
.
.
Nimezunguka na bahasha za khaki mpaka zikiniona tu zinalowa jasho;
.
.
Kila nikiwasikiliza wabunge wa JMT roho inamani kuchomoka!!
Kumbe 1 ishafika point 18

Sent using Jamii Forums mobile app
 
shule ya msingi sikufaulu ,nikaenda shule za wazazi o level nikapata one ya 13 , A level nikapata one point 4 ( CBG) ,chuo nikamaliza na ufaulu mzuri tu.

Nikili tu kuna jamaa zangu tulifail pamoja wakaanza biashara ya kuuza samaki na wengine biashara za nguo na nafaka .nikili tu jamaa wako mbali sana kunizidi na wako na pesa nyingi .

Lakini sijutiii kwenda shule hawa jamaazangu hawajiamini kabisa katika maisha wana hofu sana na maisha

Ila pia wengi waliofail wanaishi maisha magumu sanaa kupitiliza

Mpango wangu lazima hii elimu niitendee haki ,lazima nibadili hizi " A" kuwa pesa na fursa kwangu na kwa wengine

Wito kwa wasomi " tupambane tuoneshe utofauti "
Eti hawajiamini.... Kuna watu wanao jiamini kuliko wenye pesa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera sana, shule zilizokuwa zinaitwa za vipaji maalumu niliishia kuzisikia kwenye soga
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] katika familia yetu tumezaliwa watatu wote tumesoma shule kongwe mixer private

Mimi nimepiga technical school ,wengine wamepiga hizo special mmoja kagonga ya tabora mwingine ya moro
 
O-level, nikapelekwa vipaji PCB,
Kwa mara ya kwanza nilijuta kufaulu kwa shughuli niliyokutana nayo kule.

Matokeo nayo yalivyotoka......😂😂😂😂.
Sitaki mazoea humu.

Anyway
Nasajili laini kwa alama za vidole,
Naunganisha Line za chuo,
Narudisha line zilizopotea,
Naweka liquid protector
Nabadilisha ringtones,
Nasafisha nyota,

😂 😂 😂
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] katika familia yetu tumezaliwa watatu wote tumesoma shule kongwe mixer private

Mimi nimepiga technival school ,wengine wamepiga hizo special mmoja kagonga ya tabora mwingine ya moro
Nilibahatika kusoma shule kongwe, ila zilizokuwa zinaitwa za vipaji maalum zilizitamani sana ila sikubahatika.

Katika familia niliyokulia mabroo 2 walienda Tobora na Mzumbe, walini inspire sana, ila uwezo ulikuwa mdogo.

Madogo 2 wa mwisho ambao walisapotiwa na hao 2 hapo juu, wao walibahatika kuchagiliwa Ilboru na Kibaha, lakini kwao haikuwa jambo la kushangaza kwani ule maarufu wa vipaji maalumu ulikuwa umezoeleka na kuyeyuka ikawa jambo la kawaida.

Binafsi nilipopata matokeo enzi hizo wanaita kupass ilikuwa yanatoka pamoja na shule uliyochagulia, nikawa nimechaguliwa hiyo shule kongwe ya bweni, nilifurahi sana sikupata usingizi siku hiyo,nilikuwa nawaza na kuvuta picha ya mazingira nitakayoyakuta pamoja na maisha ya bweni kwa ujumla.

Huu mzuka aliwahi kuuelezea Infantry Soldier
 
O-level, nikapelekwa vipaji PCB,
Kwa mara ya kwanza nilijuta kufaulu kwa shughuli niliyokutana nayo kule.

Matokeo nayo yalivyotoka......[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Sitaki mazoea humu.

Anyway
Nasajili laini kwa alama za vidole,
Naunganisha Line za chuo,
Narudisha line zilizopotea,
Naweka liquid protector
Nabadilisha ringtones,
Nasafisha nyota,
Hahahahahaaa, wee jamaa umenichekesha sana hadi machozi yamenitoka hapa.

Mziki wa PCB sio wa kitoto kabisa
 
Nilibahatika kusoma shule kongwe, ila zilizokuwa zinaitwa za vipaji maalum zilizitamani sana ila sikubahatika.

Katika familia niliyokulia mabroo 2 walienda Tobora na Mzumbe, walini inspire sana, ila uwezo ulikuwa mdogo.

Madogo 2 wa mwisho ambao walisapotiwa na hao 2 hapo juu, wao walibahatika kuchagiliwa Ilboru na Kibaha, lakini kwao haikuwa jambo la kushangaza kwani ule maarufu wa vipaji maalumu ulikuwa umezoeleka na kuyeyuka ikawa jambo la kawaida.

Binafsi nilipopata matokeo enzi hizo wanaita kupass ilikuwa yanatoka pamoja na shule uliyochagulia, nikawa nimechaguliwa hiyo shule kongwe ya bweni, nilifurahi sana sikupata usingizi siku hiyo,nilikuwa nawaza na kuvuta picha ya mazingira nitakayoyakuta pamoja na maisha ya bweni kwa ujumla.

Huu mzuka aliwahi kuuelezea Infantry Soldier
Kuna utamu Fulani kusoma hizo shule kongwe

Juzi Kati nilienda shule moja kongwe iko pale Tanga mjini Ina advance tu aisee shule imekuwa Tamu balaa ukarabati wa Ile shule unaweza dhani Ni chuo [emoji15]

Staff office Kuna Hadi kiyoyozi na masofa ya ngozi huko njee ndio Usiseme .

Ni shule kongwe viongozi wengi maarfu wamesoma pale
 
Kuna utamu Fulani kusoma hizo shule kongwe

Juzi Kati nilienda shule moja kongwe iko pale Tanga mjini Ina advance tu aisee shule imekuwa Tamu balaa ukarabati wa Ile shule unaweza dhani Ni chuo [emoji15]

Staff office Kuna Hadi kiyoyozi na masofa ya ngozi huko njee ndio Usiseme .

Ni shule kongwe viongozi wengi maarfu wamesoma pale
Shule nyingi kongwe zilifanyiwa ukarabati kipindi cha mwendazake.

Mimi pia nilitembelea shule yangu ya Advance mwaka juzi nilikuta imekuwa nzuri sana baada ya ukarabati
 
Kuna watu wanaushambulia huu uzi utadhani kufaulu ni dhambi [emoji16][emoji16][emoji16]

Problem talk creates problems. Solution talk creates solutions

Ingependeza kama tungejikita zaidi kwenye kujadili nini kifanyike badala ya kujadili kila leo matokeo mabovu ya elimu yetu.
Je nini kifanyike? Watu wasisome? Na wewe unayeona elimu ni mbovu hutapeleka watoto wako shule? Hata mtoto wako Akipata ONE kali O level na A level hutampeleka chuo?

Na wengi wanasahau kwamba mtoto kutokwenda au kutofaulu darasani sio guarantee ya kufanikiwa kifedha. Kama ambavyo kufaulu darasani sio guarantee kufanikiwa kifedha

Anyway, O level one Ya 14 na A level one ya 6. A level Physics "A"[emoji16]
 
O- level nilifanikiwa kupata div. pointi 16. Huko mbele nikashuka. A level div. II, point 10. Chuo kikuu, GPA 4.1. Kazi iendelee....... na inaendelea.
 
Kuna watu wanaushambulia huu uzi utadhani kufaulu ni dhambi [emoji16][emoji16][emoji16]

Problem talk creates problems. Solution talk creates solutions

Ingependeza kama tungejikita zaidi kwenye kujadili nini kifanyike badala ya kujadili kila leo matokeo mabovu ya elimu yetu.
Je nini kifanyike? Watu wasisome? Na wewe unayeona elimu ni mbovu hutapeleka watoto wako shule? Hata mtoto wako Akipata ONE kali O level na A level hutampeleka chuo?

Na wengi wanasahau kwamba mtoto kutokwenda au kutofaulu darasani sio guarantee ya kufanikiwa kifedha. Kama ambavyo kufaulu darasani sio guarantee kufanikiwa kifedha

Anyway, O level one Ya 14 na A level one ya 6. Physics "A"[emoji16]
Hongera mkuu banda la Phyz Advance
 
Na mimi nilibahatika kuzi nyatia pale Nyabulogoya sec Mwanza na Ngudu high school Kwimba😁😁😁

E7F71FA4-5C7C-404C-8985-49566DAE7EA2.jpeg


5DA7D2FB-AEF3-44FC-AFBB-C592511434EA.jpeg
 
Back
Top Bottom