Umewahi kuchapwa/kupigwa na mzazi/mlezi?

Wamama wote tuko hivyo
 
Pole mkuu Mungu akutie nguvu,wazazi ni wa kuwaombea saanaa huwa tunakufa na tai shingoni inatesa familia nzima
 
Poleeee
 
Mungu akutie nguvu ndugu yangu
Asante ndugu, nilishasamehe na mungu amweke mahali pema peponi, kipigo wanaohadithia huku bado sana, Unasahau ilipo soap dish unapigwa bila nguo[emoji24] uchi kabisa, Wao bia mwendo mdundo Nyumbani ugali na mchicha aisee!! Nawashukuru sana kunisomesha mana nahisi nisingestarabika. Nimejiahidi kutouvunja moyo Wa mwanangu awae yote na hata Wa pembeni.
 
Uwiiiii BASE
 
Mama alikuwa master wa leather belt ass whooping,mdingi mpole so yeye alikuwa ni vifinyo tu.Kipigo cha mzazi shurti ulie na uonyeshe kuwa unaumia asa ww jifanye nunda.Uzuri wazazi wangu walikuwa hawachapi ovyo ovyo ni vile tu nlikuwa mtundu sana.walikuwa wanakuhesabia makosa tu ukifanya mara moja unakemewa tu ikifika mara ya tatu lazima uchezee kipondo cha kibabe.

Nakumbuka kichapo kikubwa nlichowahi chezea ilikuwa sababu ya kucheza msikitini wakati wa swala,ebana mzee aliniwamba balaa,tena fimbo nliambiwa nkachume mwenyewe.kuanzia siku hyo mpaka leo nikiingia msikitini nakuwa na utulivu wa ajabu(ushuiy).
 
Wazazi wana aina tafauti tafauti za uchapaji
-Kuna ile anakuchap huku anakusema na kukutajia kosa ulilolifanya alafu mwishowe anakuuliza "utarudia tena?" huku kichapo kinaendelea ukisema sirudii anauliza tena kwa msisitizo "UTARUDIA?"mpka aridhike na jibu lako ushachezea nyingi
>Aina nyengine ni ile unapigwa huku uko kwenye movement(freestyle),unachapwa mkwaju wa mguu ukishika mguu unalambwa ya mgongo,ukirudi nyuma unayo,ukienda mbela imo mara mnaanza kuzunguka kama mduara huku mikwaju inaendelea alimradi tu mko kwenye motion.
>Nyengine ni ile ya kimya kimya,yaani anayekuchapa haongei kitu na hataki unayechapwa ulie,unachapwa kiafsa,mara nyingi hiiq ni kwa wale wanaokaa nyumba za kupanga au mzazi asiependa ijulikane kama anakuadhibu
 
Daaa nakumbuk cku moja tumezngua mimi na kaka na dgo anaenifata,,,sas maza alivkua mtata akataft fimbo ote watatu, tukakimbia ,mimi kwa ujinga wangu hata kabla hasira hazijamuish bi mkubwa nikasema aaah ngja nirud kwan atanifanyej,,, mamaaaa!!!! nlikutana na jiwe usoni kiasi kwamba nikalal apoapo nilpokua huku damu zinamwagika usoni,,,ila damu ni nzito kuliko maji coz yy mama huyohuyo nd alini take care mpk nkarud kweny hali ya kawaida ,,,tangu cku ile mama akiwa amekasirka mimi nakaa mbaliiii yasije jirudia ya kipindi ichooo ,,,yote kwa yote nampenda sana mama yangu kunifundsh mengi
 
Hivi wazazi wa kipindi hiki wanapiga watoto kama zamani? Mimi nimepigwa ila kuna rafiki wakati tupo shule ya msingi alipigwa na mzee wake sijawahi kuona kipigo kile ingekuwa leo yule mzee jela ingemuhusu kabisa jamaa aliletwa shule hawezi kutembea amekatwa sikio, alama za visu mgongoni na bado akampiga mbele ya mwalimu mkuu walimu wakamuombea msamaha jamaa angekufa. Wakati mwingine wazazi wetu walitumia vibaya nguvu zao kutuabuse. Mada imenigusa mno
 
Wazazi wengine sijui wakoje wamelaaniwa[emoji19] [emoji19]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…