Umewahi kukuta watu wanakula chakula gani ukakishangaa?

Umewahi kukuta watu wanakula chakula gani ukakishangaa?

Niliwahi poteza demu niliye mzima baada ya kuona anakula utumbo wa kuku,na ikawa mwisho wa uhusiano hapo hapo😂
Acha basi ...utumbo wa uku Tena umeviringishwa wenye firigisi au maini ya kuku....utamu mpaka kisogoni....
 
Mnaenda Mbali sana yanii,mimi hadi na leo hii sijawahi kuwaelewa watu wanaokula MLENDA aina yoyote ya MLENDA hata ungekua unakatiwa katiwa ndani noti za ten ten,nisingewahi thubutu kula.

Hadi na Leo hii sijawahi waelewa Walevi wanaotumia vinywaji vikali (ngumu kumeza) sijawahi waelewa na sitoacha washangaa wanakunywa wanapata ladha gani.

Nimeshawahi onja sana vinywaji vyao ila hamna ladha naiona zaidi ya mateso kwenye kumeza mpka harufu.

Nyie mnaokunywa vilevi vitamu vitamu sina mashaka nanyi, Tuko pamoja eneo hilo.

Ila Mshangao wangu ni zaidi kwa wale wanaokunywa tena za bei ndefuuu achana na vi common vya mtaani kwa mangi, Naongelea maboss wa ma grants na madude hatari hatari. Mnanisurprise kila iitwayo leo.
 
Acha basi ...utumbo wa uku Tena umeviringishwa wenye firigisi au maini ya kuku....utamu mpaka kisogoni....
Najua kwa Mbagala,buza,yombo Manzese, Buguruni kila mtu atanishangaa,japo ni mboga pendwa ongeza na Ngwara na vichwa ila ndivyo ni livyo kinyaa nje nje🤔
 
Ugali wa mtama ulichanganywa na ulezi ni ugali mweusi km mkaa alafu Mchungu sio km Dona, yaan hata ukichanganya mahindi na mtama ugali unatoka mweusi mpauko alafu unakua na ladha fulani ya uchungu uchungu
 
Kuna sista duu wa masaki alikuja home akashangaa nakula ugali maharage akauliza hapa kuna shule ya boarding?

Iringa kuna mboga inaitwa mkalifya,na uroho wangu wote nilichemsha, ni chungu kuliko uchungu wenyewe
Hapo kwenye mkalifya, jamanii kamboga nakapenda sanaa ngoja nirudi iringa but kipindi cha mvua ndo inakua nyingi.
 
Matembele enzi hizo sikuyafahamu wala sikujua kuyatofautisha na marando nilipokuta yamepikwa sehemu nikashangaa kuwa wanakula marando(majani ya ambayo mizizi yake inatoa viazi vitamu)
Usukumani hata mim nlishangaa eti hawajui kama tembele nimboga wao wanaita malando
 
Back
Top Bottom