Umewahi kukuta watu wanakula chakula gani ukakishangaa?

Umewahi kukuta watu wanakula chakula gani ukakishangaa?

Niikuta wameloweka ngozi ya ng'ombe kwenye maji kesho yake mchana ikatolewa ikakwanguliwa manyoya ikakatwa vipande ikapikwa iliwa usiku. Bahati nzuri nina alergy ya nyama nyekundu kwahiyo nikapata excuse ya kutokula ile mboga
 
Majani ya maharage iringa huko, nilishangaa ila nilivyo onja nikaona mbona fresh tu. Kwetu singida majani ya maharage hayaliwi.
Na mi kwa mara ya kwanza niliyaona mbeya yanapikwa kama mboga nikala nlikua ugenini nliona yako poa. Na kukaa SGD mboga iliyonishinda ni moja tu mlenda.
 
Na mi kwa mara ya kwanza niliyaona mbeya yanapikwa kama mboga nikala nlikua ugenini nliona yako poa. Na kukaa SGD mboga iliyonishinda ni moja tu mlenda.
Japo mimi wa singida ila mlenda hapana aisee! Japo kuna watu wanaupenda "kweri kweri", namshukuru Mungu kwangu baba nanii nae hauelewi kwahiyo haupikwi kabisa. 😅
 
Kweli tembea uone
Nilikwenda Bangkok nikawa natembea usiku barabarani ambapo ndio kumekucha kwa mama lishe yaani vyakula ambavyo maisha yangu sijaona watu wanakula ila baadhi tu

Nimeona Meza wakiuza panzi wa kukaanga, mende wale wakubwa wa mabuchani ( sio wa chooni) hawa ni weusi
Pia nimeona mapaja ya vyura, popo wakiwa wamebanikwa mpaka unatamani uonje

Yaani ni mitaa mizima wamejaa na wao wanavyofakamia
Nimeona nyoka wa kila aina wakipikwa mchuzi na wa kukaangwa

Nge ndio usiseme kuna wengine wanachanganya wadudu tofauti tofauti
Unaona kabisa wanavyo enjoy kama sisi kwenye mishikaki

Kwa sasa demand ni nyingi sana wamejiongeza na kutengeneza sehemu za kuwalea na kufuga aina zote za wadudu
37cac1a3-e8bd-4466-8a8b-10aa7bfe0b51.jpg
Weird-food-of-Thailand-Insect-dishes.jpg
imag2376.jpg
feyb7x.jpg
 
Kuna sista duu wa masaki alikuja home akashangaa nakula ugali maharage akauliza hapa kuna shule ya boarding?

Iringa kuna mboga inaitwa mkalifya,na uroho wangu wote nilichemsha, ni chungu kuliko uchungu wenyewe
Mimi mchunga ulinishinda.
Unakula mboga kama unakula dawa.
 
Kweli tembea uone
Nilikwenda Bangkok nikawa natembea usiku barabarani ambapo ndio kumekucha kwa mama lishe yaani vyakula ambavyo maisha yangu sijaona watu wanakula ila baadhi tu

Nimeona Meza wakiuza panzi wa kukaanga, mende wale wakubwa wa mabuchani ( sio wa chooni) hawa ni weusi
Pia nimeona mapaja ya vyura, popo wakiwa wamebanikwa mpaka unatamani uonje

Yaani ni mitaa mizima wamejaa na wao wanavyofakamia
Nimeona nyoka wa kila aina wakipikwa mchuzi na wa kukaangwa

Nge ndio usiseme kuna wengine wanachanganya wadudu tofauti tofauti
Unaona kabisa wanavyo enjoy kama sisi kwenye mishikaki

Kwa sasa demand ni nyingi sana wamejiongeza na kutengeneza sehemu za kuwalea na kufuga aina zote za wadudu View attachment 2582049View attachment 2582050View attachment 2582051View attachment 2582052
Uyole kuanzia miaka ya 2005 kushuka chini kabla hapajachangamka wenyeji walikuwa wanakula wale panzi wakubwa wanaita paralila wenyewe, na mapanya makubwa hivi yanapenda kula viazi shambani.
 
Hapa ndio utajua swala la vyakula ni tamaduni tu,swala nini kiliwe kipi kiachwe inategemea umezaliwa ukakuta jamii yako inakula nini.mpaka sasa nimgundua kisicholiwa ni sumu tu.
Ukiwa unaogopa kabisa funza,morogoro kuna SONDO wapo kwenye magogo.wanaliwa vizuri kabisa ila kimwonekano ni kama wale funza weupe wa kwenye udongo msimu wa mvua.
 
Kwa mara ya kwanza nakaribishwa ugali na kibwando(machoma nguo) aisee nilishangaa sana nikasema nisiishie kushangaa wacha nionje nilijikuta mkurungwa mimi nagombana na waliniokaribisha waniachie bakuli lote wao watafute mboga nyingine. The same to mchunga
 
Nyama ya ng'ombe mbichi, yani watu wamebeba sahani wamesimama zizini pale ng'ombe kachinjwa wakapewa nyama wakakaa kula.....nlihisi kichefuchefu
 
Mi nikishangaa kuona watu wanakula yale majani ya magimbi.
Majani flani hivi mapana hivi, nikishangaa kumkuta jirani anayaandaa kwa kupikwa.

Kumuuliza anasema yanaliwa ila sio yale yaliyokomaa sana.
Majani ya Magimbi kule Tukuyu ni mboga, inaitwa Lyombo.
Mimi mpaka leo nashangaa watu kula ugali wa unga wa mahindi.
 
Back
Top Bottom