Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Umewahi kula upupu?Sijawahi kukutana na chakula nisichokijua!
Kwetu tunaita "mangatungu" ni matamuu balaaa.Umewahi kula upupu?
Mangatungu na upupu tofauti. Show ya upupu usichukulie poa.Kwetu tunaita "mangatungu" ni matamuu balaaa.
Wewe si mtanzaniaMajani ya Magimbi kule Tukuyu ni mboga, inaitwa Lyombo.
Mimi mpaka leo nashangaa watu kula ugali wa unga wa mahindi.
Naijua hiyo halafu unakuta mtu anaila anasifia kabisa kuwa ni tamu.Kuna sista duu wa masaki alikuja home akashangaa nakula ugali maharage akauliza hapa kuna shule ya boarding?
Iringa kuna mboga inaitwa mkalifya,na uroho wangu wote nilichemsha, ni chungu kuliko uchungu wenyewe
Uyoga ni mzuri bwana. Ni kama nyama tu.Uyoga wa kukausha wametia na karanga Kama maini vile afu wenyewe wanaenjoy kinoma
Tukuyu wanaishi sana wanyakyusa wasafwa huko sio sana.Tukuyu uko
Yale yenye manyoya hayaliki ni yale yanayopatikana kwenye miembe yanakuwa hayana manyoya yanakuwa makubwa sana.Zambia wanakula yale mawashawasha yenye manyoya yanayowasha Yana rangi rangi halafu yanatisha na tukuyu wanakula panya buku.
Hii tabia nilikutana nayo Moshi aisee. Kwanza picha linaanza naletewa nyama mbichi nile aisee nikasema nitasubiria ya kuchoma Asante mzee. Nikaletewa damu mbichi nikachomoa, round ya tatu nikaletewa damu imechemshwa na supu ikabidi ninywe tu ili nisije onekana nadharau.Nyama ya ng'ombe mbichi, yani watu wamebeba sahani wamesimama zizini pale ng'ombe kachinjwa wakapewa nyama wakakaa kula.....nlihisi kichefuchefu
Mbwembwe hii mboga na samaki namaliza ugali plate nne.Mie niliona Lushoto wanakula majani ambayo huwa tunalisha sungura (wao wanaitwa mbwembwe ama kavovo)
Hili suala la Kula ngozi ya ng'ombe watu wengi wanakula ila ukimuuliza kabla hajatambua hujifanya kuwa hawezi Kula na inaliwa sana sanaNiikuta wameloweka ngozi ya ng'ombe kwenye maji kesho yake mchana ikatolewa ikakwanguliwa manyoya ikakatwa vipande ikapikwa iliwa usiku. Bahati nzuri nina alergy ya nyama nyekundu kwahiyo nikapata excuse ya kutokula ile mboga
Wala 🐌,konokono wote,wala mende wote,wala panya wote,wala nyau wote,wala wou wote nawashangaa na wafananisha na mnyama,🦁(Animals)🤔🤔🤔Tembea ujionee, kwenye jamii kuna vyakula vya aina tofauti tofauti, kuna vingine vya unaona kabisa ni vya ajabu ila jamii husika inakula na kuvifuhia kabisa.
Nimewahi kwenda kijiji fulani nikakuta wanakula majani fulani ambayo kwetu tunayatumia kama maua ila kwao ni mboga pendwa kabisa.
Pia mara ya kwanza kuja Pwani na kukuta watu wanakula mchunga kama mboga napo nilishangaa sana kwa kuwa kwetu ni majani ya kulisha sungura si chakula cha binadamu.
Vivyo ivyo kuna watu wanakuja kwetu wanashangaa kukuta tunakula baadhi ya vitu kama askari wa mchwa na tunafurahia utamu wake kabisa nk.
Umewahi kuona chakula gani kwenye jamii ya ugegenini ukashangaa kujua kuwa ni chakula?
View attachment 2568383
Askari wa mchwa
Hata wewe ni mnyama.sio kufananisha...sisi ni wanyamaaaaaaWala 🐌,konokono wote,wala mende wote,wala panya wote,wala nyau wote,wala wou wote nawashangaa na wafananisha na mnyama,🦁(Animals)🤔🤔🤔
kwenu wapi?Majani ya maharage iringa huko, nilishangaa ila nilivyo onja nikaona mbona fresh tu. Kwetu singida majani ya maharage hayaliwi.
Niliwahi poteza demu niliye mzima baada ya kuona anakula utumbo wa kuku,na ikawa mwisho wa uhusiano hapo hapo😂Watu wana kula utumbo wa kuku na vichwa vya kuku, punda na panya kweli kweli, ni likua nasikia tu ila nilishuhudia mwenyewe......