Umewahi kukuta watu wanakula chakula gani ukakishangaa?

Umewahi kukuta watu wanakula chakula gani ukakishangaa?

Nilikuta watu wanakula aisee nilishangaa.
 
Kuna sista duu wa masaki alikuja home akashangaa nakula ugali maharage akauliza hapa kuna shule ya boarding?

Iringa kuna mboga inaitwa mkalifya,na uroho wangu wote nilichemsha, ni chungu kuliko uchungu wenyewe
Naijua hiyo halafu unakuta mtu anaila anasifia kabisa kuwa ni tamu.
 
Zambia wanakula yale mawashawasha yenye manyoya yanayowasha Yana rangi rangi halafu yanatisha na tukuyu wanakula panya buku.
Yale yenye manyoya hayaliki ni yale yanayopatikana kwenye miembe yanakuwa hayana manyoya yanakuwa makubwa sana.
 
Nyama ya ng'ombe mbichi, yani watu wamebeba sahani wamesimama zizini pale ng'ombe kachinjwa wakapewa nyama wakakaa kula.....nlihisi kichefuchefu
Hii tabia nilikutana nayo Moshi aisee. Kwanza picha linaanza naletewa nyama mbichi nile aisee nikasema nitasubiria ya kuchoma Asante mzee. Nikaletewa damu mbichi nikachomoa, round ya tatu nikaletewa damu imechemshwa na supu ikabidi ninywe tu ili nisije onekana nadharau.

Ila dah aisee
 
Niikuta wameloweka ngozi ya ng'ombe kwenye maji kesho yake mchana ikatolewa ikakwanguliwa manyoya ikakatwa vipande ikapikwa iliwa usiku. Bahati nzuri nina alergy ya nyama nyekundu kwahiyo nikapata excuse ya kutokula ile mboga
Hili suala la Kula ngozi ya ng'ombe watu wengi wanakula ila ukimuuliza kabla hajatambua hujifanya kuwa hawezi Kula na inaliwa sana sana

Kimsingi kongolo kinacholiwa pale ni ngozi ya ng'ombe pekee na ulaji wa kongolo ni mkubwa sana ktk jamii yetu inayoishi mijini
 
Tembea ujionee, kwenye jamii kuna vyakula vya aina tofauti tofauti, kuna vingine vya unaona kabisa ni vya ajabu ila jamii husika inakula na kuvifuhia kabisa.

Nimewahi kwenda kijiji fulani nikakuta wanakula majani fulani ambayo kwetu tunayatumia kama maua ila kwao ni mboga pendwa kabisa.

Pia mara ya kwanza kuja Pwani na kukuta watu wanakula mchunga kama mboga napo nilishangaa sana kwa kuwa kwetu ni majani ya kulisha sungura si chakula cha binadamu.

Vivyo ivyo kuna watu wanakuja kwetu wanashangaa kukuta tunakula baadhi ya vitu kama askari wa mchwa na tunafurahia utamu wake kabisa nk.

Umewahi kuona chakula gani kwenye jamii ya ugegenini ukashangaa kujua kuwa ni chakula?

View attachment 2568383
Askari wa mchwa​
Wala 🐌,konokono wote,wala mende wote,wala panya wote,wala nyau wote,wala wou wote nawashangaa na wafananisha na mnyama,🦁(Animals)🤔🤔🤔
 
Wala 🐌,konokono wote,wala mende wote,wala panya wote,wala nyau wote,wala wou wote nawashangaa na wafananisha na mnyama,🦁(Animals)🤔🤔🤔
Hata wewe ni mnyama.sio kufananisha...sisi ni wanyamaaaaaa
 
Watu wana kula utumbo wa kuku na vichwa vya kuku, punda na panya kweli kweli, ni likua nasikia tu ila nilishuhudia mwenyewe......
Niliwahi poteza demu niliye mzima baada ya kuona anakula utumbo wa kuku,na ikawa mwisho wa uhusiano hapo hapo😂
 
Back
Top Bottom