Ummy Mwalimu awatumbua Mkurugenzi wa Temeke (Mwakabibi) na Mkurugenzi wa Sumbawanga (Msemakweli)

Ummy Mwalimu awatumbua Mkurugenzi wa Temeke (Mwakabibi) na Mkurugenzi wa Sumbawanga (Msemakweli)

Uchunguzi wetu zaidi umebaini kwamba Mtukufu Mwakabibi ndiye DED mwenye rekodi ya kiburi na kujimwabafai kupita yeyote tangu nchi hii ipate uhuru wake 1961 , alinunua gari la kutembelea la gharama kubwa (470mil) bila utaratibu na wala kujali lolote , tuhuma hizi hazifahamiki zilikopotelea .
1619346409706.png

wakati wa maomboleza ya Mwendazake pale uwanja wa Uhuru huyu jamaa alikuwa msaidizi wa MC akishirikiana pia na Mkuu wa Wilaya Gondwe. kweli aliendesha vibaya sana na kusababisha vifo vingi, kuna wakati aliombwa na Raia pamoja na Mc mwenyewe atangaze kuwa kuna vifo uwanjani AKATAA bado wakapenyeza majina ya watoto waliopotea wakiwatafuta walezi wao yanatajwa majina, akarukia Microphone na kufuta utaratibu huo, hapo nilijua Mnyakyusa huyu aliyetokea Ukurugenzi huko Kakonko ni kichaa na sio mbabe tu, hapohapo angefukuzwa kazi, mbona mikoa mingine hawakuwa hivyo
Bravoo Ummy Mwalimu
 
Jaffo ajiangalie na huko alipo.
akitoka hapo ataenda kulima

Una uhakika hawakuwa watoto pendwa wa jiwe?
Si unaona dj mpya anavyopiga ngoma kali kali....anaweza asipende ngoma yake
 
Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amewasimamisha kazi Wakurugenzi wawili.

Wa kwanza ni Nyangi Msemakweli wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Huyu katumbuliwa kwa ubadhirifu wake na usimamizi mbovu wa miradi ya Maendeleo pia alikuwa hana maelewano na Madiwani.

Wa pili ni Lusubilo Mwakabibi, Mkurugenzi wa Manispaa ya temeke. Huyu yeye katumbuliwa kutokana na kuwa na mwenendo usiofaa na matumizi mabaya ya Madaraka.

Mwakabibi ametumbuliwa kutokana na watu kumlalamikia kwa mwenendo usiofaa na matumizi Mabaya ya Madaraka, Ubadhirifu, usimamizi mbovu wa miradi ya Maendeleo Katika Manispaa ya Temeke.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Ummy Mwalimu amewataka Wakurugenzi wote Nchini kuzingatia Mipaka yao ya kazi.

Soma hizi:
1) Mkurugenzi wa Temeke, Mwakabibi awasweka ndani waandishi wa habari ili wasihudhurie kikao chake na wafanyabiashara

2) Wizara ya habari kuchunguza tukio la DED wa Temeke kuwaweka chini ya ulinzi waandishi kwa kufika kwenye kikao chake bila mwaliko

3) Wito: ITV isusie kutangaza taarifa zote za Manispaa ya Temeke mpaka pale DED Mwakabibi atakapotimuliwa

4) Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke aache kutisha na kufedhehesha Waandishi wa Habari

View attachment 1763482
View attachment 1763546
Hongera Ummy mwalimu, bado sasa tumbua wakurugenzi wafuatao, Tarime, chunya ,ikungi, bukombe, GeitaDc, arusha dc,arusha mjini, chalinze, mtama, kilosa, Bahi,karatu, babati, Kahama,igunga, simanjiro, siha, biharamulo, nyangwale. Na ninashauri Rais asiwateue wakurugenzi kwanza asubiri ufangio wa Ummy mwalimu upite ndipo ateue.
 
Huyu DED machachali mwenye kelele nyingi za kujifisia hatimae amesimamishwa kazi kwa kushindwa majukumu na ufisadi .

Mwakibinga ambaye alikuwa shabiki mkubwa wa jpm kiasi yeye na mkewe wote kupewa u-DED alijaa tuhumu za ufisadi na ulevi was madaraka huku akionekana kupambana zaidi na DC Gondwe muda wote
View attachment 1763510
Unakimbilia wapi? Ni Mwakabibi na sio Mwakibinga. Mkiitwa misukule mnasema mmetukanwa.
 
Asije akamsahau na wa manispaa ya Kahama ,kwa mda alioachwa nao kutuligishia hilo gari inatosha saana
 
Huyo mkurugenzi wa Temeke kwa namna alivyokuwa anaendesha ofisi ni sahihi kutumbuliwa.
Malalamiko juu yake yalikuwa mengi sana, shida sijui ilikuwa wapi kwa mamlaka yenye dhamana ya uteuzi kumtoa toka awamu ile ya hayati Magufuli.
Huyu Mwakibibi lazima atakuwa mtu mjinga sana.
Hakusoma alama za nyakati hata baada ya Mama Samia kutoa onyo.
 
Back
Top Bottom