Umoja Party ni chama chenye mlengo upi, kinaamini katika maendeleo au katika Magufuli?

Umoja Party ni chama chenye mlengo upi, kinaamini katika maendeleo au katika Magufuli?

Kama kinajihusisha na mawazo machafu ya jiwe basi hakinifai
Wakijitofautisha na jiwe naweza kuwasikiliza hata kwa dakika moja.
Hatuna shida na wapigaji, ni chama cha outetea masilahi ya Tanzania na Watanzania.
 
Walishindwa kina Samuel Sitta na CCJ ndo sembuse hizi takataka zinazoanzisha chama cha kikabila?

Tatizo la Sukuma gang bado hawataki kuamini kwamba zama zao zimekwisha rasmi na utawala wao wa kifashisti ni Mungu mwenyewe ndio ameingiliabkati ili kuwaokoa Watanzania.
If true, ulipaswa ufurahi; mbona unaweweseka sasa?
 
Watu wengi ambao walikuwa sana wanaunga mkono upuuzi wa bwana yule ni watu wajinga wajinga, wenye roho mbaya, mtu yeyote mwenye akili timamu alikuwa anaweza kung'amua ujinga na uongo ule. Leo wanalalamika ripoti ya CAG, tujiulize kwanini CAG Assad alifukuzwa kazi na taarifa zilikuwa zinafanywa siri? Kwa akili ndogo tu unaona ni kwakuwa, kulikuwa na ufisadi unafichwa.
Mpo madarakani, tuonesheni huo ufisadi.
 
Hicho chama kitakwama sababu ni wazi kinapingana na team Msoga.

ACT wamejiweka kwa CCM tawala ndio maana kipo

Chadema kipo level zingine, kinakubalika na wananchi wengi kukiua ni ngumu.
Wananchi wa Moshi?
 
Jamani wale wote ambao hawako kwenye lile kundi la CCM Ina wenyewe au unanijua Mimi ni nani? Pangeni foleni kadi ni chache.
 
Jamani wale wote ambao hawako kwenye lile kundi la CCM Ina wenyewe au unanijua Mimi ni nani? Pangeni foleni kadi ni chache.
Hatuwezi kuungana na wauwaji, ni bora hata zimwi likujuwalo.

IMG_20211028_135238_003.jpg
 
Nihatari Sana kubadili msitu Kwa kuwakaribisha nyani walewale. Muhimu hapa ni kuwatathmini waanzilishi na kuona Muono mbele wao na kama watakidhi vigezo watapata wafuasi wengi vinginevyo usemi wa zimwi likujualo hali Kuli likakwisha utaendelea Kuwa wa muhimu
 
Wanakaribishwa uwanjani. Mpaka wafike level ya chadema Ni miaka ishirini ijayo. Maana Kuna stages lazima upite ili ukamate dola.
Mhhh CHADEMA ! hiyo si ilishakufa zamani wakati li jamaa lilipobadili gia angani
 
Mnadanganywa na nyie mnakubali. Muanzilishi wa chama hicho ametokea AFFP na Wala sio CCM na Wala hawafuati ajenda za Magufuli za kutekana na kuuwana.
Angalia nembo ya chama kwenye T-Shirt..
Hii ni ccm part 2
 
Watoe challenge ya kupata logo na rangi zinazovutia. Huwa Ina effect kubwa ktk kuleta mvuto wa Chama machoni. Wazingatie matakwa/mahitaji ya kundi la wapigakura wengi.
 
Probably itakuwa kitu vizuri CCM, ACT, Chadema wakaungana pamoja wanakubaliana na kuunganishwa na mambo mengi kikubwa kinachowaunganisha, sera yao kubwa ni Anti- Magufuli, chuki kwa kanda flani, kuangalia nyuma awamu ya tano na kutukana na kubeza kila kitu kilichofanywa wakati huo mazuri na mabaya.

Watanzania wote waliobaki ni vizuri wakaungana pamoja waanzishe chama kipya kitakachosimamia maslahi mapana ya Watanzania wote bila kusahau maslahi ya Tanganyika, kuangalia mbele na kuiunganisha, bila kuendekeza ukabila, udini, ukanda, matabaka, matusi, kejeli, mipasho.

Tanzania tuwe na vyama viwili tu imara.
Mtu aliyeleta ukabila wa kutisha hapa nchini unamjua na unataka tuwaunge mkono wafuasi wake. ha ha ha haaaa
 
Unafikiri watafika mbali?
Hii ni seasonal party,yaani chama cha msimu kama fashion ya mavazi.
Kama kingeanzishwa baada ya mabadiliko ya katiba mpya labda kingepata haki ya kutamalaki.

Na mara nyingi vyama sampuli hizi huanzishwa na taasisi za umma kwa malengo tofauti kabisa ya kuwahadaa wananchi.
 
Hii ni seasonal party,yaani chama cha msimu kama fashion ya mavazi.
Kama kingeanzishwa baada ya mabadiliko ya katiba mpya labda kingepata haki ya kutamalaki.

Na mara nyingi vyama sampuli hizi huanzishwa na taasisi za umma kwa malengo tofauti kabisa ya kuwahadaa wananchi.
Uko sahihi 100% lakini mbona UMOJA PARTY hakina shida na mtu.Hii roho mbaya na kukisema vibaya inatokana na nini?
 
Watu wanamkubali Mwinyi kutokana na vitendo, kazi zake, utendaji wake. Anawajibika na kuwaajibisha wote kwenye serikali yake. Hana mipasho, ngojera, vijembe, visingizio. Ameiunganisha Zanzibae.Unaweza kuona Zenji inaeelekea wapi chini ya utawala wake.

Huku bara ni visingizio kibao "bei za kila kitu lazima zipande" anasema Rais wa JMT. Sababu anakwambia ni vita vya Ukraine- Urusi, Corona.

Upinzani hawahoji chochote wanataka maendeleo ya watu sio vitu, sera za ukanda, kila tatizo sababu ni Sukuma gangs, JPM, kiongozi wao mkuu baada ya kutoka jela haizunguzii tena.

Sera kuu ya CCM, upinzani ni kumkebehi JPM wanamuita mwendazake na majna mengine mengi ya kebehi sijaona yakitumika kwa kiongozi, mtu mwingine yoyote aliyekufa. Utamaduni wetu TZ tunawaita Hayati, Marehemu.

It will interesting and fun to watch kampeni za uchaguzi CCM na upinzani wa sasa wakiuza sera zao kwa wananchi

Wananchi wakiwauliza kwanini hatuna umeme, maji, tuna kodi, tozo za ajabu, mfumuko wa bei na wao wakijibu sababu ni mwendazake.

Kwanini miradi ya kimkakati inasuasua, tunakopa hovyo, wao wakijibu ni sababu ni mwendazake.

Kwanini masoko yanachomwa moto, ajali zinaongezeka, kwanini hamna sera zenu mpya kulisaidia Taifa, Wao (CCM , upinzani) wataijibu sababu ni mwendazake, Sukuma gang, Wasukuma.

Yoyote atakayehoji, au kutoa maoni mbadala ataambiwa wewe ni Sukuma Gang.
Tatizo chuma aliyaumiza sana hayo makundi uliyoyataja hapo kwamba yanamshambulia kwa sasa.

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom