Umoja wa Israel na Marekani uko sawa na ule wa Ujerumani na Austria 1914

Umoja wa Israel na Marekani uko sawa na ule wa Ujerumani na Austria 1914

Kila mmoja anajihesabia haki ndio sababu vita haiishi.
Imepita miaka 79 tangu itokee vita baina ya mataifa makubwa, hivyo kimekuja kizazi kipya ambacho kinadhani amani ni haki yake tu, na kusahau dunia ilipotoka. Zamani watu walikuwa wakisikia Urusi kaweka silaha za nyuklia nchini Cuba walikuwa wanaogopa, siku hizi watu wanachagua upande na kushangilia.

Hata wanasiasa na wanadiplomasia wote walioishi kipindi cha vita ya pili ya dunia na vita baridi, walikuwa ni watu makini wanaofahamu madhara ya siasa za mlengo mkali. Hata kama walikuwa wanatetea maslahi ilikuwa ni lazima kuwe na mazungumzo na maelewano.

Marekani siku hizi haina wanasiasa kama Henry Kissinger, Zbigniew Brezhinski na George Kenan, ina watu kama Pompeo, Blinken na Tillerson ambao kiuhalisia ni kizazi chenye shida kidogo. Hili hata Prof Kishore Mahbubani aliwahi kulisema dhahiri kabisa.

Kizazi cha Baby Boomers, kama Putin, Trump, Jinping, Ayatollah, Netanyahu n.k wote hawakuiona vita ya pili ya dunia na waliishi nyakati za mwisho za vita baridi. Ila walau wangeshuhudia matukio kama The Siege of Leningrad, Invasion of Normandy na Bombing of Dresden ni lazima wangekuwa na uwoga fulani hivi.
 
Imepita miaka 79 tangu itokee vita baina ya mataifa makubwa, hivyo kimekuja kizazi kipya ambacho kinadhani amani ni haki yake tu, na kusahau dunia ilipotoka. Zamani watu walikuwa wakisikia Urusi kaweka silaha za nyuklia nchini Cuba walikuwa wanaogopa, siku hizi watu wanachagua upande na kushangilia.

Hata wanasiasa na wanadiplomasia wote walioishi kipindi cha vita ya pili ya dunia na vita baridi, walikuwa ni watu makini wanaofahamu madhara ya siasa za mlengo mkali. Hata kama walikuwa wanatetea maslahi ilikuwa ni lazima kuwe na mazungumzo na maelewano.

Marekani siku hizi haina wanasiasa kama Henry Kissinger, Zbigniew Brezhinski na George Kenan, ina watu kama Pompeo, Blinken na Tillerson ambao kiuhalisia ni kizazi chenye shida kidogo. Hili hata Prof Kishore Mahbubani aliwahi kulisema dhahiri kabisa.

Kizazi cha Baby Boomers, kama Putin, Trump, Jinping, Ayatollah, Netanyahu n.k wote hawakuiona vita ya pili ya dunia na waliishi nyakati za mwisho za vita baridi. Ila walau wangeshuhudia matukio kama The Siege of Leningrad, Invasion of Normandy na Bombing of Dresden ni lazima wangekuwa na uwoga fulani hivi.
Kwahiyo hao ni rahisi kupress button vita vipiganwe?? Hawana imani na maridhiano
 
Kwahiyo hao ni rahisi kupress button vita vipiganwe?? Hawana imani na maridhiano
Unaikumbuka APPEASEMENT POLICY ya Neville Chamberlain ???

Juzi Prof John Mearsheimer wa University of Chicago alikuwa anahojiwa na Judge Napolitano akasema kwamba, nchi za Urusi na Iran zimefahamu ukweli kwamba, huwezi kufanya APPEASEMENT POLICY na taifa kama Marekani na Israel.

Ametoa historia kwamba mbali na Hamas kufanya vuruga na kuua watu, matatizo yake hayakutokea hivihivi, yana historia ndefu sana. Marekani na Israel wanafahamu kabisa kwamba kuna A Two State Solution ambayo inatakiwa itekelezwe, lakini kidogo kidogo wamekuwa wakipuuza huku wakiisaidia Israeli kujitanua.

Mambo yamekuwa mengi mno.
 
Mkuu MALCOM LUMUMBA maana ya andiko hili ni kwamba USA tutegemee kuporomoka kiuchumi na Uchina kupanda?
Hapana, jibu siyo rahisi kwasababu POLITICS ARE BINARY AND UBIQUITOUS, NOT ONE WAY TRAFFIC. Unaweza kukuta Marekani akapanda kiuchumi pamoja na kushinda vita vilevile, kinyume na ambavyo wengi tunategemea. Unakumbuka kilichotokea Urusi, mbali na maelfu ya vikwazo baada ya kuvamia Ukraine ??? Urusi ilipanda na mpaka leo iko tu.

Japo, Conventional Wisdom inasema hivi: Endapo Ikitokea vita in The Persian Gulf dunia nzima itaguswa kama ilivyoguswa kwenye vita ya Ukraine. Hasahasa mataifa madogo kama sisi ambayo hayazalishi bali ni Net Importers. Wote tutatembea kwa mguu kutoka Mbezi hadi Kariakoo kwasababu mafuta yatakuwa ni bidhaa ya anasa.

Jambo la kujiuliza ni hili: Unadhani Israeli, taifa lenye watu milioni 9 linaweza kufanya vita dhidi ya Iran, taifa lenye watu takriban milioni 90 bila msaada wa Marekani ???

Kupambana vita ni rahisi sana, changamoto kubwa inakuja kwenye kufanya kitu kinaitwa OCCUPATION. Ili Israel ashinde vita dhidi ya Iran, mbali na kuipiga ni lazima afanya OCCUPATION kuhakikisha anaondoa kabisa mfumo wa kiislamu uliozaliwa na kujengwa tokea mapinduzi ya 1979.

Hili lilifanyika Ujerumani baada ya 1945, ambapo iligawanywa vipande vinne (Occupation Zones) na kimoja kikashikiliwa na Marekani, kimoja Muingereza, Kimoja USSR na kimoja Mfaransa ili kuhakikisha wanazi hawajipangi tena. Kufanya OCCUPATION siyo rahisi ndiyo maana Marekani ameondoka Afghanistan nchi yenye watu milioni 41, baada ya takribani miaka 20 kwenye nchi hiyo.

Unadhani Iran kwenye watu takribani milioni 90 wataweza kufanya kama walivyofanya Afghanistan na Iraq ??? Iraq tu ilizalisha makundi kama ISIL/DAESH, unadhani Iran itazalisha makundi ya namna gani kutokana na POWER VACUUM itakayotengenezwa baada ya kuwaondoa kina Ayatollah ??

NB 1: NAZIs walipigana vita vizuri, ila OCCUPATION ya Poland, Ukraine na Russia zikawashinda, hivyo ili kupunguza gharama ya kutunza watu na kupata resistance kama kule Ufaransa, wakaanza kupeleka watu CONCENTRATION CAMPS na kufanya MASS EXTERMINATION.

NB 2: GAZA imeonesha ni gharama kufanya OCCUPATION, ndiyo maana waziri mkuu wa Israel Ariel Sharon aliamua kuondoa vikosi mwaka 2005. Sasa ili kuzuia Hamas nyingine isizaliwe, njia ambayo Israeli itabidi atumia ni ile ya Ujerumani, Marekani na Australia, ya kuua wenyeji na kuwafukuzia mbali (Ethnic Cleansing, Extermination and Genocide)
 
Asante Sana ndg MALCOM LUMUMBA . Hizi ndo brain zinazotakiwa kuleta mada za kujadiliwa humu.

Humu wengi huwa wanaleta mada bila kushirikisha Ubungo Kwa kiwango kinachotakiwa na matokeo yake tunaishia kuwa Machawa wa tusiyoyajua na yasiyotuhusu.
Wengi huzungumzia huo mgogoro kidini na mahaba ya dini yakizidi tegemea matusi na kufedheheshana mbele.

Mwamba haiongelei kwenye mlengo huo ndio maana inavutia kusoma na kuongeza ufikirishi.
 
Ukiona mtu humu jf anapendekeza two state solution .jua ndio wale wanakariri unafiki wa China,UN Kwa masilari binafsi. Ili vita ikome hapo mashariki ya kati one state.Israel na Palestine iwe nchi moja unity is power.China naiheshimu sana ila 2 state solution ,China hapana anajari masilali yake. Ndugu Dunia inahitaji serikali moja hata Tanzania tunahitaji serikali Moja, Africa Moja. Tuache kukaririshwa na wanasiasa mwenye tamaa ya vyeo.mwisho niwapa Siri vita haitaisha mipaka Dunia ipate serikali.Sayansi principle Equilibrium.
 
Hapana, jibu siyo rahisi kwasababu POLITICS ARE BINARY AND UBIQUITOUS, NOT ONE WAY TRAFFIC. Unaweza kukuta Marekani akapanda kiuchumi pamoja na kushinda vita vilevile, kinyume na ambavyo wengi tunategemea. Unakumbuka kilichotokea Urusi, mbali na maelfu ya vikwazo baada ya kuvamia Ukraine ??? Urusi ilipanda na mpaka leo iko tu.

Japo, Conventional Wisdom inasema hivi: Endapo Ikitokea vita in The Persian Gulf dunia nzima itaguswa kama ilivyoguswa kwenye vita ya Ukraine. Hasahasa mataifa madogo kama sisi ambayo hayazalishi bali ni Net Importers. Wote tutatembea kwa mguu kutoka Mbezi hadi Kariakoo kwasababu mafuta yatakuwa ni bidhaa ya anasa.

Jambo la kujiuliza ni hili: Unadhani Israeli, taifa lenye watu milioni 9 linaweza kufanya vita dhidi ya Iran, taifa lenye watu takriban milioni 90 bila msaada wa Marekani ???

Kupambana vita ni rahisi sana, changamoto kubwa inakuja kwenye kufanya kitu kinaitwa OCCUPATION. Ili Israel ashinde vita dhidi ya Iran, mbali na kuipiga ni lazima afanya OCCUPATION kuhakikisha anaondoa kabisa mfumo wa kiislamu uliozaliwa na kujengwa tokea mapinduzi ya 1979.

Hili lilifanyika Ujerumani baada ya 1945, ambapo iligawanywa vipande vinne (Occupation Zones) na kimoja kikashikiliwa na Marekani, kimoja Muingereza, Kimoja USSR na kimoja Mfaransa ili kuhakikisha wanazi hawajipangi tena. Kufanya OCCUPATION siyo rahisi ndiyo maana Marekani ameondoka Afghanistan nchi yenye watu milioni 41, baada ya takribani miaka 20 kwenye nchi hiyo.

Unadhani Iran kwenye watu takribani milioni 90 wataweza kufanya kama walivyofanya Afghanistan na Iraq ??? Iraq tu ilizalisha makundi kama ISIL/DAESH, unadhani Iran itazalisha makundi ya namna gani kutokana na POWER VACUUM itakayotengenezwa baada ya kuwaondoa kina Ayatollah ??

NB 1: NAZIs walipigana vita vizuri, ila OCCUPATION ya Poland, Ukraine na Russia zikawashinda, hivyo ili kupunguza gharama ya kutunza watu na kupata resistance kama kule Ufaransa, wakaanza kupeleka watu CONCENTRATION CAMPS na kufanya MASS EXTERMINATION.

NB 2: GAZA imeonesha ni gharama kufanya OCCUPATION, ndiyo maana waziri mkuu wa Israel Ariel Sharon aliamua kuondoa vikosi mwaka 2005. Sasa ili kuzuia Hamas nyingine isizaliwe, njia ambayo Israeli itabidi atumia ni ile ya Ujerumani, Marekani na Australia, ya kuua wenyeji na kuwafukuzia mbali (Ethnic Cleansing, Extermination and Genocide)
Asante sana mkuu nimekuelewa

Kuhusu Ufaransa naona kama anatupiga changa la macho, sioni kama anaweza kwenda kinyume na USA kwenye kumuunga mkono Israel
 
Andiko zuri lakini naona kama umeweka utangulizi mrefu sana ili kuficha hoja yako mwishoni “Gaza Genocide”.
Gaza genocide ni neno lililoibuliwa na South Africa na kubebwa na Al Jazeera kama sehemu ya kuizuia Isreal kuendelea kuwasaka Hamas huko Gaza na sasa Hezbollah huko Lebanon.

Pamoja na historia nzuri uliyoleta lakini hoja ya Gaza genocide imeharibu kila kitu logically kwani ukweli ukichanganywa na uongo unakuwa uongo.
Kwa mtazamo wako mkuu mauaji ya Gaza unayachukuliaje
 
Naomba kuuliza tu: Nini kilipelekea matukio ya October 7 ????
=======================================================
Lakini pia kumbuka hili: Wakati Ufalme wa Judea, unapambana na Warumi mwaka 70 A.D kule kwenye ngome ya MATSADA, Wayahudi wengi wenye msimamo mkali waliamini kwamba hawewezi kushindwa vita, hivyo wakaamua kufanya uasi dhidi ya Warumi.

Jenerali Titus na baba yake Kaisari Vespasian waliwpiga vibaya mno Wayahudi. Walivunja ngome ya MATSADA na kuteketeza hekalu la Mfalme Suleimani na kuua maelfu ya Wayahudi ambao wengi walikimbilia Asia, Afrika na Ulaya. Halafu nchi ya Yudea wakaibadilisha jina na kuiita Ufilisti na kuwapa maadui wa Israeli waliokuwa wanaishi pale.

Mwisho kabisa : Mwaka 1914, Austro-Hungary na Ujerumani waliamini kwamba hawewezi kushindwa vita na taifa lolote Ulaya, kwasababu haki yao ya kutawala wengine ni Divine
==============================================
Swali langu kwako mkuu: Mwisho wa haya yote utakuwa ni upi ?
Naomba tuweke historia sawa. Hekalu la Mfalme Suleiman liliteketezwa miaka ya 580KK na majeshi ya Mfalme Nebuchadnezzar. Hekalu lililoteketezwa na Titus ni la Zerubabeli ambalo likiboreshwa na Herod the Great. Hii ni historia
Ila watu wa dini flani watakwambia pale palikuwa na mosque sijui temple na mosque ni kitu kilekile?!
 
Andiko zuri lakini naona kama umeweka utangulizi mrefu sana ili kuficha hoja yako mwishoni “Gaza Genocide”.
Gaza genocide ni neno lililoibuliwa na South Africa na kubebwa na Al Jazeera kama sehemu ya kuizuia Isreal kuendelea kuwasaka Hamas huko Gaza na sasa Hezbollah huko Lebanon.

Pamoja na historia nzuri uliyoleta lakini hoja ya Gaza genocide imeharibu kila kitu logically kwani ukweli ukichanganywa na uongo unakuwa uongo.

Kinachotokea Gaza ni genocide.
 
Andiko zuri lakini naona kama umeweka utangulizi mrefu sana ili kuficha hoja yako mwishoni “Gaza Genocide”.
Gaza genocide ni neno lililoibuliwa na South Africa na kubebwa na Al Jazeera kama sehemu ya kuizuia Isreal kuendelea kuwasaka Hamas huko Gaza na sasa Hezbollah huko Lebanon.

Pamoja na historia nzuri uliyoleta lakini hoja ya Gaza genocide imeharibu kila kitu logically kwani ukweli ukichanganywa na uongo unakuwa uongo.
Huo ni uoni wako hafifu unaotokana na udini na upofu uliokujaa. Hakuna mwenye akili timamu asiyeona genocide inayofanywa na Wazayuni waliyojificha kwenye koti la Uisraeli.
 
  1. Coincidence za matukio ya WWI ndizo zinahitimisha kwamba Sasa Kuna WWIII.
  2. Kwamba kudharau UN resolutions ndipo kunapelekea WW. UN resolutions hazijaanza kudharauliwa Leo Wala Jana. Mfano, Mwaka 2001 UN iliizuia US isivamie Iraq lakini Marekani alikiuka.
Japokuwa naamini (ndivyo inavyoaminika) WWIII itaanzia mashariki ya kati, lakini siamini kama vita itatokea Kwa mtiririko ule ule wa matukio ya 1900s (kama sijakuelewa vibaya).

US na Israel Wana mkataba wa kudumu wa kusaidiana katika shida na Raha. Israel ni mnufaika Namba Moja wa misaada ya kijeshi kutoka US (kiufundi, latest tech ya zana za kivita, nguvukazi za wanajeshi, budget ktk masuala ya ulinzi na usalama, n.k). Mwaka jana, baada ya shambulio la 2023 October 7, Marekani iliongeza budget (mpaka kufikia Us $ 12 billion) kuisaidia Israel kujiimarisha zaidi ktk medani za kivita.
Kwa hiyo, nionavyo Mimi, ili vita ya WWIII ili ije kuwa rasmi ni pale Israel atakapozidiwa na hatimaye US kuingilia kati yeye kama yeye ili kumlinda Mtoto wake ; hapo Sasa wale mahasimu wa US nao hawatakuwa mbali na mchezo wa piga nikupige.
 
Back
Top Bottom