Hata wakitokea hiyo misaada, msimamo wetu uko pale pale. Haramu ni haramu tu.
Hakuna fedha ya msaada au mmkopo inayoweza kulingana na utu wa mwanadamu, hivyo misaada au mikopo haiwezi kutunyamazisha wala ku-justify uovu dhidi ya wanadamu.
Vile vile, wakiamua kutoa misaada na kwa vyama vya siasa, tusisikie mnawaita mabeberu huku fedha zao mnapokea.
Wazungu hawa wakisimama upande wa haki, tutwaunga mkono, na wakisimama upande wa dhuluma, tutawapinga.
Nitasimama upande wa haki hata kama shetani ndio atakuwa anatoa haki hiyo, na nitapinga dhuluma hata kama inatoka kwa au ina mkono wa malaika.
Mwisho, wazungu hawa angekuwa na roho za chuki na visasi kama wakoloni weusi, hiyo misaada na mikopo wasingeitoa kwa jinsi wanavyodhalilishwa kwa kuitwa mabeberu huku Kabudi akiwatolea maneno yasiyofaa.
Msisahau na za matundu ya choo kwa watoto wetu huko St. Kayumba.