Twilumba
JF-Expert Member
- Dec 5, 2010
- 12,576
- 14,522
Kuna mmoja wenu alisema hvy,Chadema ni kama kimepigwa mkosi au laana, hiki chama kinakufa muda si mrefu
Rest Easy Bwana yule!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna mmoja wenu alisema hvy,Chadema ni kama kimepigwa mkosi au laana, hiki chama kinakufa muda si mrefu
Chadema wakati wa maridhiano walikosea mno kujiita wao ndio chama kikuu cha upinzani na blah blah nyinginezo wakavimba na maridhiano yao
Unaota kwa sauti.Chadema ni kama kimepigwa mkosi au laana, hiki chama kinakufa muda si mrefu
Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa unaoundwa na Vyama 13 vyenye usajili Nchini unazungumza na Wanahabari, leo Jumatano Januari 17, 2024.
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa, Abdul Mluya anasema "Mnamo Tarehe 13/01/2024 Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA (Freeman Mbowe) alizungumza na Waandishi wa Habari na kutangaza maandanamano kuishinikiza Serikali kuiondoa Bungeni Miswada Mitatu inayoleta mageuzi ya Kisiasa hapa Nchini, Miswada hiyo ni Muswada wa Sheria ya Uchaguzi, Muswada wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi.
"Mimi ni miongoni mwa Watu ambao tuliwasilisha Miswada yetu pale Bungeni kama Chama na Vyama vingine na Siku Mwenyekiti anafunga nilikuwa miongoni mwa Watu waliokuwepo mule ndani na alihitimisha kwa kusema Vyama 18 vimetoa maoni Bungeni, vingine kwa maandishi vingine kama tulivyokwenda lakini Taasisi mbalimbali alizitaja na Viongozi wa Dini.
"Mara baada ya tukio lile kumalizika Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Katibu Mkuu mwenzetu (John Mnyika wa CHADEMA), kazi yetu ilikuwa ni kutoa maoni sio kukosoa Muswada kwa maana ya kuutupa."
Abdul Mluya: Chama kitengeneze sera za kuungwa mkono
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa ni Katibu Mkuu wa Chama Cha DP, Abdul Mluya anasema "Tufanye siasa za hoja tusigusane maungoni, hata Sheria ya Vyama vya Siasa inasema Chama kitakuwa na wajibu wa kuunda sera kwa lengo la kuungwa mkono, hilo limekaa sahihi sana kuliko njia wanayotaka kuitumia."
Abdul Mluya: CHADEMA waache ubinafsi
Tunawasii sana viongozi wenzetu na chama chao (CHADEMA) kuendelea kutumia njia sahihi zilizopo za Kisheria kushirikina na wengine (sisi) pamoja na kuacha ubinafsi na kuacha tabia ya kupinga kila jambo.
Abdul Mluya: Mbowe aombe radhi
"Viongozi wa Kidini tunaowaheshimu sana walitoa maoni yao, sasa nikitokea Mluya Mimi nikasema utupwe maana yake ni kwamba wale wote waliotoa maoni hawana akili, kwahiyo tunamtaka huyu Kiongozi mwenzetu (Freeman Mbowe) aombe radhi kwa Viongozi wa Dini ili kuleta mustakabali bora kwa Taifa letu.
Abdul Mluya: Maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu
"Malengo yetu ni kuanzisha malengo mahsusi dhidi ya amani na Umoja wa Kitaifa wa Nchi yetu, njia hii ya maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu kwa sababu Ina viashiria vya kuvunja amani, ni haki lakini si kila haki uitumie, haki nyingine unaziacha sio maandanamano tu, ni haki kwa Chama kupeleka maendeleo kwa Wananchi wake lakini hatufanyi."
Abdul Mluya: Waliopinga Kikosi Kazi, leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa
"Inashangaza kuona waliopinga mchakato wa Kikosi Kazi leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa, huu ni unafiki, kiburi na kwenye Demokrasia kama hatutaepuka unafiki, kiburi, kutoshirikiana na wenzako hatutofika, tutaendelea kupingana mpaka pale tutakuwa sote ni wamoja, malengo yetu ya Kikatiba.
"Tunapaswa kutanguliza maslahi ya Wananchi mbele na sio maslahi yetu sisi na matumbo yetu au Vyama vyetu, leo inashangaza sana kuona leo unasikia eti maoni ya Kikosi Kazi yametupwa, maoni mengi ya Kikosi Kazi yamechukuliwa na Vyama vinaendelea kutoa maoni kuboresha Miswada husika, maoni yale tuliyoenda kutoa ni zao la Kikosi Kazi."
View attachment 2874343
Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan Doyo
Doyo: Watu 7 walikufa kabla ya maandamano Zanzibar
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo anasema “Tunaiomba Serikali isitishike kwa ajili ya maandamano ya Chama kimoja kwa faida ya wengi.
“Maandamano ni ajali, nikiwa CUF Mwaka 2001 kabla ya maandamano walikufa watu saba.”
Pia soma:
= Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu
= Kama Jeshi litafanya usafi tarehe 23-24, basi CHADEMA ifanye maandamano tarehe 25 wapite njia zikiwa safi
= Hizi ndizo sababu Watanzania hawatoshiriki maandamano ya CHADEMA
Haya mapandikizi ya CCM hayana hata ofisi
Ruzuku ya CDM ni 130M ya CCM ni 3B hakuna anayetaja ya CCM watu wanatolea macho 130 ya CDM sababu ya mafanikio yakeKumbe yanajitafutia Ruzuku .... Jamaa kaitamka ruzuku kama mara 5 hivi.
Ruzuku ya CDM ni 130M ya CCM ni 3B hakuna anayetaja ya CCM watu wanatolea macho 130 ya CDM sababu ya mafanikio yake
Haya mapandikizi ya CCM hayana hata ofisi
Hivi vyama vidogo havilalamiki chama dola kongwe CCM kukataa katiba mpya ya nchi, CCM kuendelea kupora mchakato mzima wa uchaguzi mkuu 2024 / 2025 kwa kupitia makada wake ambao ni wakurugenzi wa wilaya DED na wizara ya TAMISEMI, hali ngumu ya maisha, elimu ya kibaguzi kupitia shule za kata ....
Toka Maktaba :
17 February 2023
John Cheyo: Mazungumzo ya maridhiano kuendeshwa kwa gredi yaani ya 'ukubwa' wa vyama viwili tu siyo sahihi
Mzee John Cheyo - Hili la vyama vinavyojiita Chama Tawala na Chama Kikubwa kuteka agenda za nchi halikubaliki
Mwenyekiti wa chama cha UDP Mh. John Cheyo alalamika siasa kuwekwa "gredi" vyama gani vinaweza kujadili katiba ya nchi, maana kwa sasa suala hili linajadiliwa na vyama viwili tu kimoja kinajiita ni tawala na kingine ni chama 'kikubwa' huku vyama vingine vinavyoitwa vya mfukoni vikiachwa nje ya mjadala huu mkubwa.
Mzee Cheyo anasema umri wake umamueleza kuwa leo chama kinaweza kuwa kikubwa na tawala lakini kesho kikawa kidogo hivyo ikitokea mazungumzo muhimu je chama hicho huko miaka ijayo kitabaguliwa ?
Anaongeza kuwa ustaarabu wa kisiasa uwe katika nyanja zote na siyo lugha tu. Hili la ukubwa na huyu mtawala haikubaliki hivyo baraza la vyama la siasa lipewe hatamu na jukumu la kuongoza mazungumzo yatayojumuisha vyama vyote badala ya vyama viwili kujifungia chumbani bila wananchi kushirikishwa na ushirikishwaji ndiyo people's power ya wale rafiki zetu.
Mkongwe huyo wa siasa anasema maisha ni magumu ni katika mifuko yao wananchi inayosababishwa na bei ya mafuta kupanda. Hivyo hii ya serikali kuamua kuagiza mchele kutoka nje haitasaidia kupunguza bei ya mchele dukani.
Jibu la kukabiliana na mfumuko wa bei ni kutumia neno moja tu ruksa la rais mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi na hivyo bulk procurement ya wachache kuagiza (kununua) mafuta ndiyo mzizi wa mfumuko wa bei /root cause ya mfumuko wa bei unaonufaisha wanunuzi wachache wa mafuta kupitia bulk procurement.
Ruksa ya Mzee rais Ali Hassan Mwinyi kuacha milango wazi kwa kila kitu ndiyo jibu endelevu / sustainable la kukabiliana na mfumuko wa bei hivyo EWURA na TBS wabaki kuwa wasimamizi wa ubora wa bidhaa na baada ya hapo bei ya mafuta itakuwa chini ya Tshs 2,000 kwa lita na hili litapelekea mfumuko wa bei wa kila kitu nchini kwenda chini na maisha kuwa nafuu.
Wafanyabiashara wa vitu na bidhaa zote hata mafuta lazima wawe wengi na ndiyo unafuu kwa maisha ya wananchi utapatikana, hii zimamoto ya kusimamia bei ya mafuta au kuagiza mchele toka nje kukabiliana na ughali wa maisha siyo suluhisho la kudumu.
John Cheyo mfanyabiashara wa siku nyingi anasema watanzania zaidi ya nusu hawaishi mashambani, bali wanaishi mijini na shamba lao ni mifukoni hivyo mchele toka Katavi, Shinyanga na Mbeya kuwa juu kwa walaji wa mijini unasababishwa na bei ya juu ya nishati ya mafuta ya dizeli na siyo vinginevyo pia wala ruzuku haitasaidia jibu ni neno ruksa kuruhusu biashara huria ya wafanyabiashara wengi wa biashara za ndani na nje.
Mzee John Cheyo anafurahishwa na waziri wa kilimo Hussein Bashe kutoyumbishwa na mbinyo wa kelele za kutoa bei elekezi kwa mazao ya wakulima au kufunga mipaka wakulima kuuza soko la nje. Mazao ni Mali ya wakulima anasisitiza Mzee John Cheyo na hiyo ndiyo sera ya UDP ya kuwajaza mapesa watanzania ikiwemo wakulima. Sasa vyama kama Alliance for Democratic Change (ADC) nacho kinalalamika.
Acha ujinga, huwa siunganishi sentesi kwanza.haya mrembo
Sasa mbona wanaitafuna pamoja na kuiba mali za umma lakini hakuna kelele?Actually, CCM wanaihitaji ruzuku kuliko hata CDM ....!!
Waulize hata ofisi zao zipo wapiHalafu huyo Mwenyekiti wao anadai baada ya leo watakutana kupanga maandamano ..... sasa anapinga maandamano ya CDM halafu wanataka kupanga maanamano mengine .... ya kupinga maandamano ya CDM sijui!!?
Wamekubinafsia nn?Chadema wabinafsi sana
Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa unaoundwa na Vyama 13 vyenye usajili Nchini unazungumza na Wanahabari, leo Jumatano Januari 17, 2024.
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa, Abdul Mluya anasema "Mnamo Tarehe 13/01/2024 Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA (Freeman Mbowe) alizungumza na Waandishi wa Habari na kutangaza maandanamano kuishinikiza Serikali kuiondoa Bungeni Miswada Mitatu inayoleta mageuzi ya Kisiasa hapa Nchini, Miswada hiyo ni Muswada wa Sheria ya Uchaguzi, Muswada wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi.
"Mimi ni miongoni mwa Watu ambao tuliwasilisha Miswada yetu pale Bungeni kama Chama na Vyama vingine na Siku Mwenyekiti anafunga nilikuwa miongoni mwa Watu waliokuwepo mule ndani na alihitimisha kwa kusema Vyama 18 vimetoa maoni Bungeni, vingine kwa maandishi vingine kama tulivyokwenda lakini Taasisi mbalimbali alizitaja na Viongozi wa Dini.
"Mara baada ya tukio lile kumalizika Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Katibu Mkuu mwenzetu (John Mnyika wa CHADEMA), kazi yetu ilikuwa ni kutoa maoni sio kukosoa Muswada kwa maana ya kuutupa."
Abdul Mluya: Chama kitengeneze sera za kuungwa mkono
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa ni Katibu Mkuu wa Chama Cha DP, Abdul Mluya anasema "Tufanye siasa za hoja tusigusane maungoni, hata Sheria ya Vyama vya Siasa inasema Chama kitakuwa na wajibu wa kuunda sera kwa lengo la kuungwa mkono, hilo limekaa sahihi sana kuliko njia wanayotaka kuitumia."
Abdul Mluya: CHADEMA waache ubinafsi
Tunawasii sana viongozi wenzetu na chama chao (CHADEMA) kuendelea kutumia njia sahihi zilizopo za Kisheria kushirikina na wengine (sisi) pamoja na kuacha ubinafsi na kuacha tabia ya kupinga kila jambo.
Abdul Mluya: Mbowe aombe radhi
"Viongozi wa Kidini tunaowaheshimu sana walitoa maoni yao, sasa nikitokea Mluya Mimi nikasema utupwe maana yake ni kwamba wale wote waliotoa maoni hawana akili, kwahiyo tunamtaka huyu Kiongozi mwenzetu (Freeman Mbowe) aombe radhi kwa Viongozi wa Dini ili kuleta mustakabali bora kwa Taifa letu.
Abdul Mluya: Maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu
"Malengo yetu ni kuanzisha malengo mahsusi dhidi ya amani na Umoja wa Kitaifa wa Nchi yetu, njia hii ya maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu kwa sababu Ina viashiria vya kuvunja amani, ni haki lakini si kila haki uitumie, haki nyingine unaziacha sio maandanamano tu, ni haki kwa Chama kupeleka maendeleo kwa Wananchi wake lakini hatufanyi."
Abdul Mluya: Waliopinga Kikosi Kazi, leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa
"Inashangaza kuona waliopinga mchakato wa Kikosi Kazi leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa, huu ni unafiki, kiburi na kwenye Demokrasia kama hatutaepuka unafiki, kiburi, kutoshirikiana na wenzako hatutofika, tutaendelea kupingana mpaka pale tutakuwa sote ni wamoja, malengo yetu ya Kikatiba.
"Tunapaswa kutanguliza maslahi ya Wananchi mbele na sio maslahi yetu sisi na matumbo yetu au Vyama vyetu, leo inashangaza sana kuona leo unasikia eti maoni ya Kikosi Kazi yametupwa, maoni mengi ya Kikosi Kazi yamechukuliwa na Vyama vinaendelea kutoa maoni kuboresha Miswada husika, maoni yale tuliyoenda kutoa ni zao la Kikosi Kazi."
View attachment 2874343
Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan Doyo
Doyo: Watu 7 walikufa kabla ya maandamano Zanzibar
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo anasema “Tunaiomba Serikali isitishike kwa ajili ya maandamano ya Chama kimoja kwa faida ya wengi.
“Maandamano ni ajali, nikiwa CUF Mwaka 2001 kabla ya maandamano walikufa watu saba.”
Pia soma:
= Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu
= Kama Jeshi litafanya usafi tarehe 23-24, basi CHADEMA ifanye maandamano tarehe 25 wapite njia zikiwa safi
= Hizi ndizo sababu Watanzania hawatoshiriki maandamano ya CHADEMA
Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa unaoundwa na Vyama 13 vyenye usajili Nchini unazungumza na Wanahabari, leo Jumatano Januari 17, 2024.
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa, Abdul Mluya anasema "Mnamo Tarehe 13/01/2024 Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA (Freeman Mbowe) alizungumza na Waandishi wa Habari na kutangaza maandanamano kuishinikiza Serikali kuiondoa Bungeni Miswada Mitatu inayoleta mageuzi ya Kisiasa hapa Nchini, Miswada hiyo ni Muswada wa Sheria ya Uchaguzi, Muswada wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi.
"Mimi ni miongoni mwa Watu ambao tuliwasilisha Miswada yetu pale Bungeni kama Chama na Vyama vingine na Siku Mwenyekiti anafunga nilikuwa miongoni mwa Watu waliokuwepo mule ndani na alihitimisha kwa kusema Vyama 18 vimetoa maoni Bungeni, vingine kwa maandishi vingine kama tulivyokwenda lakini Taasisi mbalimbali alizitaja na Viongozi wa Dini.
"Mara baada ya tukio lile kumalizika Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Katibu Mkuu mwenzetu (John Mnyika wa CHADEMA), kazi yetu ilikuwa ni kutoa maoni sio kukosoa Muswada kwa maana ya kuutupa."
Abdul Mluya: Chama kitengeneze sera za kuungwa mkono
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa ni Katibu Mkuu wa Chama Cha DP, Abdul Mluya anasema "Tufanye siasa za hoja tusigusane maungoni, hata Sheria ya Vyama vya Siasa inasema Chama kitakuwa na wajibu wa kuunda sera kwa lengo la kuungwa mkono, hilo limekaa sahihi sana kuliko njia wanayotaka kuitumia."
Abdul Mluya: CHADEMA waache ubinafsi
Tunawasii sana viongozi wenzetu na chama chao (CHADEMA) kuendelea kutumia njia sahihi zilizopo za Kisheria kushirikina na wengine (sisi) pamoja na kuacha ubinafsi na kuacha tabia ya kupinga kila jambo.
Abdul Mluya: Mbowe aombe radhi
"Viongozi wa Kidini tunaowaheshimu sana walitoa maoni yao, sasa nikitokea Mluya Mimi nikasema utupwe maana yake ni kwamba wale wote waliotoa maoni hawana akili, kwahiyo tunamtaka huyu Kiongozi mwenzetu (Freeman Mbowe) aombe radhi kwa Viongozi wa Dini ili kuleta mustakabali bora kwa Taifa letu.
Abdul Mluya: Maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu
"Malengo yetu ni kuanzisha malengo mahsusi dhidi ya amani na Umoja wa Kitaifa wa Nchi yetu, njia hii ya maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu kwa sababu Ina viashiria vya kuvunja amani, ni haki lakini si kila haki uitumie, haki nyingine unaziacha sio maandanamano tu, ni haki kwa Chama kupeleka maendeleo kwa Wananchi wake lakini hatufanyi."
Abdul Mluya: Waliopinga Kikosi Kazi, leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa
"Inashangaza kuona waliopinga mchakato wa Kikosi Kazi leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa, huu ni unafiki, kiburi na kwenye Demokrasia kama hatutaepuka unafiki, kiburi, kutoshirikiana na wenzako hatutofika, tutaendelea kupingana mpaka pale tutakuwa sote ni wamoja, malengo yetu ya Kikatiba.
"Tunapaswa kutanguliza maslahi ya Wananchi mbele na sio maslahi yetu sisi na matumbo yetu au Vyama vyetu, leo inashangaza sana kuona leo unasikia eti maoni ya Kikosi Kazi yametupwa, maoni mengi ya Kikosi Kazi yamechukuliwa na Vyama vinaendelea kutoa maoni kuboresha Miswada husika, maoni yale tuliyoenda kutoa ni zao la Kikosi Kazi."
View attachment 2874343
Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan Doyo
Doyo: Watu 7 walikufa kabla ya maandamano Zanzibar
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo anasema “Tunaiomba Serikali isitishike kwa ajili ya maandamano ya Chama kimoja kwa faida ya wengi.
“Maandamano ni ajali, nikiwa CUF Mwaka 2001 kabla ya maandamano walikufa watu saba.”
Pia soma:
= Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu
= Kama Jeshi litafanya usafi tarehe 23-24, basi CHADEMA ifanye maandamano tarehe 25 wapite njia zikiwa safi
= Hizi ndizo sababu Watanzania hawatoshiriki maandamano ya CHADEMA
Yes, wanalipwa na Lumumba,.Wanasema nini hawa wapinzani wa hii nchi yetu!