Pre GE2025 Umoja wa Vyama vya Siasa: Hatukubaliani na Maandamano ya CHADEMA, walijitenga nasi, sasa hivi wanatushirikisha

Pre GE2025 Umoja wa Vyama vya Siasa: Hatukubaliani na Maandamano ya CHADEMA, walijitenga nasi, sasa hivi wanatushirikisha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa unaoundwa na Vyama 13 vyenye usajili Nchini unazungumza na Wanahabari, leo Jumatano Januari 17, 2024.

View attachment 2874297
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa, Abdul Mluya

Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa, Abdul Mluya anasema "Mnamo Tarehe 13/01/2024 Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA (Freeman Mbowe) alizungumza na Waandishi wa Habari na kutangaza maandanamano kuishinikiza Serikali kuiondoa Bungeni Miswada Mitatu inayoleta mageuzi ya Kisiasa hapa Nchini, Miswada hiyo ni Muswada wa Sheria ya Uchaguzi, Muswada wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Muswada wa Sheria ya Tume ya Uchaguzi.

"Mimi ni miongoni mwa Watu ambao tuliwasilisha Miswada yetu pale Bungeni kama Chama na Vyama vingine na Siku Mwenyekiti anafunga nilikuwa miongoni mwa Watu waliokuwepo mule ndani na alihitimisha kwa kusema Vyama 18 vimetoa maoni Bungeni, vingine kwa maandishi vingine kama tulivyokwenda lakini Taasisi mbalimbali alizitaja na Viongozi wa Dini.

"Mara baada ya tukio lile kumalizika Mwanasiasa mwenzetu ambaye ni Katibu Mkuu mwenzetu (John Mnyika wa CHADEMA), kazi yetu ilikuwa ni kutoa maoni sio kukosoa Muswada kwa maana ya kuutupa."

Abdul Mluya: Chama kitengeneze sera za kuungwa mkono
Mwenyekiti wa Umoja Umoja wa Vyama vya Siasa ni Katibu Mkuu wa Chama Cha DP, Abdul Mluya anasema "Tufanye siasa za hoja tusigusane maungoni, hata Sheria ya Vyama vya Siasa inasema Chama kitakuwa na wajibu wa kuunda sera kwa lengo la kuungwa mkono, hilo limekaa sahihi sana kuliko njia wanayotaka kuitumia."


Abdul Mluya: CHADEMA waache ubinafsi
Tunawasii sana viongozi wenzetu na chama chao (CHADEMA) kuendelea kutumia njia sahihi zilizopo za Kisheria kushirikina na wengine (sisi) pamoja na kuacha ubinafsi na kuacha tabia ya kupinga kila jambo.

Abdul Mluya: Mbowe aombe radhi
"Viongozi wa Kidini tunaowaheshimu sana walitoa maoni yao, sasa nikitokea Mluya Mimi nikasema utupwe maana yake ni kwamba wale wote waliotoa maoni hawana akili, kwahiyo tunamtaka huyu Kiongozi mwenzetu (Freeman Mbowe) aombe radhi kwa Viongozi wa Dini ili kuleta mustakabali bora kwa Taifa letu.

Abdul Mluya: Maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu
"Malengo yetu ni kuanzisha malengo mahsusi dhidi ya amani na Umoja wa Kitaifa wa Nchi yetu, njia hii ya maandamano yanakinzana na Utamaduni wetu kwa sababu Ina viashiria vya kuvunja amani, ni haki lakini si kila haki uitumie, haki nyingine unaziacha sio maandanamano tu, ni haki kwa Chama kupeleka maendeleo kwa Wananchi wake lakini hatufanyi."

Abdul Mluya: Waliopinga Kikosi Kazi, leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa
"Inashangaza kuona waliopinga mchakato wa Kikosi Kazi leo wanasema maoni ya Kikosi Kazi yamepuuzwa, huu ni unafiki, kiburi na kwenye Demokrasia kama hatutaepuka unafiki, kiburi, kutoshirikiana na wenzako hatutofika, tutaendelea kupingana mpaka pale tutakuwa sote ni wamoja, malengo yetu ya Kikatiba.

"Tunapaswa kutanguliza maslahi ya Wananchi mbele na sio maslahi yetu sisi na matumbo yetu au Vyama vyetu, leo inashangaza sana kuona leo unasikia eti maoni ya Kikosi Kazi yametupwa, maoni mengi ya Kikosi Kazi yamechukuliwa na Vyama vinaendelea kutoa maoni kuboresha Miswada husika, maoni yale tuliyoenda kutoa ni zao la Kikosi Kazi."

View attachment 2874343
Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan Doyo

Doyo: Watu 7 walikufa kabla ya maandamano Zanzibar
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo anasema “Tunaiomba Serikali isitishike kwa ajili ya maandamano ya Chama kimoja kwa faida ya wengi.

“Maandamano ni ajali, nikiwa CUF Mwaka 2001 kabla ya maandamano walikufa watu saba.”


Pia soma:
= Maandamano ni Haki ya Vyama vya Siasa, Serikali itoe kila ushirikiano kwa CHADEMA hata kama uelekeo ni Ikulu
= Kama Jeshi litafanya usafi tarehe 23-24, basi CHADEMA ifanye maandamano tarehe 25 wapite njia zikiwa safi
= Hizi ndizo sababu Watanzania hawatoshiriki maandamano ya CHADEMA



Kwamba chadema wamewaomba muandamane nao? Nchi ya hovyo hii
 
Wapuuzi tayari wamekula hela ya TISS! Nimesikia nao watafanya maandamano! Kumbe kisu kiko mfupani. CCM wanahaha, TISS wana haha! Ikulu inahaha! Policcm wanahaha!. Kutumia mabumunda kama haya hakusaidii kitu. Huyo FIsi mweusi amesema eti maandamano ya kushinikiza si yo ya amani! Ametuhumu vile vile TEC kuwa wameandikiwa maoni na Chadema bila kuelewa kuwa TEC ni wabobezi wa kila kitu!

Maandamano ni ya wananchi wazalendo wote hivyo virusi vilivyokula mlungula ili tuendelee kubaki utumwani kwa kupitia mchakato wa uchafuzi badala ya uchaguzi! Vitashindwa tu!!
Ulaya, Marekani na kote maandamano ya madai haya haya!
THis time hakuna pa kutokea trust me!!
TISS inatawala nchi kupitia CCM ndo maana mashushushu wamejazwa vyamani na serikalini
 
Back
Top Bottom