Jamani wadau nisaidieni mwenye kujua haya mambo, ni umri upi unaoshauriwa kitaalamu kumtahiri mtoto wa kiume, na je kuna njia ngapi za kufanya hiyo kitu.
Maana kuna maneno yanasema eti ukimfanyia akiwa bado mdogo kuanzia miaka 0 hadi mmoja eti atakuja kuwa dhaifu katika ile shughuli ya kikubwa, wengine wanasema ukimfanyia kakua ndio hiyo kitu itamtokea akiwa mkubwa
Pia njia ipi ni salama zaidi mimi najua ya kukata na kushonwa naambiwa ipo nyingine yakufunga na plastiki, je ipi ni nzuri?
Nategaemea msaada wenu waungwana, maana kunasehemu nilisoma eti matatizo mengi ya wanaume kushindwa kuwatimizia wepenzi wao tohara isiyo sahihi ni moja ya sababu