UN kupinga mradi wa Steigler's Gorge ni uhujumu

UN kupinga mradi wa Steigler's Gorge ni uhujumu

SG lazima tujenge hapa Dr. Magufuli namuunga mkono.

Kama UN wangemkemea na serikali yake kuacha kuharibu umoja wa kitaifa, kutumia nguvu, kuwaonea wapinzani hata kusababisha vifo vya watanzania wenzentu , kuacha watu wafanye maandamano kwa amani.
Hapo ningewaona watu wa maana na taasisi yenye akili ila kuzuia SG project wanajionesha walivyo vilaza hadi huko UN.

UN na USA wakafunge wanyama huko Washington DC au Pentagon ila sisi huku Tanzania SG lazima tujenge.

Kwa sasa, tunahitaji SG project kuliko tunavyohitaji wanyama ambao mafisadi tu ndiyo wanaofaidika kwa kuwaua na kukata pembe wakati wananchi hawana umeme.

To hell with UN but SG project must be realized for the betterment of lives of millions of Tanzanians.
 
Wewe ulitaka fact gani kwa mfano.
The pros and cons of 2,100megawatts, hilo halihitaji mjadala.
Project hii ipo inapingwa na UN toka enzi za Mwalimu.
Tukumbuke ni watu hawahawa walipinga hata ujenzi wa TAZARA miaka ya mwanzoni mwa 1970s.

Unfortunately, ingawa ni kweli TAZARA ulichangia kwa kiasi kikubwa ukombozi wa Kusini mwa Afrika lakini kibiashara ni unmitigated disaster. Wanachotuambia hawa wenzetu ni kuwa huu mradi unaweza kuwa kama ulivyo TAZARA hivi sasa.

Amandla........
 
Ni kweli ila pia sio dalili nzuri sana kwa yanayotunyemelea maana inaonekana kana kwamba tunatengwa kiaina kimataifa. Huku UN kule US kwa issue ya ushirikiano na NK. Si busara kusema tu "shikilia hapo hapo"; wao wameshikilia mpini sisi makali. Busara ni kutafuta suluhu sahihi ya namna ya kutoka tuliponasa ili tusonge mbele bila mikwaruzano isiyo ya lazima na "wakubwa". Mwisho wa siku tutaumia sisi tukiendelea kushupaza shingo. Sina hakika kama utanielewa.

Mkuu, duniani kuna watu wa ina nyingi ila aina hii ya WATU WALIOTAYARI KUVUNJA, KULIKO KUPINDISHA ni wachache mno na nadhani kwakua ndio viongozi wanaohitajika na nchi za ulimwengu huu wa tatu... Hewala Bwana, ni kauli ya kitwana.
 
Sidhani kama UN wamekurupuka kama wanapinga huu mradi wana evidence za kutosha kwa nini wanapinga huu mradi embu turudi nyuma mradi wa bomba la gesi Mtwara to Dar impact yake kwa Uchumi wa Tanzania inaonekana au ndio siasa kila kitu ndio
 
Msitake kujifanya mnaipinga UN kuhusu kugomea huo mradi, ukweli kuhusu ujenzi wa huo mradi ni kukosa hela. Laiti hela zingekuwepo leo hii huo mradi ungekuwa umeshaanza. Awamu iliyopita kelele ilikuwa ni uchumi wa gas, leo hii hakuna anayeongelea gas na tunataka kurukia mradi mwingine huku hakuna hata cent kumi. Pata majibu ya msingi kwanza kwanini sio gas bali ni stiegler gorge?


tindo,
Mkuu
Gas siyo renewable energy ila SG project ni long life project kwa hiyo bora tuiendeleze hiyo SG project.
Gas ilikuwa kisiasa zaidi na kifisadi mno mno.

Any way, ije mvua au jua ila Tanzania kwa sasa SG project ni ya muhimu sana kwa nchi hii hata hivyo imechelewa sana kutekelezwa.
 
SG lazima tujenge hapa Dr. Magufuli namuunga mkono.

Kama UN wangemkemea na serikali yake kuacha kuharibu umoja wa kitaifa, kutumia nguvu, kuwaonea wapinzani hata kusababisha vifo vya watanzania wenzentu , kuacha watu wafanye maandamano kwa amani.
Hapo ningewaona watu wa maana na taasisi yenye akili ila kuzuia SG project wanajionesha walivyo vilaza hadi huko UN.

UN na USA wakafunge wanyama huko Washington DC au Pentagon ila sisi huku Tanzania SG lazima tujenge.

Kwa sasa, tunahitaji SG project kuliko tunavyohitaji wanyama ambao mafisadi tu ndiyo wanaofaidika kwa kuwaua na kukata pembe wakati wananchi hawana umeme.

To hell with UN but SG project must be realized for the betterment of lives of millions of Tanzanians.
umeme wa gesi una tatizo gani kwani kuendelezwa? inawezekana tunahitaji vyote viwili, hebu tungoje muda hutaamua, na pengine Magu ana plan zake, mkumbuke huyu jamaa anapenda vitu vya kuonekana usishangae anataka 5000mgw nchi nzima.
 
Inasiktisha sana...

UN ni vibaraka wa Marekani...

Mbona Ethiopia hajanyoshewa kidole kwenye ujenzi wake wa Dam ya umeme...

Wakati watatumia maji ya mto Nile na kusababisha upungufu wa 2% ya maji yanayozalishwa na huo mto, kusababisha nchi zinazotegemea huo mto kuathirika...


Cc: mahondaw
 
Mradi wa steiglers gorge ni unnecessary na ecological destructive, hilo halina mjadala.

Tuna gesi ambayo mpaka leo iko under utilised.
Tuna makaa ya mawe, the cheapest source of energy tunayoweza kutumia. Its destructive pia lakini on the good side yako kwenye maeneo ambayo ni remote and not in one of the largest protected reserve site in the world.
Tuna uwezo wakuproduce wind energy in a large quantity, ila mpaka leo hakuna any signs ya kuanzisha mradi huo.
Tuna a long coastline yenye uwezo wakutuwezesha kuproduce energy kupitia tidal waves.

Ila vyote hivyo hamna mpango navyo au hamtaki kuvitekeleza in full.

Juzi juzi a few years back serikali imetoka kuiomba UN kufanya boundary change ya selous kwa ajili ya uranium mining ambayo in the end itakuja kuproduce a ton of radioactive waste ambayo ita-affect the game reserve.

Hapo hapo kuna swala la ujangili humo kwenye hiyo reserve, kwenye idadi ya tembo wameshuka toka 60,000+ in 2009 mpaka 10,000 in 2013.

Tena sasa mnataka mjenge a hydro plant ambayo ita-flood a large area of the reserve na kuharibu the ecosystem ya eneo hilo,just from the construction alone.

Yani sisi ni kuharibu haribu tuu...

Hydro plants zetu nyingi if not all, zimetengenezwa wakati wa mkoloni, hivi mnadhani wangeshindwa kujenga hiyo hydro plant kwenye hiyo reserve. Mnadhani ni wajinga sana mpaka wakaamua kuachana na hiyo idea. Tena walikuwa na uwezo both financially na engineering wise, kwasababu kama waliweza kutekeleza a large project such as reli ya kati, project kama hii isingewashinda.

Muda mwingine tusiwe wabishi, natuangalie impact ya vitu tunavyotaka kufanya.
Mkuu wewe inaelekea ni kijana wa juzi juzi tu.
Miradi karibu yote ya Hydro imejengwa na Mwalimu.
Hata huu wa Stieglers Gorge ulikuwa kwenye drawing boards.

Mimi nimeingia ndani ya Kidatu na kuona zile 4 turbines zinazofua 200MW, cha mtoto.
Nimebahatika vile vile kuingia NDANI ya Nuclear Plant moja huko Ulaya, yenye ukubwa kama jengo la Yanga.
Hiyo Plant ilikuwa inatoa 900MW!
Sasa leo hao UN waambie wakusaidie ujenge plant kama hiyo hapa nchini , wataishia kukulisha studies kama unavyozionyesha za kwako hapa mtandaoni!

Tatizo kubwa watanzania mmeaminishwa na kulishwa maneno ambayo in principle ni defeatist, mwadhani maendeleo ni lelemama na yatakuja kwa feasibility studies.

Mrusi Yuri Gagarin, binadamu wa kwanza anga za juu, alifanyiwa feasibility study ipi kufanikiwa!
Na je ile Apollo mission iliyilipuka na kuua wanaanga karibu nane wa kimarekani, yenyewe haikufanyiwa any studies?

Maendeleo ni multifaceted.
Gesi tutaitumia, makaa ya mawe yatatumika.
Wengi wenu muishio Dar wala hamjui na hamjafika maeneo ya nishati hizo, zinatumika hata leo.

Tukitegemea maendeleo yetu yatakuja kwa kumfurahisha mzungu aliyekutawala, wengine hata kiakili, maendeleo yatachelewa sana.
 
Kinacho tukwamisha Afrika ni Ujinga , Ubinafsi na tutabakia kuchonga Domo sana maendeleo zero
 
tindo,
Mkuu
Gas siyo renewable energy ila SG project ni long life project kwa hiyo bora tuiendeleze hiyo SG project.
Gas ilikuwa kisiasa zaidi na kifisadi mno mno.

Any way, ije mvua au jua ila Tanzania kwa sasa SG project ni ya muhimu sana kwa nchi hii hata hivyo imechelewa sana kutekelezwa.
Spot on mkuu!
 
Magu asilegeze kamba, ashikilie apo apo. Go Magu go. Ili tupate freedom ya nishat na hatimae ya uchumi.
Hahahaha wabongo bhana kwahyo wanaokuhujumu ndio hao hao mikopo yao mnawaomba kila siku..... Wanawajengea reli na bomba alafu wakishauri eti wahujumu ssa kma hawawatakii mema si wangewanyima mikopo

Wabongo bhana
 
Nimesoma katika gazeti la The Guardian on sunday, tar 25 Feb 2018, ati UN(Umoja wa Mataifa), wanapinga kujengwa kwa kituo cha kuzalisha umeme kiasi cha 2,100MW ati kwa sababu za mazingira.

Huu ni uhujumu, full stop!

UN inatumiwa tu, ili ujumbe uonekane ati unatoka chombo ambacho ni fair, lakini ujumbe huo ni kazima unatoka nchi zinazofaidika na matatizo yetu ya nishati.

Kampuni za kimarekani kama AGGREKO, DOWANS na nyingine nyingi ni wazi zisingependa kuona mradi huu wa Stieglers Gorge ukifanikiwa, maana watakosa ulaji wanaofaidika nao leo.

Kama ingewapendeza UN, basi Three Gorges Dam ya China, Aswan Dam ya Misri, Akosombo Dam ya Ghana vyote visingejengwa kwa sababu za kimazingira.

Nampongeza na Rais Magufuli na kumpa moyo kushika moyo ule ule ili nchi ijitawale kinishati.
Kwa Magu wataula wa chuya! Prezdaa Magu songa mbele baba, kurudi nyuma, mwiko!
Kwa mazuri unayofanya tuko nyuma yako, yale mengine hapana!
 
Mradi wa steiglers gorge ni unnecessary na ecological destructive, hilo halina mjadala.

Tuna gesi ambayo mpaka leo iko under utilised.
Tuna makaa ya mawe, the cheapest source of energy tunayoweza kutumia. Its destructive pia lakini on the good side yako kwenye maeneo ambayo ni remote and not in one of the largest protected reserve site in the world.
Tuna uwezo wakuproduce wind energy in a large quantity, ila mpaka leo hakuna any signs ya kuanzisha mradi huo.
Tuna a long coastline yenye uwezo wakutuwezesha kuproduce energy kupitia tidal waves.
Tuna uwezo wa kupower miji mingi midogo Tanzania kwa kutumia umeme wa jua tu.

Ila vyote hivyo hamna mpango navyo au hamtaki kuvitekeleza in full.

Juzi juzi a few years back serikali imetoka kuiomba UN kufanya boundary change ya selous kwa ajili ya uranium mining ambayo in the end itakuja kuproduce a ton of radioactive waste ambayo ita-affect the game reserve.

Hapo hapo kuna swala la ujangili humo kwenye hiyo reserve, kwenye idadi ya tembo wameshuka toka 60,000+ in 2009 mpaka 10,000+ in 2013. Tumekaa tu, wala hakuna serious effort kukabiliana na hilo.

Tena sasa mnataka mjenge a hydro plant ambayo ita-flood a large area of the reserve na kuharibu the ecosystem ya eneo hilo,just from the construction alone.

Yani sisi ni kuharibu haribu tuu...

Hydro plants zetu nyingi if not all, zimetengenezwa wakati wa mkoloni, hivi mnadhani wangeshindwa kujenga hiyo hydro plant kwenye hiyo reserve. Mnadhani ni wajinga sana mpaka wakaamua kuachana na hiyo idea. Tena walikuwa na uwezo both financially na engineering wise, kwasababu kama waliweza kutekeleza a large project such as reli ya kati, project kama hii isingewashinda.

Muda mwingine tusiwe wabishi, natuangalie impact ya vitu tunavyotaka kufanya.

mkuu hakuna project ambayo mkoloni aliitekeleza bila kuna na faida kwake kiuchumi, as hakua na lengo la kuiendeleza nchi kiviwanda, large projects za umeme hazikua na maana kwake. Na si kisingizio cha mazingira. Maana wangekua wanajali mazingira wasingetoboa ozone layer, hadi leo wasingeumiza watu na viumbe Niger delta.
 
Wakubwa hawa wanaotoboa ozone na kuharibu mazingira leo hii wanadai stigler's inaharibu mazingira. Sbb kubwa hawataki 'independency ya energy sector' Africa, sbb wanajua economically itawaathiri wao.
 
tindo,
Mkuu
Gas siyo renewable energy ila SG project ni long life project kwa hiyo bora tuiendeleze hiyo SG project.
Gas ilikuwa kisiasa zaidi na kifisadi mno mno.

Any way, ije mvua au jua ila Tanzania kwa sasa SG project ni ya muhimu sana kwa nchi hii hata hivyo imechelewa sana kutekelezwa.

Mkuu Poise sipingi maoni yako na ninayaheshimu sana na sipingi mradi wa maji ila tuwekane sawa kwanza ili tusiburuzwe. Umesema mradi wa Gas sio renewable, lakini tuliambiwa kwa mujibu wa matumizi yetu tungetumia nishati ya gas kwa 100yrs ukikamilika. Unasema gas ilikuwa kisiasa zaidi, lakini ambacho hujaangalia na kujiuliza hata mradi huu wa stiegler gorge unaletwa na mwanasiasa, tena aliyekuwa kwenye kundi lilikotuaminisha gas ndio mkombozi wetu, huku akirusha vijembe kwamba wapinzani wanataka kukwamisha maendeleo kwa kupinga jinsi mradi utakavyotekelezwa.

Mkuu mpaka sasa tuna miradi ya umeme ya maji na tatizo limekuwa ni upungufu wa maji kutokana na mabadiliko ya tabia nchi. Hii ndio iliyokuwa sababu kubwa ya kuhamia kwenye gas. Wakati huo huyu anayetaka kutekeleza mradi wa stiegler gorge kwa 3tr alikuwa anashangilia mradi wa gas bila kupinga waziwazi na kupendekeza huu wa maji. Kumbuka alikuwa waziri na mbunge, kumaanisha mradi wa gas ulipata baraka zake zote. Leo ni kipi kinakufanya umuamini kwa haya anayosema, huku akiwa hana hata shilingi mkononi ya huo mradi. Mkuu Poise haya ndio majukwaa ya kuhoji kwa kina, huenda mchango wako unaangaliwa na wafanya maamuzi, unapoingia kichwakichwa bila kuhoji kwa kina unaruhusu maamuzi mabovu kufanyika. Kuwa makini ndugu.
 
Back
Top Bottom