UN kupinga mradi wa Steigler's Gorge ni uhujumu

UN kupinga mradi wa Steigler's Gorge ni uhujumu

Nimesoma katika gazeti la The Guardian on sunday, tar 25 Feb 2018, ati UN(Umoja wa Mataifa), wanapinga kujengwa kwa kituo cha kuzalisha umeme kiasi cha 2,100MW ati kwa sababu za mazingira.

Huu ni uhujumu, full stop!

UN inatumiwa tu, ili ujumbe uonekane ati unatoka chombo ambacho ni fair, lakini ujumbe huo ni lazima unatoka nchi zinazofaidika na matatizo yetu ya nishati.

Kampuni za kimarekani kama AGGREKO, DOWANS na nyingine nyingi ni wazi zisingependa kuona mradi huu wa Stieglers Gorge ukifanikiwa, maana watakosa ulaji wanaofaidika nao leo.

Kama ingewapendeza UN, basi Three Gorges Dam ya China, Aswan Dam ya Misri, Akosombo Dam ya Ghana vyote visingejengwa kwa sababu za kimazingira.

Nampongeza sana Rais Magufuli na kumpa moyo kushika moyo ule ule , ili nchi ijitawale kinishati.

Ukiona Shetani anakupiga vita ujue uko sahihi, kaza mwendo! Ukiona Shetani anakuchekea ujiulize umekosea wapi! Pia ukiona UN na US wanakupiga vita ujue uko sahihi, kaza mwendo!

Ukiona hao watu wanakusifia ujue kuna mahali umekosea, tafuta hilo kosa jirekebishe, songa mbele!

Walianza na TAZARA, sasa hivi wamegeukia Umeme wetu wa SG!

Hivi na sisi tunaweza kuwapinga katika project zao zozote, km vita vya Iraq na Libya, hivyo vita haviharibu mazingira ukiachilia mbali vifo vya watu wasio na hatia?

Dr John P. J. Magufuli, usiwasikilize, sio watu wazuri hawa, wana uchungu wa makinikia uliyoyazuia Bandarini. Kaza mwendo baba!
 
Afadhali UN mmetufanya tupumue hata hivyo bajeti ya ujenzi haipo tukimaliza kununua wapinzani tutajenga

Lukwafya
 
Magufuli Magufuli Magufuli Dr.JPM
Mbona unachelewa kujenga....kuanza Mradi wa Stiegliers gorge Baba Agggrrr....wazungu Wengi hawapendi huu Mradi....wanataka tuendelee kuwakopa hela....

Makampuni ya Ulaya ya Aggreko,Songas,Moore&Prom inawezekana kabisa Wakatumia nguvu zooooote Mradi huu Ushindwe...coz Maslahi yao ya Gas,jaman Pitia JF baba usome
Kamwe USIRUDI NYUMA,UKIUACHA TUU HUU MRADI JUA UCHUMI WA VIWANDA KWISHNEY NA MITAJI YA HELA TUTAWATEGEMEA WAZUNGU MPAKA TUFE...
STIEGLIERS GORGE NDO ITALETA KITU TUNAITA "MULTIPLIERS EFFECTS" KATIKA UCHUMI.
 
Magu piga kazi achana na kelele za hawa manyumbu wa humu na hao wenzao wa huko nje
Na kwa huyu jamaa wakaanga sumu dhidi ya nchi yao wameshapoteza. Hii miradi jamaa lazima atakamilisha.
 
View attachment 701335

Nimesoma katika gazeti la The Guardian on sunday, tar 25 Feb 2018, ati UN(Umoja wa Mataifa), wanapinga kujengwa kwa kituo cha kuzalisha umeme kiasi cha 2,100MW ati kwa sababu za mazingira.

Huu ni uhujumu, full stop!

UN inatumiwa tu, ili ujumbe uonekane ati unatoka chombo ambacho ni fair, lakini ujumbe huo ni lazima unatoka nchi zinazofaidika na matatizo yetu ya nishati.

Kampuni za kimarekani kama AGGREKO, DOWANS na nyingine nyingi ni wazi zisingependa kuona mradi huu wa Stieglers Gorge ukifanikiwa, maana watakosa ulaji wanaofaidika nao leo.

Kama ingewapendeza UN, basi Three Gorges Dam ya China, Aswan Dam ya Misri, Akosombo Dam ya Ghana vyote visingejengwa kwa sababu za kimazingira.

Nampongeza sana Rais Magufuli na kumpa moyo kushika moyo ule ule , ili nchi ijitawale kinishati.
Wakitugomea kabisa turudi kwenye Umeme wa gesi maana walisema ndio suluhisho na tunazo cubic meters matrilioni mengi.

Bomba lilishajengwa hadi Dsm na Kinyerezi 1 & 2 zina tumia gesi. Au kuna shida gani kwenye gesi?
 
Usikimbilie mambo ya marekani kublack mail mataifa na vijimsaada uchwara ili yasiangukie Soviet union...hiyo haina uhusiano wowote na Tanzania kutokuwa na vipaumbele

Mlisema gesi itamaliza shida ya umeme tena mtauza mpaka DRC sasa kelele zile zimeishia wapi mpaka leo hii mseme SG ndio habari ya mujini???

Kingine unasema wazungu hivi wazungu vile..... Nachoshangaa mmesign mikataba mingi sana mkuu ambayo inawafanya muwe eligible kupata misaada flani sasa kwa kuwa nyie ni wakopaji miaka yote mmeshajifunga kwenye treaty za ajabu ajabu kuanzia za utawala bora mpaka mazingira sasa wakiisimamia kwanini mnaanza kelele??

Nilitegemea wwe kma mtu makini (i believe so) ungeweka hapa findings za UN kabla hujaconclude sio mnasema tu UN blah blah hku am sure taarifa kamili au ripoti hujaisoma mnalipeleka wapi taifa kila kitu kujifanya mnajua sana ilihali hao hao UN mnaowaponda ndio wanawafanya muwe eligible kupokea misaada ya mataifa makubwa na world bank!!!

Kama taifa tujikite kwenye mradi mmoja whether UN is right or wrong..... Gesi tumalizane nayo meanwhile tuinue kilimo na uvuvi etc uchumi ukuwe sio mkapa makaa ya mawe.. kikwete gesi.... Magu SG alafu awamu ya tano waseme SOLAR!!! Ndio nini hki sasa
Mkuu UNASEMA....TULISEMA.......maana yake haya masuala hayakuhusu!
Hivyo basi maelezo yoyote hayatakukidhi!
Endelea na msimamo wako wa kukaa kando kwenye masuala ya msingi.
 
Mkuu tujadiliane kwa uhuru na amani bila kushutumiana au kukashfiana maana hatushindani

Kupungua kwa maji Mtera wanalisema wazungu?

Mito mingi ya zamani haipitishi maji tena nalo unataka kuwasingizia wazungu?

Tunahitaji kufanya study tena 2100Mw ya miaka ya 70 hauwezi kuwa leo, vitu vingi vimebadilika na vitaendelea kubadilika
Sasa hilo la study linahusianaje na UN? Hao wanajiita conservationist linawahusu nini? Wao wanaangalia madhala ya kimazingira na siyo hasara ya kiuchumi.

UN wanahangaika na mambo ya kisiasa, sasa leo mtu analeta mambo ya bwana!
 
Mradi wa steiglers gorge ni unnecessary na ecological destructive, hilo halina mjadala.

Tuna gesi ambayo mpaka leo iko under utilised.
Tuna makaa ya mawe, the cheapest source of energy tunayoweza kutumia. Its destructive pia lakini on the good side yako kwenye maeneo ambayo ni remote and not in one of the largest protected reserve site in the world.
Tuna uwezo wakuproduce wind energy in a large quantity, ila mpaka leo hakuna any signs ya kuanzisha mradi huo.
Tuna a long coastline yenye uwezo wakutuwezesha kuproduce energy kupitia tidal waves.
Tuna uwezo wa kupower miji mingi midogo Tanzania kwa kutumia umeme wa jua tu.

Ila vyote hivyo hamna mpango navyo au hamtaki kuvitekeleza in full.

Juzi juzi a few years back serikali imetoka kuiomba UN kufanya boundary change ya selous kwa ajili ya uranium mining ambayo in the end itakuja kuproduce a ton of radioactive waste ambayo ita-affect the game reserve.

Hapo hapo kuna swala la ujangili humo kwenye hiyo reserve, kwenye idadi ya tembo wameshuka toka 60,000+ in 2009 mpaka 10,000+ in 2013. Tumekaa tu, wala hakuna serious effort kukabiliana na hilo.

Tena sasa mnataka mjenge a hydro plant ambayo ita-flood a large area of the reserve na kuharibu the ecosystem ya eneo hilo,just from the construction alone.

Yani sisi ni kuharibu haribu tuu...

Hydro plants zetu nyingi if not all, zimetengenezwa wakati wa mkoloni, hivi mnadhani wangeshindwa kujenga hiyo hydro plant kwenye hiyo reserve. Mnadhani ni wajinga sana mpaka wakaamua kuachana na hiyo idea. Tena walikuwa na uwezo both financially na engineering wise, kwasababu kama waliweza kutekeleza a large project such as reli ya kati, project kama hii isingewashinda.

Muda mwingine tusiwe wabishi, natuangalie impact ya vitu tunavyotaka kufanya.
Acha woga, aiseee.
 
Hiyo ni heading ya gazeti. Soma ndani uelewe wana maana gani? UN mkuu wake ni Secretary general. Baraza la usalama lina mkuu wake anaitwa rais. Ukisoma ndani lazima utagundua uzembe wa msomaji. UN as UN ni chombo cha kisiasa, haiwezi kuzungumzia ujenzi wa bwawa. Never! Au ni UNESCO, Au ni UNEP au nini????....
Sitakudadavulia kwa pesa yangu, kanunue na wewe usome uelewe!
 
Utadhani wana hela kumbe za kuomba. Ushamba tu. UN kazia
 
Sitakudadavulia kwa pesa yangu, kanunue na wewe usome uelewe!
Unadhani wote tunaishi msimbazi! Au umeona aibu ya kuamini heading ya gazeti. Jilazimishe kuwa msomi. Kwangu mimi nikiona heading kama hiyo, brain inajiongeza yenyewe mara moja!
 
Unadhani wote tunaishi msimbazi! Au umeona aibu ya kuamini heading ya gazeti. Jilazimishe kuwa msomi.

Mkuu mi si msomi lakini bahati mbaya nina akili kama punje ya dalahari.
Sasa hapo hapo ulipo, google hilo gazeti ulisome.
 
Yaani wewe BRAMO UMEFILISIKA KIMAWAZO ! Hivi mpaka sasa hujaelewa mradi Wa Stiegler's Gorge ukikamilika utakuwa na manufaa gani kwa Taifa ? Pole sana!!
 
Mkuu UNASEMA....TULISEMA.......maana yake haya masuala hayakuhusu!
Hivyo basi maelezo yoyote hayatakukidhi!
Endelea na msimamo wako wa kukaa kando kwenye masuala ya msingi.
Yeah MLISEMA maana nachukulia wwe mtoa taarifa umechukua upande wa serikali kwenye kutetea mradi wa Stiegler's.... Hivyo serikali hiyo hiyo ambayo leo inasema SG ndio habari ya mujini ilisema miaka 4 iliopita kwamba Gesi ndio suluhu la nishati ya umeme hapa TZ hivyo nashangaa badala nyie wasomi mhoji hizo ahadi za gesi kama zimefikia malengo ndio kwanza mnatuminisha tena kwamba SG ndio mradi wa kumaliza shida ya umeme.... Hivi hizi ahadi mpaka lini?? Wasomi tunawategemea muhoji ndio kwanza mnasupport huu ujinga wa SG

Huoni tuna miradi mingi inahitaji funding hasa ya maji vijijini ama ya kilimo cha umwagiliaji au hata kuongeza ndege kwa ajili ya ATCL..... We have a way lot than switching lanes every now on then be it from hydro to coal to gas.... And then guess what!! We are talkin about hydro again???

Duh kazi ipo
 
Hapa nafuatilia comment za wale wapenda Wazungu. Nione .
Nani anayependa wazungu kuliko serikali ambayo ndio moja ya wakopaji na wafutiwa madeni wakubwa na wazungu afterall waliingia mikataba mibovu kuanzia gesi hadi madini na kusababisha hasara ya trillion zaidi ya 400 kwa mujibu wa ripoti za kamati zote 4!!!! Nani mpenda wazungu hapo
 
Yaani wewe BRAMO UMEFILISIKA KIMAWAZO ! Hivi mpaka sasa hujaelewa mradi Wa Stiegler's Gorge ukikamilika utakuwa na manufaa gani kwa Taifa ? Pole sana!!
Hapana hajapinga anashangaa tu serikali ilisema gesi ndio suluhu ghafla tena tunarudi kwenye umeme wa kutegemea maji!!!!

Yaani kwa kuwa umeme wa gesi tulishaanza kufua basi pesa hyo ya stiegler ielekezwe kwingine mfano kilimo au uvuvi n.k ili nchi isonge mbele maadam alternative ipo kuliko miradi miwili target moja wakati kuna watu wanategemea kilimo cha mvua bado na wapo karne ya 21.... Kwanni msiwekeze huko kila siku umeme umeme wakati gesi ipo
 
Back
Top Bottom