Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Kwanini iwe ni lazima kujua majibu ya ulimwengu na kifo ili kuipinga dhana ya uwepo wa Mungu?

Unajua kuwa tunaweza kujua uongo wa kitu bila kujua ukweli halisi ni upi?




Thibitisha kwamba unaweza kujua uongo wa kitu bila kujua ukweli halisi.
 
Nimekuuliza swali la kipofu. Umejibu juu juu kwa jibu jepesi sana.

Mimi sio muanzisha hoja.. ila kwa hilo jibu sizani kama unaweza mshawishi mtu mwenye akili alikubali.

Jibu la swali lako kuhusu kifo. Kifo kipo sababu hakuna kinachodumu milele. Hata vitu tunavyovitengeneza sisi binadamu kama bulb, magari, simu, etc huwa kuna muda wake vina kufa tu.
Jua lina miaka mingapi? na je? Unaweza kuthibitisha kwamba jua litakuwa na mwisho pia?
 
Kijana unatikisa mbuyu umejikuta unatikisa makalio yako mwenyewe.

Hata kama huamini achana na hilo DUDE linaloitwa MUNGU. Lipo nje ya uwezo wako kulielewa.

tafuta muda wa peke yako, uyaangalie mazingira yako milima na mabonde, nyota angani, wanyama, samaki, wadudu, ndege, n.k (angalia usiku na muda wa mchana)

Utaanza taratibu kugundua kuwa kumuamini MUNGU inahitaji kuuvua huo ujuaji wako.

tuliza akili kijana!
Be still and know that I AM GOD!

Kama hujatulia kutafakari unaweza kusema chochote! Utakapotulia na kufanya tafakuri utajua ya kuwa yeye ni Mungu
 
Sasa kama hamjajua, kwanini mmehitimisha??
Kwa sababu hakuna hitimisho mbadala. Ww ukikuta chungu porini na huoni aliyekileta pale utahitimisha kuwa binadamu alikuwepo pale porini, ili useme sio binadamu kaleta inabidi ulete hitimisho mbadala lisilo na shaka la sababu ya uwepo wa chungu porini.

Na sisi hivyo hivyo tumeukuta Ulimwengu tunaamini kuna inteligent behind tuliyoyakuta na hiyo inteligent ni MUNGU. Sasa kama ww unajua hakuna inteligent inayoitwa MUNGU toa majibu ya uwepo wa ulimwengu yasiyo na shaka kinyume na hapo ni sawa na mlevi anashindana na sura yake kwenye kioo kuwa nani ana ulimi mrefu. Hatopatikana mshindi na anapoteza muda tu.
 
Usioonekana kwa macho ya nyama yaani ndani ya ulimwengu huu kuna ulimwengu mwingine maisha yanaendelea Ili kuuona hata kuungia ni lazima uwe na macho ya rohoni.
Pale kigamboni ferry mkono wa kulia zinapopaki boti za uvuvi kuelekea chuo cha Mwalimu Nyerere kuna mlango wa kuingia ulimwengu mwingine, pembeni Mwa ghorofa la bandarini baharini kuna mlango wa kuingia ulimwengu mwingine,kwa macho ya kawaida huwezi ona.
Viumbe vyenye uwezo wa kuona ulimwengu usioonekana ni watoto wadogo ambao awajaanza kuongea, vichaa, bubu, wachawi, waganga, watumishi original wa MUNGU,wanyama mfano mbwa,paka,nk
Unatumia uongo mmoja kuelezea uongo mwingine.

Macho ya rohoni ni yapi?
 
Kwaiyo wazungu wana nafuu kidogo kwenye kufata dini ndio maana wakabarikiwa kuliko sisi?
Asili ya maendeleo yao imetoka na Ukristo ndio uliwapa elimu na ustaarabu.
Hakuna maendeleo pasipo ustaarabu.Mtu aliyestarabika na mwenye hofu ya Mungu hawezi kuwa fisadi kwa kuiba kodi za wananchi na kwenda kununua mabus au kudhamini timu ya mpira huku maelf wakifa njaa,wakikosa huduma muhimu.

Mtu mwenye dini utanguliza maslai ya wengine kabla yake, mtu mwenye dini ulijenga taifa lake na sio tumbo lake.
 
Kwa sababu hakuna hitimisho mbadala. Ww ukikuta chungu porini na huoni aliyekileta pale utahitimisha kuwa binadamu alikuwepo pale porini, ili useme sio binadamu kaleta inabidi ulete hitimisho mbadala lisilo na shaka la sababu ya uwepo wa chungu porini.

Na sisi hivyo hivyo tumeukuta Ulimwengu tunaamini kuna inteligent behind tuliyoyakuta na hiyo inteligent ni MUNGU. Sasa kama ww unajua hakuna inteligent inayoitwa MUNGU toa majibu ya uwepo wa ulimwengu yasiyo na shaka kinyume na hapo ni sawa na mlevi anashindana na sura yake kwenye kioo kuwa nani ana ulimi mrefu. Hatopatikana mshindi na anapoteza muda tu.
Huo mfano wa chungu na Mungu vinaendana kweli?
Atleast Chungu tunajua kimetengenezwa na binadamu..pamoja na kuwa kinaweza kupelekwa na mto porini.

Lakini Mungu hata hatuna uhakika kama yupo achilia mbali kama aliumba ulimwengu.
 
Mimi ni kijana ambaye Kwa muda wa miaka 2 nimekuwa nikifatilia mijadala mbalimbali hapa Jf katika jukwaa hili la intelligence. Moja ya mijadala ambayo imekuwa ikinivutia sana ni hii ya dhana ya uwepo wa Mungu.

Swali kubwa ambalo nimeku wa nikijiuliza ni " Mungu alitoka wapi"

Baada ya kuisoma sana biblia na Quran pamoja na kuwahoji viongozi mbalimbali wa dini, hatimaye nikapata jibu la swali lililonitatiza muda mrefu, Mungu alitoka wapi?

Nimegundua kuwa muumba wa Mungu ni mwanadamu. Yes mwanadamu kama Mimi na wewe ndiye aliyemuumba Mungu.

Kwanini nimefikia hitimisho hilo?

Vitabu tunavyoaminishwa kuwa ni vya Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu ( biblia & Quran) ni vitabu vyenye makosa mengi sana ya kimantiki na habari nyingi zenye utata, jambo ambalo tusingetegemea liwepo katika kitabu kilichoandikwa kwa muongozo kutoka kwa Mungu mkuu mwenye uwezo asiyeshindwa na kitu.

Uwepo wa habari hizo zenye utata zinadhihirisha moja kati ya mambo yafuatayo.

1. Mungu hana ukuu tunaoambiwa ndio sababu ameshindwa kutoa mwongonzo mzuri katika kuandika kitabu kisicho na makosa ya kimatinki.

2. Habari hizi ni zao la fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za giza na ujinga. Mwanadamu ambae alitaka kutafuta majibu mepesi katika maswali magumu yaliyomzunguka ndio sababu zina utata.

Kama jibu ni 1 basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo Bali aliyepo ni dhaifu na mbabaishaji aliyeshindwa kuandika vizuri kitabu kinachomuelezea yeye mwenyewe.

Kama jibu ni 2 ,basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo ndiyo sababu akatokea mtu akatunga habari kutokana na fikra zake mwenyewe. Angekuepo asingeruhusu magepu katika fikra za mwanadamu ambayo yamepelekea mwanadamu huyo kujitungia majibu mepesi na habari zenye utata ili kuziba hayo magepu katika fikra zake.

Pointi zote mbili utaona zinaonyesha kuwa Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu mjuzi wa yote hayupo Bali " ama aliyepo ni dhaifu,mbabaishaji na asiye na uelewa wowote kuhusu ulimwengu, ama dhana nzima ni hadithi ya kutungwa katika fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za ujinga na kukosa access ya taarifa mbalimbali.

Nawasilisha.


Ingekutosha kama Mungu angekuumba Nyani.
 
Thibitisha kwamba unaweza kujua uongo wa kitu bila kujua ukweli halisi.
Ukiniambia 234 × 457= 12 nitajua ni uongo hata kama sijui jibu la moja kwa moja la 234×457 ni ngapi.

Kwasababu ya kanuni ya muhimu kabisa kwamba kwenye hesabu za kuzidisha namba nzima, jawabu lazima Liwe kubwa kuzidi namba zilizotumika kuzidishwa. Hapo jibu ni dogo kuliko namba Za awali hivyo sihitaji kujua jibu halisi la 234×457 ni ngapi ili kujua kuwa jibu la 12 ni uongo
 
Kijana unatikisa mbuyu umejikuta unatikisa makalio yako mwenyewe.

Hata kama huamini achana na hilo DUDE linaloitwa MUNGU. Lipo nje ya uwezo wako kulielewa.

tafuta muda wa peke yako, uyaangalie mazingira yako milima na mabonde, nyota angani, wanyama, samaki, wadudu, ndege, n.k (angalia usiku na muda wa mchana)

Utaanza taratibu kugundua kuwa kumuamini MUNGU inahitaji kuuvua huo ujuaji wako.

tuliza akili kijana!
Hakuna hakika kuwa mungu yupo.
 
Mimi ni kijana ambaye Kwa muda wa miaka 2 nimekuwa nikifatilia mijadala mbalimbali hapa Jf katika jukwaa hili la intelligence. Moja ya mijadala ambayo imekuwa ikinivutia sana ni hii ya dhana ya uwepo wa Mungu.

Swali kubwa ambalo nimeku wa nikijiuliza ni " Mungu alitoka wapi"

Baada ya kuisoma sana biblia na Quran pamoja na kuwahoji viongozi mbalimbali wa dini, hatimaye nikapata jibu la swali lililonitatiza muda mrefu, Mungu alitoka wapi?

Nimegundua kuwa muumba wa Mungu ni mwanadamu. Yes mwanadamu kama Mimi na wewe ndiye aliyemuumba Mungu.

Kwanini nimefikia hitimisho hilo?

Vitabu tunavyoaminishwa kuwa ni vya Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu ( biblia & Quran) ni vitabu vyenye makosa mengi sana ya kimantiki na habari nyingi zenye utata, jambo ambalo tusingetegemea liwepo katika kitabu kilichoandikwa kwa muongozo kutoka kwa Mungu mkuu mwenye uwezo asiyeshindwa na kitu.

Uwepo wa habari hizo zenye utata zinadhihirisha moja kati ya mambo yafuatayo.

1. Mungu hana ukuu tunaoambiwa ndio sababu ameshindwa kutoa mwongonzo mzuri katika kuandika kitabu kisicho na makosa ya kimatinki.

2. Habari hizi ni zao la fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za giza na ujinga. Mwanadamu ambae alitaka kutafuta majibu mepesi katika maswali magumu yaliyomzunguka ndio sababu zina utata.

Kama jibu ni 1 basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo Bali aliyepo ni dhaifu na mbabaishaji aliyeshindwa kuandika vizuri kitabu kinachomuelezea yeye mwenyewe.

Kama jibu ni 2 ,basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo ndiyo sababu akatokea mtu akatunga habari kutokana na fikra zake mwenyewe. Angekuepo asingeruhusu magepu katika fikra za mwanadamu ambayo yamepelekea mwanadamu huyo kujitungia majibu mepesi na habari zenye utata ili kuziba hayo magepu katika fikra zake.

Pointi zote mbili utaona zinaonyesha kuwa Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu mjuzi wa yote hayupo Bali " ama aliyepo ni dhaifu,mbabaishaji na asiye na uelewa wowote kuhusu ulimwengu, ama dhana nzima ni hadithi ya kutungwa katika fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za ujinga na kukosa access ya taarifa mbalimbali.

Nawasilisha.
Zab 53:1 Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu

Ukiona tuu huamini katika uwepo wa Mungu basi mtari huu unakuhusu .
 
Hakuna mungu, ndio maana ukiwahoji maswali wanakutisha.

Mungu ni mchongo wa upigaji ulioletwa kutudumaza akili.
 
Back
Top Bottom