Unajua Mungu aliumbwa na nani?

Unajua Mungu aliumbwa na nani?

ushuhuda kidogo tafadhali ilikutokea nini..
Mambo mengine niyakukaa kimya tu kama mtu anachakuongea
Sio kilakitu mtu anaweza ku expose kwa kila mtu hasa mtandaoni ila usichokijua ni usiku wa kiza maan uchawi upo na kama uchawi upo basi na Mungu yupo
Nashaa anajibu comment za wengin kam vle aon zang
 
Nakuchapa kwa aya tuu!

Bado kofi lenye maelekezo ya kashifa juu ya mola wako! Wewe si unajua tukana mamba angali kuvuka mto bado, Na usubiri habari yako baladhuri mjaa laana wewe!
Unafanya personal attack.

Hoja zimekushinda kujibu?
 
Unafanya personal attack.

Hoja zimekushinda kujibu?
Na hapana mnyama katika ardhi, wala ndege anaye ruka kwa mbawa zake mbili, ila ni umma kama nyinyi. Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote. Kisha kwa Mola wao Mlezi watakusanywa.
 
Mkuu
Unajua kuwa unazidi kuthibisha madai yangu kwamba imani hizi zinasababishwa na uvivu wa kufikiri?

Daktari akishindwa kutibu ugonjwa tunakimbilia kusema ni uchawi au majini bila ya kujishughulisha kutafuta kujua tatizo ni nini ambapo inawezekana linaelezeka kibaiologia katika namna ambayo sisi hatujaielewa bado.

Umesema sayansi imeshindwa kutoa majibu kuhusu chanzo cha uhai. Ni kweli ,sayansi haijaelezea kila kitu lakini kwa nini hiyo isiwe chachu ya sisi kushughulisha akili zetu kufanya uchunguzi ili tupate majibu mazuri zaidi yasiyo na utata na yanayothibitishika na badala yake tunajitungia majibu mepesi yasiyothibitishika na yenye utata?

Unasema sayansi imeshindwa kuelezea laana, maisha baada ya kifo mikosi n.k

kwanza kabisa sayansi sio tu imeshindwa kuvielezea, hata haijathibitisha kama vipo. Ni dhana za kifikirika zaidi hivyo haviwezi kuthibitishika hivyo haziwezi kuelezeka.
Boss Sayansi itaendelea kufanya kazi yake na wenye imani tutaendelea kuwa na imani.

Imani ya uwepo wa MUNGU ni matumaini pale ambapo hakuna majibu, ulinzi pale pasipo na ulinzi, sheria pale pasipo na sheria.

Ghafla bin Vuu watu wafute imani ya MUNGU ndani yao dunia itakuwa ya aina gani? Ushakutana na binadamu wasiomfahamu MUNGU wanavyofanana?

Unadhani sheria pekeyake zinatosha kuudhibiti unyama wa binadamu? MUNGU pekee ndiye anayesababisha stability duniani, tukimkataa na kumkana mawazoni petu katika nyakati hizi tutakuwa na kizazi ambacho hakina stability.

Huko maporini ambapo sheria haina macho watu watachinja wamama wajawazito ili wapate moyo wa kichanga kama kitoweo, viongozi walio juu ya sheria hawatakuwa na hofu yoyote na mengine mengi sana ambayo nina hakika dunia ya sasa esp huku Afrika hatutamani kuyashuhudia.

Imani ya uwepo wake ni muhimu sana kwetu binadamu. Yatupasa tuamini uwepo wa MUNGU nyakati zote na kumuabudu katika roho na kweli ila tuwe na kiasi, tusiwe wajinga na pale sayansi inapofanya sehemu yake turuhusu mawazo mbadala katika akili zetu.
 
Mambo mengine niyakukaa kimya tu kama mtu anachakuongea
Sio kilakitu mtu anaweza ku expose kwa kila mtu hasa mtandaoni ila usichokijua ni usiku wa kiza maan uchawi upo na kama uchawi upo basi na Mungu yupo
Nashaa anajibu comment za wengin kam vle aon zang
Nlikua sijaona post yako.

Una uthibitisho wa uwepo wa mungu?
 
Kijana unatikisa mbuyu umejikuta unatikisa makalio yako mwenyewe.

Hata kama huamini achana na hilo DUDE linaloitwa MUNGU. Lipo nje ya uwezo wako kulielewa.

tafuta muda wa peke yako, uyaangalie mazingira yako milima na mabonde, nyota angani, wanyama, samaki, wadudu, ndege, n.k (angalia usiku na muda wa mchana)

Utaanza taratibu kugundua kuwa kumuamini MUNGU inahitaji kuuvua huo ujuaji wako.

tuliza akili kijana!
Nakazia . Ukweli kuhusu Mungu huuwezi kuupata kwenye vitabu tulivyo letewa. Ukitaka kumjua Mungu nitazame mwili wako itazame nature.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Hapa ubishi upo kwenye Nguvu inayo endesha dunia kuitwa jina "Mungu" naona hapa ndio mleta mada anapinga.

Nguvu iliyo anzisha dunia na vyote vilivyomo ndani yake ipo.

Lakini swali na utata unakuja kwa hapa:
Kwa nini hii "Nguvu" ili itwa na kupewa jina Mungu?

Aliyeipa na kuiita hii Nguvu jina "Mungu" ni nani???

Lakini mimi naamini Dunia ilianzishwa na NGUVU fulani na hiyo nguvu ndio ina control kila kitu....Lakini linapokuja swala la hii nguvu kuitwa jina "Mungu" ndio ubishi huanza hapa, Kwa nini iwe jina Mungu na sio jina lingine??.

Kwa hiyo kila mtu (Binadamu) ana namna ya kuamini hii nguvu ki namna yake.wengine huita Mungu, wengine wana amini Sayansi ndio nguvu yenyewe, wengine mizimu/wachawi ndio nguvu yenyewe.. Wengine wana amini kuna nguvu tu ila haina jina...nameless...
 
Sema: Mwaonaje Mwenyezi Mungu akanyakua kusikia kwenu, na kuona kwenu, na akaziziba nyoyo zenu, ni mungu gani asiye kuwa Mwenyezi Mungu ataye kuleteeni hayo tena? Angalia vipi tunavyo zieleza Ishara, kisha wao wanapuuza.
 
Sawa tuanze taratibu.
Laana ni nini?
Mabalaa yapi unayazungumzia?

Kwanini vipimo vya daktari kutoona ugonjwa kufanye ugonjwa huo uwe wa kichawi?

Unatambua kuwa yanaweza kuibuka magonjwa mapya ambayo hatujayajua kabla?

Laana ni mkusanyiko wa mabaya yote yanayompata mtu: misukosuko katika kazi au ndoa n.k. laana huleta mateso mengi.

Kuachika hovyo, je unafahamu ya kwamba unaweza ukaoana au shirikiana na mtu mwenye mikosi ukashangaa mambo hayaendi au ukishiriki mapenzi na mtu fulani mambo yanaenda.
Thus nimekwambia kuna magonjwa ya kiroho na magonjwa ya kihospitali, kuna tiba za hospital na tiba za kiroho yaani waganga na watumishi wa MUNGU au watu waliopewa karama za uponyaji.

Kama mtu anateseka kwa tatizo na uonekana kimwili lakini wanapima vipimo vyote vya kisayansi tena mitambo ya kisasa kabisa havionyeshi tatizo, kwann isilete shaka. Then mtu huyo akaenda kupata tiba za kiroho nje ya sayansi na akawa mzima kabisa kwann tusiamini kwamba zipo elimu zingine nje ya sayansi.
 
Nakaxia . Ukweli kuhusu Mungu huuwezi kuupata kwenye vitabu tulivyo letewa. Ukitaka kumjua Mungu nitazame mwili wako itazame nature.
Nakazia. kama huna imani ya uwepo wa MUNGU na hujui asili ya ulimwengu na asili yako basi una tatizo la akili.
 
Sema: Mwaonaje, ikikufikieni adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa ghafla, au kwa dhaahiri?
 
Mkuu unaweza thibitisha kuwa umeumbwa na Mungu? AU kwasababu hujui umetokana na nini basi wewe umeamua kusema ni Mungu baada ya kukosa jibu!
Ungekuwa umejileta mwenyewe duniani ungekuwa sahihi kusema kuwa hakuna Mungu.
 
Nlikua sijaona post yako.

Una uthibitisho wa uwepo wa mungu?
Atathibitisha kwa kukupa nn zaidi ya hayo yanayokuzunguka? Ww kwann usimthibitishie kuwa imani yake kwa MUNGU ni batili kwa kumpa sababu ya anayoyaona?

HIVI KWANN MNAKAZANA SANA WATU WASIAMINI KUHUSU MUNGU? KUNA MADHARA GANI IWAPO WANAAMINI NA HAYUPO? MNAUTAMANI ULIMWENGU USIO NA HOFU YA MUNGU MTAUMUDU?
 
Boss Sayansi itaendelea kufanya kazi yake na wenye imani tutaendelea kuwa na imani.

Imani ya uwepo wa MUNGU ni matumaini pale ambapo hakuna majibu, ulinzi pale pasipo na ulinzi, sheria pale pasipo na sheria.

Ghafla bin Vuu watu wafute imani ya MUNGU ndani yao dunia itakuwa ya aina gani? Ushakutana na binadamu wasiomfahamu MUNGU wanavyofanana?

Unadhani sheria pekeyake zinatosha kuudhibiti unyama wa binadamu? MUNGU pekee ndiye anayesababisha stability duniani, tukimkataa na kumkana mawazoni petu katika nyakati hizi tutakuwa na kizazi ambacho hakina stability.

Huko maporini ambapo sheria haina macho watu watachinja wamama wajawazito ili wapate moyo wa kichanga kama kitoweo, viongozi walio juu ya sheria hawatakuwa na hofu yoyote na mengine mengi sana ambayo nina hakika dunia ya sasa esp huku Afrika hatutamani kuyashuhudia.

Imani ya uwepo wake ni muhimu sana kwetu binadamu. Yatupasa tuamini uwepo wa MUNGU nyakati zote na kumuabudu katika roho na kweli ila tuwe na kiasi, tusiwe wajinga na pale sayansi inapofanya sehemu yake turuhusu mawazo mbadala katika akili zetu.
Nimekuelewa.
Kwanza kabisa sijasema kuwa imani ya uwepo wa mungu haina umuhimu. Ina faida kama hizo ulizozitaja hapo juu na ndio lengo hasa LA hizo imani.

Lakini je hata sasa ambapo watu wanaamini imani hiyo, watu hawachinjani?, ubakaji haupo, viongozi miungu watu hawapo?

Point yangu ni kuwa sio lazima tung'ang'anie imani hizi ili kuwa na amani kwenye jamii.
Yawezekana kukawa na amani zaidi kusipokuwa na imani hizi.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kijana unatikisa mbuyu umejikuta unatikisa makalio yako mwenyewe.

Hata kama huamini achana na hilo DUDE linaloitwa MUNGU. Lipo nje ya uwezo wako kulielewa.

tafuta muda wa peke yako, uyaangalie mazingira yako milima na mabonde, nyota angani, wanyama, samaki, wadudu, ndege, n.k (angalia usiku na muda wa mchana)

Utaanza taratibu kugundua kuwa kumuamini MUNGU inahitaji kuuvua huo ujuaji wako.

tuliza akili kijana!

Uzi ufunge kabisa umemaliza kila kitu, sitaki kuongezea Neno
 
Nimekuelewa.
Kwanza kabisa sijasema kuwa imani ya uwepo wa mungu haina umuhimu. Ina faida kama hizo ulizozitaja hapo juu na ndio lengo hasa LA hizo imani.

Lakini je hata sasa ambapo watu wanaamini imani hiyo, watu hawachinjani?, ubakaji haupo, viongozi miungu watu hawapo?

Point yangu ni kuwa sio lazima tung'ang'anie imani hizi ili kuwa na amani kwenye jamii.
Yawezekana kukawa na amani zaidi kusipokuwa na imani hizi.
Boss, binadamu tuna historia, umezaliwa ukakutana na ibada sababu hapo nyuma kuna sababu ilipelekea ibada zikawepo. Tusibishane na nyakati, nyakati za majibu zitafika ila kwa sasa salama yetu ni tulio wengi kuwa na hofu ya MUNGU.

Hayo matukio yanatokea sasa katikati ya uwepo wa MUNGU na sheria za binadamu, imagine MUNGU hayupo yatafanana vipi.
 
Mimi ni kijana ambaye Kwa muda wa miaka 2 nimekuwa nikifatilia mijadala mbalimbali hapa Jf katika jukwaa hili la intelligence. Moja ya mijadala ambayo imekuwa ikinivutia sana ni hii ya dhana ya uwepo wa Mungu.

Swali kubwa ambalo nimeku wa nikijiuliza ni " Mungu alitoka wapi"

Baada ya kuisoma sana biblia na Quran pamoja na kuwahoji viongozi mbalimbali wa dini, hatimaye nikapata jibu la swali lililonitatiza muda mrefu, Mungu alitoka wapi?

Nimegundua kuwa muumba wa Mungu ni mwanadamu. Yes mwanadamu kama Mimi na wewe ndiye aliyemuumba Mungu.

Kwanini nimefikia hitimisho hilo?

Vitabu tunavyoaminishwa kuwa ni vya Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu ( biblia & Quran) ni vitabu vyenye makosa mengi sana ya kimantiki na habari nyingi zenye utata, jambo ambalo tusingetegemea liwepo katika kitabu kilichoandikwa kwa muongozo kutoka kwa Mungu mkuu mwenye uwezo asiyeshindwa na kitu.

Uwepo wa habari hizo zenye utata zinadhihirisha moja kati ya mambo yafuatayo.

1. Mungu hana ukuu tunaoambiwa ndio sababu ameshindwa kutoa mwongonzo mzuri katika kuandika kitabu kisicho na makosa ya kimatinki.

2. Habari hizi ni zao la fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za giza na ujinga. Mwanadamu ambae alitaka kutafuta majibu mepesi katika maswali magumu yaliyomzunguka ndio sababu zina utata.

Kama jibu ni 1 basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo Bali aliyepo ni dhaifu na mbabaishaji aliyeshindwa kuandika vizuri kitabu kinachomuelezea yeye mwenyewe.

Kama jibu ni 2 ,basi Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu hayupo ndiyo sababu akatokea mtu akatunga habari kutokana na fikra zake mwenyewe. Angekuepo asingeruhusu magepu katika fikra za mwanadamu ambayo yamepelekea mwanadamu huyo kujitungia majibu mepesi na habari zenye utata ili kuziba hayo magepu katika fikra zake.

Pointi zote mbili utaona zinaonyesha kuwa Mungu mkuu asiyeshindwa na kitu mjuzi wa yote hayupo Bali " ama aliyepo ni dhaifu,mbabaishaji na asiye na uelewa wowote kuhusu ulimwengu, ama dhana nzima ni hadithi ya kutungwa katika fikra za mwanadamu aliyeishi katika zama za ujinga na kukosa access ya taarifa mbalimbali.

Nawasilisha.
Bange za utotoni
 
Hakika miongoni mwa Watu wa Kitabu wapo wanao muamini Mwenyezi Mungu na yaliyo teremshwa kwenu na yaliyo teremshwa kwao, wakimnyenyekea Mwenyezi Mungu. Hawabadili Aya za Mwenyezi Mungu kwa thamani duni. Hao wana ujira wao kwa Mola wao Mlezi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.
 
Kijana unatikisa mbuyu umejikuta unatikisa makalio yako mwenyewe.

Hata kama huamini achana na hilo DUDE linaloitwa MUNGU. Lipo nje ya uwezo wako kulielewa.

tafuta muda wa peke yako, uyaangalie mazingira yako milima na mabonde, nyota angani, wanyama, samaki, wadudu, ndege, n.k (angalia usiku na muda wa mchana)

Utaanza taratibu kugundua kuwa kumuamini MUNGU inahitaji kuuvua huo ujuaji wako.

tuliza akili kijana!
Nakazia hapa. Mbuyu na uheshimiwe, ifike kipindi watu waone huruma ya makalio yao. Yanatikiswa sana kwa kupambana na mbuyu.
 
Back
Top Bottom