Unapenda movies? Pitia hapa kidogo

Unapenda movies? Pitia hapa kidogo

Halafu kuna movie naitafuta ila siikumbuki vyema niliangalia muda kidogo.

Iko hivi kuna kama mji ulitelekezwa na ukawekewa uzio kwamba hakuna anayeruhusiwa kuusogelea umetandwa na maji hivi (swamp)
Sasa inaanza kuna madogo wawili mmoja anavaa miwani siku hiyo jioni wakaamua kwenda. Kufika pale kuingia ndani ya jengo moja wapo wakakuta kuna sauti zinawaita kufata wakakuta kuna mtu amefungwa. Dogo mmoja yule asiyevaa miwani akamfungulia. Baada ya kumfungulia yule aliyefunguliwa akamuua yule dogo kwa kumchana mdomo.
Yule dogo mwenye miwani akakimbia. Ule mji ukaja ukafunikwa wote na maji. Kukawa na kama ziwa hivi lakini bado kukawa na mauzauza hapo ziwani na kwenye kijiji cha jirani.
Niliingalia muda kidogo nafikiri 2009.
Tungoje msaada...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ni mwandishi wa vitabu? Sijui soko la vitabu likoje lakini wewe ni mwandishi na mchambuzi mzuri sana. Nimevutiwa namna ulivyozichambua movie hizo. Nitatafuta moja baada ya nyingine nisione

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ni mwandishi mkuu, mwanafasihi, mchambuzi wa filamu na pia mwanahabari huru ninayejitegemea (a freelance journalist).

Pitia na post #45 kuna movies za ziada. Hakika hutajuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika movie za hivi karibuni maze runner ile ya kwanza kabisa imebaki kuwa muvi yangu bora kabisa....mkuu ingependeza kama ungenijulisha muvi zenye mfanano na maze runner
Me nime angalia Maze runner zote, naona ziko vizuri Yaani zile hekaheka ndo zinazonifurahisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo Papillon niliona documentary yake, jela aliyokuwa amefungwa huyo jamaa ipo kwenye kisiwa cha devil island French Guinea ambacho kwa sasa ni kituo cha utalii kwa wale watalii wanaopenda kurandaranda na cruise ships.
Huwa wanaenda kuangalia cell ya Papillon na aliandika jina lake sakafuni.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna movie inaitwa interstellar nimeiangalia sijaielewa hata kdg
Nimekupa hint hapo mkuu, ungefanya ka-udadisi kidogo ungefungua fumbo lako. Jina la Meli, AEOLUS, ndo lina habari kuhusu hiyo movie ambapo mtoto wa AEOLUS, aitwaye Sisyphus, alikuwa mtawala katili na mdanganyifu hivyo kupelekea kupewa adhabu ya kupandisha jiwe kubwa mlimani, kisha jiwe linarudi chini na kuanza tena upya pasipo kumaliza.

Kwenye movie ya TRIANGLE tunamwona Jess akimwakilisha Sisyphus kwa kuwa mama katili kwa mtoto wake lakini pia mdanganyifu (unaweza ona hili kwa ile ahadi alompatia dereva taksi kwamba anarudi ingali hakufanya hivyo), na yule dereva taksi ni kama kiashiria cha kifo kwani alimbeba Jess baada ya kupata ajali na mwanaye na pengine wote kufa lakini tunaona Jess akiwa anakataa kifo, anataka kurekebisha makosa yake kwa mtoto.

Hapati hiyo nafasi. Anatumikia adhabu yake kwa kurudia palepale mpaka atakapokata shauri ya kuondoka na 'dereva taksi' yakwishe.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo Papillon niliona documentary yake, jela aliyokuwa amefungwa huyo jamaa ipo kwenye kisiwa cha devil island French Guinea ambacho kwa sasa ni kituo cha utalii kwa wale watalii wanaopenda kurandaranda na cruise ships.
Huwa wanaenda kuangalia cell ya Papillon na aliandika jina lake sakafuni.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Jamaa alikuwa mwamba sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pitia kidogo hapa



1. Pet sematary - imekuwa inspired na Novel ya Steph King. Niliipenda idea yake ya eneo la ajabu ambalo hutumika kuzikia wanyama wa ndani (pets) kisha wanyama hao hurudi kuwa hai tena lakini katika namna ya ajabu kabisa. Shida inakuja pale familia moja ilipoamua kumzika mtoto wao mdogo hapo sababu ya kutokuwa tayari kumpoteza, matokeo yake familia nzima ikajikuta ardhini!

2. The Others - achilia mbali wazo lilizoeleka la nyumba fulani kufuatwa na mizimu na roho za ajabu, humu kilichonifurahisha ni muda wote nlokuwa natazama movie kumbe nilikuwa najiongopea, maana niliyekuwa namdhania ndiye akiteseka na mizimu, kumbe yeye ndiye mzimu wenyewe. Na wale waliokuwa wanadhaniwa ni mizimu ndo binadamu walokuwa wanakuja ndani ya nyumba hiyo.

3. The Orphan - familia moja iliyopoteza mtoto wao kichanga tumboni inaamua kum-adopt yatima wamlelee kama mtoto wao, ajabu ni kwamba mtoto huyo si mtoto bali ni mwanamke mwenye miaka 33 ila kutokana na matatizo ya hormones na pia make-ups amefanikiwa kujiweka kama mtoto. Mbali na hapo, anayeshuhudia mambo ya ajabu anayofanya yatima huyo ni mtoto bubu, kuhadithia hawezi akaeleweka.

4. The sixth sense - hapa mwanasaikolojia wa watoto anahangaika kumsaidia mtoto ambaye anajinasibu kuwa na uwezo wa kuona watu waliokufa. Haamini katika haya mambo lakini baadae anaanza kuamini anachosema.mtoto huyo lakini shida inakuja kwamba, mwanasaikolojia huyo naye alikuwa tayari ameshakufa na ndo mana akawa ana uwezo wa kuzungumza na huyo dogo. [emoji23][emoji23] si mchezo humo!

5. Get Out - nilipenda idea yao ya ku-transform mambo ya racism kwenda kwenye horror ambapo familia moja inamtumia binti yao kama chambo cha kuwavuta wanaume weusi nyumbani kwao ili wapate kuwafanyia surgery na kuwawekea ubongo wa wazungu wazee ama walemavu! Yani humo inaitwa kuingia ni BURE ila kutoka na roho yako sasa ndo KISANGA chenyewe!

6. The Visit - hapa watoto walikwenda kutembelea babu na bibi yao kwa mara ya kwanza kabisa ingali mama akiwa vacation. Watoto hawa wanaona vitu vya ajabu ajabu wakiwa huko. Baadae mama anakuja gundua kuna kitu hakipo sawa baada ya kuona picha za watoto wake na bibi na babu hao wanaoishi nao. Hakuwa anawatambua kama wazazi wake. Hakuwa anawajua kabisa! Na kumbe bibi na babu halisi walishakufa. Hao waliopo ni wagonjwa waliotoroka hospitali ya vichaa!



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo pet sementary pekee ndo nimeiona kijana una madini
 
hizi movie kwa uchambuzi wako nimezielewa sana nipe namna ya kuzipata (kuzipakua ) nifanye kweli usiku huu
 
Kuna movie inaitwa interstellar nimeiangalia sijaielewa hata kdg

Sent using Jamii Forums mobile app
Nini hujaelewa mkuu? Mbona ipo clear. Bwana mmoja, mwanasayansi wa mambo ya anga, anapewa kazi maalum ya kutafuta makazi mapya ya binadamu baada ya dunia kukumbwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na majanga ya asili kama vile ukame na vimbunga.

Kutokana na majanga hayo kumekuwa hakukaliki hivyo NASA wanafanya namna kutafuta makazi mengine ambayo yatamkidhi binadamu mbali na dunia wanayoishi. Lakini sabb ni hatari kupeleka watu wote kwa mkupuo maana hawana taarifa zaidi kuhusu huko, ndo wanaamua kuwatuma baadhi.

Filamu hii inachanganya kidogo maana inahitaji uelewa wa mambo ya sayansi ya space. Nadhani uliona mambo kama vile wormhole na dimensions. Sasa Wormhole ni njia za kinadharia ambazo zinaaminika zinafupisha safari ndefu za mambo ya anga za juu, yani kama vile shortcuts kwenye space. Na ndo hiyo wanayoitumia wanasayansi hao kufikia huko kwenye ulimwengu mpya wapate kuona kama pataweza kalika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nipe tofauti Kati ya hizi thriller movie na horror movie
Thrilller mara nyingi huwa na mambo ya kiuwerevu, uhalifu, udadisi na ujasusi na visa vyake husababisha kimuhemuhe (suspense).

Horror lengo lake kuu ni kuchochea hofu, woga na mshtuko.

So unakuta muda mwingine movie inaweza ikawa horror na pia ikawa thriller. Mfano MARA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom