Unasomea Udaktari miaka mingi, kisha unakuja kulipwa hivi

Hapo aliesoma diploma, yaani alifeli form four, akapata four, akaenda kusoma certificate ya tax, kisha diploma ya tax, yaani miaka 3 baada ya form 4 akaajiriwa tra anavuta 1.8m bila jasho. Mwenzake aliepata division 1 ya 7 akaenda advance akapiga miaka 2 akapata divisheni 1 ya 3, akaenda Muhimbili akasoma miaka 6, jumla 8, yule aliepata four ana miaka 5 kazini anapiga mpunga wa 1.8m halafu huyu wa muhimbili akiajiriwa ataambulia 1.5, mkopo juu, mwenzake ana miaka 5 na amepandishwa daraja anavuta 2.1m bila jasho.

Bongo kuna fani ukisoma haijalishi ulipata division 1 ama nini utaishia kua masikini tu.

Madaktari, walimu wa vyuo vikuu, hawa walisoma vizuri wakapata ufaulu mzuri ila maisha wanayoishi hata muuza mahindi ya kuchoma barabarani ni afadhali. Sasa jichanganye zaidi uwe mwalimu wa shule za kawaida hizi, ndio balaa.

Bro wangu alikua mojawapo ya Tanzania 1 (alikua kwenye top 3) miaka ya 90 kwa form six, aliishia kua mwalimu chuo kikuu, hu anasema ana vyeti mbwa haruki lakini anaishi maisha magumu sana, tuliofuata tukastuka maisha ya ualimu tutakufa masikini, tukasomea kuosha magari, kuchomelea vyuma na udalali vyuo vikuu, mambo ni bambam😂.
 
Noma Sana ndugu....
Kwa kulisema hili, kuna watu wameenda mbali na kuhisi najikweza wakat naongea uhalisia. Hiyo pesa ni nying kwa mtoto wa shule aliyetoka chuo na kuanza kazi na maisha ya kujitegemea, lakin kwa mtu wa kawaida kabisa mwenye majukumu hiyo oesa haitoshelez hasa kama huna vyanzo vingine vya mapato
 
1.Fani zipi watu walisoma na sasa ni matajiri?
2.kua walimu wa chuo kikuu nao ni miongoni mwa watu masikini hapa Tanzania?
 
Hata Kama ni mwanao, mbele ya umma mpe heshima yake. Mengine mkiwa wawili huko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…