Unatumiaje laki tatu kwa mwezi?

Unatumiaje laki tatu kwa mwezi?

1. Ishi ndani ya uwezo wako,
2. Acha anasa kama michepuko na gambe
3. Usinunue vitu mdomdo, nunua vya pamoja kama unga, mchela mafuta na maharage
4. Mshirikishe mama yoyoo ajue hali halisi

Cha msingi: tafuta chazo kingine cha mapato,

Mtafutie mke kitu cha kufanya
Ushauri wa maana sana.
 
Mshahara kama huo unakuaje na familia aisee? Huo mshahara hata bachelor haumtoshi kabisa sembuse wewe mwenye Mke na watoto? Mnatoa wapi Nguvu ya Kuoa na Kipatao tia tia maji ivo, Ungekuwa mwenyewe ungepambana ila tayari una familia apo utaishi kama Shetani
Dah acha tu mm wakat nafanya kazi mshahara wangu ulikuwa lak 6 take home ila still nilioma hautoshi kwasababu ya kufanya investment za mbeleni..
 
Laki tatu Hana uwezo wa kutoboa Kwa familia ya mke na watoto wawili tuache kumpa matarajio hewa ...

Mke na watoto wawili wanahitaji Milo miratu Kwa siku ,....hapa tuseme amenunua ...

Kilo Kumi za Michele -25,000
Unga Kila 10 ,- 20,000
Mafuta ya Kula Lita 5- 25,000
Sukali kilo 5-16,000
Maharage kilo 5-10,000

Hapo tuseme Laki imeisha Kwa vitu vya mhimu sanaaaaa.....hivyo vyakula nimeassume vitamaliza mwezi japo Sina uhakika .....

Hapo Laki imeisha imebaki Laki mbili (200,000)


Twende matumizi mengine ..

-Kubadili mboga mboga ,dagaa ,nyama kidogo ,mchicha ,sio Kila siku mtakula mahalage ...---20,000
-gesi au mkaa --25,000
-chumvi ,majani ya chai --4000
-sabuni ,kipande na Unga &steel wire kusugulia sufuria -5000

Maji ya kununua Kwa mwezi /bill -5000

Umeme kulipa Kwa mwezi -5000

Nauli ya kwenda kazin na Kurudi baba pekee yake -30,000

Nauli za mke na watoto kutoka sehemu kwenda sehemu Kwa emergency, mkee hawezi kaa nyumbani kama jiwe ,kwenda sokon n.k-20,0000

Hapo umetumia Laki na uchafu (130,000) ...



Baada ya yote hayo imebaki 70k..

Hujanunua vocha ya kuwasiliana na mkeo tuseme Kwa mwezi utatumua -5000

Mtoto amepata kikohozi ,au kichwa kinauma ,umenunua hata Panado .n.k -5000

Kanisani hujatoa sadaka wewe na mke ,Kwa mwezi wote wawili tuseme -10,000

Hela ya takataka ,ulinzi shirikishi mtaani maana mjumbe atakuja kudai [emoji23]-5000

Mwanaume hauwezi kaa nyumbani tu utaangalia hata mpira ,bia moja ,-20,000

Hapo hujanunua nguo ,mkeo hajaenda saloon ,wewe hujaenda saloon kunyoa ndevu ,watoto hawajaenda hata kutembea kokote hata beach ,watoto hujawanunulia hata biscuit,ndugu hujawapa hata 100, mama mzazi hajakuomba hata 5000,,,, hujapata emergency ya kuumwa hata hospital,,hujahonga Kwa michepuko ,hujapoteza pesa (maana kuna hela zinapotea tu automatic bila kujua sababu [emoji23]...

Laki tatu hutoboi aiseee....

Na hapo ili utoboe mwezi lazima uishi kama shetani kwa matumizi ya hapo juu.....


Ulichokiandika kinakaribiana sana na uhalisia

300K kwa mwezi bila kujiongeza haitoshi
 
Hakikisha unakodi shamba ekari moja. Lima mahindi nusu eka na maharage nusu eka.
Hapo utakuwa kwanza umetatua changamoto ya misosi.
Wapigie simu ndugu zako kijijini wakutafutie shamba la kukodi.
Tuma hela ya kulimia, mbegu na mbolea.
Kwa mwaka utaweza kuokoa hadi Tsh milioni moja kwenye gharama za chakula.
Hizo hela anatoa wapi sasa mtu analipwa laki3 na ana familia, ata-save vipi pesa ya kukodi shamba na ghalama za kulimia
 
Jamani wanajamiiforums ninapokea mshahara laki tatu na nina mke na watoto wawili ninalipa kodi 30,000 kwa mwezi, kinachonitesa ni hesabu za kubalance mpaka hiyo hela ieneee mpaka mwisho we mwezi nifanyaje ili niweze kubakisha kiasi niweke akiba.

Msaada wenu please..
Ukibajeti vizuri laki 3 inaweza kutosha kwa matumizi ya kujibana ya kawaida mwezi mzima kwa familia ya watu 4. Fanya hivi.

Chakula120,000/= mchele kg 15-20, mahindi debe 1, ngano kg 5, mafuta 5ltr, tambi elfu 15.

Energy ya kupikia 35,000 (gas & mkaa).

30,000 kodi, elfu 20 bili za maji na umeme.
Mkeo unamuachia elfu 50 matumizi mengineyo. Unabaki na elfu 40 unatamba nayo mwezi mzima, Hapo utajua hujui kiukweli maisha yamepanda laki tatu haitoshi.
 
Maisha ni tofauti aana mm napokea 2.5 m hazinitoshi sipati ya kuweka akiba
 
Kodi umeshasema 30,000/-, nauli ya kwenda kazini au kwenye shughuli unayojipatia kipato ni kiasi Gani? Na chakula Kwa siku unatumia kiasi Gani huko kazini? Hayo ni matumizi ya lazima na ndio mtaji wenyewe unaokupatia hiyo 300,000/-

Ila tukubaliane mshahara haujawahi kutosha. Kuna watu wanalipwa Mara 10 ya hii pesa na Bado Wana Hali ngumu kuliko huyu Mwamba. Hawana furaha kabisa.

Watakaopenda Kuna kitabu nimeambatanisha wanaweza kukisoma wakajifunza hapo "The Richest Man in Babylon"
Kweli mshahara haujawahi kutosha na hata ukiongezeka na mahitaji hayo yanaongezeka.
Ila pia wakati mwingine mazingira yanaweza kuamua upate saving kwenye kimshahara chako au usiweze kusave.
Mfano kwa mshahara wa rafiki yetu kwa mazingira ya mjini mfano Dar huo mshahara ni ngumu kidogo kufanya saving hasa ukizingatia ana familia inayotegemea ihumiwe kwa mshahara huo ila ukiwa mazingira ya vijijini kwa mshahara huo unafanya saving.
 
Jamani wanajamiiforums ninapokea mshahara laki tatu na nina mke na watoto wawili ninalipa kodi 30,000 kwa mwezi, kinachonitesa ni hesabu za kubalance mpaka hiyo hela ieneee mpaka mwisho we mwezi nifanyaje ili niweze kubakisha kiasi niweke akiba.

Msaada wenu please..
We ni mwalimu uko halmashauri gani
 
Jamani wanajamiiforums ninapokea mshahara laki tatu na nina mke na watoto wawili ninalipa kodi 30,000 kwa mwezi, kinachonitesa ni hesabu za kubalance mpaka hiyo hela ieneee mpaka mwisho we mwezi nifanyaje ili niweze kubakisha kiasi niweke akiba.

Msaada wenu please..
Kwanza;- 300k ni nyingi sana ukiamua kukabiliana na maisha na sio anasa za dunia

Pili;- Mtangulize Mungu katika kazi zako
•Mshirikishe mwanamke wako katika kila unalo lipanga wanawake wetu ni mibaraka katika kila hatua tunayo piga

Tatu;- Jua katika maisha ya ndoa na kazi ili mambo yaende inabidi uangalie source of income yako inaendaje usitegemee mshahara tu
•Kwa sisi tulio kulia maisha ya vijijini baba anafanya kazi kiwandani anapata 7k per day mama yupo nyumbani lakini hakuacha kumshirikisha

NOTE:- Wanawake wamebarikiwa akili ya utambuzi kwa haraka katika hali ya maisha nitakupa mfano Leo unaona single mother wengi walio na utambuzi wanatoboa kwasababu chukua ilo mshirikishe mke wako lakini msikilize pia mawazo yake

Nne;- Jua jinsi ya budgeting, hapa ninacho maanisha angalia vitu muhim kwanza nyumbani
•Utahitaji chakula ili kesho uwe na nguvu ukafanye kazi
•Watoto watahitaji kalamu na daftari waende shule
•Utahitaji maji na umeme au vyanzo muhim katika nyumba
•Mkeo mpe pesa yaa kutunza mji
•Anzisha biashara ambayo itakusaidia wew kujaza kibaba ndani kwa msaada wa mke wako

Tano;- Jua kutunza taarifa (Record keeping) hii itakusaidia wew kujua mwezi huu nipo katika hatua gani na utatambua je mwezi ulio pita nilitumia kiasi gani sehem flan na mwezi huu nimetumia kiasi flan, Kumbuka kila siku vitu vinapanda bei.

Muhim zaidi jifunze pia mfundishe mke wako kuangalia fursa mbali mbali na kuzitumia
Pia mkumbushe mke wako lengo la familia tukumbuke wanawake wapo vizuri lakini wengi wanajisahau pale unapo anza kuingiza 6k per day wakati juzi ulikuwa unaingiza 3k.
 
Laki tatu Hana uwezo wa kutoboa Kwa familia ya mke na watoto wawili tuache kumpa matarajio hewa ...

Mke na watoto wawili wanahitaji Milo miratu Kwa siku ,....hapa tuseme amenunua ...

Kilo Kumi za Michele -25,000
Unga Kila 10 ,- 20,000
Mafuta ya Kula Lita 5- 25,000
Sukali kilo 5-16,000
Maharage kilo 5-10,000

Hapo tuseme Laki imeisha Kwa vitu vya mhimu sanaaaaa.....hivyo vyakula nimeassume vitamaliza mwezi japo Sina uhakika .....

Hapo Laki imeisha imebaki Laki mbili (200,000)


Twende matumizi mengine ..

-Kubadili mboga mboga ,dagaa ,nyama kidogo ,mchicha ,sio Kila siku mtakula mahalage ...---20,000
-gesi au mkaa --25,000
-chumvi ,majani ya chai --4000
-sabuni ,kipande na Unga &steel wire kusugulia sufuria -5000

Maji ya kununua Kwa mwezi /bill -5000

Umeme kulipa Kwa mwezi -5000

Nauli ya kwenda kazin na Kurudi baba pekee yake -30,000

Nauli za mke na watoto kutoka sehemu kwenda sehemu Kwa emergency, mkee hawezi kaa nyumbani kama jiwe ,kwenda sokon n.k-20,0000

Hapo umetumia Laki na uchafu (130,000) ...



Baada ya yote hayo imebaki 70k..

Hujanunua vocha ya kuwasiliana na mkeo tuseme Kwa mwezi utatumua -5000

Mtoto amepata kikohozi ,au kichwa kinauma ,umenunua hata Panado .n.k -5000

Kanisani hujatoa sadaka wewe na mke ,Kwa mwezi wote wawili tuseme -10,000

Hela ya takataka ,ulinzi shirikishi mtaani maana mjumbe atakuja kudai [emoji23]-5000

Mwanaume hauwezi kaa nyumbani tu utaangalia hata mpira ,bia moja ,-20,000

Hapo hujanunua nguo ,mkeo hajaenda saloon ,wewe hujaenda saloon kunyoa ndevu ,watoto hawajaenda hata kutembea kokote hata beach ,watoto hujawanunulia hata biscuit,ndugu hujawapa hata 100, mama mzazi hajakuomba hata 5000,,,, hujapata emergency ya kuumwa hata hospital,,hujahonga Kwa michepuko ,hujapoteza pesa (maana kuna hela zinapotea tu automatic bila kujua sababu [emoji23]...

Laki tatu hutoboi aiseee....

Na hapo ili utoboe mwezi lazima uishi kama shetani kwa matumizi ya hapo juu.....
Jinga sana [emoji1] [emoji1787] [emoji23] [emoji38]
 
Wasomi wetu kwa kujiendekeza watu wanatumia laki kwa mwezi na ana familia na watoto wanaenda shule na maisha yanaenda safi kabisa.
 
Back
Top Bottom