Unayoyajua na usiyoyajua kuhusu wanyama wa kufugwa

Unayoyajua na usiyoyajua kuhusu wanyama wa kufugwa

Wakuu
Tumekuwa tukifuga sana wanyama majumbani mwetu kwa miaka mingi hasa jamii za kiafrika.
Ingawaje tumekuwa tukiwatendea unyama uhuni wanyama tuwafugao.

Hapa nitaeleza kwa ufupi niliyoyajua na kuyaona kwa wanyama wa nyumbani hasa wafugwao na tabia zao ambazo ni very rare kuziona ..!

PUNDA.
Kwanza huyu hafugwi. Ndiyo HAFUGIKI. Why? Twende taratibu.
Panda amekuwa akifugwa kwa muda mrefu sana na binadamu
Akitumika kwa shughuli mbalimbali kama kulima.na kubeba mizigo mbalimbali.

Ingawaje kuna tabia zake ambazo ni rare sana kuziona utazijua tu punde ukimtendea vizuri yaani usiwe mkatili kwake.

Kwanza ana akili kuliko ng'ombe na wanyama wengine

Kuna kipindi wakati nipo mdogo kijijini kwetu Punda wetu baada ya kuona kazi nyingi sana mtindo mmoja na viboko vingi sana
Akaona bhana eeh! Chakufia nini? Akasepa zake kama miezi miwili hatumuoni.

Kumbe alikuwa kaenda tu nyumba nyengine usiku karuka zizi kaingia kukaa na ng'ombe katulia!
Mwenye mifugo kaamka asubuhi wala hajauliza sanaaa. Kampa chakula kidogo then kamuacha maana anajua wazi kabisa ukimpa kazi nyingi huyo punda anasepa zakeee..!

Baada ya miezi miwili usiku tena punda yule akarudi maskani kwa mtindo ule ule wa kuruka zizi asubuhi mnamkuta katulia zake ...!

Alipokuwa na ujauzito tulitegemea atazaa tu vizuri guess what??
Tuliona tu punda karudi kutokea porini hana tumbo kubwa tena na hana mtoto! Kamuacha wapi??

Ikabidi wazee wamzunguke na kuanza kumtandika viboko mfululizo mpaka punda yule alipoenda kuonesha alipomuacha mtoto ambapo tungechelewa tungekufa kajifia zake.

Najua unajua au hujui lakini punda anakula sana ukoko ukitaka ahamie kwako mazima mpe kila siku!

Next time nilipokuwa nimekaa tu kariba na zizi nikaona punda wetu mwengine aliyekuwa na mimba , anahangaika sana yaani hatulii !

Ukweli mimi yule punda alinipenda sana na hata nikiwa nimetulia alikuwa akinifuata na kuanza kusugua shingo yake miguuni mwangu , it was my best friend..!

Akanifuata mbio mbio then anageuka ananionesha mbususu yake, nikajua moja moja kwa huyu punda anataka kusaidiwa kujifungua na mimi bwana mdogo sikujua how to do it, ikabidi niwaite wajuzi waje kumsaidia mtoto atoke.. kwa kweli nilishuhudia namna wanyama wakizaa ni tabu tupu wanapata..!

Unatakiwa ujue kuwa punda ni mchungaji mzuri wa mifugo hasa ng'ombe na mbuzi, anaongoza njia na kuwaelekeza pa kupita mifugo sababu anakariri sana njia.

Pia anafukuza sana wanyama pori hasa fisi wanaokamata mbuzi [shughuli yake wanaijua vizuri]

NG'OMBE..

Huyu ni mnyama ambaye tuseme anashika nafasi ya pili kwa kuchinjwa akiongozwa na nguruwe!

Ng'ombe ni mnyama ambaye yuko so friendly na binadamu.
Iwapo tu ukimpenda na kumjali sio kila mara viboko noo

Kwa wasukuma.ni kawaida kukuta ng'ombe mmoja kavunjika pembe kwa viboko

Ng'ombe hawezi kujifungua mwenyewe au akiweza atazaa kwa tabu sana au ndama kufa!

Kama akikuozea sana atakufuata then atakeukia kukuonesha "bwana eeh mwanangu anataka kutoka nisaidie" then utatakiwa kumsaidia kumvuta ndama atoke [hili nimeshuhudia personal]

Watu wa dar kuleni nyama tu hivi hivi tu lakini mngejua namna wafugaji wanavyopata tabu.

Ndama anapotoka inatakiwa mmoja anyonye haraka kwenye pua'mdomo' maskio ili ndama asife otherwise mtampoteza..!

MBUZI
Huyu yeye anafugwa sana sana kwa kitoweo au biashara unakuta mtu kakwama anauza chap mbuzi mmoja kama 70k kutatua kamzozo fulani.

Mbuzi yeye ni muoga sana Hali inayopelekea kuwa na akili
Mara nyingi mbuzi hukaa zizini na mifugo mingine ili kusudi kutoa alert iwapo litatokea tatizo mfano fisi ameingia zizini ama lah
Yeye akiona tu labda kondoo amedakwa na fisi [fisi anapenda kondoo kuliko mbuzi] basi atapiga yowe "jamani baba mwenye nyumba eeh huku kuna muujiza tumevamiwa"

Na kikawaida mbuzi ana Saudi tofauti tofauti ndani ya mlio mmoja! Ndiyo' skia mzee iko hivi.

Mbuzi anatoa Sauti tofauti kabisa ikiwa kuna hatari' either akiona kitu ama akidakwa hata na fisi utajua tu.


Ana sauti ya maumivu, nk
Shida ya kondoo huwa nj jeuri hata akidakwa anataka kufa kiume halipigi kelele, ndio maana unasked watu wanasema kufa kikondoo hence muweke mbuzi na kondoo wakae zizi moja..

Unajua nini kuhusu wanyama?
Mengi hapa siyo ukweli. Yaani umefikia conclusion kwa mambo machache ambayo inaonekana na wewe ulisimuliwa au umekopi mahali na kuleta hapa. Utawapata tu hao hao waliozaliwa mjini na hawajui maisha ya hawa wanyama. Sisi wengine tuliozaliwa vijijini wanyama kama hawa walikuwa ni sehemu ya maisha yetu.
 
fact chache za wanyama hawa.
Ukiwa na mbwa dume hesabu maumivu kama huna fence usiku anaenda kutafuta mademu

Ng'ombe dume wa kazi hatakiwi kupewa chumvi inapunguza nguvu

Nguruwe akila kitunguu maji kibichi anakufa, ila akila nyoka hafi.

Kuhusu punda kama una moyo mwepesi unaweza ukaua wanakera sana hasa wakichoka anaweza akatupa mzigo halafu akatoka kibati.

UJANJA WOTE WA PUNDA ANAOGOPA SANA MAJI KWA SABABU HAJUI KUOGELEA
 
Mengi hapa siyo ukweli. Yaani umefikia conclusion kwa mambo machache ambayo inaonekana na wewe ulisimuliwa au umekopi mahali na kuleta hapa. Utawapata tu hao hao waliozaliwa mjini na hawajui maisha ya hawa wanyama. Sisi wengine tuliozaliwa vijijini wanyama kama hawa walikuwa ni sehemu ya maisha yetu.
Kwahiyo unanijua?
Kama unajifanya unajua sana sawa elezq
Ila mimi utaniambia nini mmasai? Kuhusu mifugo?
Nimeshinda na wanyama,nimekua nao na mpaka kulala zizini kusubiri ng'ombe ajifungue?

Huna unalolijua kama unalo eleza
 
fact chache za wanyama hawa.
Ukiwa na mbwa dume hesabu maumivu kama huna fence usiku anaenda kutafuta mademu

Ng'ombe dume wa kazi hatakiwi kupewa chumvi inapunguza mihogo

Nguruwe akila kitunguu maji kibichi anakufa, ila akila nyoka hafi.

Kuhusu punda kama una moyo mwepesi unaweza ukaua wanakera sana hasa wakichoka anaweza akatupa mzigo halafu akatoka kibati.

UJANJA WOTE WA PUNDA ANAOGOPA SANA MAJI KWA SABABU HAJUI KUOGELEA
Kuhusu punda ni kweli kabisa na ndio maana tumesema punda huwa hafugwi
Akili zake anazijua mwenyewe
Hata anaweza kutoweka week usimuone
 
Sikujua hii ya ng'ombe kusaidiwa, au kunyonywa pua, maana mtaalamu mmoja aliniambia sio wote wanahitaji kusaidiwa, juzi usiku a.k.a Sabrina ikiwa ni mimba ya kwanza kwake akajifungua usiku, hatukusikia kelele zozote, only in the morning tukakuta ndama hatunaye. She was devastated to say the least.
Kujifungua - reserved word kwa heshima ya binadamu similar to kufariki. Wanyama huzaa; hawajifungui only binadamu hujifungua.
 
fact chache za wanyama hawa.
Ukiwa na mbwa dume hesabu maumivu kama huna fence usiku anaenda kutafuta mademu

Ng'ombe dume wa kazi hatakiwi kupewa chumvi inapunguza nguvu

Nguruwe akila kitunguu maji kibichi anakufa, ila akila nyoka hafi.

Kuhusu punda kama una moyo mwepesi unaweza ukaua wanakera sana hasa wakichoka anaweza akatupa mzigo halafu akatoka kibati.

UJANJA WOTE WA PUNDA ANAOGOPA SANA MAJI KWA SABABU HAJUI KUOGELEA
Na pia mbwa kufuga mmoja ni utachoka bora wawili yaani jike na dume watatulia home angalau kidogo kuliko kufuga madume mawili kwa pamoja. Mbona patachimbika hapo?

Dume lazima lisepe likatafute utelezi huko mitaani then. Wezi wanakuja wanapita na flat screen yako😅😅😅
 
Hapo kwenye punda umenikumbusha Hadithi za kiswahili (YouTube) punda alikuwa mvivu hataki kubeba mizigo kuvuka nayo mto, sasa siku moja akapata wazo kwakuwa mizigo ili kuwa ni chumvi.
Basi alivyo fika pale mtoni akaa kwenye maji chumvi yote ikayeyuka Punda alifurahi sana hakuhisi uzito kwenye mgongo wake, Hiyo ndio ikawa tabia yake .. Nimecheka sana
 
Kwa kiasi ukweli kwa kiasi umeongeza chumvi mkuu
Punda anafanya kazi ukimlisha vizuri ana nguvu lakini kiusalia ni mvivu sana

Akilala utachapa sana ndiyo haamki lakini ukichukua majani makavu muwekee mgongoni yawashe moto anaamka fasta then hapo ndio atalima fasta fasta amalize kumbuka ana akili sana

[emoji28][emoji28][emoji28] daah
 
Hapo kwenye punda umenikumbusha Hadithi za kiswahili (YouTube) punda alikuwa mvivu hataki kubeba mizigo kuvuka nayo mto, sasa siku moja akapata wazo kwakuwa mizigo ili kuwa ni chumvi.
Basi alivyo fika pale mtoni akaa kwenye maji chumvi yote ikayeyuka Punda alifurahi sana hakuhisi uzito kwenye mgongo wake, Hiyo ndio ikawa tabia yake .. Nimecheka sana
Sababu punda akili yake ni kubwa kuliko wanyama wengine anafikiria sana
 
Kitu namisi ni kuona zile battle za madume ya mafahali.

Tukiwa machalii wadogo tulikuwa tunachonganisha mafahali halafu tunakaa kuangalia battle.

Wale mafahali wanafikia hatua ya kuwa na bifu na unakuta wako busy kunoa pembe zao kwenye vichuguu.

[emoji28][emoji28][emoji28] nimefanya sana hii,achilia mbali ya kukamata jike la mbuzi na kuona jinsi madume yanavyo mpanda. [emoji28][emoji28] gone those old days.
 
fact chache za wanyama hawa.
Ukiwa na mbwa dume hesabu maumivu kama huna fence usiku anaenda kutafuta mademu

Ng'ombe dume wa kazi hatakiwi kupewa chumvi inapunguza nguvu

Nguruwe akila kitunguu maji kibichi anakufa, ila akila nyoka hafi.

Kuhusu punda kama una moyo mwepesi unaweza ukaua wanakera sana hasa wakichoka anaweza akatupa mzigo halafu akatoka kibati.

UJANJA WOTE WA PUNDA ANAOGOPA SANA MAJI KWA SABABU HAJUI KUOGELEA

[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Usihofu tunaenda taratibu mkuu
Alafu punda anasifa moja;

Ukim'bebesha mwanae mzigo haendi, utapiga viboko umuue, m'bebeshe yeye mizigo yote mwanae atembee free.

Nimewaona sana kule Usafwani(Mbeya) wakibebeshwa mahindi,mkaa na viazi.

Punda akifika lami ni mjinga sana, gari inakuja wala hakimbii anaficha tu kichwa anaacha mwili wote anagongwa.
 
Back
Top Bottom