Unazeeka jione hapa

Unazeeka jione hapa

.
IMG_20191031_112042.jpeg
 
31..ndio kwanza niponipo tu hata bei ya tofali siijui, maisha bwana yakiamua kukupa kisogo
Aisee!!
Zile stori zako za vipindi vya redio Tanzania na matumizi ya vitu vya zamani (koroboi, pasi ya mkaa, n.k) kumbe ulikuwa una simuliwa na mwalimu.... mkiwa jikoni?

Acha nimfikishie huu ujumbe yule Msukuma mwenye jina la mnyama aje ashuhudie "uandaeitini" wako,ajue kuwa yote iliyokuwa unasimulia ulikuwa unajimwambafai [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Kabisa. Mimi huwa nasema haya maisha kwa Mungu ni kama kibao ni sekunde tu kugeuza mshale uelekee upande wa pili.

Mimi mpaka nikifika 45 sina kitu ndio ntasema hapa basi, lkn kwa hii 31 bado sana.

Na asikudanganye mtu, sister, ukiona mtu ana miaka 31 lakini tayari ana vitu vyote muhimu jua ni mwizi.
Ukiwa na mawazo hayo utabweteka.
 
Wee acha tu huyu mzee wakati anaingia nilikuwa na 20+ sasa hivi nataamaki ngoma hii hii hapa 25+ [emoji15]

Ukileta mzaha unashangaa ngoma 30+ hii bado unayega yega.
For sure. Umri bana kitu cha ajabu sana unajiona bado bado kumbe ndio miaka inazidi kusonga
 
Huu uzi unanipa mashaka ya moyo. Nashangaa siku hizi nikipa sehem watu hawasemi baba, naambiwa mhudumieni mzee dah! Mwanzoni nilikua kama nashikwa na gubu nikakumbuka wakati ukuta, hauwezi kushindana nao.

Inabidi kujiweka sawa kwenda na majira.
Ha ha ha ha halafu huyo anaekuita hivyo sio mdogo!
 
Back
Top Bottom