Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Sina kijana yoyote ila kama mwananchi mpenda haki inabidi nitetea vijana wote wa Dar. Shida yako naona unadhani kuwa (kama walivyo watanzania wengi) tatizo mpaka likupate wewe au mtu wako wa karibu ndiyo inabidi upige kelele. Ndiyo maana umeshafikia conclusion kuwa nina ''kijana wangu'' amekuwa victim. Mimi naumia sana kuona binadamu wenzangu wanateseka na kuuawa kwa bila kufuata sheria. Pengine wewe unadhani uko mbali sana na huu mfumo mbovu wa utawala, lakini nakuhakikishia hauko mbali. Kuna siku utakumbuka maneno yangu kwa sababu siyo lazima uathiriwe na hii ua ua au kamata kamata ya panya road tu, kuna mengi mengine unaweza kuja kuwa victim au mtu wako wa karibu.
sijawai ona ukitetea wez wasichomwe moto ila upo hapa kutetea watoa roho za watu , unanufaikaj mwenzetu Mwakipesile ?
 
Kwa hii stori ni kwamba panya road wanafahamika ila raia wema wanaogopa kuwataja kwa kuhofia usalama wao kwa hao hao panya road.
Kama ndio hivyo hao raia wema wafunguliwe mashtaka kwa kuwa wanashirikiana na wahalifu kwa kukataa kutoa ushirikiano kwa vyombo vya usalama.
Ikifanyika hivi ushirikiano watatoa na wahalifu halisi watapatikana na adhabu stahiki wapate badala ya kuzoa zoa na kusomba watu ambao wengine pengine wala hawahusiki.

Polisi wanashindwa kujiongeza tu. Wakiamua kuwawekea mtego hao panya road ni rahisi tu. Sidhani kama hawayajui maeneo yao ya kujidai.
na ndo wanawataj sasa hv kwa kuwakatisha uhai kbs ili wasirud tena mtaan , kaish vingunguti majina yao utayasikia tu
 
Ni kweli nikikumbuka mauaji waliyofanya dhidi ya Yule kijana Kule Mtwara naumia Sana ,majitu yanaua na kupora sasa Yana tofauti gani na panya road ?
duh una akili fupi so unawashaur polisi wawaache hao panya road kisa wao waliua mtwara , sio ? kwan polis wa mtwara ndo hawa wanadhibiti panya road hapa dar ? Wabongo tuna ttzo kubw sana la kuchanganya mafaili
 
Sina kijana yoyote ila kama mwananchi mpenda haki inabidi nitetea vijana wote wa Dar. Shida yako naona unadhani kuwa (kama walivyo watanzania wengi) tatizo mpaka likupate wewe au mtu wako wa karibu ndiyo inabidi upige kelele. Ndiyo maana umeshafikia conclusion kuwa nina ''kijana wangu'' amekuwa victim. Mimi naumia sana kuona binadamu wenzangu wanateseka na kuuawa kwa bila kufuata sheria. Pengine wewe unadhani uko mbali sana na huu mfumo mbovu wa utawala, lakini nakuhakikishia hauko mbali. Kuna siku utakumbuka maneno yangu kwa sababu siyo lazima uathiriwe na hii ua ua au kamata kamata ya panya road tu, kuna mengi mengine unaweza kuja kuwa victim au mtu wako wa karibu.
Wewe unaonesha unatetea hata ushoga.

Hao unaowatetea, panyarodi, wao wanatazama haki za binaadam?
 
Habari!

Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.

Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.

Sasa polisi wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wale wanaowashuku kuuza au kuvu bangi kisha kuwaua kinyama. Misiba ni mingi mitaani, inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.

Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai. Upelelezi wa kutosha umefanyika? Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia. Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.

Rais Samia utakuwa na mwisho mbaya. Police wamegeuza Kitonga Dar kuwa machinjio ya binadamu. Hata familia zenu zina vijana wa hovyo, wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road. Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.

NB: Mimi si mhalifu, ni raia safi kabisa, sijapoteza ndugu yangu kwa hii operation na wala sina ndugu mhalifu, ila nimeumia tu na haya yanayotokea. Misiba ni mingi, huzuni na vilio. Huku viunga vya Kitonga ambako wamekugeuza machinjio ndiko ninakoishi. Jana nilienda uswahilini Tandika na Buza ni huzuni.
Hao panya road wakiua na kujeruhi watu wasio na hatia, nyie watetezi uchwara wa haki za binadamu huwa mnakuaga wapi ?!!
 
Habari!

Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.

Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.

Sasa polisi wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wale wanaowashuku kuuza au kuvu bangi kisha kuwaua kinyama. Misiba ni mingi mitaani, inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.

Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai. Upelelezi wa kutosha umefanyika? Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia. Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.

Rais Samia utakuwa na mwisho mbaya. Police wamegeuza Kitonga Dar kuwa machinjio ya binadamu. Hata familia zenu zina vijana wa hovyo, wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road. Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.

NB: Mimi si mhalifu, ni raia safi kabisa, sijapoteza ndugu yangu kwa hii operation na wala sina ndugu mhalifu, ila nimeumia tu na haya yanayotokea. Misiba ni mingi, huzuni na vilio. Huku viunga vya Kitonga ambako wamekugeuza machinjio ndiko ninakoishi. Jana nilienda uswahilini Tandika na Buza ni huzuni.
Bado hujajua kitu! Jifunze kwanza
 
Mkuu hata wewe jiangalie sana, epuka hayo makundi unayozurula nayo hata wewe unaweza kukanyagwa shaba tu sisi hatuangalii
 
Hao panya road siku ukikutana nao utarudi hapa kuedit huu uzi wako. Omba usikutane nao.
 
Msirudishe watu enzi za ujima kwa kuwapangia wafanye mambo yao mchana tu.
Wewe kama kijana unajua vizuri operation linaloendelea sasa ni kuwasaga 'panya road' halafu wewe bado unakaa maeneo hatarishi usiku mkubwa eti unavuta bang.

Polisi haiwezi kutofautisha kibaka na mvuta bangi endapo utakutwa usiku sehemu isiyoeleweka na ukaamriwa ujisalimishe kisha ukatoka nduki lazima risasi zikuhusu mkuu.

Siungi mkono mauaji ya aina yoyote yale ila kipindi hiki cha operation maalum tujihadhari sana na kuzurura usiku pasipo sababu inayoeleweka.
 
Msirudishe watu enzi za ujima kwa kuwapangia wafanye mambo yao mchana tu.
Hawa watu wana stress.
Kwenye katiba hakuna mahali imekataza kukusanyika, kutembea usiku na hakuna mahali polisi anaruhusiwa kumuua mshukiwa wa uvutaji bangi.
Watu wamelelewa kihuni ndio maana wana roho mbaya kutaka wenzao wafe
 
Hawa watu wana stress.
Kwenye katiba hakuna mahali imekataza kukusanyika, kutembea usiku na hakuna mahali polisi anaruhusiwa kumuua mshukiwa wa uvutaji bangi.
Watu wamelelewa kihuni ndio maana wana roho mbaya kutaka wenzao wafe
Kweli tuna Roho mbaya ila lazima panyarodi wapelekwe kwa Sir God

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom