Unyanyasaji wa kibinaadamu hasa kwa wezi siyo mzuri

Unyanyasaji wa kibinaadamu hasa kwa wezi siyo mzuri

Kama kosa linadhaminika ni haki yake kupata dhamana ila mwisho wa siku kesi itaenda mahakamani na hpo vifungu vya sheria ndio vitatumika na sio hisia mkuu.
Tatizo ni hizo Tambo mtaani baada ya kuipata hiyo dhamana na anatishia kabisa kwamba atadill na nyie mliyemkamata

Mimi binafsi siwezi kupigwa mwizi ila Kwa walichonifanyia 2012 Mimi hata nikute mwizi anachinjwa Wala siumii
 
Sisi tumepanga mtaani kwetu tutakayemkata sasa hivi tunakata vidole vyote vya miguu, na vya mikononi tunamuachia kidole cha kati... kisha tunamwacha...
Tumetangaza kabisa hivyo atayeiba anaijua adhabu yake...
Kwa Nini kidole cha kati[emoji44]
 
Tofautisha kuvamiwa na self defense! Hapo kama umeua ilikuwa ni self defense. Ila sasa mmemkamata yanini kuanza kumbonda mawe hadi kifo ndio swali langu?
Wanakera, fikiria umepambana umejinyima walau ukafanikiwa kununua kitu chako Cha thamani halafu eti linakuja jitu lisilojua taabu ulizopata halafu likuibie na kukujeruhi juu asee nadhani hayajakukuta bado
 
Habari za asubuhi wana jamii! Hope mko poa na Xmass ilienda good. Kuna jambo limenitatiza kidogo kuna kijana amekamatwa akiiba nyumbani kwa jirani hapa, ila cha kushangaza badala ya kumpeleka polisi wakamfungulie mashtaka wameishia kumtesa, kumdhalilisha na kumnyanyasa.

Wamekoroga cement na kumlazimisha ainywe mbaya zaidi wamemfunga kamba mikono na kuimwagia petrol kisha wakaichoma moto, jamani sio uungwana hata kidogo hii ni jamii ya namna gani ya kutesa wezi na vyombo vya sheria vipo. Mbona jamii imekuwa na watu katili kiasi hiki?

Tukataeni unyanyasaji wa aina yoyote ile katika jamii zetu. R.I.P kibaka walimwengu ni makatili sana.
Wewe ni kati yao una watetea kwa sababu gani kama sio mwenzao? unajua machungu ya kuibiwa lakini?
 
Wezi wanazingua nao kuna wakati nilikuwa na mtazamo kama wa kwako ila nilikuja badilika kabisa baada ya kuona mwizi amemchoma dada mmoja jirani yangu kisu cha mgongo ili tu afanikishe wizi wa simu apumzike kwa amani rafiki yangu yule..[emoji120]
 
Nazungumzia hayo mateso waliyompa na sitayari wamemkamata? Kwanini wakoroge.cement wamnyweshe? Kwanini wamfunge mikono wamwagie petrol na kumchoma sio haki kabisa! Acha kutetea unyanyasaji wa kibinaadamu.
Mkuu, kibaka anatembea na bisibisi, kukutoboa utumbo ni sekunde tu hapo anabahatisha elfu kumi mfukoni kwako. Ukipona hapo shukuru Mungu. Hao ndo panya road. Wanavamia mara wabake mara waue watu wasio na hatia. Vibaka Wakipelekwa polisi wanatoka kwa dhamana kesi imeisha ndo maana wananchi hawaelewi. Sitetei yeye kuuwawa ila usiombe ndugu yako akutwe na kibaka chobingo wamkabe wamuue maumivu yake hutoweza kueleza. Kikubwa warudi vijijini wakalime. Kukaa mjini watazidi kudokoa watauwawa.

Serikali ingeamua kila kibaka akishikwa akalime lime hata mwezi shamba au afanye kazi eneo flani ndo aachiwe kidogo ingepunguza wao kuchomwa. Sasa unakuta kibaka ana ndugu yake ana mtolea dhamana. Huku keshawaliza asubuhi mnamuona anadunda.
 
Kuna kesi moja nliwahi kuisikia hakimu aliwapa mvua 30 majambazi kwa kesi ya armed robbery. Sikumbuki kama wali appeal au walitumikia kifungo kikaisha. Ila walipotoka tu baada ya siku tatu waliuwawa wote kama walivyo kwenye tukio jingine la armed robbery. Hadi unajiuliza psychology ya mwadamu sijui ikoje. Kama sijakosea kumbukumbu nadhani wali appeal then hakimu aliwaachia kulikua na loop hole kwenye ushahidi wakati ni kweli walihusika. So walishaandikiwa kufa kwa njia hiyo, pengine wangefungwa saizi wangekua wanakaribia kumaliza kifungo.
 
Uuaji ni uuaji!
Panyarodi aliyeua mtu, na mtu aliyemuua panyarodi wote, ni wauaji!

Kwa wasio na dini, uuaji wa kulipa kisasi Kama hivyo ni halali!

Kwa wenye dini wote, wakumbuke dini zao zinafundisha juu ya haki zilizoamriwa na Mwenyezi Mungu!
Wakumbuke mamlaka za ulimwengu zilizosimamishwa na Mwenyezi Mungu!

Mamlaka hizi zipo kusimamia haki na kutoa hukumu!

"Eti tusikulaumu kuua kwa sababu wewe ndio ulioibiwa! Chefuuu!

Kwani sheria zilizowekwa za kutoa hukumu hazijui kuwa wewe na wenzako munaibiwa?

"Eti ukipeleka polisi mwizi anarudi mtaani,"
Watu wazima hovyoo

Atarudi kwa sababu hamuendi kutoa ushahidi,. Mbona kumuua munashirikiana watu zaidi ya ishirini, kwanini ushirikiano huo musiupeleke polisi Kisha mahakamani? Watu ishirini wote mutashindwaje kumtia mtu hatiani?

"Eti serikali yenyewe haiwajibiki na hivyo acha wahalifu wauawe!" Khaaah
Mbona kila kukicha munashangilia viongozi wa Serikali?
Mbona hamuwapindui kwa kura zenu au hata maandamano?
Na ajabu haohao wanaoshadadia wauwaji wa wahalifu wakiamini vyombo vya dola haviwajibiki, Ni UVCCM wakubwa!
Kukicha Ni kumwaga sifa kwa serikali yao!

Lazima tukubali jamii imetawaliwa na roho za kikatili! Mwizi katili na walioibiwa Ni katili pia!
Haiwezekani roho njema ishangilie mateso na kifo Cha mtu aliyeiba television nyumbani kwako!
Nooooo! Lazima kwanza uwe na roho mbayaaa!
Lazima jamii hii ibadilike iwe ya kistaarabu yenye kuwajibika chini ya sheria zetu wenyewe
Cha kushangaza jamii inalalamika pale kiongozi anapoongoza kikatili bila kujali sheria, na tunasahau huyo ni kiongozi kutoka jamii yetu ambayo haioni thamani ya kuishi kwa kufuata sheria!
Kuna tofauti gani kiongozi kuagiza raia anayokwamisha serikali auawe, na raia kumuua mwizi aliyokwapua pochi ya sista du kule mburahati?




Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SI kweli,
Kasome maeneo ya huo mstari
(Luka 6:37-38, 41-42)

1“Usihukumu ili usije ukahukumiwa. 2Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.

3“Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? 4Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe? 5Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.

6“Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
 
(Luka 6:37-38, 41-42)

1“Usihukumu ili usije ukahukumiwa. 2Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.

3“Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? 4Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe? 5Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.

6“Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
Mstari niliotoa ni WA kipindi Cha Musa na Torati ilikuwa ni kuuwawa tu kama ilivyo Sheria ya kunyongwa kwenye baadhi ya nchi.
Ujio wa Kristo umebadili Kila kitu👇

Lakini sasa katika agano jipya la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo..wanadamu hatujapewa tena mamlaka ya kuhukumu kutoka kwa Mungu, kama wana wa Israeli walivyopewa amri ya kuhukumu na Mungu mwenyewe. Hatuna tena hukumu ya jino kwa jino, jicho kwa jicho, mguu kwa mguu, Wakati huu wa sasa wa agano jipya, Hukumu yote amekabidhiwa Yesu Kristo
 
Mstari niliotoa ni WA kipindi Cha Musa na Torati ilikuwa ni kuuwawa tu kama ilivyo Sheria ya kunyongwa kwenye baadhi ya nchi.
Ujio wa Kristo umebadili Kila kitu👇

Lakini sasa katika agano jipya la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo..wanadamu hatujapewa tena mamlaka ya kuhukumu kutoka kwa Mungu, kama wana wa Israeli walivyopewa amri ya kuhukumu na Mungu mwenyewe. Hatuna tena hukumu ya jino kwa jino, jicho kwa jicho, mguu kwa mguu, Wakati huu wa sasa wa agano jipya, Hukumu yote amekabidhiwa Yesu Kristo
amadala
Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha.
3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.
4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.
5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?
6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.
8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.
10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?
11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]
 
Habari za asubuhi wana jamii! Hope mko poa na Xmass ilienda good.

Kuna jambo limenitatiza kidogo kuna kijana amekamatwa akiiba nyumbani kwa jirani hapa, ila cha kushangaza badala ya kumpeleka polisi wakamfungulie mashtaka wameishia kumtesa, kumdhalilisha na kumnyanyasa.

Wamekoroga cement na kumlazimisha ainywe mbaya zaidi wamemfunga kamba mikono na kuimwagia petrol kisha wakaichoma moto, jamani sio uungwana hata kidogo hii ni jamii ya namna gani ya kutesa wezi na vyombo vya sheria vipo? Mbona jamii imekuwa na watu katili kiasi hiki?

Tukataeni unyanyasaji wa aina yoyote ile katika jamii zetu. R.I.P kibaka, walimwengu ni makatili sana.
Hujawahi kuibiwa wewe, siku ukiibiwa nahisi wewe ndo utakuwa mtu wa kwanza kutafuta kidumu cha wese lq kumchomea
 
Nimewahi kuibiwa ila siwezi tesa mwizi kiasi hicho. Lazima uwe na huo moyo wa ukatili kwanza. Kama ule wa kumchoma mtoto mikono kwa kuiba mia mbili na kununulia mihogo.

Huo ukatili lazima uwe nao kwanza, usisingizie eti kisa umeibiwa. Ni kama yule anayemlawiti mwanaume aliyemfumania na mkewe. Huyo ni kawaida yake kuwala machoko.
Wewe uliibiwa lakini hujawahi kusafishwa na wezi, utakuja kunadili msimamo wako japo wapo watu wenye roho mbaya
 
Back
Top Bottom