Uongozi ni akili si mabavu, hongera Rais Samia!

Uongozi ni akili si mabavu, hongera Rais Samia!

muafi

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2015
Posts
2,557
Reaction score
6,128
Nimependezwa jana na hotuba ya Jana ya Mapendekezo ya Bajeti Kuu ya 2022/2023.

Bajeti inekaa vizuri sana. Nampongeza Mh Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha.

Hakika serikali imeonesha nia ya kubana matumizi kwa akili kubwa sana. Jana ndio nilijua hivi kumbe Kuna watu wanalipwa mishahara ambayo hawaifanyii kazi?

Yaani ndani ya halmashauri moja wanaweza kua watu 14 wanalipwa mshahara wa mkurugenzi ilihari sio wakurugenzi eti kisa huko nyuma waliishakua wakurugenzi kisha wakayenguliwa?

Kwahiyo ndani ya wizara moja unaweza kukuta watu zaidi ya 20 wanalipwa mshahara wa katibu mkuu ilihari wako na kazi zingine? Unakuta mhasibu analipwa mshahara wa mkurugenzi?

Nashauri serikali itengue hilo mara moja itasaidia pia mtu kulinda cheo chake kwa kuongeza ufanisi kazini.

Vilevile naafiki swala la kuwakopesha magari watumishi wenye hadhi ya kuwa na magari katika majukumu yao, hii itasaidia kabisa utunzaji wa mali hizo naomba pia hata wale maafisa kilimo watendaji nk hata wao wasipewe pikipiki za serikali isipokua wakopeshwe!

Nawaomba wabunge wote kwa pamoja muipitishe hii bajeti kwa kishindo.

Hongera Rais Samia hongera serikali ya Tanzania
 
Hakuna kitu serikali imepatia kama kuamua kushusha makato ya 42% ya transactions za miamala ya simu...
Halafu ikaenda kutengeneza kodi ya kichwa, huku Mwigulu akisema wamedhamiria kumpunguzia mtanzania mzigo wa gharama za maisha!

Rasilimali za hili taifa hazimsaidii chochote Mtanzania, no wonder wameanza kuzigawa bure kwa waarabu, wameshaona hazina maana.
 
Halafu ikaenda kutengeneza kodi ya kichwa, huku Mwigulu akisema wamedhamiria kumpunguzia mtanzania mzigo wa gharama za maisha!

Rasilimali za hili taifa hazimsaidii chochote mtanzania, no wonder wameanza kuzigawa bure kwa waarabu, wameshaona hazina maana.
umeandika utoto mwingi
 
Halafu ikaenda kutengeneza kodi ya kichwa, huku Mwigulu akisema wamedhamiria kumpunguzia mtanzania mzigo wa gharama za maisha.
Kwenye mifugo wamekuja na kodi ya kengele lazima ulipie alama za mifugo ambayo nayo ni kodi sababu ni lazima
 
Hakuna kitu serikali imepatia kama kuamua kushusha makato ya 42% ya transactions za miamala ya simu. Kutoa makato ya juu ya 7,000/= mpaka kiwango cha juu kuwa 4,000/=

Hii akili ni ya Makamu Wa Rais, wala sio akili ya Waziri Wa Fedha Mwigulu Mchemba.
Ni kelele za mitandaoni mkuu, tena inapashwa ishuke mpk 2,000 watu wataacha kwenda kwenye ATM
 
Bila shaka hii proposal ya kila mtanzania miaka 18 and above alipe kodi ni proposal iliyoanzia hapa JF. Mi binafsi nishawahi kuandika huko nyuma kwamba serikali kuondoa kodi ya kichwa huko nyuma haikuwa na maana ya kwamba mzigo huo wa kodi uwaelemee watu wachache sana -- yaani wafanyakazi na wafanyabiashara tena walioko maeneo yanayoonekana au wanaofanya biashara inayoonekana. Ni jambo jema sana kama hao jamaa wa serikalini wameliona na kuanza kulifanyia kazi.

Eneo jingine tutakaloishauri serikali ni hii dhana yao ya kuamini kwamba njia ya kuboost utalii ndani ya nchi yetu ni staili ya Royal Tour. Yaani kujizungusha huko nje kujitangaza kwa mamovie na madrama kibao kuhusu Tanzania. That style wont work maana hii nchi tayari inajulikana sana. Njia bora ya kuboost utalii ni kutengeneza mazingira ya miundo mbinu bora kwenye vivutio vya utalii -- tengeneza barabara bora za lami kuelekea kwenye mbuga za wanyama (mfano how can you expect mtalii arudi home kwao na good news kuhusu mbuga ya Ruaha baada kupitia barabara mbovu kabisa kuelekea huko mbugani), wekeza kwenye weledi wa tour guides, n.k., in short mfanye mtalii awe na positive experience ya kuitemebelea Tanzania kwa ujumla wake nje na ndani ya vivutio. Siyo tu kufikiri kwamba eti mtalii kinachomtoa Ulaya na kuja Tanzania ni kuangalia mawanyama wenu. Hao wanyama wanao kwenye mazoo yao tayari, na wengine mnaendelea kuwauzia. Ebo!
 
Vilevile naafiki swala la kuwakopesha magari watumishi wenye hadhi ya kuwa na magari katika majukumu yao, hii itasaidia kabisa utunzaji wa mali hizo naomba pia hata wale maafisa kilimo watendaji nk hata wao wasipewe pikipiki za serikali isipokua wakopeshwe!
Madereva wanapigwa chini? Au ndo itakuwa mambo ya wabunge, kupewa posho ya kumlipa dereva?

Master plan ni ipi? Kama wanavyodai katiba mpya, wadai kuwepo na Master plan, sio kusubiri kiki za kila mwaka wa bajeti.

Master plan isimamiwe bila kujali nani kaingia madarakani, na iwe ni lazima na kwa mujibu wa sheria kutekeleza yaliyo kwenye master plan ya nchi.

Nchi masikini, lazima ijiwekee mipango ya kuvuka hatua moja baada ya nyingine kwa mpangilio, sio bajeti zisizoeleweka na kutekelezeka, huku wao wakijichotea hela na kuwahonga bongo movie.
 
Umri haulipi Kodi kwa hiyo anaezalisha alipe Kodi..
Sijaelewa jambo, niweke sawa kuhusu hiyo kodi wanayoisema, kwamba kuanzia miaka 18 walipe kodi? Kuwa watakatwa kodi wakifanya miamala?

Niliona kuwa wanampongeza raisi kwa kuongeza umri wa utegemezi, kutoka 18 hadi 21, hii ina maana gani kulinganisha na hilo la kodi kwa miaka 18?
 
Sijaelewa jambo, niweke sawa kuhusu hiyo kodi wanayoisema, kwamba kuanzia miaka 18 walipe kodi? Kuwa watakatwa kodi wakifanya miamala?

Niliona kuwa wanampongeza raisi kwa kuongeza umri wa utegemezi, kutoka 18 hadi 21, hii ina maana gani kulinganisha na hilo la kodi kwa miaka 18?
TIN ni namba ya utambulisho wa mlipa Kodi,lengo ni kutambua watu wanaostahili kulipa Kodi yaani workforce..

Baada ya kutambua humo ndani otajulikana nani mwanafunzi na nani ni jobless na nani anashughuli ya kufanya Ili alipe Kodi..

Kiufupi ni kwamba wanataka watambue idadi ya wanaostahili kulipa Kodi ilimradi una Kazi ya kuingiza mapato yanayostahili kulipiwa Kodi..
 
Back
Top Bottom