Idara ya Usalama wa Taifa iweke wazi Ofisi zake zilipo na iajiri kwa wazi kama CIA wanavyofanya. Sio mambo yote ya kufanyia gizani
Hawa usalama wa taifa wana shida sana aisee na wanakera sana wana shida mbili iko hivi wao wanajiona ndo wao wakati kiuhalisia ni watoto wadogo sana,
Iko hivi kuna siku nilikuwa Kigoma kikazi sasa siku iyo kulikuwa kuna vijana wa JKT walikuwa wanafanya usafi kwenye holi moja wapo ambalo waziri mkuu alitakiwa aje pale.
Sasa mm nilikuwa kama msimamizi wa wale vijana wa JKT natoa code tuu sijali wala nn [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Hii ni true story aisee.
Sasa bhana katika kufanya usafi wale madogo hawa usalama wa taifa si wakaja bhana sasa kama mnavyojua sisi wazee wa kitenge hakuna kitu tuna heshimu kama bendera na katiba yani bendera tunaheshimu vibaya mno..
Ww ukitaka zinguana na sisi basi mess up katika hivyo vitu viwili bendera na katiba,[emoji41][emoji41] mana sisi tupo kwa ajiri ya kusave hivyo vitu viwili tu bendera na katiba basi na si kingine tuna viheshimu sana
Sasa bana siku iyo ilikuwa saa kumi na mbili jioni mzee madogo wakawa wanashusha bendera sasa ujue bana kama nilivyosema sisi wa kwetu kwetu huwa tunaheshimu bendera vibaya mno bendera ikishushwa lazima tuheshimu.
Bwana wee yule dogo wakati anashusha bendera aisee kuna uyo usalama wa taifa anajifanya eti anakagua kagua mazingira na wakati filimbi imepigwa watu tumesimama yy anajikuta anatembea tembea na kukagua kagua mazingira tulimuacha mpaka bendera ilivyoshushwa.
Sasa baada ya kushushwa bendera tukamfata tukamwambia ww ni mzarendo gani usiheshimu bendera akawa mjuaji anaoongea shit aloo tulichukua fimbo tukanza mchapa aisee chapa sana akajifanya kutoa eti kipisto chake akapiga juu..
Tukamwambia ww ni mpuuzi eeh yani unatutishia sisi pisto na wakati sisi tunacheza na silaa ambazo ww tokea uzaliwe ujawai ziona hata tulimzingua likawa bonge moja la vagi mpaka wakuu wakaja.
Wakuu walikuwa wakuu wao na wakuu wetu mana ugomvi ulikuwa mkubwa sana ishu ikasoviwa pale frsh
Sasa bhana kesho yake tulivyoshusha bendera wote wakawa wamesimama wakaheshimu,hivyo basi usalama wa taifa inatakiwa uwe na weledi kama ilivyo usalama wa jeshini IO..usalama wa sikuhivi si wazalendo hawana siri ni wana mambo ya hovyo sana...