Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Idara ya Usalama wa Taifa iweke wazi Ofisi zake zilipo na iajiri kwa wazi kama CIA wanavyofanya. Sio mambo yote ya kufanyia gizani
[emoji16][emoji16][emoji16], wazo lako zurii lakini kwa kipindi tulichonacho sidhani. Watu wanasema yule brother aliyeachiliwa hivi majuzi kutokea kule kwa kaskazini eti na yeye alikuwa ni member wa tiss! Kama ni kweli ndo idara yetu ina vijana wa design hiyo taifa lipo kwenye totoro kiza!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa sisi wananchi tumekusikia.

Sasa unataka Mfumo ubadilishweje? Toa mapendekezo ya namna ya kubadili mfumo!? Sisi wananchi, Hatutaki malalamiko ya kero tu tunataka utuandikie mapendekezo ya namna ya kuondoa kero hizo.

Rasimu ya jaji Warioba ilibeba namna bora ya uongozi katika nchi hizi. Ila CCM waliogombea rasimu ile na kubadilisha mapendekezo ya wananchi ili kuendana na uchu wao wa madaraka.
 
Ajabu ni kwamba kuna mtu anakopa mabilioni benki 5 kubwa na kukimbia nchi.

Hao tiss wapo busy kukamata kina mbowe.
 
Dah kwhy mnajazana maofisi kwa kazi gani ,,,Kazi yenu kupeleka umbea kwa maboss ,,,
Hicho kitengo Cha audit kimefanya nn kwa Taifa ???
 
Upande wa siri ni kama wewe ulivyokuja kumuanika agent hapa.
 
Hata mimi juzi nilimzabua mwanajeshi mmoja hivi kisa eti kanipa amri kusimama nikagoma wakati sipo kambini kwao wala eneo hatarishi ,,,wakati ananisogelea nikamsoma macho take nikaona ni mchumba tu nikamziba vibao akina mama waliokuwa pale wakapiga kelele Mimi sikujali nikamburuza na magwanda take,,,badae akaja mzee mmoja ana busara akayamaliza kiutu uzima mjeda akabaki na aibu zake haoni hata njia ya kupita kwa aibu,,sasa hivi natembea na kisu changu najua atanivizia na wenzake siku hiyo watajuta mbwa wake maana mkono naujua
 
Sawa sisi wananchi tumekusikia.

Sasa unataka Mfumo ubadilishweje? Toa mapendekezo ya namna ya kubadili mfumo!? Sisi wananchi, Hatutaki malalamiko ya kero tu tunataka utuandikie mapendekezo ya namna ya kuondoa kero hizo.
Sasa wewe inerpol na wenzio mliendaga nje ya Nchi kujifunza Nini,,Mana kwa zama hizi za transformations wewe t es es unataka sisi walala hoi tukufundishe kazi,,,,mnamaliza kodi zetu..

Mnachojua Ni kutuwekea bastola vichwani ili watawala wapite bila kupingwa
 
wakati TISS ikiajiri staff wake kwa kufuata mifumo ya kizamani toka mataifa ya kikomunisti, huko CIA mambo ni kama hivi.
[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
Browse CIA Jobs - CIA
Sio hao tu taasisi zote hadi MSS ya China nayo hutangaza kazi zao japo wao wameelekeza kazi kwa Police Dep
 
Tatizo ni pale ambapo idara hii wanachukuana makada wa CCM, bila kujali u-smart kichwani ,uzalendo n.k.
Kazi yao kubwa ni kuvaa masuti meusi,kulinda viongozi na kuteka ama kuua wapinzani wa serikali.
Hii sio sawa.
Naililia NCHI yangu Tanzania.
Mtu aliyeshindwa elimu akakimbilia jeshini anau-smart gani?
 
Sasa usalama wa Taifa unaeingilianaje na ufisadi,TAKUKURU kazi yao nini?
Ni kazi yao kuhakikisha hakuna uhujumu uchumi ufisadi wala ubadhirifu wa mali za umma.

Kiutendaji TISS inatakiwa isimamie usalama wa nchi, uchumi na siasa za kitaifa.

Ila kwa huu mfumo mbovu hawatimizi majukumu yao.
 
Jifundishe pakuweka R na pakuweka L.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…