Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Ngoja nikusaidie kazi ya tiss ni kukusanya taarifa kuzichakata/kuzichambua na kuzipeleka kunakohusika na kushauri wenye mamlaka ya kuchukua hatua ni wale wanaopelewa taarifa na wanatimiza Sana majukumu ipasavyo.

Ile kwenda kwenye uchaguzi na kulazimisha mgombea wa CCM atangazwe bila kujali matokeo halisi, ni sehemu ya huo wajibu wao?
 
Linaweza kuwa swali lisiloeleweka haraka, Labda nianze na simulizi kwanza

Mwaka 1979 Tanzania iliingia kwenye vita na Uganda maarufu kama vita ya KAGERA. Mwaka 1995 nilikutana na mzee Mkumbi(marehemu) mmoja wa watu ambao walikaribia kabisa kupigana vita hiyo. Miongoni mwa mambo aliyonisimulia ni kuwa yeye alirudia eneo la mwisho ambalo angetoka hapo ilikuwa ni moja kwa moja anaingia uwanja wa vita. Anasema alifurahi sana kwani akiwa kwenye eneo la mwisho ambalo daktari alikuwa anawapima afya ndipo alinusurika, kilichomnusuru ni kukutana na daktari ambaye alikuwa ndugu yake, akamuokoa kwa kueleza kuwa afya yake si mzuri.

Binafsi ingawa sikusema nilimshangaa sana huyu mzee kwa sababu alichokifurahia ni kukwepa majukumu yake ya msingi kama Mwanajeshi, hata huyo daktari kwangu bado hakuwa Mzalendo alitaka mtoto wa nani afe na wa nani abaki? Na hawa ndio wale ambao ni wengi wanaajiriwa kwenye majeshi yetu kwa njia za upendeleo lakini je tumeangalia nini athari yake?

Kuna hii idara maarufu ambayo wengi wanatamani kuajiriwa ambayo ni usalama wa Taifa, Licha ya mshahara na marupurupu yake upande wa pili wa idara hii ukoje(side effect yake ni ipi?) Kuna jamaa waliibuka kwa ahadi za kuajiri watu kwenye Idara hiyo ambapo walikuwa wanahongwa Mil 1 na kuendelea ili kuwapatia watu kazi kwenye Idara hiyo, Hivi ni kweli watu wanaoingia kwa mtindo huo watayaweza hayo majukumu? Au kazi yenyewe ni ile ya kupita kurekodi tu watu wanaomkosoa Rais kwenye vijiwe vya kahawa? Hakuna majukumu ambayo yanamtaka mtu kujitoa ambayo yanaweza kumfanya mtu akwepe kutimiza wajibu wake kama yule mzee aliyekwepa kwenda kupambana Uganda?

NAULIZA TU.
Mkuu

Unafikiri wanaoiba hawana uzalendo!!?

Sio kweli ni wamekata tamaa baada ya kuujua ukweli fulani tena deep ukweli ambao hawaoni future yoyote huko mbele!

Unafikiri wazungu walitupa uhuru bila kumwaga damu bure tena kupitia secret society kama makanisa kwa kumfanya kijana wao awe kiongozi!!!?

Think hapo kwa kina!!kuna mali zao zipo humu ardhini wanamiliki sasa unafikiri usipoiba kwenye nafasi yako hao wazungu watakuja kuonea huruma kizazi chako!!!?


Hivi unafikiri kikwete,mwinyi,mkapa,jpm hawakua wazalendo na wenye huruma kwetu!!?

Ni kwamba walifikiria sana wakaona majamaa yamewatinga na hawawezi kupambana nao wakaamua wale tu na wao kwa ajili ya vizazie vyao basi !!!

Kuna jambo kubwa sana hawa watu wanagundua ndio maana wanaoiba wakiwa na akili timamu sio wajinga hao!!

Omba Mungu nawe upate nafasi uke kwa nafasi yako jua HIVYO mkuu!!!!

Hata marehem jpm na uzalendo wake wa wanyonge aliiba pia utambue hilo mkuu!!!
 
Hawa usalama wa taifa wana shida sana aisee na wanakera sana wana shida mbili iko hivi wao wanajiona ndo wao wakati kiuhalisia ni watoto wadogo sana,

Iko hivi kuna siku nilikuwa Kigoma kikazi sasa siku iyo kulikuwa kuna vijana wa JKT walikuwa wanafanya usafi kwenye holi moja wapo ambalo waziri mkuu alitakiwa aje pale.

Sasa mm nilikuwa kama msimamizi wa wale vijana wa JKT natoa code tuu sijali wala nn [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Hii ni true story aisee.


Sasa bhana katika kufanya usafi wale madogo hawa usalama wa taifa si wakaja bhana sasa kama mnavyojua sisi wazee wa kitenge hakuna kitu tuna heshimu kama bendera na katiba yani bendera tunaheshimu vibaya mno..


Ww ukitaka zinguana na sisi basi mess up katika hivyo vitu viwili bendera na katiba,[emoji41][emoji41] mana sisi tupo kwa ajiri ya kusave hivyo vitu viwili tu bendera na katiba basi na si kingine tuna viheshimu sana

Sasa bana siku iyo ilikuwa saa kumi na mbili jioni mzee madogo wakawa wanashusha bendera sasa ujue bana kama nilivyosema sisi wa kwetu kwetu huwa tunaheshimu bendera vibaya mno bendera ikishushwa lazima tuheshimu.

Bwana wee yule dogo wakati anashusha bendera aisee kuna uyo usalama wa taifa anajifanya eti anakagua kagua mazingira na wakati filimbi imepigwa watu tumesimama yy anajikuta anatembea tembea na kukagua kagua mazingira tulimuacha mpaka bendera ilivyoshushwa.


Sasa baada ya kushushwa bendera tukamfata tukamwambia ww ni mzarendo gani usiheshimu bendera akawa mjuaji anaoongea shit aloo tulichukua fimbo tukanza mchapa aisee chapa sana akajifanya kutoa eti kipisto chake akapiga juu..


Tukamwambia ww ni mpuuzi eeh yani unatutishia sisi pisto na wakati sisi tunacheza na silaa ambazo ww tokea uzaliwe ujawai ziona hata tulimzingua likawa bonge moja la vagi mpaka wakuu wakaja.


Wakuu walikuwa wakuu wao na wakuu wetu mana ugomvi ulikuwa mkubwa sana ishu ikasoviwa pale frsh


Sasa bhana kesho yake tulivyoshusha bendera wote wakawa wamesimama wakaheshimu,hivyo basi usalama wa taifa inatakiwa uwe na weledi kama ilivyo usalama wa jeshini IO..usalama wa sikuhivi si wazalendo hawana siri ni wana mambo ya hovyo sana...
Nilikuwepo hiyo siku pale mesi
 
Wengi wanaishia kwenye Pombe na Umalaya tu.Kuna kipindi nilikua na wakuu wakitengo maeneo flani walinchukua tukatembee nipate kujua maeneo kidogo ila cha kushangaza walipiga bia kama 19 kila MTU ila mmoja alizidiwa na kuanza kuropoka mission zao na majukumu waliyoyakamilisha Nilijifanya siwaelewi ila mmoja akabadili story kwa staili yaaina yake by that time nilikua napata soft drinks na kiepe changu.Mpaka sasa mmoja ananitaftaga sana kunifanya niwe karibukaa

Wengi wanaishia kwenye Pombe na Umalaya tu.Kuna kipindi nilikua na wakuu wakitengo maeneo flani walinchukua tukatembee nipate kujua maeneo kidogo ila cha kushangaza walipiga bia kama 19 kila MTU ila mmoja alizidiwa na kuanza kuropoka mission zao na majukumu waliyoyakamilisha Nilijifanya siwaelewi ila mmoja akabadili story kwa staili yaaina yake by that time nilikua napata soft drinks na kiepe changu.Mpaka sasa mmoja ananitaftaga sana kunifanya niwe karibu
Kaa nae Kwa umakini Hawa jamaa sio wa kuwaamini,akikununulia pombe usiwe mropokaji Sana,halafu wengi pombe hawaziwezi hata,
 
ID yako inaonesha unaishi kwa dadaako ndiyo maana una-support ujamaa
Isingekuwa ujamaa usingekuwa unabwabwaja hapa mitandaoni, maana kama si ujamaa, mnala wa kukufanya uweze Kupata mawasiliano ya simu usingesimikwa apo ufipanii.
 
Isingekuwa ujamaa usingekuwa unabwabwaja hapa mitandaoni, maana kama si ujamaa, mnala wa kukufanya uweze Kupata mawasiliano ya simu usingesimikwa apo ufipanii.
Na kweli ndiyo maana hadi leo Kenya katupita kiuchumi licha ya kuwa tunamzidi rasilimali
 
Hawa usalama wa taifa wana shida sana aisee na wanakera sana wana shida mbili iko hivi wao wanajiona ndo wao wakati kiuhalisia ni watoto wadogo sana,

Iko hivi kuna siku nilikuwa Kigoma kikazi sasa siku iyo kulikuwa kuna vijana wa JKT walikuwa wanafanya usafi kwenye holi moja wapo ambalo waziri mkuu alitakiwa aje pale.

Sasa mm nilikuwa kama msimamizi wa wale vijana wa JKT natoa code tuu sijali wala nn [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Hii ni true story aisee.


Sasa bhana katika kufanya usafi wale madogo hawa usalama wa taifa si wakaja bhana sasa kama mnavyojua sisi wazee wa kitenge hakuna kitu tuna heshimu kama bendera na katiba yani bendera tunaheshimu vibaya mno..


Ww ukitaka zinguana na sisi basi mess up katika hivyo vitu viwili bendera na katiba,[emoji41][emoji41] mana sisi tupo kwa ajiri ya kusave hivyo vitu viwili tu bendera na katiba basi na si kingine tuna viheshimu sana

Sasa bana siku iyo ilikuwa saa kumi na mbili jioni mzee madogo wakawa wanashusha bendera sasa ujue bana kama nilivyosema sisi wa kwetu kwetu huwa tunaheshimu bendera vibaya mno bendera ikishushwa lazima tuheshimu.

Bwana wee yule dogo wakati anashusha bendera aisee kuna uyo usalama wa taifa anajifanya eti anakagua kagua mazingira na wakati filimbi imepigwa watu tumesimama yy anajikuta anatembea tembea na kukagua kagua mazingira tulimuacha mpaka bendera ilivyoshushwa.


Sasa baada ya kushushwa bendera tukamfata tukamwambia ww ni mzarendo gani usiheshimu bendera akawa mjuaji anaoongea shit aloo tulichukua fimbo tukanza mchapa aisee chapa sana akajifanya kutoa eti kipisto chake akapiga juu..


Tukamwambia ww ni mpuuzi eeh yani unatutishia sisi pisto na wakati sisi tunacheza na silaa ambazo ww tokea uzaliwe ujawai ziona hata tulimzingua likawa bonge moja la vagi mpaka wakuu wakaja.


Wakuu walikuwa wakuu wao na wakuu wetu mana ugomvi ulikuwa mkubwa sana ishu ikasoviwa pale frsh


Sasa bhana kesho yake tulivyoshusha bendera wote wakawa wamesimama wakaheshimu,hivyo basi usalama wa taifa inatakiwa uwe na weledi kama ilivyo usalama wa jeshini IO..usalama wa sikuhivi si wazalendo hawana siri ni wana mambo ya hovyo sana...

Recruit pool ni mbovu. Ndio maana tunapata product za hovyo
 
Hebu rudi form two usome vizuri features za modes of production uone utofauti
Masikini ya Mungu, unajivunia elimu ya form2 mpaka Leo. Inamaana Niko napoteza mda na matu anayetumia rejea za f2? Haya Bwana ulalee tuu. Mmmmh
 
Masikini ya Mungu, unajivunia elimu ya form2 mpaka Leo. Inamaana Niko napoteza mda na matu anayetumia rejea za f2? Haya Bwana ulalee tuu. Mmmmh
Nimekurejesha huko maana akili yako haijafika huko...halafu nina wasi wasi wewe unaweza kuwa miongoni mwa hawa form four failures, kama sijakosea.

maana nakupatia ideas jinsi ya kupanga logistics zako ili uonekane walau kama msomi, unaleta ubishi vipi humo kichwani kuna kitu...haloooooh
 
Back
Top Bottom