Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Usiogope wewe nenda kale pesa hawana kazi ngumu wala weledi wowote zaidi ya kuwa watumwa kwa wanasiasa
Acha kauli za kejeli huenda kuna mapungufu yapo kulingana na katiba yao lakin kumbuka wanajitoa zaid kulinda taifa
 
Napenda ule mjengo wao ukiuangalia toka angani Uko kama mwewe Eagle
 
Acha kauli za kejeli huenda kuna mapungufu yapo kulingana na katiba yao lakin kumbuka wanajitoa zaid kulinda taifa
Sasa kama katiba ina mapufu wamefanya nini ili kuhakikisha inakaa sawa sasa kama mambo ya kitafa yanawashinda watayaweza ya kimataifa hapo ndo walipo prove that they are nothing and useless
 
Kazi hii ni nzuri hasa ikiwa ulizaliwa kwa ajili hiyo, hivyo adha zake unazimudu tu na kuzifurahia; lkn kwa wale watafuta ajira na misifa utaishia 'kuokotwa kisimani' ukiwa maiti (snitched) maana ETHICS zake zitakufanya ujione mtumwa usiyeweza kuvumilia utumwa na hivyo kujitoa ufahamu matokeo yake ndio hivyo.
Ndio maana duniani kote mashushushu na majasusi lazima wawe 'INTELLIGENT' something which is natural!

Mie siipendi kabisa kazi hii maana unawinda huku ukiwindwa. Ni sawa na jambazi kuingia nyumbani kwa mtu akidhani HAONEKANI kumbe ANASUBIRIWA tu kwa hamu!

Mchango wako unaonyesha kuwa at least kila mmoja aliumbwa akiwa anapenda kufanya kilicho kizuri, na kwa mantiki hiyo inapotokea watu wamefanya vile ambavyo ni vibaya, inakuwa ni nje ya matarajio yao.. Looks like kila mtu anapenda kufanya kazi ya usalama, wakati sijawahi kusikia kuwa ndiyo kazi inayoongoza kwa maslahi mazuri.Inaweza kuwa ina maslahi mazuri ndiyo lakini sina uhakika kama nii kazi inayoongoza kwa maslahi mazuri. Kwa hiyo watu wanaoitamani hasa inakuwa si kwa ajili ya maslahi, isipokuwa ni nature ya kazi yenyewe wanaipenda. Nadhani zaidi ya asilimia 90 ya watu watakuwa wanapenda kazi hii. Neno INTELLIGENCE/USALAMA, ndiyo kivutio hasa, na si maslahi ya kazi,..., au ninakosea? Everybody would love to be regarded as INTELLIGENT.

Ni kama mtoto mdogo anapokuwa ansoma shule ya Msingi, anapopata alama nzuri huwa anafurahi sana si kwa sababu anataka kuja kupata kazi nzuri huko baadaye hapana. Ni kwa sababau alama nzuri ni nzruri kwake, basi!
 
Mkuu heshma kwako
Niliokuambia hao ni watu Wangu wakaribu Mkuu ila sipendi wafahamu hizi mambo nafatilia hata kwa njia yoyote ile iwe kwa kusoma tu au kutazama movies za kiintelijensia Mkuu kumradhi sitaweza kuwakutanisha "Nisameheme kwa hili" Karibu St Francis!!
Ndo unashtuka sasa kuwa jamaa nae ni kachero? Hahaa umeanza kukana stori yako
 
Lakini mara nyingine TISS haiwezi kushughulikia maadui wa taifa bila kuwahusisha TPDF @ JWTZ,
Kuna matukio mengi ya kihatari ambayo yanakuwa Para-militaristic sana na TISS hawawezi kuyamaliza wenyewe. Inahitaji ukusanywaji wa taarifa na mikakati ya kijeshi ili kuweza kukamilisha kazi kwa ufanisi wa hali ya juu sana.

Kikubwa zaidi ni kwamba TISS ina mkono mrefu sana kuliko TPDF @ JWTZ,
Kwasababu ni CIVILIAN INTELLIGENCE na inahusika na raia kwa moja kwa moja.
TPDF @ JWTZ Jurisdiction yao iko very limited kwasababu wao ni Purely Military tofauti kabisa na TISS.

Japo sasa,
Majasusi wengi wa TISS ambao ni heavy duty wanatokea JWTZ.
Kwasababu mfano tu, mwanajeshi Special Forces (Marine) anakuwa na uwezo mkubwa sana wa kufanya kazi za kijasusi wa kijeshi kama Reconnaissance, Kutegua mabomu, kuchambua na kutafsiri mikakati ya kijeshi ya nchi za adui kuliko jasusi ambaye yuko uraini kila siku . Kikubwa ambacho jasusi wa TISS atamshinda huyu Jasusi aliyetoka jeshi ni "Broad Mind" kwasababu mwisho wa siku kila taarifa za kijasusi ziwe za Kijeshi au Kiraia (Raw Intelligence) ni lazima ichakatwe (Processed) kwa ajili ya matumizi ya Kiutawala(Civilian Administrative Purposes). Wanaochakata ni Analysts ambao ni Think Tanks kutokea TISS kwasababu wanakuwa na mtazamo wa kiraia... ..Hili ndilo linawafanya TISS wawe hatua kumi mbele ya JWTZ @ TPDF kama taasisi.

NB 1: TISS wanafanya kazi bampa tu bampa na JWTZ kwasababu Its the duty of the TISS to make sure the army behaves and remains royal to the government and the state at by and large......!!!! Hivyo contractors wengine wa TISS wanakuwa ni wanajeshi katika asilimia 100% na maisha yao yote ni kwenye Barracks za kule Lugalo au Ngerengere.

Tuseme ukweli,
TISS na JWTZ ni mapacha wasiofanana (Fraternal Twins)
Hakuna anayeweza kufanya kazi bila kumtegemea mwenzake.
TISS IMARA=JWTZ IMARA..........

NB 2: Tusisahau pia kwamba JWTZ nao wana kitengo chao cha Intelijensia.
MILITARY INTELLIGENCE nacho kinafanya kazi na oparesheni kubwa sana za kijeshi.
Kazi yake ni kushughulikia maadui wa taifa covertly/clandestinely ambao ni purely Militaristic of Para-Militaristic in nature........

Cc: zitto junior , Consigliere , ISIS , mngony , mng'ato , Poise , chige, Da'Vinci
Kwanini mnaliweka pembeni jeshi la polisi na kukomaa na Jwtz pekee?Ina maana ni kweli hamjui kwamba jeshi la polisi lina taarifa nyingi na muhimu kabisa za kiusalama kuliko hata Jwtz?
 
Hii kazi ngumu, jamaa wanajitoa sadaka kwa ajili ya taifa hili, hii si kazi ya kuikimbilia kisa malupulupu na mshahara mkubwa inatakiwa dhamira ya zati kutoka moyoni.
Acha wewe, hakuna anaejitoa sadaka kww ajili ya taifa hili bila kuangalia upande wa pili kwa maslahi yake[emoji41] [emoji41] [emoji41] [emoji377] [emoji377] [emoji377]
 
Kwanini mnaliweka pembeni jeshi la polisi na kukomaa na Jwtz pekee?Ina maana ni kweli hamjui kwamba jeshi la polisi lina taarifa nyingi na muhimu kabisa za kiusalama kuliko hata Jwtz?
halijasahaulika,ila ni ishara kwamba linajitegemea halihitaji msaada kutoka taasisi nyingine katka utendaji wake.ndio maana hujaona likihusishwa hapo.
 
Hii kazi ngumu, jamaa wanajitoa sadaka kwa ajili ya taifa hili, hii si kazi ya kuikimbilia kisa malupulupu na mshahara mkubwa inatakiwa dhamira ya zati kutoka moyoni.

Mkuu siku za Nyerere kulikuwa na ulaji hatari. Kuna Mzee fulani hivi sasa ni marehemu, yeye alikuwa akizitumia pesa kwenye kuifadhili timu ya Yanga kwenye mambo ya kishirikina.
 
Tiss wanafanya kazi Yao Barabara toka 1961 mpaka hapa tulipo sio haba kwa kuwa wao sio Malaika mapungufu machache yatakuwepo hila kwa ujumla wake wanafanya kazi vizuri sana pia wapo wanaichafua kwa kujiita usalama kumbe sio wanachonga vyeti feki..Kwa ujumla wake vyombo vya usalama na ulinzi vinafanya kazi zao vizuri.
 
Tiss wanafanya kazi Yao Barabara toka 1961mpaka hapa tulipo sio haba kwa kuwa wao sio Malaika mapungufu machache yatakuwepo hila kwa ujumla wake wanafanya kazi vizuri sana pia wapo wanaichafua kwa kujiita usalama kumbe sio wanachonga vyeti feki..Kwa ujumla wake vyombo vya usalama na ulinzi vinafanya kazi zao vizuri.


Mkuu unanikumbusha jamaa yangu fulani anaishi majuu, alikuja kutembea .
Wakati anatoka uwanja wa ndege vijana wako wa TISS wakamfuatia .Bila aibu wakaanza kumtaka atoe chochote au watamfanyia zengwe. Kwa bahati alikuja kupokewa na Mzee fulani ambaye alivalia ki-smart kama yule mnajimu Marehemu Sheikh Yahya Hussein. Jamaa walipomwona tu walijikata kama wadudu. Haya ni wakati wa Rais Mkapa
 
Ni mbaya kuliko JWTZ @ TPDF kwani wapo kazini saa 24 kwa siku saba. Pia hamjui adui na anatakiwa amfahamu kiundani hasa. Hana adui maalum kwani yote yake mradi usalama wa taifa uwe salama. Tiss personnel are supposed to detect and eliminate in covert and/or clandestine way any threat to national security.

Huo ndio ubaya wa TISS. TPDF anasubiri tuvamiwe ndo aingie kazini.
TPDF ndio wenye nchi
 
Back
Top Bottom